Gwajima anawakilisha lile kundi linalotaka kumkwamisha Mama kuongoza nchi, hili la Chanjo ni kisingizio tu

Gwajima anawakilisha lile kundi linalotaka kumkwamisha Mama kuongoza nchi, hili la Chanjo ni kisingizio tu

mngony

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2012
Posts
5,555
Reaction score
6,972
Tunakumbuka kuwa kulikuwa kuna fununu za jitihada za kutaka Mama asishike usukani baada ya Mzee kufariki, na hali hiyo ilichangia kuchelewa kutangawaza kifo cha Mzee mpaka pale Mkubwa wa Mapiganaji wetu alivyoingilia kati

Tunakumbuka wakati wa mazishi ya Mzee kule kijijini Mkubwa wa Mapiganaji alimwambia Mama Wapiganaji wetu wanaahidi utii kwake kama Mkubwa wetu na akamwambia ana dokezo la siri atampa wakiwa wawili tu

Ni wazi lile kundi au Genge halikuishia hapo, tulianza kusikia fununu za kutaka kutenganisha kofia ya Ukuu wa Chama na Nchi katika jitihada za kumkwamisha Mama kutawala.

Kundi/Genge hilo linaongozwa na wabunge wakiwemo Gwajima, walianzia Bungeni katika kile kilichoonekana kulinda utendaji wa Mzee, mpaka pale Mama alipotamka kuwa wanapoteza muda kubishana kwa mambo yasiyo ya msingi.

Matukio ya mifumo ya umeme kama lile la luku, moto soko kariakoo ambalo linahudumia sehemu kubwa wananchi na yanayofanana na hayo ni moja tu viashiria vya hujuma

Baada ya majaribio ya kihaini kushindwa kwa sasa, wanachofanya sasa ni kumkwamisha katika kuongoza kwa kumtanguliza mtu mwenye ujasiri na uzoefu wa kuropoka lakini pia mwenye platform ya kuongea kila mara, mtu anayezua utata ambaye akiongea atasikika na wengi, naye ni Gwajima ambaye ana nafasi kuongea kila Jumapili

Ndio kama Raia ana haki ya kutoa maoni,mawazo, dukuduku au ushauri kama Raia anayewajibika lakini ukiangalia namna ya uwasilishaji wake unagundua hana nia hiyo kama Raia anayewajibika bali ni 'vita binafsi' na Mkubwa wa nchi

Maneno kama " utaona kesho au kesho kutwa wanachanja, hizo ni feki MWAMBIENI ACHANJE ZOTE MILIONI MOJA ALIZOAGIZA"

" Hizo chanjo wanawataka mchanje kwa sababu WAMESHAKULA HELA ZA JUU wapewa pesa"

Hizo ni tuhuma, kejeli na kashfa za moja kwa moja, ni wazi wamemtanguliza front na watakuja wengine

Ukiangalia ni kwamba anamshambulia Mama sio Serikali, na hili suala chanjo ni moja tu uwanja wa MAPAMBAMO YA LILE KUNDI/GENGE DHIDI YA MAMA, haitoshia kwenye chanjo tu watakuja na kwengine lengo ni kumkwamisha na kuhakilisha 2025 wanaweka mtu wa lile kundi kama walivyotaka wao kipindi kile kabla ya kufeli.

Gwajima ni kifaranga tu, atafutwe Mama aliyempandisha kwenye chungu

Tumevuka salama kama Taifa kipindi kigumu lakini bado watu wanataka kuliingiza taifa katika mtanziko, HUU NI UHANI

MAMA umezungukwa na wengi wa hilo genge, chukulia mfano baada ya ile kaichanganya jamii na kuleta sintofahamu tulitarajia Waziri wa Afya, Katibu Mkuu wake kuongea chochote badala yake wanaongea watu wa mtaani wakina Kambakamba na Vigwangala, wasaidizi wako wamekususia hawako na wewe

Nije kwenye chanjo, serikali ilishasema sio lazima ni hiari, zimekuja chanjo tofauti mtu achague, Kama tunawasiwasi na Wazungu na Wamarekani kuna chanjo za jamaa zetu URUSI, CHINA, CUBA na hata INDIA

Haikutakiwa kuwa mjadala na kushutumu viongozi, unaweza ukawaambia watu wako wasichome ukawapa sababu, lakini kuna makundi kama vile wanafunzi wanaosoma nje, wafanyabiashara, wanaokwenda kufanya kazi nje, na hata wanaokwenda kweye ibada kuhiji Israel, Makkah hata Vatican huko ni lazima chanjo. Sasa utawanyima vipi haki yao hawa? Mwaka huu ndugu zetu Waislam wengi wamekosa ibada ya hija kwa kutokuwa na chanjo

USHAURI KWA CHAMA TWAWALA, Msimfukuze uanachama na muacheni na ubunge wake, hilo ndilo analitaka litokee yeye na waliomtuma kwa namna anavyotenda, ni makusudi kabisa ni calculated movement
 
Ningekuwa mwenyekiti wa CHAMA ningemgukuza GWAJIMA...ningemfuta UANACHAMA......

Mambo aliyofanya huyo jamaa si ya kuvumilika ...si ya kuvumiliwa haswa.....

#SiempreCCM
#HastaLaVictoriaTanzania
#UtiiNiLazima
 
Ningekuwa mwenyekiti wa CHAMA ningemgukuza GWAJIMA...ningemfuta UANACHAMA......

Mambo aliyofanya huyo jamaa si ya kuvumilika ...si ya kuvumiliwa haswa.....

#SiempreCCM
#HastaLaVictoriaTanzania
#UtiiNiLazima
Hapana hilo lisifanyike maana ndio anachotaka
 
Hapana hilo lisifanyike maana ndio anachotaka
Lifanyike tu mkuu wangu....

Hakutokuwa na madhara yoyote....

CCM iliwahi kuwafukuza nguli wake kama Augustine Mrema ,Hayati Maalim Seif Sharrif Hamad wakakimbilia UPINZANI.....

Mh.Gwajima hana kaliba yoyote ya kisiasa kuwazidi hao......

UKIUTAKA UGOMVI WA MAWE USIISHI NYUMBA YA VIOO

HASHTAG GWAJIMA afukuzwe CCM

#GwajimaAfukuzweCCM
 
So tunakumbuka kuwa kulikuwa kunafununu za jitihada za kutaka Mama asishike usukani baada ya Mzee kifariki, na hali hiyo ilichangia kuchelewa kutangawaza kifo cha Mzee mpaka pale Mkubwa wa Mapiganaji wety alivyoingilia kati

Sote tunakumbuka wakati wa mazishi ya Mzee kule kijijini Mkubwa wa Mapiganaji alimwambia Mama jeshi linaahidi utii ana akamwambia anadokezo la siri

Ni wazi lile kundi au Genge halikuishia hapo, tulianza kusikia fununu za kutaka kutenganisha kofia ya Ukuu wa Chama na Nchi katika jitihada za kumkwamisha Mama yetu kutawala.

Kundi/Genge hilo linaongozwa na wabunge wakiwemo Gwajima, walianzia Bungeni katika kile kilichoonekana kulinda utendaji, mpaka pale Mama alitamka kuwa wanapoteza muda kubishana kwa mambo yasiyo ya msingi.

Matukio ya mifumo ya umeme kama lile la luku, moto soko kariakoo ambalo linahudumia sehemu kubwa wananchi na yanayofanana na hayo ni moja tu viashiria vya hujuma

Baada ya majaribio ya kihaini kushindwa kwa sasa, wanachofanya sasa ni kumkwamisha katika kuongoza kwa kumtanguliza mtu mwenye ujasiri na uzoefu wa kuropoka lakini pia mwenye platform ya kuongea kila siku, mtu anayezua utata ambaye akiongea atasikika na wengi, naye ni Gwajima ambaye ana nafasi kuongea kila Jumapili

Ndio kama Raia ana haki ya kutoa maoni,mawazo, dukuduku au ushauri kama Raia anayewajibika lakini ukiangalia na ya uwasilishaji wake unagundua hana nia hiyo kama Raia anayewajibila bali ni 'vita binafsi' na Mkubwa wa nchi

Maneno kama " utaona kesho au kesho kutwa wanachanja, hizo ni feki MWAMBIENI ACHANJE ZOTE MILIONI MOJA ALIZOAGIZA"

" Hiziochanjo wanawataka mchanje kwa sababu WAMESHAKULA HELA ZA JUU wapewa pesa"

Hizo ni tuhuma, kejeli na kashfa moja kwa moja, ni wazi wamemyanguliza front na watakuja wengine

Ukiangalia ni moja kwa moja anamuattack Mama sio Serikali, na unagundua suala chanjo ni moja tu uwanja wa MAPAMBAMO YA LILE KUNDI/GENGE DHIDI YA MAMA, haitoshia kwenye chanjo tu watakuja na kwengine lengo ni kumkwamisha na kuhakilisha 2025 wanaweka mtu wa lile kundi kama walivyotaka wao kipindi kile kabla ya kufeli.

Gwajima ni kifaranga tu, atafutwe Mama aliyempandisha kwenye chungu

Tumevuka salama kama Taifa kipindi kigumu lakini bado watu wanataka kuliingiza taifa katika mtanziko, HUU NI UHANI

Kwa kumalizia tu MAMA umezungukwa na wengi wa hilo genge, chukulia mfano baada ya ile kaichanganya jamii na kuletr sintofahamu tulitarajia Waziri wa Afya, Katibu Mkuu wake kuongea chochote badala yake wanaongea watu wa mtaani wakina Kambakamba na Vigwangala, wasaidizi wako wamekususia hawako na wewe

Nije kwenye chanjo, serikali ilishasema sio lazima ni hiari, zimekuja chanjo tofauti mtu achague, Kama tunawasiwasi na Wazungu na Wamarekani kuna chanjo za jamaa zetu URUSI, CHINA, CUBA na hata INDIA

Haikutakiwa kuwa mjadala na kushutumu viongozi, unaweza ukawaambia watu wako msichome ukawapa sababu, kuna makundi kama vile wanafunzi wanaosomanje, wafanyabiashara, wanaokwenda kufanya kazi nje, na hata wanaokwenda kweye ibada kuhiji Israel, Makkah hata Vatican huko ni lazima chanjo. Sasa utawanyima vipi haki yao hawa?

USHAURI KWA CHAMA TWAWALA, Msimfukuze uanachama muacheni na ubunge wake, hilo ndilo analitaka litokee yeye na waliomtuma.

Mama alishasema chanjo ni hiari. Sasa anakwamishwaje hapo?

Na leo amechanja kwa hiari yeye na watu wengine

 
Hakuna atakayeuza wala kununua bila huu mhuri wa COVID 19


Ufunuo wa Yohana 13​

Mnyama kutoka Baharini​

1 Kisha niliona mnyama mwenye pembe kumi na vichwa saba akipanda kutoka baharini. Kila pembe yake ilikuwa na taji. Alikuwa na kumkufuru Mungu lililoandikwa kwenye kila kichwa.
2 Mnyama huyu alionekana kama chui, miguu yake ilikuwa kama ya dubu. Mdomo wake ulikuwa kama wa simba. Joka akampa huyo mnyama uweza wake wote, kiti chake cha enzi na mamlaka kuu.

3 Kichwa kimoja cha mnyama kilionekana kama kimejeruhiwa na kuuawa, lakini kidonda cha mauti kilipona. Watu wote ulimwenguni walishangaa, na wote walimfuata mnyama.
4 Watu waliliabudu joka kwa sababu limempa nguvu mnyama, na pia walimwabudu mnyama. Waliuliza, “Nani ana nguvu kama mnyama? Nani anaweza kufanya vita dhidi yake?”

5 Mnyama aliruhusiwa kujigamba na kumtukana Mungu na kutumia nguvu zake kwa miezi arobaini na mbili.
6 Mnyama alifungua kinywa chake ili amtukane Mungu, alitukane jina lake, mahali anapoishi, na wale wote wanaoishi mbinguni.
7 Alipewa uwezo wa kufanya vita na watakatifu wa Mungu na kuwashinda. Alipewa uwezo juu ya kila kabila, asili, lugha na taifa.
8 Kila anayeishi duniani angemwabudu mnyama. Hawa ni watu wote ambao majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwanakondoo tangu mwanzo wa ulimwengu. Mwanakondoo ndiye yule aliyeuawa.

9 Kila mtu anayesikia mambo haya azingatie hili:

10 Yeyote ambaye ni lazima awe mfungwa,
atakuwa mfungwa.
Yeyote ambaye ni wa kuuawa kwa upanga,
atauawa kwa upanga.
Hii inamaanisha kwamba watakatifu wa Mungu lazima wawe na subira na imani.

Mnyama Kutoka Nchi Kavu​

11 Pia nikaona mnyama mwingine akija kutoka katika nchi. Alikuwa na pembe mbili kama kondoo, lakini anaongea kama joka.
12 Mnyama huyu alisimama mbele ya mnyama wa kwanza na kutumia nguvu ile ile ya mnyama wa kwanza. Alitumia nguvu hii kumfanya kila mtu aishiye duniani amwabudu mnyama wa kwanza. Mnyama wa kwanza ndiye mwenye jeraha la mauti lililopona.
13 Mnyama wa pili alifanya miujiza[a] mikuu. Alitengeneza hata moto ushuke kutoka mbinguni kuja duniani watu wakiangalia.

14 Mnyama huyu wa pili aliwadanganya watu wanaoishi duniani kwa kutumia miujiza ambayo amepewa uwezo wa kuifanya kwa ajili ya mnyama wa kwanza. Aliwaamuru watu kutengeneza sanamu ili kumheshimu mnyama wa kwanza, aliyejeruhiwa kwa upanga lakini hakufa bali akawa hai tena.
15 Mnyama wa pili alipewa uwezo wa kuipa uzima sanamu ya mnyama wa kwanza. Kisha kinyago kiliweza kuongea na kuamuru watu wote ambao hawakukiabudu wauawe.
16 Pia mnyama wa pili aliwaamuru watu wote, wakubwa na wadogo, matajiri na maskini, walio huru au watumwa, wawekewe alama kwenye mikono yao ya kulia au kwenye vipaji vya nyuso zao. 17 Hakuna ambaye angeweza kununua au kuuza bila ya kuwa na alama hii. (Alama hii ni jina la mnyama au namba ya jina lake.)

18 Kila mwenye uelewa anaweza kujua maana ya namba ya mnyama. Hili linahitaji hekima. Namba hii ni namba ya mtu. Nayo ni 666.
 
Ukiangali vizuri Gwajima na kundi lake ndio wanachotaka afukuzwe ili apambane vizuri
Wasiwasi wako anaweza kuidhuru CCM?!!

Wasiwasi wako anaweza kumdhuru kisiasa mh.SSH ?!!

Gwajima hana KALIBA HIYO....si kwa CCM......

GWAJIMA alikuwa MSHENGA aliyempeleka mh.Lowassa kwa mh.Mbowe....

CCM inamjua vyema tu kama "dalali"......

Ok mkuu AGREE TO DISAGREE👍
 
Wasiwasi wako anaweza kuidhuru CCM?!!

Wasiwasi wako anaweza kumdhuru kisiasa mh.SSH ?!!

Gwajima hana KALIBA HIYO....si kwa CCM......

GWAJIMA alikuwa MSHENGA aliyempeleka mh.Lowassa kwa mh.Mbowe....

CCM inamjua vyema tu kama "dalali"......

Ok mkuu AGREE TO DISAGREE👍
Kutoa onyo inatosha,anatakiwe apuuzwe. Hizi ni calculated movements, kama draft tu mtu anakupa kete moja au mbili unaliwa 3 au 4 na kingi anaingia inamrahisishia kupambana mchezoni

Kama unakubali dalali, je unadhani yeye hajui kuwa anahatatisua kufukuzwa na kupoteza milioni ngapi kwa miaka mi4? Maana yake kuna maslahi zaidi kwenye via yake kwani inalenga 2025.
 
Wasiwasi wako anaweza kuidhuru CCM?!!

Wasiwasi wako anaweza kumdhuru kisiasa mh.SSH ?!!

Gwajima hana KALIBA HIYO....si kwa CCM......

GWAJIMA alikuwa MSHENGA aliyempeleka mh.Lowassa kwa mh.Mbowe....

CCM inamjua vyema tu kama "dalali"......

Ok mkuu AGREE TO DISAGREE👍

Inahitaji utafiti kuhakikisha chanjo tunazopata ni salama

Na inahitaji ujasiri na maamuzi mgumu pia ili kuhakikisha kwamba tuzigomea hizi chanjo sababu mwisho wa siku huna chanjo huwezi cross boarder. Je, tuna huo uwezo wa kujifungia???

Mungu ibariki Tanzania Mungu mbariki rais wetu Samia Suluhu Hassan na wasaidizi wake wote
 
Back
Top Bottom