GSM mliopo hapa JamiiForums tafadhali naomba Majibu yenu ya upesi sana kwa haya Maswali yangu yafuatayo

Kati ya watu wajinga na hovyoo wewe n mmoja wao, hivi GSM ndiye wakukaa na vilabu au Bodi ya ligi?. Ungekuwa na akili ungeuliza Bodi ya ligi ilikuwa wapi mpk TFF anafanya mkataba na GSM, na sio kumhoji GSM ambaye kimsingi Inawezekana aliwaambia anataka nini ili awe mdhamini mwenza.

Hebu km una akili waulize Bodi ya ligi kazi zao ni zipi? Au nikupanga ratiba?, Ujinga wako na chuki kwa aliyekizidi maendeleo zinakufanya uwaze kijinga sana.
 
Maswali yako kiasi Fulani ni magumu kujibika kwa sababu hatuwezi kuyajibu bila ya kuuona huo mkata waliokubaliana Kati ya GSM na TFF. Ila vijilabu vidogo bongo vinanjaa ya kijinga sana, ilkuwaje wakae kando kuhusu makubaliano ya mkataba na kuja kukubali kuutekeleza?
 
Terms of conditions zinapofeli ndipo temination of conduct inatokea. Huenda walikubaliana ila baadhi ya mambo yafanyike under a certain time na huo mda umefika bila kutekeleza. Kila mkataba huwa na If
Sawa unakua na if. Kwaupande mmoja ua kwa pande zote mbili
 
Sawa unakua na if. Kwaupande mmoja ua kwa pande zote mbili
[https://res]

MWENYEKITI wa Bodi ya Ligi Kuu Bara, Steven Mnguto, ameibuka na kusema licha ya wadhamini wenza Kampuni ya GSM kutangaza kujiondoa katika udhamini lakini hakuna klabu yoyote iliyolipwa.


Kauli hiyo imekuja ikiwa ni siku moja tangu GSM watangaze kujiondoa kudhamini klabu za ligi ambazo awali waliingia mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya Sh 2.1Bil.


Akizungumza na Championi Jumatano, Mnguto alisema kuwa, hilo suala wamepanga kulizungumza hivi karibuni
mara baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) watakapokutana.


Mnguto alisema kuwa, wanasubiria wanasheria wao walipitie suala hilo na mwisho wa siku watalitolea ufafanuzi
kwa undani.


“Kiukweli tangu tuliposaini mkataba na GSM nikiri klabu hazijapata chochote. Klabu zimeitangaza GSM kwa muda wa miezi mitatu sasa, kwa hiyo tunasubiri wanasheria walipitie suala hilo tujue tunafanyaje.

“Hata suala la zile nembo kwenye mabega sijui kama zinaweza kutolewa haraka lakini hata hilo litafanyiwa
kazi kisheria,” alisema Mnguto.

Naye Mkurugenzi wa Habari na Masoko wa TFF, Boniface Wambura, akizungumzia hilo alisema: “Sisi
baada ya kupata barua kutoka GSM, suala la mkataba ni Bodi ya Ligi na ni vema akatafutwa Mnguto lakini
kwa upande wa sisi TFF hatuwezi kuzungumzia kila jambo.


“Tayari tumetoa tamko letu jana (juzi) kuhusiana na hilo baada ya kupata barua GSM.” Juzi TFF ilitoa taarifa
kuwa, Februari 7, mwaka huu walipokea barua ya kuvunja mkataba wa udhamini mwenza wa Ligi Kuu Bara
ya NBC kutoka Kampuni ya GSM, hivyo Shirikisho hilo linafanyia kazi barua hiyo na litatoa taarifa kwa wadau.
 
The super jiniasi nimependa hapa, "kwani kwa sasa mna taabu ya Pesa (Uchumi wenu) umeyumba kidogo na Magodoro yenu Magumu kama Matofali ya Kampuni ya [ color=red]Strabag hayanunuliki tena."
Hivi kuna matofali magumu kama ya Strabag kweli!!!????
 
Kunywa maji kwanza ili upooze huo mzuka uliopanda,halafu ujifunze kuandika.
... ujui ni hujui.
... ata ni hata.
... ndo ni ndio.
... alafu ni halafu.
... unapoferi ni unapofeli.
... automaicaly ni automatically
... ayo ni hayo.
... ayawahusu ni hayawahusu.
 
Tff alisema ligi Ina timu 16 ambazo zitavaa logo na kuweka mabango viwanjani wakati wa mechi zao, kumbe walidanganya Wana timu 15 TU zitakazovaa logo na kuweka mabango ya GSM kwenye mechi zao. Uongo huu ndio ulioadhibiwa na GSM. Hivyo TFF atalazimika kuilipa GSM na timu 15 zilizovaa logo na kuweka mabango.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…