el nino
JF-Expert Member
- Nov 5, 2013
- 4,712
- 5,058
Nadhani watu wengi tunakumbuka ile Barcelona ya 2009-2012 ambayo kwa wengi ni timu bora kabisa katika kizazi hiki cha soka, kuanzia ugawaji wa vipigo,kandanda safi na uwezo binafsi wa wachezaji.
Wakati Guardiola akiiongoza Barcelona kugawa vichapo vya hatari hadi kumtetemesha mzee wetu Ferguson kwenye fainali ya Uefa 2011 wengi walikuwa wanammbeza kwa kusema anacheza ligi ya timu 2, ooh mara kabebwa na messi, wengine wakasema ana bahati.
Guardiola akaondoka zake kwenda Bundesliga, huko nako akagawa vichapo vya kutosha, ila wadau wa England wakaendelea kumponda kuwa anaiogopa England maana sio size yake [emoji23](wakajisahaulisha kilichokuwa kinazikumba timu za England zilipokutana na Barcelona).
Haya sasa , mara Guardiola akaja hapo England, ni kweli msimu wa kwanza hakufanya vizuri ila wadau wa England wakatamba sana eti alidhani yupo la liga au ligi nyingine nyepesi, hii ndio England bwana, timu zote kali!!!!
Msimu wake wa pili, akaanza kwa kasi ndogo, wakaongea sana,alipoanza kugawa vichapo wakasema ngoja tumuone, hawezi fika mbali hii ndio England, mara kashinda game 10 mfululizo, akashinda nyingine 5(still counting), humo kagawa vichapo na kuupiga mpira mwingi mno ikiwemo nyumbani kwa timu vigogo kama Man untd na chelsea.
Sasa hivi England ni ligi ya timu moja tuu, Man city imegeuka kama msalaba wa jumuiya ambao unapita kila nyumba, Guardiola hajawahi kuwa na timu iliyokusanya pointi nyingi hivi ndani ya mechi 16 za kwanza, cha kushangaza huku ambapo Guardiola anajipigia tuu watu ndio tunaambiwa ni ligi ngumu lakini kule ambapo alikuwa na timu ya Dunia alikuwa hashindi hivi tunaambiwa ile ligi ni mbovu/rahisi.!!
Kinachotokea sahizi si kingine bali ni E.P.L kuumbuka, tayari Pep amejipigia vigogo wote wa E.P.L wengine kwa aibu ya goli 5....,tungojee mwisho wa msimu tuone mambo yatakuwaje ila nina uhakika Man city watachukua ubingwa
Wakati Guardiola akiiongoza Barcelona kugawa vichapo vya hatari hadi kumtetemesha mzee wetu Ferguson kwenye fainali ya Uefa 2011 wengi walikuwa wanammbeza kwa kusema anacheza ligi ya timu 2, ooh mara kabebwa na messi, wengine wakasema ana bahati.
Guardiola akaondoka zake kwenda Bundesliga, huko nako akagawa vichapo vya kutosha, ila wadau wa England wakaendelea kumponda kuwa anaiogopa England maana sio size yake [emoji23](wakajisahaulisha kilichokuwa kinazikumba timu za England zilipokutana na Barcelona).
Haya sasa , mara Guardiola akaja hapo England, ni kweli msimu wa kwanza hakufanya vizuri ila wadau wa England wakatamba sana eti alidhani yupo la liga au ligi nyingine nyepesi, hii ndio England bwana, timu zote kali!!!!
Msimu wake wa pili, akaanza kwa kasi ndogo, wakaongea sana,alipoanza kugawa vichapo wakasema ngoja tumuone, hawezi fika mbali hii ndio England, mara kashinda game 10 mfululizo, akashinda nyingine 5(still counting), humo kagawa vichapo na kuupiga mpira mwingi mno ikiwemo nyumbani kwa timu vigogo kama Man untd na chelsea.
Sasa hivi England ni ligi ya timu moja tuu, Man city imegeuka kama msalaba wa jumuiya ambao unapita kila nyumba, Guardiola hajawahi kuwa na timu iliyokusanya pointi nyingi hivi ndani ya mechi 16 za kwanza, cha kushangaza huku ambapo Guardiola anajipigia tuu watu ndio tunaambiwa ni ligi ngumu lakini kule ambapo alikuwa na timu ya Dunia alikuwa hashindi hivi tunaambiwa ile ligi ni mbovu/rahisi.!!
Kinachotokea sahizi si kingine bali ni E.P.L kuumbuka, tayari Pep amejipigia vigogo wote wa E.P.L wengine kwa aibu ya goli 5....,tungojee mwisho wa msimu tuone mambo yatakuwaje ila nina uhakika Man city watachukua ubingwa