Habari Leo - Wasichana vyuo vikuu hufaulishwa kwa kuridhia ngono kwa wahadhiri


Umenena vema Mkuu!!
Ukweli utabaki kuwa ukweli...
Hata bahari ya damu haiwezi kuuzamisha ukweli...
Wahadhiri wetu jitakaseni, hasa vyuo vya serikali ndiyo kumejaa uoza wa rushwa ya ngono
 
Umenena vema Mkuu!!
Ukweli utabaki kuwa ukweli...
Hata bahari ya damu haiwezi kuuzamisha ukweli...
Wahadhiri wetu jitakaseni, hasa vyuo vya serikali ndiyo kumejaa uoza wa rushwa ya ngono

Nimeshtushwa hata vyuo ambavyo vilijijengea heshima vinavyoendeshwa na makanisa kama St. Augustine kuangukia kwenye kashfa hii. Nilielewa kama vyuo hivyo ndivyo vyenye kujenga mwelekeo wa kujali haki za msingi kwa wanavyuo na wahadhiri wao pamoja na kukuza maadili kwa wanafunzi na waadhiri kuwa wakufunzi wa kuigwa na vyuo vingine.
 
Ni kweli na halina ubishi lkn tutakutana kwenye soko la AJIRA
 

wote wanashawishiana hapa ifm kuna binti mmoja anaitwa violeth.ndosi anasoma it mwaka wa pili group b.alifanya mtihani supplimentally ya c progamming baada ya kuona jinsi madudu aliyofanya hachomokii yeye mwemyewe alimshawishi mwalimu akatembea naye sasa anasoma mwaka pili.mabinti wengi wanaendekeza starehe badara kusoma mwisho wasiku ni kujiregeza kwa waadhili
 
kama wanawake wanafaulu kwa kutembea na wahadhili,je wanaume wanafauluje?,na sio kwamba wasichana wengi hawapendi kujituma matokeo yake wanaangukia mikononi wa wahadhili walafi?
 
mwandishi uyu ameweka ukweli mtupu,wanaobisha watakuwa wana interest,au hawajapitia chuoni. Basi hata jiulizeni leo kwa nini wahadhiri leo kila anayetangaza ndoa ni kuwa anamuoa mwanachuo wa mwaka wa tatu au mhitimu wa chuo icho anakofundisha,ina maana uhusiano umeanza lini?je wale wanaolambwa na kutupwa ni wangapi?
 
Kwa wale waliopitia chuo watakubaliana kuwa kusoma ni kazi ngumu sana,mabinti wengi wakifika vyuo wanakuwa kama wamewehuka vile wanajiingiza kwenye mapenzi kwa kasi ya kutisha hata hao malecture uwa wanakula makombo make mabinti wengi wanakuwa wameharibika tayari,pindi mitihani inapofika mabinti wenyewe uwa wanajilegeza/kujitongozesha kwa malecture.

Anayebisha ufuska huu wa mabinti zetu tunaomba aende apige kambi ya masaa hata mawili tu kwenye vyuo vyetu aone jinsi mabinti wanavyofuatwa na kurudishwa kwa hiyo 'kazi',ni aibu tupu.
 
ni ukweli usiopingika....dada zetu wanatoa rushwa ya ngono sana ili wapate matokeo mazuri/wapewe mitihani...mifano tunayo sana tu hata pale UDSM
 
pia kwa chuo kama st joseph na sua wasichana hufaulishwa kwa sababu ya jinsia yao. Hata akiandika madudu ktk mtihani maksi anazo


Asante kwa observation nzuri! Mijitu mingine inafikiria kingonongono tu! Ndio maana kila kukicha wanawaona dada zetu waliofanikiwa eti wamefanikiwa kwa kutoa hongo ya ngono! Nimefarijika sana na jibu lako. Kauli za mwandishi hazina ishara hata moja ya utafiti, ni hisia tena zenye kuwatukana wahadhiri wanaoteseka kufundisha na kina dada wanaokazana kujiendeleza!
 


Hebu tutajie msichana au mhadhiri aliyewahi kukumbwa na hayo masahibu.
 
Hebu tutajie msichana au mhadhiri aliyewahi kukumbwa na hayo masahibu.

Hili ni suala nyeti kwa maana ya kulinda jina na heshima ya wahusika, si busara kufanya kama unavyofikiria kirahisi wewe kwa vile wengi wachangiaji hapa na hata mwandishi aliyefanya utafiti wanalinda taaluma ya kazi yao kwa kuhakikisha hawamharibii mtu heshima yake kutokana na kashfa hii. Tunachojadili hapa ni kuwatahadhalisha wahusika na pengine tunaweza kupata ushauri wa njia bora ya kuwanusuru hawa dada kutumia sehemu ya viungo vya miili yao kuwa kitega uchumi kwa wahadhiri kuwafaulisha masomo.
 
Hivi mwenye masomo 8 na lecturers tofauti tofauti, je wote atawapa rushwa ya ngono ili wamfaulishe?
 
my avatar says it all,nlipokuwa chuo fulani hapa bongo alikuja ticha fulani kutokea masomoni ambaye kiukweli alikuwa bado kijana.
Jamaa alikuwa anapenda ngono vibaya na madenti wa classes alizokuwa anafundisha. Darasani kwetu alikuwa anawapanga kama kawaida na mbaya zaidi walikuwa wanafahamiana na mwisho wa siku walikuwa wanafaurishwa kwa course alizokuwa anafundisha.
Wanaobisha hii kitu ama hawajawahi kuona au wanataka kuficha ukweli. The matter of fact hii issue ni kweli tupu na inafanyika kwenye vyuo vyetu hapa bongo.
 
pia kwa chuo kama st joseph na sua wasichana hufaulishwa kwa sababu ya jinsia yao. Hata akiandika madudu ktk mtihani maksi anazo


kaka uko sahihi kabisa 100 percent !mimi nimemaliza sua miaka 5 iliyopita, hiyo tabia imekubuhu na sasa hivi hali ni mbaya zaidi kwa sababu faculty nyingi zimeanza kuajiri vijana (tutor assistant/lecturers), hali ni mbaya nduguzangu!ukiwa na demu wako hapo na ikatokea jamaa naye anawafundisha na anamtaka, basi usipokuwa makini utapotezwa wewe mvulana au wote, but wasichana wengi huwakubari walimu hao malaya, mbali ya kwamba wengi wa hao walimu wameoa na baadhi yao wake zao wa ndoa nao wanasoma hapohapo. Nyakati mbaya zaidi huja pale mnapokuwa mwaka wa tatu na mnampoanza research maarafu kama sp. Hapo kama kwa huyo supervisor uko na msichana au wasichana basi we mvulana jiandae kusumbuliwa mnooo na huyo ticha mara kazi ovyo kaanze upya mara hujui kuandika heading ya research yako! Lakini kwa wasichana kwao mambo ni safi tu! Mfano halisi,ni darasa langu lilikuwa na wasichana 18 takribani wasichania 16 walikuwa na mahusiano na hao walimu. Mimi mwenye ni muhanga wa mada hii, nilipata usumbufu sana kumaliza research yangu kumbe huyo supervisor alikuwa na mahusiano na msichana(mpenzi) wangu. Alimtishia mambo mengi sana. So ni serious issue na tunapoelekea ni kupata wataalamu wabovu sana watakaoliangamiza taifa, anayebisha hii maada labda yeye ndio mojawapo ya hao walimu wa vyuoni wazinzi. Mfano halisi na wa mwisho, kuna jamaa yangu hivi sasa yuko udsm alitakiwa agraduate mwaka jana 2011 anarudia pepa alifelishwa na mwalimu kisa demu, ishu ilikuwa hot mpaka ilifika kwa mkandala. So mnao bisha labda hamjapita vyuo vya hapa bongo! Kwa mchezo wa hawa jamaa ukimwi utatumaliza, kwasababu wao wapo stagnant pale but kila mwaka wanafunzi wapya wanakuja na kuondoka, so piga hesabu kama ana ukimwi atakuwa amewaambukiza wangapi kwa miaka 20-30 atakayokuwa anafundisha hapo.
 

Nadhani huyu mwandishi ametumia lugha ya kueleweka kwamba ni baadhi ya wahadhiri na ni baadhi ya wanafunzi wanaokubaliana na hili. Hakumaanisha kwamba kila mwanachuo wa jinsia ya ke akifaulu basi ni kwa ajili ya mchezo huo mchafu.
Halafu kiuhalisia kwa tuliopoitia vyuo vikuu, kwani si kweli kwamba haya mambo yapo? Nani asiyefahamu kuhusu Sexual Transmitted Marks (STM)? Haya mambo yapo si vyuo vya serikali tu hata vyuo vya binafsi na tumekwishaona watu wanakamatwa (SUP) sababu labda ya kuwakataa wahadhiri ama kutembea na watu wao. Sioni haja ya kumnanga huyu mwandishi kwa vitu ambavyo vipo!
 
Naungana nawewe nduguyangu! Looh hari ni mbaya mbaya kuliko! wanaobisha hii maada sijui hata niwaambie nini, juzi tu hapa kuna mwalimu hapo mzumbe kafunga ndoa na mwanafunzi wake ambaye sasa ndio ameingia mwaka wa tatu! Swala la kujiuliza kama ulivyosema wameanza lini hayo mahusiano? kabla huyo ticha ya kumuoa huyo binti je amepita na wangapi? daaha INASIKITIKISHA INASIKITISHA SANA TUTAKWISHA, Coz hao mabinti ndio tulionao now maofisini na ndio watu tunawachumbia kuwaoa nakadhalika! Ninamifano mingi sana ya hii maada na mimi mwenyewe nikiwa muhanga, huyo ticha mwingine aliyefanya huo upuuzi yuko sua hapo faculty of science! hawana maana kabisa hawa walimu wasio jiheshimu na ndoa zao!
 
Mbona jengo na kilichoandikwa ndani havina uhusiano? Nimenagalia jengo lakini nasikia SUA, IFM, UD nk je hilo jengo liko kwenye hivyo vyuo? Je haya maswala kama yako hivi ina maana vyuo havina uongozi? Maana ninavyojua wahadhiri inabidi watumie muda mwingi kwenye research na siyo kufanya mambo kama haya.

Najua sheria za chuo mwadhiri akigundulika anafanya haya ni kufukuzwa chuo. Jamani inabidi serikali ifanye uchunguzi kama vyuo vyenyewe vimeshindwa kubaini watu hawa. Chuo ni tahaluma siyo mambo ya ngono.
 
Uko sahihi kaka, hata sua hapo sasa mambo si mambo kabisa karibu faculty zote ni hovyo wakiongozwa na faculty ambazo hazina hata prof mmoja! wamejaa vijana tu!. WASICHANA WANAFANYIWA RESEARCH KAMA KAWA! HAWA WALIMU WASIOHESHIMU TAALUMA ZAO WATATUUA NA UKIMWI!
 

Mkuu idara za ushauri na utetezi kwa wanafunzi zipo kiaina.

Vyuo vikuu vya umma hapa TZ vina ofisi za dean of students, ambapo kunakua na mshauri na mtetezi wa wanafunzi.
Ila kusema ukweli idara hizo siwezi kuzilinganisha na idara kama hizo kwa majuu (ambako kuna students counseling services za hali ya juu mno). Hata hivyo, idara hizi katika vyuo vyetu haziwezi kukwepa lawama katika matatizo kama haya; kwani hazifanyi kazi zake ipaswavyo licha ya kua na wataalamu wa masuala ya ushauri (counseling and guidance). Pia mfumo wa hizi idara katika vyuo vyetu haupo katika hali ya kuweza kweli kuwatetea wanafunzi pale wahadhiri wanapokua na hatia; kwani ni wahadhiri hao hao ndio wapo katika nafasi za maamuzi katika idara hizo. Hivyo inakua ni sawa na kesi dhidi ya ng'ombe kupelekwa ikaamuliwe na nyati!! Mfano ni kesi ya mhadhiri mmoja pale UD ambae anasifika sana kwa kuongea maneno machafu (matusi) darasani; kesi ilipelekwa na masista ambao hawakufurahishwa na mwenendo wa mhadhiri huyo. Kesi ilifika kwa nyati, nyati na ng'ombe wakaelewana na kupeana madongo ya hapa na pale. Kisha mhadhiri huyo alirudi darasani na kujitapa kwamba anawashangaa hao walioenda kumshtaki; na aliendelea na tabia yake hadi kesho!!

Pia kuna jambo jingine ambalo hata wakuu humu wameligusia; nalo ni kuwepo kwa wanafunzi ambao wanatumia kila mbinu ili kuwa tempt wahadhiri katika kufanya ngono kwa manufaa ya kufaulu. Na wakati mwingine kuna extreme cases ambapo wanfunzi hao wameweza hata kutengeneza scenarios za kubakwa ili kuwa tempt wahadhiri wawepe maksi nzuri. Mifano ipo mingi sana; pale UD kuna wahadhiri watatu ambao walishakumbwa na visa vya kusingiziwa wamebaka wanafunzi (kusingiziwa na wanafunzi wanao claim kubakwa). Mmoja wa kitivo cha sheria, mwingine wa kitivo cha elimu na mwingine kitengo cha Archaeology

Kuna mwanafunzi mmoja wa shahada ya pili (alikua dada kutoka nchi moja ya Afrika Magharibi), kwa mujibu wa supervisor wake, huyo dada alikua academically weak. Hivyo alikua akipata shida kuweza kuandika chapisho (thesis) lake vyema; basi katika kuweza kutafuta njia za mkato, huyo dada pamoja na mhadhiri mmoja wa kike katika kitengo hicho hicho alicho supervisor wake, wakapanga kutengeneza scenario ya kubakwa. Yule mhadhiri wa kike ana ofisi katika floor moja na ilipo ofisi ya supervisor wa yule dada, ingawa kuna ofisi kama nne kati ya ofisi zao. Basi katika zoezi hilo, dada alienda katika ofisi ya supervisor wake katika kujaribu kumshawishi supervisor alegeze kamba juu ya chapisho lake; kwa mujibu wa supervisor huyo, yeye alikataa, ndipo dada akararua nguo zake na kupiga kelele kwamba anabakwa. Na mtu aliesikia kelele hizo ni yule mhadhiri alie ofisi kama ya tano kutoka ofisi ya supervisor, yeye ndie alikua wa kwanza kuja kwenye eneo la tukio. Na yeye ndie akawa shahidi wa dada yule!! Basi maskini mhadhiri wa watu akawa suspended akisubiri kesi kusikilizwa. Wakati wa kesi, watu wenye common sense wakauliza ilikuaje mtu alie na ofisi mbali vile asikie kelele za mtu kubakwa ilhali kulikua na watu wenye ofisi karibu ambao hawakusikia kelele hizo!?! Basi badae mdada alikuja kukiri na kusema namna walivyopanga na mhadhiri yule wa kike.

Pia pale kitivo cha sheria; kwa wale waliopita UD wanajua namna gani wahadhiri wa sheria wanavyobania maksi. Basi kuna mdada moja nae alitengeneza scenario ya kubakwa; alienda kwenye ofisi ya mhadhiri mmoja kudai apewe maksi nzuri, mhadhiri akagoma. Basi binti alifunga mlango na kuweka funguo ndani ya brassiere, akararua nguo yake ya juu na kuanza kupiga kelele za kubakwa; watu kusikia kelele, wakaja na kukuta mlango umefungwa na binti funguo katia chobisi!! Sasa kwa hali hiyo kweli mpaka huyo mhadhiri akaaminiwe si itakua kazi!! Pia ni udharirishaji wa hali ya juu kwa mhadhiri ambae ana sifa, familia na marafiki!!

Kwa hiyo mkuu, wakati mwingine wanafunzi ndio uwa wakorofi na wanajaribu kila mbinu ya kuwawezesha kupata maksi nzuri. Njia ya kuepusha scenarios kama hizo ni kuwa na umakini katika namna ya kudeal na watoto wa kike. Kwa mfano, Palamagamba pale UD ana utaratibu wa kwamba, daima haachi funguo katika mlango wake akiwa ofisini na pia endapo binti anashida ya kuja ofisini kumwona, ni aidha aje na mwenzake (yaani wawe wawili). Na hii ni kutokana na aibu aliyoipata mhadhiri mwenzake.

Kwa upande mwingine wa shilingi; ni kweli kuna wahadhiri ambao wanawashawishi mabinti katika kufanya nao ngono ili wapate maksi nzuri. Pale SUA kuna profesa mmoja alikua na mchezo huo sana, kiasi kwamba kukawa na utani kwamba, binti yeyote atakaeitwa na huyo profesa ofisini kwake, basi ajiandaa kabisa kwa kubeba condom!! Pia UDOM kuna kesi za wahadhiri kuitwa shemeji na wanafunzi kutokana na wao kutembea na wanafunzi wa kike!! Hadi kuna mhadhiri mmoja nasikia aliandikiwa barua na wanafunzi wa kike (barua zilisambazwa kila ofisi!!) kutokana na tabia yake ya kutembea nao.

Kwa hiyo mkuu licha ya hizo case mbili, kuna haja ya kufanyika utafiti wa kina kabisa (nashangaa watu wanaosoma sociology au psychology wanasubiri nini hapa!!) katika kutafuta ukweli wa jambo hili. Pia kuna haja ya idara za ushauri na utetezi wa wanafunzi kuongozwa na watu wasio wahadhiri (watu watakao kua neutral).
 

Haina hata haja ya uchunguzi hii. Iko wazi sana, hata km mletamada asingeileta hapa, bado hatuwezi kupinga ukweli kuwa, haya mambo yapo.

Ma lectures na ma dean of faculty wanafanya haya mambo sana sana.

Cha muhimu hapa ni wadada kusimama kidete na kusimamia misimamo na kuungana pamoja kuona wanafanyaje kulitokomeza hili.
Though wadada wengine wanapenda na wanaona sawa tu.
Mimi kaka yangu walimdisco, hakujua sbb bcz alikuwa vizuri, baadae ndo anakuja kuambiwa yule binti uliyekuwa ukiandamana nae ni chakula cha lecturer, too late
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…