Group la WhatsApp latumika kuchangisha mifuko 300 ya saruji ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Nachingwea Boys

Group la WhatsApp latumika kuchangisha mifuko 300 ya saruji ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Nachingwea Boys

Safi sana hayo ndo mambo tunataka sio unakuta baadhi ya magroup ya WhatsApp kutumiwa vibaya na memba wake.
Naam naam

Mitandao ya kijamii ikitumika vizuri huleta manufaa, hata wale walio mbali na Tanzania wanaweza kujumuika na wenzao hapa Tanzania muda wote
 
Kitambo sana nachingwea.

Nawaona class met wangu hapo wamekuwa wazee wengine wamekuwa wamama kabisa kumbe watoto wa 90 tu hahhahhhha.

Hongereni wana nachingwea wasalimieni sana hapo nachingwea days,nambambo days shule ambazo zinashindana katika ufaulu hapo mjini.

Nakumbuka enzi za miaka ya 2011 wkuna vijana walituwakilisha vizuri sana kaka wenye majina ya kufanana mmoja akitoka nambambo mwingine akitoka nachingwea.

Ila nachingwea mnaacha kuchanga kufanya vitu vya maana mnajenga shule kwa wakati huu,hamko siriaz.

Hapo nachingwe wananchi wanashida nyingi tu achilia mbali na elimu.

Yani kama bado wana nachingwea mnawaza kuwa elimu iko chini kwa sababu ya majengo basi poleni sana sana sana sana sana sana

habari kiongozi, Ni kweli changamoto zipo nyingi lakini hatuwezi kushughulikia zote kwa wakati mmoja

group la WhatsApp la Nachingwea Yetu limekuwa Kama sehemu tu ya wadau ambapo pamoja na Mambo mengine hutumika Kama jukwaa na mfano wa kuwahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu ktk miradi ya wananchi na kufanya kazi kwa bidii

pia tunaamini kuwa unaweza kuwa Kama alert ya kuwafanya wananchi kuwa wamoja ili kutatua changamoto mbalimbali

PIA members wa group hili wamekuwa wakishirikiana kwa pamoja kuwafikia wenye uhitaji na hata kushiriki ktk kusaidia miradi ya sekta nyingine kwa kadri ya uwezo wao kutimiza wajibu wa mwananchi kushiriki ktk kutatua changamoto mbalimbali

aidha, ukiacha mradi mkubwa ule wa boma ambao wananchi walipambana kuondokana na ghala la kikoloni, wananchi wameamua kwa namba nyingi kuja na mradi mkubwa wa kimkakati ambao Ni huu wa NACHINGWEA BOYS HIGH SCHOOL

Kama Ni mwenyeji wa Nachingwea utakubaliana na Mimi mpk sasa hakuna shule kubwa ya bweni kuanzia kidato Cha Kwanza Hadi Cha sita

Aidha shule hii utaweza kuwa Kama chachu ya wilaya Yetu kujulikana zaidi kwa kuwa ukamilifu wa shule hii itachukua wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali nchini baada ya makubaliano na serikali kuu

KARIBU TUJUMUIKE PAMOJA KUIJENGA NACHINGWEA
 
Baadhi ya wananchi wa Nachingwea ambao wapo ktk kundi sogozi la WhatsApp la NACHINGWEA YETU, wamekabidhi mifuko 300 ya saruji kuunga mkono ujenzi wa mradi mpya wa Nachingwea boys high school inayojengwa kwa kutumia mapato ya ndani ya halmashauri ya wilaya ya Nachingwea iliyopo mkoa wa Lindi

Shule hiyo inatarajiwa kukamilika kwake kuchukua wanafunzi 1600 kuanzia kidato Cha Kwanza Hadi Cha sita.

Aidha shule hiyo mpya ya wavulana inatarajiwa kuwa na jumla ya majengo 54 ikiwemo madarasa, mabweni, nyumba za walimu, duka, zahanati na sehemu ya kula chakula.

Shule hiyo inajengwa nje kidogo ya mji wa Nachingwea katika kijiji Cha chiumbati kata ya chiumbati tarafa ya Naipanga

Akizungumza wakati wa kupokea mchango huo, aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri hiyo ambaye kwa sasa Ni katibu tawala mkoa wa DSM Bwn Hassan Abasi Rugwa, amewashukuru wadau hao wa Nachingwea Yetu Whatsapp group kwa mchango wao na kuwasisitiza wananchi wa Nachingwea kuendelea kushikamana kwa pamoja ili kufanya Mambo makubwa zaidi.

Serikali imeonesha Nia ya kuunga mkono ujenzi wa shule hiyo baada ya kuona jitihada za dhati zinazofanywa na wananchi

View attachment 1809113

View attachment 1809115
Hapo bado admin mpokeaji wa hela alishapiga za kwake [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Sijui kwa sasa kuna changamoto gani ila nina uhakika nachingwea hakuna changamoto ya majengo ya shule bali changamoto ni kwa watoto wetu.

Hatujawekeza kwa watoto tunawekeza kwwnye majengo tu wakati watakaokuja kuyatumia majengo hayo bado hawajaamka wamelala fofofo.

Acheni mambo ya kujenga mashule angalieni mnatatua vipi changamoto za maji,na changamoto zingine za maisha na sio kupoteza kwenye majengo ya shule tu.

Mnaweza kujichanga mkaanzisha mradi wowote ule wa maendeleo ya wana nachingwea kama suala la maji nadhani bado ni changamoto kubwa watu hamuwazi mtarahisisha vipi watu wasiende tena kule kwa Mungu hataki badala yake waende kuchota maji safi na salama kwenye mradi fulani ulioanzishwa na michango ya wananchi wenyewe.

Bahat nzuri naskia munae mkuu wa wilaya msikivu na mstaarabu,tumieni.

Achaneni na majengo ya shule angalieni mtarahisisha vipi changamoto zenu za maisha.

Kwenye korosho mnashindwa kuangalia kuna fursa gani.
Kwenye vilimo vingi tunashindwa kuangalia kuna fursa gani.

Nyie mnadhani kwa sasa elimu itatukomboa.

Sisi ndo runatakiwa tuikomboe hii elimu.

Na kuikomboa elimu sio kujenga majengo,nini mnakomboa majengo badala ya kuikomboa elimu.

Kaeni na huyo mkuu wa wilaya mtulize vichwa muachache na majengo ya shule ambayo watoto hawajajua umuhimu wake

Habari kiongozi, maoni yako yamesikika, yatafanyiwa kazi

kuhusu maji, kuna mradi mkubwa wa maji wa MBWINJI unaohudumiwa na MANAWASA, maeneo mengi ya mjini yamefikiwa na huduma ya maji na hata ktk baadhi ya vijiji

kwa sasa RUWASA INAENDELEA na jitihada za kuhakikisha vijiji vyote vinafikiwa na maji baridi

REA nap hawako nyuma, wanaendelea na jitihada za kusambaza umeme ktk Kila Kijiji (je una taarifa kuwa umeme umefika mpaka Ngunichile?)

kuhusu sekta ya kilimo, jitihada zinaendelea ktk kuongeza uzalishaji wa mazao ya kibiashara ikiwemo korosho, ufuta na mbaazi

Kuna maboresho makubwa yanaendelea ktk sekta ya afya na sekta zingine

karibu TUJUMUIKE PAMOJA tuweze kutatua changamoto mbalimbali

kama we Ni mdau wa maendeleo ya wilaya yetu na upo tayri kushiriki nasi, basi njoo inbox nikuunge ktk group


Kuhsu Ishu ya madarasa, Target yetu kwa sasa Ni kuwa na shule za bweni ambazo zitawachanganya wanafunzi wetu na wa mikoa mingine ili waweze kujifunza vitu bingo zaidi kutoka kwa wenzao

lakini pia shule za bweni zinampa mwanafunzi muda mwingi wa kujifunza, kupunguza utoro na hata kumuepusha mwanafunzi na mazingira hatarishi
 
Kama Ni mwenyeji wa Nachingwea utakubaliana na Mimi mpk sasa hakuna shule kubwa ya bweni kuanzia kidato Cha Kwanza Hadi Cha sita
Mkuu kwanza niwapongeze kwa juhudi mnazochukua na kunitoa hofu kwamba mnashughulikia changamoto nyingi kwa kadri ya uwezo wenu.

Nawaombea kwa Mungu muzitatue changamoto hizo.

Kama Ni mwenyeji wa Nachingwea utakubaliana na Mimi mpk sasa hakuna shule kubwa ya bweni kuanzia kidato Cha Kwanza Hadi Cha sita
Hapa naomba nichangie kuwa lengo sio kuwa na shule ya boys form one -form six hapana.

Lengo ni kupata elimu bora.

Suala la wanafunzi kuchanganyika na watu wengine hili sio suala ambalo unaweza kulijengea hoja kuwa eti suala hili liwashawishi ninyi kufanya mradi wa kujenga shule ati kwa kuwa watoto wa nachingwea watachanganyika na watoto wa mikoa mingine.

Hili la kuchanganyika hitakiwi liwe kipaumbele,bali hili libaki kama faida ya ziada huku faida kuu ikiwa ni kupata elimu bora na kukuza ufaulu katika wilaya ya nachingwea.
Aidha shule hii utaweza kuwa Kama chachu ya wilaya Yetu kujulikana zaidi kwa kuwa ukamilifu wa shule hii itachukua wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali nchini baada ya makubaliano na serikali kuu
Hii pia haitakiwi kuwa hoja na faida ya kipaumbele ya kuwafanya nyie muhamasike kujenga shule hiyo.

Hii itakuwa mnatumia nguvu kubwa sana kwa ajili ya kutafuta faida ndogo ambayo ingeweza kupatikana katika mambo mengine ya kijamii huku nguvu mliyotumia mngewekeza katika mambo mengine.

Hamuwezi kutumia nguvu kubwa kwa kutaka mkoa ujulikane zaidi wakati kuna mambo ya msingi sana ambayo mashuleni wanafunzi wanakosa alafu mtu unakuja kuongeza hsule zingine kwa wakati huu badala ya kutatua changamoto zilizoko mashuleni.
Aidha shule hii utaweza kuwa Kama chachu ya wilaya Yetu kujulikana zaidi kwa kuwa ukamilifu wa shule hii itachukua wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali nchini baada ya makubaliano na serikali kuu
Nachimgwea girls pale benki mbele ipo,mumetumiaje shule hii kujulikana zaidi kama ambavyo mtatumia hiyo shule tarajiwa kujulikana.

kama we Ni mdau wa maendeleo ya wilaya yetu na upo tayri kushiriki nasi, basi njoo inbox nikuunge ktk group
Asante sana mkuu.

Kwa sasa sipo nachingwea kimakazi acha nijumuike na watu wa huku niliko kujenga taifa huku nyumbani nikijenga familia. Wa nachingwea jengeni taifa nachingwea sisi wa huku tutajenga taifa huku kwa sababu tunajenga jengo moja ila tunatofautiana huyu kashika ukuta ule huyu ukuta ule
lakini pia shule za bweni zinampa mwanafunzi muda mwingi wa kujifunza
Sio kweli mkuu.

Nataka kusema kuwa tatizo sio kwamba shule za kata hazimpi mwanafunzis muda mwingi wa kujifunza.

Tatizo ni hawa wanafunzi wenyewe,tataioz ni wanafunzi na mindset za wazazi na wala tatizo sio shule kabisa.

Nakupa mfano.

Katika shule moja hapo wilayani kuna kijana wangu amefaulu vizuri akamshinda rafiki ake ambaye anasoma shule ya bweni nje ya nachingwea.

Kwa nini huyu wa mbweni akapitwa ufaulu na huyu wa kata ?

Shida ni bweni au juhudi ya mwanafunzi ?
Na hapo jumlisha na changamoto za uhaba wa waalimu utaona kuwa shina la tatizo sio shule bali shina la tatizo ni wanafunzi wenyewe.

Sasa hapo nawapa challenge wana nachingwea mnajipanga vipi kutatua hili kuhakikisha wanafunzi wanakuwa na juhudi kwanza ya kusoma.

Aproach mtakayoitumia nitaona tena kama mna maono ya kweli na vijana au mnawekeza kwenye majengo tu.
kupunguza utoro
Shule za bweni hazipunguzi utoro kabisa kabisa mkuu.mnachotakiwa kujua ni kuwa majengo hayambadilishi mwanafunzi bali kitakachombadilisha kwanza ni aina ya watu na utayari wa mind yake.

Usitegemee kuwa mtoto fulani akihamishwa shule ya kata huku alikuwa mtoro kisha akapelekwa bweni ukadhani atakuwa mtulivu sio kweli.

Kwani hakuna kesi za kupatikana kudoji kwa vipindi watoto wanaosoma bweni ?

Kama zipo kesi hizo kwa nini zitokee katika shule za bweni alafu wewe unahamasika kujenga mbweni kwa kutaka kuondoa jambo hili ?
hata kumuepusha mwanafunzi na mazingira hatarishi
Naomba kusema tena nachingwea hakuna mazingira hatarishi ukilinganisha na mazingira mengine ya nchi kama vile dar es salaa..

Naomba uniambie mfano wa hayo mazingira hatarishi ambayo yamekuwa na ulazima mkubwa wa kujenga shule za bweni ?

Kuna shule kama azania inafanya vizuri sana na ni day tu lakini imezungukwa na mazingira hatarishi kabisa lakini vijana wanasoma sana tofauti hata na nachingwea.

Katika sekta ya elimu hasa nachingwea changamoto sio shuele wala majengo.

Changamoto ni waalimu na mindset za wazazi na wanafunzi.

Leo tuna vijana kibao ambao wamemaliza shule wamefaulu vizuri sana lakini hawana ajira yeyote,na vijana hawa wanaweza kuwasaidia wanafunzi waliopo mashuleni.

Mnawaangalia vipi hawa vijana kuhakikisha kuwa wanawasaidia wenzao kufaulu (msijekutaka wafanye kazi ya kanisa)

Nachingwea day na nambambo day ni shule zilizoko mjini ni mfano kwa shule nyingi hapo nachingwea,lakini shule hizi unaweza ukaenda ukakuta mwalimu wa mathematics ni mmoja shule nzima.

Masomo ya sayansi kabisa walimu ni tatizo.

Nyie mnafocus katika majengo wakati kinachofanyika katika hayo majengo bado kinahitaji sapoti kubwa sana.

Wekezeni rasilimali watu,tumieni vijana wanaomiza kukuza elimu,msitumie pesa zenu kukuza majengo mkuu.

Badala ya kuboresha vilivyokuwepo mnataka kuanzisha vipya ambavyo vitakutana na changamoto inayokutana navyo hivi vilivyokuwepo
 
Mkuu kwanza niwapongeze kwa juhudi mnazochukua na kunitoa hofu kwamba mnashughulikia changamoto nyingi kwa kadri ya uwezo wenu.

Nawaombea kwa Mungu muzitatue changamoto hizo.


Hapa naomba nichangie kuwa lengo sio kuwa na shule ya boys form one -form six hapana.

Lengo ni kupata elimu bora.

Suala la wanafunzi kuchanganyika na watu wengine hili sio suala ambalo unaweza kulijengea hoja kuwa eti suala hili liwashawishi ninyi kufanya mradi wa kujenga shule ati kwa kuwa watoto wa nachingwea watachanganyika na watoto wa mikoa mingine.

Hili la kuchanganyika hitakiwi liwe kipaumbele,bali hili libaki kama faida ya ziada huku faida kuu ikiwa ni kupata elimu bora na kukuza ufaulu katika wilaya ya nachingwea.

Hii pia haitakiwi kuwa hoja na faida ya kipaumbele ya kuwafanya nyie muhamasike kujenga shule hiyo.

Hii itakuwa mnatumia nguvu kubwa sana kwa ajili ya kutafuta faida ndogo ambayo ingeweza kupatikana katika mambo mengine ya kijamii huku nguvu mliyotumia mngewekeza katika mambo mengine.

Hamuwezi kutumia nguvu kubwa kwa kutaka mkoa ujulikane zaidi wakati kuna mambo ya msingi sana ambayo mashuleni wanafunzi wanakosa alafu mtu unakuja kuongeza hsule zingine kwa wakati huu badala ya kutatua changamoto zilizoko mashuleni.

Nachimgwea girls pale benki mbele ipo,mumetumiaje shule hii kujulikana zaidi kama ambavyo mtatumia hiyo shule tarajiwa kujulikana.


Asante sana mkuu.

Kwa sasa sipo nachingwea kimakazi acha nijumuike na watu wa huku niliko kujenga taifa huku nyumbani nikijenga familia. Wa nachingwea jengeni taifa nachingwea sisi wa huku tutajenga taifa huku kwa sababu tunajenga jengo moja ila tunatofautiana huyu kashika ukuta ule huyu ukuta ule

Sio kweli mkuu.

Nataka kusema kuwa tatizo sio kwamba shule za kata hazimpi mwanafunzis muda mwingi wa kujifunza.

Tatizo ni hawa wanafunzi wenyewe,tataioz ni wanafunzi na mindset za wazazi na wala tatizo sio shule kabisa.

Nakupa mfano.

Katika shule moja hapo wilayani kuna kijana wangu amefaulu vizuri akamshinda rafiki ake ambaye anasoma shule ya bweni nje ya nachingwea.

Kwa nini huyu wa mbweni akapitwa ufaulu na huyu wa kata ?

Shida ni bweni au juhudi ya mwanafunzi ?
Na hapo jumlisha na changamoto za uhaba wa waalimu utaona kuwa shina la tatizo sio shule bali shina la tatizo ni wanafunzi wenyewe.

Sasa hapo nawapa challenge wana nachingwea mnajipanga vipi kutatua hili kuhakikisha wanafunzi wanakuwa na juhudi kwanza ya kusoma.

Aproach mtakayoitumia nitaona tena kama mna maono ya kweli na vijana au mnawekeza kwenye majengo tu.

Shule za bweni hazipunguzi utoro kabisa kabisa mkuu.mnachotakiwa kujua ni kuwa majengo hayambadilishi mwanafunzi bali kitakachombadilisha kwanza ni aina ya watu na utayari wa mind yake.

Usitegemee kuwa mtoto fulani akihamishwa shule ya kata huku alikuwa mtoro kisha akapelekwa bweni ukadhani atakuwa mtulivu sio kweli.

Kwani hakuna kesi za kupatikana kudoji kwa vipindi watoto wanaosoma bweni ?

Kama zipo kesi hizo kwa nini zitokee katika shule za bweni alafu wewe unahamasika kujenga mbweni kwa kutaka kuondoa jambo hili ?

Naomba kusema tena nachingwea hakuna mazingira hatarishi ukilinganisha na mazingira mengine ya nchi kama vile dar es salaa..

Naomba uniambie mfano wa hayo mazingira hatarishi ambayo yamekuwa na ulazima mkubwa wa kujenga shule za bweni ?

Kuna shule kama azania inafanya vizuri sana na ni day tu lakini imezungukwa na mazingira hatarishi kabisa lakini vijana wanasoma sana tofauti hata na nachingwea.

Katika sekta ya elimu hasa nachingwea changamoto sio shuele wala majengo.

Changamoto ni waalimu na mindset za wazazi na wanafunzi.

Leo tuna vijana kibao ambao wamemaliza shule wamefaulu vizuri sana lakini hawana ajira yeyote,na vijana hawa wanaweza kuwasaidia wanafunzi waliopo mashuleni.

Mnawaangalia vipi hawa vijana kuhakikisha kuwa wanawasaidia wenzao kufaulu (msijekutaka wafanye kazi ya kanisa)

Nachingwea day na nambambo day ni shule zilizoko mjini ni mfano kwa shule nyingi hapo nachingwea,lakini shule hizi unaweza ukaenda ukakuta mwalimu wa mathematics ni mmoja shule nzima.

Masomo ya sayansi kabisa walimu ni tatizo.

Nyie mnafocus katika majengo wakati kinachofanyika katika hayo majengo bado kinahitaji sapoti kubwa sana.

Wekezeni rasilimali watu,tumieni vijana wanaomiza kukuza elimu,msitumie pesa zenu kukuza majengo mkuu.

Badala ya kuboresha vilivyokuwepo mnataka kuanzisha vipya ambavyo vitakutana na changamoto inayokutana navyo hivi vilivyokuwepo

Boss, ahsante kwa maoni yako
 
Boss, ahsante kwa maoni yako
Sawa mnatakiwa kubadili mitazamo yenu.

Msidhani kudumisha elimu ni kuwa na majengo mengi.

Muhakikishe mnatatua changamoto za majengo yaliyopo kabla ya kuyaongeza majengo mengine.
 
safuher naanza kuuona uwalakini mkubwa ulio nao licha ya kua umezaliwa na umesoma nachingwea toka chekechekea mpaka 4m4 ,kiufupi tu niseme au nihitimishe kwa kusema kua wewe pia ni mmojawapo kati ya watu ambao pengine haukunufaika kwa lolote kwa chochote kwa elimu yako ulioipata Nachingwea.
Nashangaa kuona unaibeza kabisa harakati ya kibabe iliofanywa na wanakundi hawa kuhakikisha wanasonga mbele !
Alichokifanya mhusika si kwa nachingwea ,Tanzania nzima ukiondoa tu Mkoa mmoja Kilimanjaro naimani kote kulikobaki kuna changamoto kama hii iliokutwa na kufikiwa na wanakundi hawa hadi kuamua kuiunga mkono serikali ila mwenzangu hujaliona hilo?
Shule za advance wilaya nzima iko shule moja tena ya Government .Olevel hazifiki 20 kama sijakosea na hakuna private hata moja.
Tuna uhaba wa vyuo pia ikumbukwe tuna chuo kimoja tu TTC .
Serikali mpka inaamua kuanzisha mradi huu unatka kusema kua hawajatambua uhaba wa majengo ( Kama unavyouita) / shule adi. Ukaamua wewe kusema tuboreshe tuliyo nayo ? Yapi hayo kiongozi .Nisije kosea nikaandika na mengine ingekua ndugu yangu anaelewa kisukuma ningemwambia akutafsirie maana ya hili neno
( NYANOKO ), MIE NAPITA KUSHOTO SIKU NJEMA
 
safuher naanza kuuona uwalakini mkubwa ulio nao licha ya kua umezaliwa na umesoma nachingwea toka chekechekea mpaka 4m4 ,kiufupi tu niseme au nihitimishe kwa kusema kua wewe pia ni mmojawapo kati ya watu ambao pengine haukunufaika kwa lolote kwa chochote kwa elimu yako ulioipata Nachingwea.
Nashangaa kuona unaibeza kabisa harakati ya kibabe iliofanywa na wanakundi hawa kuhakikisha wanasonga mbele !
Alichokifanya mhusika si kwa nachingwea ,Tanzania nzima ukiondoa tu Mkoa mmoja Kilimanjaro naimani kote kulikobaki kuna changamoto kama hii iliokutwa na kufikiwa na wanakundi hawa hadi kuamua kuiunga mkono serikali ila mwenzangu hujaliona hilo?
Shule za advance wilaya nzima iko shule moja tena ya Government .Olevel hazifiki 20 kama sijakosea na hakuna private hata moja.
Tuna uhaba wa vyuo pia ikumbukwe tuna chuo kimoja tu TTC .
Serikali mpka inaamua kuanzisha mradi huu unatka kusema kua hawajatambua uhaba wa majengo ( Kama unavyouita) / shule adi. Ukaamua wewe kusema tuboreshe tuliyo nayo ? Yapi hayo kiongozi .Nisije kosea nikaandika na mengine ingekua ndugu yangu anaelewa kisukuma ningemwambia akutafsirie maana ya hili neno
( NYANOKO ), MIE NAPITA KUSHOTO SIKU NJEMA
Hahaha sawa mkuu.

Uwe na siku njema pia.
 
Sawa mnatakiwa kubadili mitazamo yenu.

Msidhani kudumisha elimu ni kuwa na majengo mengi.

Muhakikishe mnatatua changamoto za majengo yaliyopo kabla ya kuyaongeza majengo mengine.
Miundombinu ya majengo ni kitu cha muhimu sana ktk elimu kabla ya kuhangaika na walimu na vitendea kazi
 
Miundombinu ya majengo ni kitu cha muhimu sana ktk elimu kabla ya kuhangaika na walimu na vitendea kazi
Mkuu kwa sehemu kama nachingwea kuongeza majengo ni sawa na kuongeza ukubwa wa ndoo wakati unataka lijae maji.
 
Hongera kwa waliojitoa kwa kidg, kujali elimu ya wadogo zetu ama watoto wetu..Mungu awabariki
 
Back
Top Bottom