Graduates sikilizeni kutoka kwa malegend wa kitaa...

Hahahahahah watu wanakwepa vi guruneti
 
Kujikomba ndio njia pekee na nyepesi ambayo unaweza kuitumia kuchomoka kimaisha kwa hali ya sasa ilivyo!

Jipendekeze kwa watu wenye connection kubwa hutakosa pa kupachikwa hata ikiwa sio leo wala kesho ila in a long run utatoboa!
 
Acha Mkuu hii hali niliipitia kabisa

Na nilibakia kichwa Tu

Ashukuriwe Mungu hata Kwa hii stage niliyobarikiwa but I dream higher!
Hongera mkuu! Heshima na utu huwa unapotea kabisa kipindi ukiwa dead broke hata nzi wanaweza kuja kubanduana juu ya utosi wako na hamna kitu utafanya😂

Mkiona wazee wanagombania nafasi za kubaki ofisini na kufoji miaka ndio muelewe! Its not easy being broke
 
Me baada ya kugraduate nilipata kazi kwenye NGO flani, miezi miwili badae kazi ikaisha. Nikasugua bench hadi akiba ikaisha. Nikawa beach boy, daily bahari beach kuogelea. Nikapata marafiki wavuvi, nikajifunza uongo maana hakuna watu waongo kama wavuvi.

Anakudanganya wazi eti aliwahi kuona jini limesimama juu ya maji

Nilichakaa vibaya sana. Nikabaki na pens moja, suruali moja na tshirt mbili. Nguo nyingine ziliisha.
 
Usiombee huo mtaji uwe uliupata kwa kujibana bana kwny boom. Inauma knoma[emoji848]
 
Kujikomba ndio njia pekee na nyepesi ambayo unaweza kuitumia kuchomoka kimaisha kwa hali ya sasa ilivyo!

Jipendekeze kwa watu wenye connection kubwa hutakosa pa kupachikwa hata ikiwa sio leo wala kesho ila in a long run utatoboa!
Tatzo sio kila mtu anaweza kujikomba. Sie wengne hata ile kumsalimia salimia mtu kila mda tunaonaga n vgumu.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Baada ya wiki lile bando linaisha,
unaamua ku hide last seen ya whatsapp,
Nywele ulizokuwa ukizitunza kwa garama unanyoa.
Unafikiria kazi ya kufanya unagundua hauna mtaji na uzoefu, unachoka
Unauza simu, unafuga kuku na wanakufa wote[emoji23][emoji23]
Unakosa dira, unaamua kuwa rough.
Unabadilika rangi ya ngozi na unakufa[emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…