Habib Halahala: Mwandishi wa habari wa Rais Nyerere na Rais Mwinyi aliyefariki kifo kibaya

Habib Halahala: Mwandishi wa habari wa Rais Nyerere na Rais Mwinyi aliyefariki kifo kibaya

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Habib Halahala alichaguliwa kuwa mwandishi wa habari na mpiga picha wa Rais Nyerere mwishoni mwa utawala wa Rais Nyerere kwenye miaka ya 1980.

Ilipofika mwaka 1985, Mwl Nyerere aling'atuka ofisini kama Rais wa kwanza wa Tanzania mara baada ya takribani miongo miwili na robo madarakani.

Habib Halahala aliendelea na majukumu yake ya uandishi wa habari katika awamu ya pili ya Rais Ali Hassan Mwinyi. Moja ya sifa ya yeye kuendelea ni uchapaji wake kazi mzuri uliomvutia Rais Mwinyi.

Mwanzoni mwa miaka 1990, Nchi ikakumbwa na mafuriko makubwa sana na kusababishaathari kubwa sana kwa wananchi hasa kusini mwa Tanzania.

Ikabidi Rais Mwinyi afanye ziara kuangalia athari hizo huku akitumia ziara hiyo kama sehemu ya kuwafariji wananchi waliokumbwa na kadhia ya mafuriko.

Siku ya ziara ilipofika, Rais Mwinyi alitumia usafiri wa helikopta, kuelekea kusini mwa Tanzania, katika msafara huo alikuwepo pia ndugu Habib Halahala. Walipofika eneo la tukio, Helikopta ilipotua tu, miongoni mwa watu wa mwanzo kushuka ni Habib Halahala, aliwahi kushuka ili kupiga picha ya Rais akishuka kwenye helikopta hiyo.

Bahati mbaya wakati anashuka panga za helikopta bado zilikuwa zinazunguka kwa kasi, bila kujua Habib Halahala hakuinamisha kichwa lile panga la helikopta likapita nae kwenye shingo. Akafariki kifo kibaya cha maumivu makubwa sana.

Nimeona niilete leo jukwaani kwa faida ya kizazi hiki ambao wengi wao hawamfahamu wala hawakuwahi kusikia tukio hilo...wasalaaam

Pia soma - Nini chanzo cha kifo cha Habibu Halahala aliyekuwa mpiga picha wa Hayati Mwalimu Nyerere?

476CF57D-4932-4CFC-8A2E-BB574612ADA2.jpeg
 
Habib Halahala alichaguliwa kuwa mwandishi wa habari na mpiga picha wa Rais Nyerere mwishoni mwa utawala wa Rais Nyerere kwenye miaka ya 1980.

Ilipofika mwaka 1985, Mwl Nyerere aling'atuka ofisini kama Rais wa kwanza wa Tanzania mara baada ya takribani miongo miwili na robo madarakani.

Habib Halahala aliendelea na majukumu yake ya uandishi wa habari katika awamu ya pili ya Rais Ali Hassan Mwinyi. Moja ya sifa ya yeye kuendelea ni uchapaji wake kazi mzuri uliomvutia Rais Mwinyi.

Mwanzoni mwa miaka 1990, Nchi ikakumbwa na mafuriko makubwa sana na kusababishaathari kubwa sana kwa wananchi hasa kusini mwa Tanzania.

Ikabidi Rais Mwinyi afanye ziara kuangalia athari hizo huku akitumia ziara hiyo kama sehemu ya kuwafariji wananchi waliokumbwa na kadhia ya mafuriko.

Siku ya ziara ilipofika, Rais Mwinyi alitumia usafiri wa helikopta, kuelekea kusini mwa Tanzania, katika msafara huo alikuwepo pia ndugu Habib Halahala. Walipofika eneo la tukio, Helikopta ilipotua tu, miongoni mwa watu wa mwanzo kushuka ni Habib Halahala, aliwahi kushuka ili kupiga picha ya Rais akishuka kwenye helikopta hiyo.

Bahati mbaya wakati anashuka panga za helikopta bado zilikuwa zinazunguka kwa kasi, bila kujua Habib Halahala hakuinamisha kichwa lile panga la helikopta likapita nae kwenye shingo. Akafariki kifo kibaya cha maumivu makubwa sana.

Nimeona niilete leo jukwaani kwa faida ya kizazi hiki ambao wengi wao hawamfahamu wala hawakuwahi kusikia tukio hilo...wasalaaam

Pia soma - Nini chanzo cha kifo cha Habibu Halahala aliyekuwa mpiga picha wa Hayati Mwalimu Nyerere?

Nalikumbuka hili tukio tena kuna picha Alhaj Mwinyi kapigwa picha kashika kichwa kwa masikitiko picha ile ilikua kwny gazeti la Daily News
 
Nakumbuka baada ya hili tukio tukiwa watoto tulikuwa tukidanganyana kuwa feni la helicopter lina sumaku inayomvuta mtu juu akipita chini yake.
 
Habib Halahala alichaguliwa kuwa mwandishi wa habari na mpiga picha wa Rais Nyerere mwishoni mwa utawala wa Rais Nyerere kwenye miaka ya 1980.

Ilipofika mwaka 1985, Mwl Nyerere aling'atuka ofisini kama Rais wa kwanza wa Tanzania mara baada ya takribani miongo miwili na robo madarakani.

Habib Halahala aliendelea na majukumu yake ya uandishi wa habari katika awamu ya pili ya Rais Ali Hassan Mwinyi. Moja ya sifa ya yeye kuendelea ni uchapaji wake kazi mzuri uliomvutia Rais Mwinyi.

Mwanzoni mwa miaka 1990, Nchi ikakumbwa na mafuriko makubwa sana na kusababishaathari kubwa sana kwa wananchi hasa kusini mwa Tanzania.

Ikabidi Rais Mwinyi afanye ziara kuangalia athari hizo huku akitumia ziara hiyo kama sehemu ya kuwafariji wananchi waliokumbwa na kadhia ya mafuriko.

Siku ya ziara ilipofika, Rais Mwinyi alitumia usafiri wa helikopta, kuelekea kusini mwa Tanzania, katika msafara huo alikuwepo pia ndugu Habib Halahala. Walipofika eneo la tukio, Helikopta ilipotua tu, miongoni mwa watu wa mwanzo kushuka ni Habib Halahala, aliwahi kushuka ili kupiga picha ya Rais akishuka kwenye helikopta hiyo.

Bahati mbaya wakati anashuka panga za helikopta bado zilikuwa zinazunguka kwa kasi, bila kujua Habib Halahala hakuinamisha kichwa lile panga la helikopta likapita nae kwenye shingo. Akafariki kifo kibaya cha maumivu makubwa sana.

Nimeona niilete leo jukwaani kwa faida ya kizazi hiki ambao wengi wao hawamfahamu wala hawakuwahi kusikia tukio hilo...wasalaaam

Pia soma - Nini chanzo cha kifo cha Habibu Halahala aliyekuwa mpiga picha wa Hayati Mwalimu Nyerere?

Ahsante mkuu, binafsi sikuwah sikia ata ili jina.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pumzika kwa Amani Habib,

Kifo chake kilistua na kuhuzunisha sana.

Mara nyingi Helicopter kabla hujapanda uwa kuna elimu fulani inatolewa, kukupa ufahamu kwa jambo lolote ambalo linaweza kutokea ukiwa angani na hata baada ya kutua na namna utakavyoshuka haijalishi panga zinazunguka ama zimetulia.

Wakati wa kushuka ni muhimu kichwa kiwe kimeinama kama bado panga zinazunguka na uelekeo wako uwe sambamba na mlango wa kutokea ,usiende nyuma ni hatari kwa maisha yako.

Kilichotokea pale kwenye ajali nafikiri ni hiyo elimu ya ufahamu haijalishi una uzoefu kiasi gani kusafiri na helicopter , muhimu uwa ni kukumbushana kama ilivyo ada kwenye safari za angani nahisi hicho kitu hakikufanyika.
 
Pumzika kwa Amani Habib,

Kifo chake kilistua na kuhuzunisha sana.

Mara nyingi Helicopter kabla hujapanda uwa kuna elimu fulani inatolewa, kukupa ufahamu kwa jambo lolote ambalo linaweza kutokea ukiwa angani na hata baada ya kutua na namna utakavyoshuka haijalishi panga zinazunguka ama zimetulia.

Wakati wa kushuka ni muhimu kichwa kiwe kimeinama kama bado panga zinazunguka na uelekeo wako uwe sambamba na mlango wa kutokea ,usiende nyuma ni hatari kwa maisha yako.

Kilichotokea pale kwenye ajali nafikiri ni hiyo elimu ya ufahamu haijalishi una uzoefu kiasi gani kusafiri na helicopter , muhimu uwa ni kukumbushana kama ilivyo ada kwenye safari za angani nahisi hicho kitu hakikufanyika.
Naona helicopter za siku hizi panga zipo juu wameoona dosari hiyo
 
Bahati mbaya wakati anashuka panga za helikopta bado zilikuwa zinazunguka kwa kasi, bila kujua Habib Halahala hakuinamisha kichwa lile panga la helikopta likapita nae kwenye shingo. Akafariki kifo kibaya cha maumivu makubwa sana.
Weee!! mzee acha uongo!! japo ni kweli lkn tukio hilo halikuwa km unavyosema weye!!! ilikuwa hivi; wooote abiria akiwemo Rais na mkewe walikuwa wamesha shuka chini ya helikopita....

sasa yeye huyo mwandishi akataka kuchukua picha ya matukio flani ya tukio...........ameshikilia kamera yake kwa mbele hivi ......anarudi nyuma sasa ili apate focus nzuri!! kwa bahati mbaya sana

akawa amefikia usawa wa yale mapanga boi ya helikopita! yakamkata faster ... kumbuka ile helikopita haikuzima mpaka mwisho wa tukio!....

Mwinyi na Mama siti mwinyi walikuwa wanaangalia hilo tukio kwa msisimko mkubwa na picha ile ni hii hapa!! sasa swali km alikuwa wa kwanza kuteremka yeye Rais na Mkewe na wenginewe

walisisimuka vipi wkt bado wako ndani ya helikopita??
 
Ni ile Rotterblade ya nyuma ndio iliyoleta simanzi.

Alikuwa anataka angle nzuri
 
...Picha Nzuri Sana kuhusu hili Tukio in ilitolewa na Daily News ukurasa wa Mbele ikimuonyesha Raisi Ali Hassan Mwinyi amesimama na ameshikwa kichwa Kwa Mshituko na Majozi huku mama Siti Mwinyi, Mkewe, amemkumbatia kifuani akiwa na yeye ana Mshituko Mkuu!
Ni picha Nzuri Sana iliyopigwa dakika chache baada ya Habib kukatwa Kichwani na Pangaboi la Helicopter.
 
Back
Top Bottom