Huyo anaimba nyimbo za kijamii, siyo GOSPEL !
Mkuu Chachasteven, Gozbert mimi mwenyewe nilikuwa namtilia mashaka sana mara niliposikia nyimbo zake kwa mara ya kwanza, lakini wimbo huu alioutoa ndio ulithibitisha kwamba huyo hakiki sio Mtumishi, yaani sio muimbaji wa Nyimbo za Injili bali huyo ni wale wanaoitwa wasanii wa nyimbo za injili, itoshe tu kutambua na hakuna haja ya kubishana hapa, naamini hata yeye mwenyewe analijua hilo, na anashangaa anapoona kuna watu wanamtetea, Kuimba Injili inataka Mtu uwe na Wito na pia Ushuhuda, sio kujiimbia tu kwa sababu unaweza kuimba, sijajua wewe msimamo wako kiimani ni upi, yawezekana unaweza kuwa unamtetea ukifurahi kuona jinsi anavyowapoteza watu wengi watakaochagua kumfuata, lakini kama wewe unatamani kuona watu wanapewa iliyo kweli kwenye Injili nadhani tusaidiane kuwakosoa watu kama Gozbert waache mara moja kusaidia wanaoutukana Ukristo kwa sababu ya style zao za Uimbaji, nakuhakikishia asipokemewa atakuja kufanya vituko sana kwenye aina hiyo ya uenezaji wa Injili.Mkuu Author, Unachokifanya hakiakisi hata tone ya vile unavyojiita. Niliposoma kichwa cha uzi wako na jina lako nilihamasika sana kufungua huu uzi wako lakini nimesikitika sana baada ya kuona na kusoma ulichoandika kwa sababu kadha wa kadha.
Kwanza, Umeshindwa kuchunguza na kuelewa kuwa Gospel ambayo anaimba msanii wa Tanzania ni Bongo Fleva pia. Kwa lugha nyepesi umeandika bila kuelewa undani wa hicho unachokiandika. Pole sana.
Pili, Gospel sio lazima iimbwe juu ya biti za vinanda. Hio ni kwa sababu Gospel ni ujumbe na sio uzuri au ubaya wa biti. Swali ni kwamba ujumbe aliouonyesha Gozbert humo unahamasisha injili au unapinga injili??
Naomba unielewe kuwa sikatai kuwa unachokisema ni sahihi. Unaweza kuwa sahihi au usiwe sahihi. Ninachoshangaa ni kwamba umeshindwa kuthibitisha malalamiko yako. Ni kama watu wanaotaka bangi ihalalishwe - huwa wapo sahihi, ila hawajui kuitetea hoja yao.
Anyways, Ukijibu hayo maswali hapo juu naomba nikupe home work. Nenda uisikilize Album ya Kanye West, Jesus is King.
Alipopanda tu jukwaa la fiesta nikasema basi yameisha
Hiyo ni njia ya kutoka aliyoshauriwa na jasiri muongoza njia marehemu Rugemalira.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hata wewe ubaweza kuchangia mada za aina hii ??!!.
Ninazochangia siku zote zipoje?Hata wewe ubaweza kuchangia mada za aina hii ??!!.
Aah zile za tunda na masihara naona ndio hua zinakukoga
UmenifananishaAah zile za tunda na masihara naona ndio hua zinakukoga
Demi wa kufananishwa na nani ??
Nikuukize wewe. Nachangia mada yoyote ila kwenye siasa sio sanaDemi wa kufananishwa na nani ??
umejibu kama goodluck, au manager wake! Umeeleza VyemaMkuu Author, Unachokifanya hakiakisi hata tone ya vile unavyojiita. Niliposoma kichwa cha uzi wako na jina lako nilihamasika sana kufungua huu uzi wako lakini nimesikitika sana baada ya kuona na kusoma ulichoandika kwa sababu kadha wa kadha.
Kwanza, Umeshindwa kuchunguza na kuelewa kuwa Gospel ambayo anaimba msanii wa Tanzania ni Bongo Fleva pia. Kwa lugha nyepesi umeandika bila kuelewa undani wa hicho unachokiandika. Pole sana.
Pili, Gospel sio lazima iimbwe juu ya biti za vinanda. Hio ni kwa sababu Gospel ni ujumbe na sio uzuri au ubaya wa biti. Swali ni kwamba ujumbe aliouonyesha Gozbert humo unahamasisha injili au unapinga injili??
Naomba unielewe kuwa sikatai kuwa unachokisema ni sahihi. Unaweza kuwa sahihi au usiwe sahihi. Ninachoshangaa ni kwamba umeshindwa kuthibitisha malalamiko yako. Ni kama watu wanaotaka bangi ihalalishwe - huwa wapo sahihi, ila hawajui kuitetea hoja yao.
Anyways, Ukijibu hayo maswali hapo juu naomba nikupe home work. Nenda uisikilize Album ya Kanye West, Jesus is King.
Vigezo vya kujua huyu anaimba GOSPEL ni vip ?Habari wana JF,
Moja kwa moja kwenye mada, kama tujuavyo neno Gospel maana yake ni Habari njema kwa watu wote (kutokana na imani ya kikristo). Na kuna waimbaji wengi (hatuwaiti wasanii maana hamna usanii kwenye dini) wanaimba kama njia ya kumtumikia Mungu.Wapo wengi kama kina Bahati Bukuku, Rose Muhando,Christina Shusho n.k
Mwanzo nilikuwa nasita kupinga kuwa Goodluck gozbert sio muimbaji wa Injili ila ni mziki wake ni wa Bongo flavour tu. Hili linajidhirisha vyema kupitia nyimbo yake ya 'Nibadilishe' ambayo ndani yake mahadhi ya nyimbo na style za kucheza hazitofautiani na zile za kina Harmonise, Diamond, Burna Boy n.k. Hii inaniaminisha kuwa huyu si muimbaji wa gospel bali anafanya Bongo flavour kwa kivuli cha dini. Kama hujaona wimbo huo...Angalia kwenye link hapa chini....
Sent using Jamii Forums mobile app
Hili ni swali zuri sana, ila najua mleta uzi hawezi kulijibu kwa sababu hajafanya tafiti za kutosha juu ya malalamiko yake. Simlaumu, hata hivyo, kwa sababu ni haki ya kila mtu kuhoji ingawa maswali aliyonayo kayaweka kama mtazamo na hali halisi. Yaani hajataka kuuliza ila amekuja kutuambia Gozbert sio muimba Gospel na anataka tukubali. Kigezo alichokitumia sasa! Ni taabu tupu.Vigezo vya kujua huyu anaimba GOSPEL ni vip ?
Anecdotes are not facts. Bring us facts. Only facts. Not mere words, brother.