Green Card kumbe ni kweli aisee tucheze hii kitu

Green Card kumbe ni kweli aisee tucheze hii kitu

Huwa inaanza October



Kwa kifupi kabisa, Green Card Lottery, formally DV Lottery ni bahati nasibu inayoendeshwa na serikali ya Marekani ambapo kila mwaka, inachagua applicants 50K randomly kutoka sehemu mbalimbali duniani, na hawa applicants hupewa Green Card. Ukipata Green Card unakuwa ni kama Mmarekani tu, kwa sababu unakuwa na haki karibu zote wanazopata raia wa Marekani. Linapokuja suala la ajira, unakuwa na haki ya kufanya kazi hadi serikalini EXCEPT, kwenye nafasi nyeti hususani za usalama!

Hulipii hata sent 5, lakini ukishinda, ni wajibu wako kulipia makaratasi ya hapa na pale lakini sio ghali sana! Aidha suala la utafikaje US, na utaenda kuishi wapi na vipi ni wajibu wako mwenyewe! Mwaka jana waliingiza utaratibu mpya kwamba kama unataka kuomba basi ni lazima uwe na passport. Kama tayari una passport, basi subiri October 07, kisha ingia hapa kwa ajili ya kujiandikisha! Condition nyingine (kama haitabadilik) unatakiwa kuwa na angalau diploma!
Hapo kwenye angalau diplona sasa...mmh
 
Upo sahihi; niliposema "nafasi" sikumaanisha "kada fulani" bali "specific sections"! Kwa mfano, unaweza kuingia hata jeshini lakini unaweza kuwa restricted kwenye baadhi ya nafasi ambazo ni very sensitive! Unajua mtu hata kama upo nchi kwako kabisa, kuna baadhi ya nafasi ni lazima wakuchunguze sana!!
Yes mfano hata huko jeshini kwenyewe ukiingia hauwezi kuwa commissioned officer hadi uwe raia ukiingia na green card mara nyingi unaishia kuwa enlisted soldier tu
 
Unajilipia mwenyewe...

Kawaida green card wanashinda watu wenye kada zao za kazi, elimu, kipaji, n.k na sio hohehae tu, sababu ukifanikiwa kupita hatua zote unatarajiwa kuomba kazi huko kwao na kupata haki zote za kuishi kama raia...
Mkuu hapa mimi mgeni kabisa kwa hivyo inachezwa kama bahat nasibu au ni kitu gani naomba kujuzwa samahani

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Unategemea ukae chini uweke bango lako "I'm hungry and homeless" usaidiwe?... America ina kazi nyingi sana za kufanya zenye hela hao ma homless wameamua kuwa hivyo na wengi ni watumia madawa ya kulevya... America isn't for Lazy people... Homeless wapo kila mahali hata Dar es salaam wapo pia...Maisha ni magumu kila mahali.
 
Sikuwa naamini Kuhusu Green card ila sasa nimeamini kweli kuna jamaa yangu mwalimu kapata yupo nyarugusu uko anaondoka Na familia yake Mungu kweli humpa anayemtaka
The Sense of where you Belong itamuandama milele!! Kwenda kuishi nchi ya ugenini hakuna tofauti na utumwa!! Ajitafutie maisha nchini kwake!? Huko ni Mateso TU anatafuta
 
Unategemea ukae chini uweke bango lako "I'm hungry and homeless" usaidiwe?... America ina kazi nyingi sana za kufanya zenye hela hao ma homless wameamua kuwa hivyo na wengi ni watumia madawa ya kulevya... America isn't for Lazy people... Homeless wapo kila mahali hata Dar es salaam wapo pia...Maisha ni magumu kila mahali.
Kariakoo ukipita muda Kuna walalahoi kibao wamelala kwenye sakafu za vibaraza vya maduka wametandika mabox
 
Fursa imejileta yenyewe nyumbani njoo tukujazie kwa 5,000 TSH tu.
NB: Tutakupiga Passport-Size Photo (yenye background nyeupe) na kuiweka kwenye vipimo stahiki
 
Faida za Green Card ni nini? Kuna jamaa nakumbuka long time sana alipata Green Card akaingia huko maandishi matatu ,cha kushangaza zaidi ya miaka 15 hajarudi bongo.
 
Kama kuna mtu anahitaji msaada kumsaidia kumjazia anishtue,pia mwenye maswali mbalimbali kuhusu Marekani
 
Back
Top Bottom