Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Hakuna mtu mwenye akili anaependa kuwa mkimbizi (refugee), labda kidoogo mwanamke ambae anaweza kuolewa na kuishi kokote. Lakini mwanaume (hazina ya ukoo) kuwa mkimbizi ni msiba mzito sana na laana kwa ukoo husika na hata taifa. Hata Nabii Yusuf alirudi kwao pamoja kuwa aliuzwa utumwani. Nawashangaa hawa watu wetu weusi waliokuwa wameuzwa utumwani kukataa kurudi kwao hata baada ya kufahamu asili yao ilikuwa wapi, shame upon them.
Huu ni ukweli tupu, huwezi kuwa na uhuru wa kifikra kama unaishi ugenini........kama ulivyosema kwa wanawake inaweza isiwe tatizo, lakini mwanaume halisi kitu anachojitahidi sana kulinda katika maisha yake ni identity na uhuru wa kifikra.
 
Kwa sababu nyumba yako ina kunguni, basi suluhisho ni kuhamia kwa jirani......jirani akikuwekea masharti ya kukudhalilisha utamlalamikia nani? wakipita na maandamano yao yale ya mashoga basi na wewe kama zuzu unaenda kuungana nao usije kuonekana unaenda kinyume na mila zao wakakufungasha virago, ukimwambia mtu huo ni utumwa anafikiri unamwonea wivu.​
kavulata said:
mimi nina akili nyingi balaa, passport yangu imejaa safari za kuja na kutoka Marekani, lakini sio kukaa na kulipa kodi huko kama zuzu, I proud of my homeland.

Akili nyingi balaa ni Passport kujaa! Nawajua watu kama nyinyi wamejana Wizarani na safari nyingi nje ya Nchi bila tija yoyote! Na kinachosikitisha zaidi hakuna chochote wanachojifunza! Katika watu waharibifu wa pesa za Umma ni kama ninyi!
Ina kera zaidi pale umeona dunia unakuja na mwazo duni kama haya! Shule umekwenda! Ila umekuwa Zuzu! Elimu za Africa hizo ziko kwenye display! Unawakilisha wasomi wengi! Sindano! Viberiti, karatasi za chooni! bado tunaagiza toka nje! Na bado tunawaita watujengee vyoo vya kunya watoto wetu! Hivi kweli kuna mategemeo watu kama ninyi wakichukua nchi!

Kweli unazidii kujiumbua. sasa wewe na Mwanakijiji aliyeko Litembo una tofauti gani!Au na mtu aliyekomea standard 7 tofauti kubwa na wewe ni ipi hasa?

Miaka 60! HAKUNA UMEME, HAKUNA MAJI na kuna jitu linajisifu Passport kujaa! Wazungu wanatucheka sana! Sasa kama kila siku unadhurura Duniani nini hasa umejifunza? Ndio kuleta uzi huu? Mbona unajiumbua mkuu!

Unasema hutaki kukaa Marekani kulipa kodi! Huna haja kabisa! Maana kuna kodi za wanyonge ambao umeshirikiana na Chama tawala kuwagawiya fulana za njano/Kijani na khanga, kuiba uchaguzi, hata dhamira na haya hunazo!

Akili balaa ni kujaza Passport! Sio kutatua tatizo la ajira au nishati! Na vijana tunaowajaribu kuwapa uthubutu wa kujaribu nje unawatisha! Najua unajua wazi wakitoka watafunguka macho! Ndio maana mna hofu na uraia wa nchi mbili!
Sijui hata kama una imani ya dini! Maana dhamira ingekuhangaisha! Akili imekufa kiasi cha kwamba akili inapimwa kwa kujaza karatasi za Passport! Na kwako mgao wa maji na umeme ni kitu cha kawaida! Hufikirii hata utambuzi! Unangoja Warsha na semina za kimataifa!

Huwa nawaona watu kama ninyi Airport! mmevaa Kaunda suti, au Suti za safari, na briefcases mikononi! Utafikiri mnakuja kufanya ya maana kumbe shopping!

Siwezi kuwa najibisha na mweye akili anayoipima kwa kujaza Passport!
 
Mimi nishapambana sana bongo lakini mpaka leo bilabila sasahivi ndoto zangu kubwa nikutoka hapa shimoni ,kila nikiangalia mbele naona giza sioni kama kutakuwa na unafuu wowote sana sana naona machafuko mbeleni baada ya watu kuchoka kubuluzwa na CCM.
 
Mimi nishapambana sana bongo lakini mpaka leo bilabila sasahivi ndoto zangu kubwa nikutoka hapa shimoni ,kila nikiangalia mbele naona giza sioni kama kutakuwa na unafuu wowote sana sana naona machafuko mbeleni baada ya watu kuchoka kubuluzwa na CCM.
Mkuu pole, unajaribu kutoa mawazo anakuja jamaa anasema ana akili kibao! LAKINI haonyeshi hata njia ya kutatua tatizo kama hilo! Amebakia kusema Manamba, manamba! kumbe ni zuzu anayezura duniani kwa pesa za wananchi! Na anajisifu kwa kujaza Passport! Ndio uwezo wake wa akili umekomea hapo!
 
Itoshe kusema ty wewe jamaa uloanzisha huu uzi ni PIMBi
Dumbi aliyeanzisha uzi huu anasema ana akili balaa! Kisa kajaza karatasi za Passport! Ndio kipimo cha akili yake! Dumbi Tanzania tulilogwa! Sijui na nani! Huyu ndio msomi nguli! Anayezunguka Duniani
 
Hakuna mtu mwenye akili anaependa kuwa mkimbizi (refugee), labda kidoogo mwanamke ambae anaweza kuolewa na kuishi kokote. Lakini mwanaume (hazina ya ukoo) kuwa mkimbizi ni msiba mzito sana na laana kwa ukoo husika na hata taifa. Hata Nabii Yusuf alirudi kwao pamoja kuwa aliuzwa utumwani. Nawashangaa hawa watu wetu weusi waliokuwa wameuzwa utumwani kukataa kurudi kwao hata baada ya kufahamu asili yao ilikuwa wapi, shame upon them.

kavulata said:
mimi nina akili nyingi balaa, passport yangu imejaa safari za kuja na kutoka Marekani, lakini sio kukaa na kulipa kodi huko kama zuzu, I proud of my homeland.

Mwenye akili balaa ni wewe uliyejaza Passport! Umetembea nje imeshindwa hata kubadili tone la akili yako! Ni ile ile ya Standard Seven!

Elimu inapimwa kwa kubuni kuondoa matatizo, wewe kipimo chako ni kujaza Passport! Mmejazana watu kama ninyi mawizarani! tunawaona ndani ya ma V8! Na Kaunda suti! kwa nje mnapendeza kumbe ndani ni kama makaburi mmejaa mifupa mitupu!

Kama kurudi nyumbani na kukutana na watu kama wewe, itakuwa ni kurudi Jehanamu! kwa kifupi haimpeleki popote nchi, ni walaji wakubwa kwa kutumia migongo ya wananchi! Lugha za siasa za Nyerere mlikuwa mnaitwa kupe!

Na kinachoumiza zaidi ni kuwakatisha tamaa Watanzania wenye nia ya kuthubu! Hofu ni kwamba tunakupunguzia watu wa kuwapanda migongoni!

Umekaa ukafikiri ukaleta mada hii, nilikuwa najiuliza sasa msukumo wako wa kuleta hii mada nini! Unaogopa hasa hiki kipindi cha Greencard itakupunguzia unawanyonya!
 
Daah! umenena, nini nafahamu kuwa furahi ya mtu haitokani na kuwa na pesa nyingi tu bali mjumuiko wa mambo mengi na hela ikiwemo. Nimekutana na kijana ambae huko majuu ambae analala kwenye gari yake maisha, nilipomuuliza kwanini kwanini huna chumba chako aliniambia ninafanya kazi shift 3 kwa siku hivyo muda wa kulala sina, hata hiyo nyumba naona nitapoteza pesa zangu bure wakati silali humo. Akanambia ana madeni mengi yanayohitaji ku service (kulipa) hivyo lazima afanye kazi zaidi ya 1 ili apate ziada. kaka kijana huyu hajawahi kula chakula cha nyumbani kwake zaidi ya kule fast foods mitaani, makato mengi na anashindwa kutuma pesa nyumbani maana wafyeka hela nyingi sana. kaka kuna mitaa/maduka/malls ukiingia mwenye ngozi nyeusi wanadhani huna pesa ya kuingia hapo bali unataka kuiba, ubaguzi bado haujakwisha tunalazimisha tu.

Nguvu, muda, juhudi, maarifa na akili mnazozitumia kumudu kuishi huko hata zingewekezwa japo nusu tu kwenye jangwa zingetoa matunda. Vijana wetu huku ni wavivu sana ni wavivu sana na ni wavivu sana ndio maana wanapata tamaa ya green card wakidhani huko US pesa ziko kwenye viroba tu ni za kuzoa na kutumia.

Kama asili na chanzo kikuu cha ushoga huko ni maisha magumu, watu wanaunganisha nguvu ili kumudu maisha bila kulazimika kuwa na watoto wa kutunza, yaani kuona mwanamke ni kuongeza ugumu kwenye ugumu. bahati mbaya mimi nimeishi huko sana tena vijijini kabisa ambako maisha ni kama haya hapa ya tandika na kwamtogole, kuchafu na idadi kubwa ya ombaomba wazungu mitaani ambao wanapatiwa nguo kule salvation army na kwingineko kwenye malls kama vile Walmart zenye madirisha ya watu maskini (wazungu) kupatiwa misaada.

kaka usiwadanganye watu ukawapa hope na kuja kuishia kuolewa na wanaume wenzao, wanaofanikiwa ni watu kidogo sana kati ya hao wahamianji. Wengi wao wanaishia kwenye vyombo vya usalama kufungwa na hata kuuliwa.
kavulata said:

mimi nina akili nyingi balaa, passport yangu imejaa safari za kuja na kutoka Marekani, lakini sio kukaa na kulipa kodi huko kama zuzu, I proud of my homeland.

Akili nyingi katika ubora wake! In full display!
 
Wakoloni walitusafirisha kwa majahazi kama watumwa kwenda kwao kuwafanyia kazi bure (manamba) kwenye mashamba, viwanda na majumbani kwao, history mbaya sana hii kukumbukwa, maana sio tu kwenda kuwafanyia kazi wazungu bure lakini wengi wao walikufa njiani wakati wakisafirishwa kwa kutoswa majini, msongamano mkubwa, njaa na ugonjwa njiani.

LEO hii miaka 60 baada ya uhuru sababu zilezile za kusafirisha manamba kwenda Marekani, Ulaya na uarabuni ndio sababu hizihizi za watu kwenda huko kwa Green card lottery, Jamani hali hii ni mpaka lini? what are you looking for? Kilichobadilika ni kitu kimoja kutoka manamba kwenda green card ni sifa tu watu wanaohitajika kusafirishwa, Wakati ule walihitaji watu wakubwa wenye nguvu za kufanya kazi za wakati ule na sasa hivi kwa kutumia green card wanahitaji watu wenye elimu na ujuzi maalum kwaajili ya kufanya kazi za wakati huu, zama hizi baasi.

Hii ni kujitafutia balaa wewe mwenyewe na familia yako kwa matumaini feki kabisa huku ukijua kuwa utakwenda kule kufanyakazi kubwa na nyingi sana ili upate chochote kitu wakati nguvu, juhudi na akili hizo ungeweza hata kuziwekeza hapahapa nchini kwako na kupata mafanikio makubwa sana ya ajabu pamoja na kutoa mchango kwenye ujenzi wa taifa lako kwa njia za kodi, tozo na huduma kwa jamii yako.

Jaamaani, Si shauri uombe hiyo kitu, nyambafu!!!!


kavulata said:
mimi nina akili nyingi balaa, passport yangu imejaa safari za kuja na kutoka Marekani, lakini sio kukaa na kulipa kodi huko kama zuzu, I proud of my homeland.

Akili nyingi ikiwa kwenye full display! Passport yake imejaa safari za Marekani! Msaidie mwenzetu!
 
Kavulata: Unajua unachokisema au umekaririshwa? Niko Marekani, sikuja kwa kufungwa mnyororo,na hata nikitaka kuondoka hakuna kamba iliyonifunga.
Ushauri kila siku kwa vijana wa kitanzania, kama unaona opportunities zimebana Tanzania jaribu popote, nina mifano mingi mno, na nimeona kwa watu toka mataifa mbali mbali niliokutana nao US!
Ukiwa na focus, na documents halali na yote unayoyasikia kuhusu Marekani, ni mahali unaweza kufikisha ndoto zako, sisemi ni rahisi, lakini kuna nyenzo ambazo hupati katika nchi nyingi za Kiafrica.
Sijahonga au kumuona yoyote watoto wangu kupata mikopo ya vyuo vyao, sikuwa na connection zozote zile watoto wangu kupata white color jobs! In short mtoto wangu alikuwa recruited akiwa bado chuoni, na leo akiwa na miaka24 is making almost $ 85,000/ Wenzake aliowaacha bongo waliomaliza chuo wanasaka ajira!
Sasa sijui ni utumwa wa aina gani huo!
Ni kweli Marekani/ Canada zinataka nguvu kazi, lakini ukiingia huku ni juhudi zako na akili yako! Wengine wataenda juu, na wengine chini, sawasawa na wazawa! Anayenifyekea majani nyumbani kwangu ni mzungu! Maana sina muda! Na kila baada ya wiki mbili au tatu ananipigia simu kama yameota aje kufyeka! Na ameniambia ni fundi katika serikali yetu ya mtaa anatafuta pesa ya ziada! Hii ndio Marekani, simdharau najua anachotafuta!
Hivyo usikaririshwe na akina Lumumba.
Hulazimishwi ni akili yako tu! Wengine wanatumia hapo bongo wanatoka! Wengine mambo yanakataa! Maisha popote pale!
Asee nimecheza Lottery ya mwaka huu.. Ikitiki ntakutafuta mkuu unipe ABCs..
 
Mleta Mada sema tuu hujui kizungu bana!! aaah! kule kutamu hakuna kutekana weweee! mara mutwe wafanyakazi hewa!! mara mbanwe na vibaka temeke mara mkose elimu nzuri!

viongozi wakubwa woote watoto wao wanasoma nje! hata rjiv gandhi, watoto wa Rais wa syria wamesomea huko wewe nani nyau kabisa usiende hukooooo! acha ujinga! umekuwa mkubwa sasa!
 
Kwani umelazimishwa? Hutaki acha! Sio lazima! Baki nyumbani kwenu huko tulia! Dunia haina mipaka ya kusema kwamba ni lazima uishi tu sehemu moja kama mti..kila mtu na mtazamo wake...wewe kama unaona Green card lottery ni ujinga ni kwako tu na mtazamo wako.. Usipangie watu maisha na makazi ya kuishi...Mungu alipotuumba alisema "Enendeni ulimwenguni kote mkaijaze Dunia" hakusema tubaki sehemu moja kama Mti, jiwe au jabali.
Hutaki green card Achaaaaaa!!!!! Hulazimishwi!!!! Kila mtu aishi anapo penda
Over!
Ahsante kwa kunifurahisha
 
Huu ni ukweli tupu, huwezi kuwa na uhuru wa kifikra kama unaishi ugenini........kama ulivyosema kwa wanawake inaweza isiwe tatizo, lakini mwanaume halisi kitu anachojitahidi sana kulinda katika maisha yake ni identity na uhuru wa kifikra.
Mwanaume halisi! Huna aibu! Mnaita watu kuwachimbia choo! Hakuna maji wala umeme,mwanaume halisi haoni kuna tatizo mahali! Nchi ina miaka 60! Kuna mito na maziwa! Kila mwaka mnakimbiza mwenge uzidi kudumaza akili! Bila kujua true identity iliisha potential siku nyingi!
Na cha kusikitisha kabisa wasomi kama wewe, ambao tungetegemea mawazo mapya, mtoe hybrid ya shule mlizokwenda, na experience ya kutoka nje ya nchi, nyie ndio mnakuja na ideas ambazo zinarudisha nyuma taifa zaidi ya 1960!
Angalia msomi mwenzio, anadai ana elimu balaa, kwa sababu kajaza page za passport!
Sasa International air hostesses watasemaje! Huo ndio uwezo wa IQ yake ulipofika!
Tunajaribu kutoa tu options za wale walioshindwa kufikisha ndoto zao Tanzania, mnawatisha bila kutoa alternative! Ni roho mbaya au uchawi!
Mara unajua uzalendo! Wazalendo kina Sokoine wako wapi! Kina Magufuli wako wapi! Hata uko China kina Mao wako wapi!, kina Lumumba Congo wako wapi!
Mwisho wa siku ni wewe na maisha yako, na mipango yako!
Usiku Mwema!
 
kavulata said:
mimi nina akili nyingi balaa, passport yangu imejaa safari za kuja na kutoka Marekani, lakini sio kukaa na kulipa kodi huko kama zuzu, I proud of my homeland.

Akili nyingi balaa ni Passport kujaa! Nawajua watu kama nyinyi wamejana Wizarani na safari nyingi nje ya Nchi bila tija yoyote! Na kinachosikitisha zaidi hakuna chochote wanachojifunza! Katika watu waharibifu wa pesa za Umma ni kama ninyi!
Ina kera zaidi pale umeona dunia unakuja na mwazo duni kama haya! Shule umekwenda! Ila umekuwa Zuzu! Elimu za Africa hizo ziko kwenye display! Unawakilisha wasomi wengi! Sindano! Viberiti, karatasi za chooni! bado tunaagiza toka nje! Na bado tunawaita watujengee vyoo vya kunya watoto wetu! Hivi kweli kuna mategemeo watu kama ninyi wakichukua nchi!

Kweli unazidii kujiumbua. sasa wewe na Mwanakijiji aliyeko Litembo una tofauti gani!Au na mtu aliyekomea standard 7 tofauti kubwa na wewe ni ipi hasa?

Miaka 60! HAKUNA UMEME, HAKUNA MAJI na kuna jitu linajisifu Passport kujaa! Wazungu wanatucheka sana! Sasa kama kila siku unadhurura Duniani nini hasa umejifunza? Ndio kuleta uzi huu? Mbona unajiumbua mkuu!

Unasema hutaki kukaa Marekani kulipa kodi! Huna haja kabisa! Maana kuna kodi za wanyonge ambao umeshirikiana na Chama tawala kuwagawiya fulana za njano/Kijani na khanga, kuiba uchaguzi, hata dhamira na haya hunazo!

Akili balaa ni kujaza Passport! Sio kutatua tatizo la ajira au nishati! Na vijana tunaowajaribu kuwapa uthubutu wa kujaribu nje unawatisha! Najua unajua wazi wakitoka watafunguka macho! Ndio maana mna hofu na uraia wa nchi mbili!
Sijui hata kama una imani ya dini! Maana dhamira ingekuhangaisha! Akili imekufa kiasi cha kwamba akili inapimwa kwa kujaza karatasi za Passport! Na kwako mgao wa maji na umeme ni kitu cha kawaida! Hufikirii hata utambuzi! Unangoja Warsha na semina za kimataifa!

Huwa nawaona watu kama ninyi Airport! mmevaa Kaunda suti, au Suti za safari, na briefcases mikononi! Utafikiri mnakuja kufanya ya maana kumbe shopping!

Siwezi kuwa najibisha na mweye akili anayoipima kwa kujaza Passport!
Tulitegemea vijana kama nyie mnaochukia mngejiopenyeza kwenye siasa ili mtatue shida za umeme, maji na ajira badala ya kuwa wakimbizi ughaibuni kufanywa manamba, Bro huwezi kutajirika kwa kuajiliwa kufanya kazi za mtu mwingine. Hakuna tajiri duniani ambae amesajiliwa na mtu mwingine.
 
Tulitegemea vijana kama nyie mnaochukia mngejiopenyeza kwenye siasa ili mtatue shida za umeme, maji na ajira badala ya kuwa wakimbizi ughaibuni kufanywa manamba, Bro huwezi kutajirika kwa kuajiliwa kufanya kazi za mtu mwingine. Hakuna tajiri duniani ambae amesajiliwa na mtu mwingine.
Akili fupi hiyo! Nani kakwambia natafuta utajiri! Kuna utajiri zaidi pesa! Kavulata, naona wewe ni mshamba mkubwa!
Safari za nje ambazo hujawahi hata kutoa senti mfukoni mwako unakuja kujianika mtandaoni!
Shame on you!
 
We mpumbavu wa kazula mimba ignorance na stupidity vinakusumbua ,watu mamilioni wanatoka India ,China ,South Korea ,Singapore ,Japan na kila nchi unauoijua wewe wanaingia kila siku USA unadhani ni wapumbavu sio ? ,Hizo nchi zina uchumi wa kuwalisha nchi nzima ya Tz for 100 of years ,
We hapo Tz unajiona dunia yote yako sio ?
Mkuu toka atoke kijijini kwao na kupata ajira serikalini kapofuka macho! Hakutegemea kabisa kufika hapo, na kajaa na roho mbaya na wivu!
Tunajaribu kutoa options kwa wale ambo wanaona bongo opportunities zimebuma anakuja na blah blah zake!
Anajiona super genius kwa kujaza Passport kwa ziara za kiserikali! Ushamba mkubwa!
 
Tulitegemea vijana kama nyie mnaochukia mngejiopenyeza kwenye siasa ili mtatue shida za umeme, maji na ajira badala ya kuwa wakimbizi ughaibuni kufanywa manamba, Bro huwezi kutajirika kwa kuajiliwa kufanya kazi za mtu mwingine. Hakuna tajiri duniani ambae amesajiliwa na mtu mwingine.
Maisha niliyokuwa Tanzania kabla sijaja US sidhani hata sasa umeyafikia! Na si kwa Per Diem za serikali!
Wigo wako wa maisha duni sana! Ni reflection ya background yako!
 
huyo jamaa anaesaidia kuwajazia hiyo green card mwenyewe muonekano hashawishi kama kuna life huko la kueleweka.
Ni porojo tu,kusubiria hela za viewers youtube.
Mtu serious huko US unapataje muda kuja hamasisha watu kuomba green card?
kuna asiyejua hiyo green card toka enzi na enzi ipo.
mwenyewe anakiri we mpaka ufike huko na kusettle na family andaa dola 10,000!
mtu ana dola 10000 kweli atawaza kuhama aende huko kuanza upya badala ya kujiendeleza hapo alipo.
Sijamwelewa huyu jamaa
 
Akili fupi hiyo! Nani kakwambia natafuta utajiri! Kuna utajiri zaidi pesa! Kavulata, naona wewe ni mshamba mkubwa!
Safari za nje ambazo hujawahi hata kutoa senti mfukoni mwako unakuja kujianika mtandaoni!
Shame on you!
Akili ndefu ni kuwa mkimbizi na kulikana taifa lako na uraia wako? shame. Ikitokea xenophobia unatetemeka na kutafuta pa kujificha. PATA SEMA lakini Mimi ni maskini jeuri, sijuti kuwa mtanzania Wala kuishi Tanzania.
 
huyo jamaa anaesaidia kuwajazia hiyo green card mwenyewe muonekano hashawishi kama kuna life huko la kueleweka.
Ni porojo tu,kusubiria hela za viewers youtube.
Mtu serious huko US unapataje muda kuja hamasisha watu kuomba green card?
kuna asiyejua hiyo green card toka enzi na enzi ipo.
mwenyewe anakiri we mpaka ufike huko na kusettle na family andaa dola 10,000!
mtu ana dola 10000 kweli atawaza kuhama aende huko kuanza upya badala ya kujiendeleza hapo alipo.
Sijamwelewa huyu jamaa
Hata tofauti na akina tiptip waliokuwa wanatafuta watumwa/manamba wa kusafisha wanakohitajika, tofauti Yao ni kwamba Tiptip alitumia nguvu ya bunduki lakini hawa wanaotumia nguvu ya kushawishi na kuhadaa vijana kuwa Kuna kazi kibao huko.
 
Back
Top Bottom