Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Huyo jamaa ni fala ,wala usijibizane naye
Zamani zile wafanyakazi kutoka Afrika kwenda kufanyakazi za wazungu walikuwa wanapatikana kwenye masoko ya Watumwa, hapa kwetu masoko ya watumwa yalikuwa pale Bagamoyo na Zanzibar. bahati mbaya watumwa kutoka masoko ya bagamoyo na Zanzibar hawakupelekwa wengi Marekani bali walipelekwa Ulaya na Uarabuni na hii ilitokana na kuwa masoko ya bagamoyo na Zanzibar hayakuwa na watumwa wenye maumbo makubwa na nguvu nyingi kuweza kumudu soko la marekani Kusini na kaskazini. Hivyo, watumwa wengi waliopelekwa masoko ya Amerika walitoka Afrika magharibi hasa nchi za Senegal, Ghana, Mali na Bukina Faso ambako yalipatika watu wenye mili mikubwa na nguvu nyingi (gar people) waliopelekwa huko Caribbean na Amerika kwenye mashamba na viwanda. Kumbuka kuwa Wakoloni shida yao kubwa ilikuwa kupata nguvukazi ya bei nafuu (manamba na watumwa), kupata malighafi na masoko ya bidhaa zao. Ukoloni na utumwa vinaonekana kuwa vimekwiaha lakini Shida hizi 3 za wafanyakazi wa bei nafuu, malighafi na masoko bado wanazo mpaka leo.

Baada ya ukoloni na utumwa kwisha na masoko/minada ya watumwa kufungwa ndio wakabuni njia nginine za kupata watumwa (wafanyakazi wa bei nafuu), malighafi na masoko ya bidhaa zao. Njia wanazotumia kupata wafanyakazi wa bei nafuu ni mbili kuu ambazo ni kuhamishia viwanda/shughuli zao kutoka marekani na Ulaya kwenda nchi maskini kwa jina la uwekezaji na kuajili wazawa kwa ujira mdogo sana, na pili kutoa vivutio(chambo) kama Greencards na scholarships za masomo ili kupata cheap labor kwa kazi ambazo ziko kwenye mataifa yao ambazo hazihamishiki. Hapa kwenye greencards ndipo panapowachanganya mazuzu wetu, wanasahau kuwa greencard ni mbadala wa soko la watumwa la bagamoyo na Zanzibar kwa jina lingine.

Siku moja nilitembelea pale Zanzibar kuona ofisi moja ambayo watu wanasajili vijana wa kike na kiume kwenda kufanyakazi Uarabuni, roho yangu iliniuma sana tena sana kuona watu wanafanyakazi zilezile kama za soko la watumwa. Wanatumia ujanjaujanja kuwapata watu kwenda uarabuni eti kuna kazi nyingi sana huko. Vijana wamejaa kwenye ofisi ile wakisubiri kusajiriwa wengine kwa vyeti vya utambulisho bandia.

Mpaka karne hii yuko mtu anashangilia kama zuzu kupata greencard ili akawe kijakazi na kutumikia taifa lingine. Yaani anaacha ardhi, mashamba na vyakula fresh kwenda ugenini akaishi kama mkimbizi maisha ya dhiki, hofu na wasiwasi kubwa. Yaani anapishana na wazungu kwenye ndege wakija kwao kukamata mapande makubwa ya ardhi yao na yeye kwenda kwao akawe kibarua wao akahudumie wazee, watoto na watu wao na kula vitu vikuukuu kama hot dog (fast foods) na kununua vitu vya kwenye clearance.

Hapa sio maswala ya wivu bali ni maswala ya ukombozi wa kifikra wa vijana wetu. Mimi nitakuwa mtu wa kwanza kumshangalia kijana wetu aliyekwenda kule na kurudi kwao na mtaji, elimu, uzoefu, ujuzi na exposure kuja kubadilisha mambo (uchumi, huduma, siasa na matazamo) kwao.
 
Zamani zile wafanyakazi kutoka Afrika kwenda kufanyakazi za wazungu walikuwa wanapatikana kwenye masoko ya Watumwa, hapa kwetu masoko ya watumwa yalikuwa pale Bagamoyo na Zanzibar. bahati mbaya watumwa kutoka masoko ya bagamoyo na Zanzibar hawakupelekwa wengi Marekani bali walipelekwa Ulaya na Uarabuni na hii ilitokana na kuwa masoko ya bagamoyo na Zanzibar hayakuwa na watumwa wenye maumbo makubwa na nguvu nyingi kuweza kumudu soko la marekani Kusini na kaskazini. Hivyo, watumwa wengi waliopelekwa masoko ya Amerika walitoka Afrika magharibi hasa nchi za Senegal, Ghana, Mali na Bukina Faso ambako yalipatika watu wenye mili mikubwa na nguvu nyingi (gar people) waliopelekwa huko Caribbean na Amerika kwenye mashamba na viwanda. Kumbuka kuwa Wakoloni shida yao kubwa ilikuwa kupata nguvukazi ya bei nafuu (manamba na watumwa), kupata malighafi na masoko ya bidhaa zao. Ukoloni na utumwa vinaonekana kuwa vimekwiaha lakini Shida hizi 3 za wafanyakazi wa bei nafuu, malighafi na masoko bado wanazo mpaka leo.

Baada ya ukoloni na utumwa kwisha na masoko/minada ya watumwa kufungwa ndio wakabuni njia nginine za kupata watumwa (wafanyakazi wa bei nafuu), malighafi na masoko ya bidhaa zao. Njia wanazotumia kupata wafanyakazi wa bei nafuu ni mbili kuu ambazo ni kuhamishia viwanda/shughuli zao kutoka marekani na Ulaya kwenda nchi maskini kwa jina la uwekezaji na kuajili wazawa kwa ujira mdogo sana, na pili kutoa vivutio(chambo) kama Greencards na scholarships za masomo ili kupata cheap labor kwa kazi ambazo ziko kwenye mataifa yao ambazo hazihamishiki. Hapa kwenye greencards ndipo panapowachanganya mazuzu wetu, wanasahau kuwa greencard ni mbadala wa soko la watumwa la bagamoyo na Zanzibar kwa jina lingine.

Siku moja nilitembelea pale Zanzibar kuona ofisi moja ambayo watu wanasajili vijana wa kike na kiume kwenda kufanyakazi Uarabuni, roho yangu iliniuma sana tena sana kuona watu wanafanyakazi zilezile kama za soko la watumwa. Wanatumia ujanjaujanja kuwapata watu kwenda uarabuni eti kuna kazi nyingi sana huko. Vijana wamejaa kwenye ofisi ile wakisubiri kusajiriwa wengine kwa vyeti vya utambulisho bandia.

Mpaka karne hii yuko mtu anashangilia kama zuzu kupata greencard ili akawe kijakazi na kutumikia taifa lingine. Yaani anaacha ardhi, mashamba na vyakula fresh kwenda ugenini akaishi kama mkimbizi maisha ya dhiki, hofu na wasiwasi kubwa. Yaani anapishana na wazungu kwenye ndege wakija kwao kukamata mapande makubwa ya ardhi yao na yeye kwenda kwao akawe kibarua wao akahudumie wazee, watoto na watu wao na kula vitu vikuukuu kama hot dog (fast foods) na kununua vitu vya kwenye clearance.

Hapa sio maswala ya wivu bali ni maswala ya ukombozi wa kifikra wa vijana wetu. Mimi nitakuwa mtu wa kwanza kumshangalia kijana wetu aliyekwenda kule na kurudi kwao na mtaji, elimu, uzoefu, ujuzi na exposure kuja kubadilisha mambo (uchumi, huduma, siasa na matazamo) kwao.
True hapa bongo kuna fursa tele na rahisi kutajirika kuliko nje ukiwa macho,chek wachina wanavyosomba pesa zetu kupitia bidhaa za machinga na bodaboda hawa wote ni madalali wa viwanda vya china na India wakituma kuukuza uchumi wa nchi hizo.
 
IQ yako ni ndogo sana, Ukraine imenyang'anywa na Urusi mikoa 4, kwahiyo unataka kusema Ukraine ni mazuzu?

DR Congo wanaporwa mali zao kwa mtutu wa bunduki na wazungu kwa mgongo wa Rwanda na Uganda. Msumbiji wanataka kunyang'anywa gesi yao, Sudan Kusini wamenyang'anywa mafuta yao na wazungu kwa mgongo wa vita ya wenyewe kwa wenyewe wanaopatiwa silaha na wazungu. Nani kakwambia kuwa M23 wana uwezo wa kupigana na serikali DRC?
Kama wanamali na hawazitumii kwann wasinyang'anywe?
Leo hii uende kijiji fulani ukute wazee wanachezea dhahabu bao. Unawaomba tena unawapa hela wanakataa. Si unawanyang'anya
Ndiyo Afrika. Rasilimali nyingi lkn bara masikini. Wazungu wanabeba sabb wanashida zao na wafrika hawana shida nazo.
Duniani tunaishi kama kwenye mbuga za wanyama.
 
True hapa bongo kuna fursa tele na rahisi kutajirika kuliko nje ukiwa macho,chek wachina wanavyosomba pesa zetu kupitia bidhaa za machinga na bodaboda hawa wote ni madalali wa viwanda vya china na India wakituma kuukuza uchumi wa nchi hizo.
Mbona nchi yako tangu kupata uhuru mpk sasa bado inahangaika na umeme wa mgao na maji?
Fursa? Maisha popote unaona Mabili ni muafrika lkn anacheza timu ya taifa ya Austarilia. Afrika kuna ujinga mwingi sana
 
Mbona nchi yako tangu kupata uhuru mpk sasa bado inahangaika na umeme wa mgao na maji?
Fursa? Maisha popote unaona Mabili ni muafrika lkn anacheza timu ya taifa ya Austarilia. Afrika kuna ujinga mwingi sana
Lakini ndo rahisi kutajirika ukiwa macho.
 
True hapa bongo kuna fursa tele na rahisi kutajirika kuliko nje ukiwa macho,chek wachina wanavyosomba pesa zetu kupitia bidhaa za machinga na bodaboda hawa wote ni madalali wa viwanda vya china na India wakituma kuukuza uchumi wa nchi hizo.
Ona vijana wa kichina wanakimbilia kuja kwenye nchi yetu kwa wingi halafu vijana wetu wanahamasishana kukimbilia Marekani kwa wingi. Mwalimu Nyerere aliwaita mazuzu watu wa namna hii. Aliwabeza na kuwacheka Wale waliodanganywa wakabadilisha almasi zao kwa kupewa golori (chupa) za kuchezea kwakuwa glori zinaonekana nzuri sana kwa kuwa zina rangi zinazong'ara. Ulaya na Marekani kunavutia na kupendeza sana kuliko Tanzania by far, lakini vijana wetu wakifika kule wanaishi maisha bandia ili kujaribu kumudu kuishi na kufanya savings angalau wabaki na kitu.
 
Mbona nchi yako tangu kupata uhuru mpk sasa bado inahangaika na umeme wa mgao na maji?
Fursa? Maisha popote unaona Mabili ni muafrika lkn anacheza timu ya taifa ya Austarilia. Afrika kuna ujinga mwingi sana
Kijana mwenye akili halikimbii tatizo, bali analitafutia majibu yake. Unachotaka kuwaambia watu ni kwamba ni heri tungeendelea kutawaliwa na wakoloni hadi leo. Wale wazee akina Nyerere, Nkrumah, Kenyatta, Obote, Mugabe, nk kazi yao ilikuwa kuwafukuza wakoloni tu wewe Wong Fei na mimi na wengine kazi yetu ni kuleta maji, umeme, na fedha mifukoni kwa wananchi kwa kuondoa vikwazo vyote vinavyozuia umeme, maji na fedha mifukoni visipatikane hata ikibidi kwa kuwanyonga au kuwapindua wale wote wanaokwamisha upatikanaji wake. Dawa sio vijana barobaro nguvu kazi yenye mawazo mapya kuikimbia nchi yao. Hata hizo nchi tunazokimbilia kulikuwa hakuna umeme, maji, demokrasia wala uhuru wa kujieleza, lakini vijana wao kwa hali na damu walichachamaa dhidi ya vikwazo vyao vyote hadi wakafika hapo sisi tunapopatamani leo.
 
Kama wanamali na hawazitumii kwann wasinyang'anywe?
Leo hii uende kijiji fulani ukute wazee wanachezea dhahabu bao. Unawaomba tena unawapa hela wanakataa. Si unawanyang'anya
Ndiyo Afrika. Rasilimali nyingi lkn bara masikini. Wazungu wanabeba sabb wanashida zao na wafrika hawana shida nazo.
Duniani tunaishi kama kwenye mbuga za wanyama.
Hujui au umesahau vitu vingi sana. Rasilimali zetu zipo nyingi lakini vifaa vya kuchimbia madini na masoko ya kuuzia bidhaa hizo wanavimiliki wao, yaani wao ndio wanaoamua kuuzie kifaa gani kwa bei gani, lakini wao pia ndio wanaoamua wanunue nini kwako chenye ubora gani kwa bei gani. Utachomokaje hapo? na kiongozi atakaejifanya mjanja wana ama mtafutia sababu ya kumuwekea vikwazo vya kiuchumi, ama kususia kununua bidhaa zake, ama kumnyima misaada na mikopo, ama kupinduliwa, au kumuua. Na ukumbuke pia kuwa viongozi wengi kama sio wote wa Afrika wanawekwa na wazungu kwa maslahi yao au wanageuzwa kuwa marafiki wao kwa kutumia misaada, mikopo, uwekezaji, kupendelewa au kutishiwa kukubaliana na matakwa yao la sivyoo......, Hii ndiyo maana hata kama mkibadilisha chama tawala au kiongozi hali ya mambo inabakia ileile. Mfano, unaweza kusema kama tukibadilisha katiba na kuiangusha CCM kutoka madarakani tutapata nafuu ya mambo, ukweli ni kwamba hapanaaaa. kenya, malawi, Zambia, Uganda, Rwanda, Burundi walifanikiwa kubadilisha katiba na vyama vyao vya ukombozi lakini maisha yao hayakubadilika kama walivyotarajia, ni kama sisi tu ambao tuna katiba ileile na chama kilekile tangu uhuru. Hii ni kuonyesha kuwa shida yetu sio katiba, vyama tawala wa viongozi bali shida yetu inatoka nje ya bara la Afrika. Dawa yake ni Afrika kuungana kwa kujilinda wenyewe, kutembeleana kwa uhuru, kuuziana bidhaa wenyewe kwa wenyewe zaidi na kuazimana (vitu, wataalam na utaalam, bidhaa, fedha, mitaala ya elimu) wenyewe kwa wenyewe.

Waarabu hawana uchaguzi, demokrasia wala katiba mpya lakini mambo yao yanakwenda kuliko sisi.
 
Shida kuipataa greencard ni zaidi ya Vita

Sent using Jamii Forums mobile app
Usidanganyike kaka hakuna ugumu wowote ule kwenye kupata greencard. Kama nilivyosema green card ni aina nyingine ya soko la watumwa, mahali ambao wafanyakazi wa bei rahisi wanapatikana kwa urahisi. Hata wakati ule wa utumwa sio kila mtu alifaa kununuliwa na kusafirishwa kwenda ulaya na marekani, bali walikuwa wanatakiwa watumwa wenye nguvu na vijana barobaro. Hata kwenye soko hili la utumwa mamboleo (green card) kuna vigezo ambavyo ni lazima uwe navyo ili kufanikiwa kusafirishwa huko kwa ndege. Na vigezo hivyo ni pamoja na:
1. Umri wako - lazima uwe kijana (sifa hii haijabadilika tangu enzi zilee za utumwa)
2. Uwe na nguvu, usiwe mlemavu (sifa hii pia haijabadilika tangu enzi zilee za utumwa)
3. Uwe na elimu kubwa kumudu kufundisha vyuo vikuu au ujuzi maalum kama fundi bomba kuzibua vyoo, uuguzi kutunza wazee, mifugo kuhudumia wanyama, mazingira, ujenzi, IT. HIzi ni sifa muhimu za ziada ambazo ukiwa nazo uwezo wako wa kupata green card ni mkubwa mno mno mno ajabu kama kumsukuma mlevi.
4. Kujua kuongea Kiingereza kizuri. Hii nayo ni sifa muhimu ya ziada sawa na kuweka siagi kwenye mkate. Ndio maana utakuta Wakenya, Wamalawi, Wazimbabwe, Wahindi, Waphilipino, waninigeria, Wazambia wengi wanapata green card kuliko watanzania. Kaka anza kwenda pale British Council ukajifunze kiingereza chao.
5. Wenye mitaji ya kuwekeza Marekani. Sifa hii ni muhimu kweikwei.
6. Usiwe nkorofi wa nhalifu (unlawful)

Kaka kama unasifa hizi hukai foleni sana, wasikudanganye kuwa ni bahati na sibu, sioooooo kweeeeli, vigezo na masharti huzingatiwa hata kama wanatafuta manamba.
 
Kazi zipo njooni Marekani, ukiangalia vizuri hapo utamuona jamaa yenu anaewaita

 
Kavulata: Unajua unachokisema au umekaririshwa? Niko Marekani, sikuja kwa kufungwa mnyororo,na hata nikitaka kuondoka hakuna kamba iliyonifunga.
Ushauri kila siku kwa vijana wa kitanzania, kama unaona opportunities zimebana Tanzania jaribu popote, nina mifano mingi mno, na nimeona kwa watu toka mataifa mbali mbali niliokutana nao US!
Ukiwa na focus, na documents halali na yote unayoyasikia kuhusu Marekani, ni mahali unaweza kufikisha ndoto zako, sisemi ni rahisi, lakini kuna nyenzo ambazo hupati katika nchi nyingi za Kiafrica.
Sijahonga au kumuona yoyote watoto wangu kupata mikopo ya vyuo vyao, sikuwa na connection zozote zile watoto wangu kupata white color jobs! In short mtoto wangu alikuwa recruited akiwa bado chuoni, na leo akiwa na miaka24 is making almost $ 85,000/ Wenzake aliowaacha bongo waliomaliza chuo wanasaka ajira!
Sasa sijui ni utumwa wa aina gani huo!
Ni kweli Marekani/ Canada zinataka nguvu kazi, lakini ukiingia huku ni juhudi zako na akili yako! Wengine wataenda juu, na wengine chini, sawasawa na wazawa! Anayenifyekea majani nyumbani kwangu ni mzungu! Maana sina muda! Na kila baada ya wiki mbili au tatu ananipigia simu kama yameota aje kufyeka! Na ameniambia ni fundi katika serikali yetu ya mtaa anatafuta pesa ya ziada! Hii ndio Marekani, simdharau najua anachotafuta!
Hivyo usikaririshwe na akina Lumumba.
Hulazimishwi ni akili yako tu! Wengine wanatumia hapo bongo wanatoka! Wengine mambo yanakataa! Maisha popote pale!
Sure! US unachagua maisha unayotaka wewe, hakuna kitu US hakuna, mtoto akizaliwa US kuna asilimia kubwa ya kutimiza ndoto zake, kitu kikubwa ni kuwa na ndoto, Elon Musk ametokea Africa lakini angekuwa Africa sidhani kama leo hii angekuwa 1st billionare, alifahamu ndoto yake na akajua ni mahali gani anaweza kwenda na kuitimiza.
 
Sure! US unachagua maisha unayotaka wewe, hakuna kitu US hakuna, mtoto akizaliwa US kuna asilimia kubwa ya kutimiza ndoto zake, kitu kikubwa ni kuwa na ndoto, Elon Musk ametokea Africa lakini angekuwa Africa sidhani kama leo hii angekuwa 1st billionare, alifahamu ndoto yake na akajua ni mahali gani anaweza kwenda na kuitimiza.
Yeah sure [emoji817]
 
Sure! US unachagua maisha unayotaka wewe, hakuna kitu US hakuna, mtoto akizaliwa US kuna asilimia kubwa ya kutimiza ndoto zake, kitu kikubwa ni kuwa na ndoto, Elon Musk ametokea Africa lakini angekuwa Africa sidhani kama leo hii angekuwa 1st billionare, alifahamu ndoto yake na akajua ni mahali gani anaweza kwenda na kuitimiza.
ndoto za alinacha hizo, hata Tanzania wako akina Bakheresa, Mo Dewji, Diamond, Millard Ayo, Mengi Reginald, Mutahaba, Lowasa, Masoud Kipanya KP anatengeneza magari ya umeme, Mlimani City Mall, nk. Maisha ni kutoka kwenye comfortable zone yako tu.
 
Unajua wewe ni Mjinga! Hao vijana unaowasema hata hapa Tanzania wapo.

Your level of Stupidity render me speechless!

Baki na Negativity zako.
Sasa kaka yangu wewe unabisha nini? Unabisha kuwa green card ni mbadala ya biashara ya utumwa na watumwa? Unabisha kuwa sababu za kupeleka watu kwa green card rottary ni zilezile sababu za kupeleka watu kwa biashara ya watumwa? Unabisha kuwa kodi yako itasaidia kuijenga marekani? Unabisha kuwa Tanzania haikukusomesha kwa kodi za walipakodi wa tanzania? Unabisha kuwa maisha kule marekani ni magumu sana kuliko Tanzania? Unabisha kuwa kule usipofanyakazi huli?

Unabisha kuwa baada Rais Abraham Linkon alipoyafunga masoko ya watumwa kulitokea uhaba wa wafanyakazi wa bei rahisi? Au unabisha nini mzee?
 
Sure! US unachagua maisha unayotaka wewe, hakuna kitu US hakuna, mtoto akizaliwa US kuna asilimia kubwa ya kutimiza ndoto zake, kitu kikubwa ni kuwa na ndoto, Elon Musk ametokea Africa lakini angekuwa Africa sidhani kama leo hii angekuwa 1st billionare, alifahamu ndoto yake na akajua ni mahali gani anaweza kwenda na kuitimiza.
 
Sure! US unachagua maisha unayotaka wewe, hakuna kitu US hakuna, mtoto akizaliwa US kuna asilimia kubwa ya kutimiza ndoto zake, kitu kikubwa ni kuwa na ndoto, Elon Musk ametokea Africa lakini angekuwa Africa sidhani kama leo hii angekuwa 1st billionare, alifahamu ndoto yake na akajua ni mahali gani anaweza kwenda na kuitimiza.
Wacha uongo wa kijinga wewe, ebo!! unachagua maisha wewe mmatumbi!!! Unaona hao wanaume 2 hapo, hiyo ndiyo sample ya watu walikuwa wanatakiwa kwenye soko la marekani wakati ule, big and tall.
 
Kavulata: Unajua unachokisema au umekaririshwa? Niko Marekani, sikuja kwa kufungwa mnyororo,na hata nikitaka kuondoka hakuna kamba iliyonifunga.
Ushauri kila siku kwa vijana wa kitanzania, kama unaona opportunities zimebana Tanzania jaribu popote, nina mifano mingi mno, na nimeona kwa watu toka mataifa mbali mbali niliokutana nao US!
Ukiwa na focus, na documents halali na yote unayoyasikia kuhusu Marekani, ni mahali unaweza kufikisha ndoto zako, sisemi ni rahisi, lakini kuna nyenzo ambazo hupati katika nchi nyingi za Kiafrica.
Sijahonga au kumuona yoyote watoto wangu kupata mikopo ya vyuo vyao, sikuwa na connection zozote zile watoto wangu kupata white color jobs! In short mtoto wangu alikuwa recruited akiwa bado chuoni, na leo akiwa na miaka24 is making almost $ 85,000/ Wenzake aliowaacha bongo waliomaliza chuo wanasaka ajira!
Sasa sijui ni utumwa wa aina gani huo!
Ni kweli Marekani/ Canada zinataka nguvu kazi, lakini ukiingia huku ni juhudi zako na akili yako! Wengine wataenda juu, na wengine chini, sawasawa na wazawa! Anayenifyekea majani nyumbani kwangu ni mzungu! Maana sina muda! Na kila baada ya wiki mbili au tatu ananipigia simu kama yameota aje kufyeka! Na ameniambia ni fundi katika serikali yetu ya mtaa anatafuta pesa ya ziada! Hii ndio Marekani, simdharau najua anachotafuta!
Hivyo usikaririshwe na akina Lumumba.
Hulazimishwi ni akili yako tu! Wengine wanatumia hapo bongo wanatoka! Wengine mambo yanakataa! Maisha popote pale!
Cassavaleaves unajuwa kuwa unapata dhambi kuwadanganya vijana wenzako watanzania kuwa maisha huko ni bull bull. Hebu angalia hii uone kama iko kwamtogole au wapi
 
Back
Top Bottom