GSM kuweni na utu, msimfanye Haji Manara kama Msukule

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001

Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.

Ndio kuna biashara,ndio kuna pesa. Lakini kumbukeni kuna utu na heshima mbele za watu.Zaidi ya yote kuna Akhera.

GSM mnajua kabisa huyu mtu ana msongo mkubwa wa mawazo baada ya kufukuzwa Simba Sc. Tunatambua nyinyi mlikuwa marafiki zake wakubwa hata kipindi akiwa Simba. Sasa urafiki gani huu usiojali utu na ubinaadamu.

Mnamtumia huyu ndugu kama msukule bila kujali utu wake mbele ya jamii?

Haya yanayoendelea yanaweza kumletea madhara makubwa zaidi kisaikolojia zaidi ya mvuta bangi. Msaidieni kiungwana,mbona kuna wapenzi wa Simba kama Ommy Dimpoz tunaona anatangaza bidhaa zenu bila kujihusisha na mambo ya Yanga? Tunzeni utu wa huyu ndugu anaoza ndani kwa ndani
 
Duh People This is Football / Soccer / Watani wa Jadi

Tusichukulie vitu Serious..., Kina Manara wanaongeza Chachu kwenye Hii Tasnia na huu utani wa tangia Jadi..., Hili game halihitaji mtu kuwa Serious
 
Acha wafu wazikane wenyewe
 
Kama manara anatoa utu wake kiasi hichi na alichoongea leo basi ni kweli alikuwa anaihujumu Simba ,Hongera sana uongozi wa Simba msaliti ameonekana,anayehujumu timu ameonekana kwa matendo yake .Tuliona anaonewa na kujiliza kumbe unafki tu alikuwa anahujumu Simba
 
Hakika Marehemu Ruge Mutahaba uliona mbali sana pale uliposema kuwa tukiwa hapa duniani tuogope mno Mungu na Teknolojia.

Akiongea mwenyewe leo Asubuhi katika Kipindi Bora cha Michezo cha Sports Headquarters cha EFM Msemaji wa Yanga SC Haji Manara alisema kuwa alipokuwa akiipamba Simba SC alipokuwa huko alikuwa hamaanishi na kwamba alikuwa amelewa.

Pamoja na kwamba kasema kuwa alikuwa amelewa ila Watangazaji wa Redio zote alizokuwa akienda wamesema alikuwa hajalewa na alikuwa mzima na isitoshe hata Kimaadili tu hakuna Redio inayoruhusu Mlevi Kuingia Studio na Kuhojiwa labda Yanga SC na GSM wakianzisha Redio yao wataruhusu Walevi na Mlevi mwenzao Manara wawe Wanatangaza.

Katika hali isiyokuwa ya Kawaida baada ya Kumaliza Interview yake EFM Haji Manara katika Hali inayooshesha na hata Kuthibitisha kuwa huenda akawa na tatizo Kubwa la Akili ( Dementia ) amemtumia Meseji ( Rununu ) Mtangazaji Ibrahim Masoud Maestro akikataa kuwa Yeye hakusema kuwa huko nyuma alipokuwa Msemaji wa Simba SC alipokuwa akiipamba Simba alikuwa amelewa.

Haji Manara laana inaanza Kukuumiza!!!
 
Yani kila siku we ni kuanzisha uzi kuongelea yanga hivi huna jambo lingine lakuongelea kwenye mpira wa Tanzania?

Unaweza ukaiongelea hata mbeya kwanza au vifundo fc au hata ukaongelea mechi ya Jana ya coastal vs simba ya kirafiki ..... Kungelea Yanga kila saa kunaonesha jinsi gani ulivo na hofu na uwoga juu ya Yanga.
 
Ipo siku atawasema na wao
 
Msikilize tena hapa
Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…