GPSA: Tuhuma za ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka na mengineyo

GPSA: Tuhuma za ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka na mengineyo

Kazi kweli kweli. Ila TAKUKURU hawako huru. Taarifa kama hii ni nzuri lakini hawawezi kuifanyia kazi. Kuna sababu mbili;
1. Mpaka watumwe na Viongozi wa juu wa Serikali hasa Rais

2. Taarifa kama hii ikitoka wataitumia kuombea na kupokea RUSHWA kutoka kwa mlengwa. Kwa hiyo kutoa mada unakuwa kama umewapa ulaji hao TAKUKURU.

Ni maoni yangu tu kutokana na kesi ninazoziona zikiendelea Mahakamani ambazo kwa asilimia kubwa ni zile zilizo na msukumo wa Viongozi wa juu wa Serikali.

Kesi zinazopelekwa na whistle blowers siyo nyingi na zinawanufaisha wao TAKUKURU tu.
Sio kweli Mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ufisadi mwingine na wizi upo kwenye ile office ya kutoa mizigo bandarini ambayo ipo chini ya GPSA, mhasibu wake ni fisadi mkubwa sana
Toa ushahidi mkuu ili TAKUKURU na serikali wajue pa kuanzia wapi najua lazma watapita hapa,...toa neno japo kidogo kuhusu huyo Mhasibu.

Na kwa GPSA sehemu yoyote ya upipagi mkubwa lazma kuwe na mkono wa DBSS au CEO mwenyewe...yaani taasisi imeharibiwa kabisa kwa uroho wao
 
Kuna baadhi ya taarifa zinazohusu Ufisadi na matumizi mabaya ya ofisi ya Hawa viongozi tutaziweka hapa leo ikiwemo kupostiwa kwenye page ya mange na kigogo kule Twitter.

Maliki Aram(DBSS) najua unapitia huu uzi, nipo kwenye hayo magroup ya wasap uliyounga ghafla baada ya hii habari kusambaa.. ..ninakuchora tu unavyojitahidi kutafta taarifa, uzuri huko mjadala ukianza tutachangia wote...usisumbuke kabisa kunitafuta maana hutonifahamu kwa Sasa lakini siku ukitiwa pingu Mimi nitakuwepo utanifahamu na hili halina mda mrefu
Weka ndani jizi hilo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna baadhi ya taarifa zinazohusu Ufisadi na matumizi mabaya ya ofisi ya Hawa viongozi tutaziweka hapa leo ikiwemo kupostiwa kwenye page ya mange na kigogo kule Twitter.

Maliki Aram(DBSS) najua unapitia huu uzi, nipo kwenye hayo magroup ya wasap uliyounga ghafla baada ya hii habari kusambaa.. ..ninakuchora tu unavyojitahidi kutafta taarifa, uzuri huko mjadala ukianza tutachangia wote...usisumbuke kabisa kunitafuta maana hutonifahamu kwa Sasa lakini siku ukitiwa pingu Mimi nitakuwepo utanifahamu na hili halina mda mrefu
Ni vyema usitoe updates za namna hii, ni rahisi kujulikana kama atakuwa na watu makini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Government Procurement Service Agency (GPSA) tatizo ni management kama yule DBSS hafai kabisa kuwa ofisini ni fisadi halafu mbinafsi na mbaya Zaidi anawahonga wakaguzi wanapokuja kumkagua na mambo yanaisha, na ili kulinda ugali wake anawala (anawagegeda) wafanyakazi wa kike walio wepesi kutongozeka ili wawe wanampelekea umbeya ambapo wengi wao anazawadia kwa kuwapa kipaumbele cha visafari na semina pale inapotokea yaani kama una mke wako anafanya GPSA humu jamaa hajali yeye anachovya tu,..na wa kiume nao anaselect wa kuwa wanampelekea umbeya kuhusu wafanyakazi wengine..

Ukiwa hujipendekezi GPSA maisha yako yanakuwa magumu, na CEO naye amemezwa na DBSS na mpenda sifa na maJungu Zaidi ya ufanisi wa kazi anatumia pesa nyingi kuhamisha watumishi kwa sababu ya umbeya tu anaopelekewa, kiufupi hana weledi wa kuongoza taasisi, na hawezi kuifikisha mbali na mara mia angepewa Liliani aliyekuwa ana - kaimu.

GPSA inatakiwa iwe juu ya MSD kimapato na kimaslahi kwa watumishi wake,tuna vyanzo vingi vya mapato lakini viongozi wanawaza ufisadi tu, sasa eti wafanyakazi wa mikoani tunalipwa posho kidogo kulinganisha na makao makuu kisa tuko mikoani tunatakiwa kulipwa tofauti na wa makao makuu, sasa kama hatuna umuhimu kisa tuko mikoani si bora tuhamishiwe wote makao makuu na mikoani kusiwe na wafanyakazi kama hawaoni umuhimu wetu na posho sio ya uhakika mpaka viongozi waanze kupiga majungu na kuchagua watu wa kuwapa…

KINACHOTOKEA SASA watu majembe wote wanaondoka, asilimia 90 ya wafanyakazi wa GPSA hawana moyo wa kufanya kazi kwenye ofisi hiyo wapo wakisubiri wapate nafasi waondoke sehemu zingine
.
serikali ingetakiwa ipangue management ya GPSA YOTE, wengine wangetakiwa wawe magerezani kabisa kama DBSS..

Wanaidhinisha makato ya mshahara ya watumishi bila idhini yetu, eti mfuko wa faraja GPSA. Yaani unashangaa mshahara unatoka unakutana na makato usiyoyaelewa, sawa ni jambo jema.. why wasingekata hata kwenye nauli..mishahara yenyewe ni midogo na ndio tunategemea kuikopea, wanaongeza makato kitu ambacho kinatupunguzia kiwango cha mkopo bank wakati walikuwa na option ya kukata hiyo pesa ya mfuko kwenye posho zingine.

Hii tasisi watu hawaipendi kiasi kwamba ni vigumu kukuta watu wamevaa fulana ya GPSA maofisini, zaidi tukipewa huwa tunawapa wafanyakazi wetu wa ndani wavae au wpigie deki, ama tunawapa mama ntilie

GPSA. Mkurugenzi wa miaka ile enzi ya Mkapa alikuwa baba yangu Mkubwa. Bwana Lenard Mwavala. GPSA ya wakati ule ilikuwa na hadhi sana.

Maelezo Yako ni mazuri Sana Ila unapotoa claims next time kama hizi unatakiwa uainishe shida ipo wapi badala ya kuandika mfumo wa chuki na majungu. Serikali mara nyingi inafanyia kazi matatizo na Sio chuki.

Aidha, binafsi naunga mkono GPSA kutumbuliwa. Kwanza kwa Sasa hivi taasisi zote zinazofanya manunuzi zenyewe kama MSD, mizigo yake inatakiwa kuwa cleared na GPSA. Balaa linaanzia hapo; mzigo unaweza kukaa hapo bandarini mwezi mzima ukifuatilia malipo pale MSD unaambiwa MZIGO haujafika.

Wakati mzigo upo bandarini miezi 2.

Ukienda GPSA unaambiwa bado tunashughulikia, matokeo yake mizigo unatoka ukiwa unakaribia ku expire. Najiuliza taasisi za umma zinashida gani ?

Suala la kuhonga wakaguzi ni suala la taasisi za umma nyingi sana wanafanya hivyo. Lakini kiujumla GPSA inahitaji reform for sure.

Taasisi ambazo serikali izitolee macho na zenye ufisadi wa Hali ya juu uliojificha na wanaotumia pesa nyingi kuhonga wakaguzi ;
GPSA, MSD, TTCL, TANROADS, HESLB, Utumishi ( wale wanaopeleka watu Duce kwa interview), Ofisi ya Mkuu wa Mkoa -Dar, you name them.

Serikali tunatoa hizi taarifa fanyieni kazi ni Taarifa muhimu sana inawezekana watu wa system nao waliokwenye taasisi hizo wana maslahi yao hivyo hawatoi taarifa sahihi.

Ndio maana Mpaka Kesho kuna wafanyakazi hewa kwenye taasisi hizo na upigaji.
 
Duh...!.
Maadam nia yako ni habari hizi zifike kule kunako, tayari zimefika wala aliyezifikisha sio mimi bali zimemfikia mhusika kwa yeye mwenyewe in person kuzisoma

Hili la Kusikia kuwa mimi ni TISS, naomba usiendelee kusikia tuu kwa wengine, mimi ni li TISS lenyewe haswa born and breed TISS na humu jf nimejitaja wazi kabisa bila kuficha kitu

Hivi uongo kwamba TISS hawastaafu kwanini unaaminiwa? - JamiiForums
P

Na tunaambiwa kuwa barua ya waziri Mkuu kuhusu Bodi ya Mikopo imeshamfikia Rasmi waziri Mkuu. Hongereni TISS
 
Pia andika barua ya siri kwenda Ikulu na PM.
Eleza kila kitu. Halafu hapo GPSA mbona kuna Informer wengi sana ( wanakazi gani?)
That's why unaona mambo kama haya yanaanza ili likianza sekeseke chanzo kinakuwa ni hapa jf, na ndio maana nasema huyu hana ubavu wa kunijua Mimi ni mchokoza mada tu ili watu wafanye yao
 
That's why unaona mambo kama haya yanaanza ili likianza sekeseke chanzo kinakuwa ni hapa jf, na ndio maana nasema huyu hana ubavu wa kunijua Mimi ni mchokoza mada tu ili watu wafanye yao

Jana alifanikiwa kuhonga baadhi ya vijana wa jf wakafuta uzi, ilibidi tumuendee hewani Mello umerudishwa ukiwa unamis baadhi ya vitu

Hana uwezo kama huo;na kwanza Taarifa iliyotolewa ni ya kuisaidia serikali sio ya kukinzana na Serikali l.

Na ninakubaliana na we GPSA inahitaji Mkurugenzi mwenye akili timamu. Ukitaka kujua GPSA ni jipu waulize MSD ambao kwa Sasa wamelazimishwa mizigo yao iwe cleared na GPSA na hiyo kauli imetoka kwa Doto baada ya MSD Kuonekana inatumia gharama nyingi kwenye kufanya Clearing.

Sasa unaambiwa mizigo inakaa miezi 3 inaozea hapo bandarini .

Yaani magufuli amchukue mtu akili kubwa ndio amuweke GPSA.

Ukweli GPSA kuna hela yaani ni sehemu yenye rushwa na upigaji kirahisi sana.

Pamoja na yote and I swear to my ass , sijajua kazi ya Informer kwenye taasisi za Umma. These people are goodl for nothing yaani haya mambo yanatokea Tangu muda mrefu sana lakini
Still hawa Jamaa hawapeleki taarifa kitengo. Au ndio mambo yale ya JK, anapewa Taarifa halafu yeye anachagua ipi ya kufanyia kazi.

Usalama wengi ni honesty na wanakula viapo, na magufuli kawajaza kwenye taasisi zote : Sasa I am still wondering what is wrong mpaka taarifa kama hizi zinakuja kutolewa JF huku usalama wapo na ni sehemu ya kazi yao.
 
Government Procurement Service Agency (GPSA) tatizo ni management kama yule DBSS hafai kabisa kuwa ofisini ni fisadi halafu mbinafsi na mbaya Zaidi anawahonga wakaguzi wanapokuja kumkagua na mambo yanaisha, na ili kulinda ugali wake anawala (anawagegeda) wafanyakazi wa kike walio wepesi kutongozeka ili wawe wanampelekea umbeya ambapo wengi wao anazawadia kwa kuwapa kipaumbele cha visafari na semina pale inapotokea yaani kama una mke wako anafanya GPSA humu jamaa hajali yeye anachovya tu,..na wa kiume nao anaselect wa kuwa wanampelekea umbeya kuhusu wafanyakazi wengine..

Ukiwa hujipendekezi GPSA maisha yako yanakuwa magumu, na CEO naye amemezwa na DBSS na mpenda sifa na maJungu Zaidi ya ufanisi wa kazi anatumia pesa nyingi kuhamisha watumishi kwa sababu ya umbeya tu anaopelekewa, kiufupi hana weledi wa kuongoza taasisi, na hawezi kuifikisha mbali na mara mia angepewa Liliani aliyekuwa ana - kaimu.

GPSA inatakiwa iwe juu ya MSD kimapato na kimaslahi kwa watumishi wake,tuna vyanzo vingi vya mapato lakini viongozi wanawaza ufisadi tu, sasa eti wafanyakazi wa mikoani tunalipwa posho kidogo kulinganisha na makao makuu kisa tuko mikoani tunatakiwa kulipwa tofauti na wa makao makuu, sasa kama hatuna umuhimu kisa tuko mikoani si bora tuhamishiwe wote makao makuu na mikoani kusiwe na wafanyakazi kama hawaoni umuhimu wetu na posho sio ya uhakika mpaka viongozi waanze kupiga majungu na kuchagua watu wa kuwapa…

KINACHOTOKEA SASA watu majembe wote wanaondoka, asilimia 90 ya wafanyakazi wa GPSA hawana moyo wa kufanya kazi kwenye ofisi hiyo wapo wakisubiri wapate nafasi waondoke sehemu zingine
.
serikali ingetakiwa ipangue management ya GPSA YOTE, wengine wangetakiwa wawe magerezani kabisa kama DBSS..

Wanaidhinisha makato ya mshahara ya watumishi bila idhini yetu, eti mfuko wa faraja GPSA. Yaani unashangaa mshahara unatoka unakutana na makato usiyoyaelewa, sawa ni jambo jema.. why wasingekata hata kwenye nauli..mishahara yenyewe ni midogo na ndio tunategemea kuikopea, wanaongeza makato kitu ambacho kinatupunguzia kiwango cha mkopo bank wakati walikuwa na option ya kukata hiyo pesa ya mfuko kwenye posho zingine.

Hii tasisi watu hawaipendi kiasi kwamba ni vigumu kukuta watu wamevaa fulana ya GPSA maofisini, zaidi tukipewa huwa tunawapa wafanyakazi wetu wa ndani wavae au wpigie deki, ama tunawapa mama ntilie
KAMA.UNAANDIKA BADO UKO OFISINI AINA MAANA HAMA KWANZA NDIO UWASHE MOTO
KAMA BADO WANAKUPAUGALI UNAPATA CHOOKIKUBWA NO
 
Sio kweli Mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli ni upi? Mbona taarifa za RUSHWA zinaletwa kwenu, then mnamjuliisha mhusika anawapa hela halafu mnafunika.

Hasa RUSHWA zinazohusu vigogo wenye fedha, ila za watu wadogo ndiyo mnakimbia nazo.

Hakuna TAASISI ambayo haina tija kwa Taifa kama TAKUKURU, imebakia ku kufuatilia wale wanaokuwa targeted na RAIS tu.
 
Majungu hayo. Kama una ushaidi toa taarifa kwenye vyombo husika.
Niko barabarani lakini baada ya kuona hii comment yako imebidi nipaki gari pembeni nikujibu japo kidogo kwa sababu tangu juzi nilipotoa comment yangu ya namna gani viongozi wa GPSA hawana Weledi zaidi ya kuwepo kimaslahi sikutokea tena hapa kwa sababu za kimajukumu.

Kinachoongolewa hapa Wala sio majungu ni uhalisia uliopo kwa viongozi wa GPSA, Kama ulikuwa hujui sio wote walioko GPSA ni wafanyakazi wa kawaida wengine wanaona ambayo wewe huwezi kuyaona japokuwa sipo kwa Sasa GPSA kikazi lakini naweza kuwa na uelewa wa taasisi kuliko hata wewe nikugusie kidogo tu kuhusu madili yanayopigwa na DBSS na CEO wa sasa halafu baadae nikiwa nimetulia nitarudi kuongezea.

1) Kuna mwaka (nimeusahau kidogo, nikifika nyumbani nitaungalia kwenye file zangu then nitaedit) DBSS alikuwa anaenda likizo, akajiandikia malipo ya likizo Kama 8m kama sikosei(nitaenda kuangalia upya pia) Kinyume kabisa na utaratibu wa malipo ya likizo file lilipofika pale utawala kipindi hicho ofisi ilikuwa na ma-HR (Ally, Mamboleo na Leah..sijui Kama Kuna mtu nimemsahau) na meneja utawala alikuwa anakaimu Leah Jericko (now yuko ofisi za stamico Kama sikosei, nitaangalia documents zangu vizuri baadae) huyu Leah alishtukia yale malipo hakusaini, zilipita Kama siku nne wakawa safari kikazi yeye na Ally na Ofice ya utawala akakaimu Mamboleo, DBSS akaona huu ndio mwanya wa kupitisha malipo yake akapitisha na Mamboleo hakuwa na nguvu za kuzuia, haya malipo yalishawahi kuhojiwa na wakaguzi ila Kama alivyosema CuteJancs anatoa pesa na mambo yanaisha.

2Kwa taarifa za uhakika tena nilizopewa, Mwaka Jana alienda Likizo akajiandikia malipo ya 3m, yakafika kwa CEO japo CEO ni mtu wake akashtuka ikabidi aombe ushauri kwa mwanasheria, na mwisho haya malipo hayakuweza kufanyika( nitaenda kuangalia documents zangu nikifika nitaongezea kitu).

3) Kuna manunuzi ya Upigaji ya CCTV camera, hizi CCTV kwenye document za GPSA inaonesha CCTV zimenunuliwa na kuwekwa kwenye vituo vya mafuta vya kurasini-Dar na Dodoma( hapa dodoma kulikuwa na CCTV za zamanj ziliharika na kushindwa kufanya kazi), na zingine inasemekana zimewekwa baadhi ya sehemu za makao makuu,... Hebu nenda kaangalie thamani ya manunuzi ya hizi CCTV na habari mbaya zaidi dodoma hakuna CCTV mpya iliyopelekwa Kama inavyodaiwa kwenye document zao.

4) Ma-supplier wote wanaofanya kazi na GPSA za kusupply vifaa huwa wanatoa hongo kwa wakubwa, Hii huwafanya wapendelee watu wa kuwapa tenda huku wakijifanya kufuata utaratibu (Hapa Kuna ushahidi wa sauti za simu kati ya viongozi hawa na massupplier ambao nisingependa kuwataja majina kwa Sasa) baada ya kupewa tenda na kusambaza mzigo hawa viongozi (CEO, DBSS na DPAS) huwatuma watu ambao nisingependa kuwataja majina ili wakawachukulie pesa kwa hawa masupplier,..Hawa watu wanaotumwa wapo pale GPSA na Wala sio wafanyakazi wapo na hawana kazi maalum na wanajulikana na system kinachonishangaza ni kwa nini wanachelewa kuwachukulia hatua (Hapa upo ushahidi wa sauti za simu)

5) Kuna madili DBSS huwa anawatumia madereva zake japo wao wenyewe huwa hawajui kinachoendelea, wanapewa bahasha na wanaagizwa wa kumpelekea au wanaagizwa wafuate bahasha sehemu kipindi DBSS na hao wahusika wanakuwa wameshamalizana kwenye simu na kiasi wanachotakiwa wapeane ( ushahidi upo na hao watu wanajulikana mpaka majina na namba zao)

6) GPSA ilitumia pesa nyingi kimagumashi kununua mfumo wa mafuta(FMIS) ambao kwa Sasa hautumiki, unajua kwa nini haufanyi kazi mpaka Sasa japo ulinunuliwa kwa mda mrefu? Unafahamu ulinunuliwaje na kwa kiasi gani?Unajua ni nani anaeupinga usifanye kazi na kwa maslahi gani, wakati ndiye huyo aliyeutetea ununuliwe? Unajua walifaidikaje katika manunuzi ya huu mfumo? ukijua haya huwezi kusema huu ni umbeya.

Meneja wa ICT ( nimemsahau jina, nitaangalia kwenye document zangu nikifika then nitaedit) yuko pale Kama shati tu viongozi wanamzunguka wanapiga pesa kwenye manunuzi yote ya vifaa vya kielectronic, na kwa taarifa za uhakika Kuna mifumo mingi haifanyi kazi na Wala haijawahi kufanyiwa ukaguzi.

7) Kuna scandal niliambiwa na nikafatilia nikakuta ni ukweli ilikuwa inahusu ununuzi wa gari aina ya Scania ya kubebea watalii Mali ya maliasili na utalii ( Mwaka nimeusahau nitaenda kuangalia ila ni hivi karibuni) yenye gharama ya zaidi ya Tsh 500m+ pesa za kitanzania ambazo waliingiziwa na maliasili wawanunulie gari mpya, kilichotokea ikanunuliwa gari kukuu kutoka Scania ambayo baadae Maliasili waliikataa (hii kesi anaijua katibu mkuu wizara ya fedha na katibu mkuu wizara ya Maliasili na utalii), Watu waliokuwepo PMU ( nimewasahau majina nitaenda kuwaangali) walijitahidi kusolve hili na mwisho wa siku walifanikiwa na baada ya kufanikiwa kuficha hi scandal, viongozi walijilipa pesa kwa ajili ya kujipongeza kujinasua kwenye huu mtego( sijui Kama umeelewa hii scenario)

8) Unajua hawa viongozi wa GPSA walipanga kutumia billions of money kununua flowmeter Kinyume na utaratibu na isiyo na maslahi kwa taasisi zaidi ya maslahi yao binafsi?

9) Huyu DBSS alikuwa na kampuni yake ya forwarding and Clearing iliyokuwa inafanya kazi sawa na ambazo taasisi yake inafanya, hapa pia mhasibu wa ugomboaji(Allen) nae alikuwa na kampuni ya namna hii kilichokuwa kinafanyika walikuwa wana-divert kazi zilizokuwa zipitie GPSA zikawa zinapitia kwenye kampuni zao Kinyume kabisa na sheria za utumishi wa umma matokeo Kitengo Cha ugomboaji kikachoka sana kimekuja kufufuka baada ya maagizo ya rais magufuli.

Niishie hapa nitarudi...ngoja niendelee na safari
 
Tuna safari ndefu sana kama Taifa. Wizi umetamalaki na vyombo vyetu vya kudetect haya mambo vimepalalaizi.

Ukipitia maelezo ya hao watoa taarifa unaona kabisa kunamapungufu katika vyombo vya utambuzi wa haya mambo,mainfoma wako wap?Takukuru je? Na si kwa taasisi hii tu ya umma hivi nani asiejua traffic wanakula rushwa?tena hadharani ila vyombo vinavyotakiwa kuwawajibisha vimepigwa ganzi sijui kwa manufaa ya nani?

Sasa wizi huu pengine Rais ndio aingilie kati daah namuonea huruma sana rais wangu...!!!?.Wasaidizi wake msaidieni kama ni ngumu tupeni hiyo kazi tuwasaidie tupo wazalendo tunaoumizwa na huo wizi.
 
Hapa tunasaidia vyombo vya usalama na serikali hasasa raisi magufuli ambaye dhamira yake ni kuipatia nchi maendeleo Kama taasisi hizi za umma zitawapata watu wazalendo, wenye akili na weledi, na wasio na maslahi binafsi...
TAKUKURU, TISS na vyombo vingine vya sheria mkienda GPSA anzeni na wakaguzi wa nje waliokuwepo wanakagua hi taasisi, chunguzeni hadi mawasiliano yao sisi tunawapa mwanga tu nini kimetokea ili nyie mkamilishe, Kuna wakaguzi pale huwa wanapewa hadi tiketi za ndege na pesa taslimu Kama hongo ili kuficha ufisadi wa pale, Hawa kuleni nao sahani moja hawafai katika utawala huu wa magufuli.

Mtafuteni CEO aliyestaafu.. mwambega huyu hakufaa kuwa hata uraiani, angetakiwa awe amefilisiwa na awekwe korokoni...huyu yake ni mengi sana..mkigusa tu mnayapata huyu yeye aligeuza Mali zote za ofisi Kama zake TAKUKURU msaidieni raisi wetu kwenye haya muokoe hii taasisi maana habari za uzi mnazo na mnaendelea kuzisoma hapa.

Pale Finance alikuwepo Meneja anaitwa somebody Mwanahamisi nendeni mkafahamu nini kilimtoa pale mpaka wakamkaimisha wa sasa ambae Kama sikosei anaitwa Adella.. Huyu Dada sitaki kumuingiza kwenye upigaji kwa sababu sio fisadi, tatzo lake hana ujasiri wa kupinga ovu analoona linapita kwake Kama finance Manager anaekaimu,.. Naye yuko pale Kama koti kwenye pesa chafu zinapita kwake anaidhinisha akiwa anajua ni kosa akiwa hana uwezo wa kuhoji, japo kiukweli hafaidi kwenye mgao wa hizo fedha.

Nendeni mkachunguze malipo ya nyumba anayokaa CEO Masaki inayolipiwa na taasisi kwa dollar za kimarekani Kila mwezi, na muangalie pesa ya nyumba iliyopo kisheria anayotakiwa kulipiwa kwa mwezi Kama mtendaji mkuu wa taasisi kama ni sahihi,mtapata majibu

Uzalendo ni kuipenda nchi yako na kuzuia ufisadi, tumsaidie raisi wetu mpendwa magufuli katika hili.
Mimi nitafanya kwa nafasi yangu wewe je?


Karibuni, Malaika Beach hotel tupige maji huku tukipakua mafile ya ufisadi wa GPSA...na kilichonitia moyo TISS, TAKUKURU na serikali washapata hii habari, nendeni mkamalizie tu pale sisi tutaendelea kuwambia hapa.



Weekend njema, ngoja nilewe tukutane usiku sana hapa kwa mara nyingine
 
Back
Top Bottom