Hadi sasa Paul Makonda hajashitakiwa popote

Hadi sasa Paul Makonda hajashitakiwa popote

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Sakata la Mkuu wa Mkoa wa zamani wa Dar es Salaam, Paul Makonda lililopo Mahakamani limekuwa likiwatatiza wengi hasa baada ya awali kuonekana kwa wengi ni kama anaipotezea Mahakama kabla ya kujitokeza hivi karibuni kupitia mwanasheria wake.

Kupitia Kolamu ya Yakub Na Sheria inayoandikwa na Bashir Yakub, leo Jumanne Machi 8, 2022 anafafanua uhalisia wa nini kinachoendelea katika sakata hilo lilipo fika hadi sasa:

--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Hadi sasa Makonda hajashitakiwa popote

Kesi iliyo mahakamani dhidi ya Makonda si mashtaka ya jinai. Kilicho mahakamani mpaka sasa ni maombi tu ya Saed Ahmed Kubenea.

Wala Makonda hatafutwi kukamatwa na mahakama yoyote, wala taasisi nyingine ikiwamo Polisi. Nimeona hadi magazeti
yanayoheshimika yakisema Makonda ana jinai za kujibu mahakamani, mara anatafutwa kukamatwa, si kweli.

Ni hivi, Saed Ahmed Kubenea anaomba ridhaa ya kumshitaki Makonda. Kawaida ya sheria ni kuwa DPP (Mwendesha Mashtaka wa Serikali) ndiye mwenye mamlaka ya kushitaki na kuendesha kesi ya mtu yeyote aliyeonewa katika jinai
zote.

Anaendesha kesi za jinai kwa iaba ya raia au mtuu aliyeonewa ama aliyekosewa (aliyeibiwa, aliyeumizwa,
aliyebakwa nk).

Hata hivyo mtu binafsi anaweza pia kushitaki na kuendesha kesi yake ya Jinai mwenyewe bila kupitia kwa DPP.

Lakini ikiwa mtu binafsi atataka kuendesha kesi yake mwenyewe bila kupitia kwa DPP, basi anatakiwa
kuomba ridhaa ya Mahakama kwanza, kupitia maombi (application) maalumu, chini ya vifungu vya 99(13), 128(2), na
392A(1)2) vya Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai.

Haya maombi ya ridhaa ndiyo yaliyo mahakamani mpaka sasa na si jinai dhidi ya Makonda. Maana yake Kubenea anaomba ridhaa yeye kama yeye ili aweze kumshitaki Makonda.

Hiki ndicho kilicho mahakamanı. Kwa hiyo Kubenea anaweza akakubaliwa kumshitaki Makonda yeye kama yeye bila DPP ama akakataliwa. Na hiyo ni mpaka hapo hiyo Mahakama ya Kinondoni yalipo hayo maombi 1takapotoa uamuzi kuhusu
hilo.

Katika maombi hayo utamualika DCI, utamualika DPP na utamualika yule unayetaka kumshitaki, ambao nao kila mmoja kwa nafasi yake anaweza kujibu maombi kwa kupinga ama kukubali.

Na kwa haya maombi ya Kubenea, DCI na DPP tayarı wamejitokeza na kupinga asishitaki yeye kama yeye. Makonda hajajitokeza kujibu lakini kwa kuwa haya ni maombi tu (application), basi halazimishwi. Wanaruhusiwa kuendelea tu bila yeye kujibu ama kuwapo (exparte).

Ikiwa Kubenea atakubaliwa kumshitaki Makonda yeye kama yeye bila kupitia kwa DPP, basi hapo ndipo kesi ya jinai dhidi ya Makonda itaanza, na hapo sasa ni lazima Makonda kufika mahakamani atake asitake, na akikosa.

Kwa hiyo tuelewane kuwa mpaka sasa Makonda hana kesi yoyote ya jinai katika mahakama yoyote, wala hatafutwi kukamatwa.

------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Source: Jamhuri

Tumia hii.jpg
 
Sakata la Mkuu wa Mkoa wa zamani wa Dar es Salaam, Paul Makonda lililopo Mahakamani limekuwa likiwatatiza wengi hasa baada ya awali kuonekana kwa wengi ni kama anaipotezea Mahakama kabla ya kujitokeza hivi karibuni kupitia mwanasheria wake...
Nani wakujitolea kuifungua tafadhali.
 
Aombe muumba wake ili DPP asionyeshe nia kwa jambo hili pia DCI na yeye asitoe ushirikiano - vinginevyo aisee wahenga walishasemaga, mchwa kashambulia kamba......
 
Sakata la Mkuu wa Mkoa wa zamani wa Dar es Salaam, Paul Makonda lililopo Mahakamani limekuwa likiwatatiza wengi hasa baada ya awali kuonekana kwa wengi ni kama anaipotezea Mahakama kabla ya kujitokeza hivi karibuni kupitia mwanasheria wake.

Kupitia Kolamu ya Yakub Na Sheria inayoandikwa na Bashir Yakub, leo Jumanne Machi 8, 2022 anafafanua uhalisia wa nini kinachoendelea katika sakata hilo lilipo fika hadi sasa:

--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Hadi sasa Makonda hajashitakiwa popote

Kesi iliyo mahakamani dhidi ya Makonda si mashtaka ya jinai. Kilicho mahakamani mpaka sasa ni maombi tu ya Saed Ahmed Kubenea.

Wala Makonda hatafutwi kukamatwa na mahakama yoyote, wala taasisi nyingine ikiwamo Polisi. Nimeona hadi magazeti
yanayoheshimika yakisema Makonda ana jinai za kujibu mahakamani, mara anatafutwa kukamatwa, si kweli.

Ni hivi, Saed Ahmed Kubenea anaomba ridhaa ya kumshitaki Makonda. Kawaida ya sheria ni kuwa DPP (Mwendesha Mashtaka wa Serikali) ndiye mwenye mamlaka ya kushitaki na kuendesha kesi ya mtu yeyote aliyeonewa katika jinai
zote.

Anaendesha kesi za jinai kwa iaba ya raia au mtuu aliyeonewa ama aliyekosewa (aliyeibiwa, aliyeumizwa,
aliyebakwa nk).

Hata hivyo mtu binafsi anaweza pia kushitaki na kuendesha kesi yake ya Jinai mwenyewe bila kupitia kwa DPP.

Lakini ikiwa mtu binafsi atataka kuendesha kesi yake mwenyewe bila kupitia kwa DPP, basi anatakiwa
kuomba ridhaa ya Mahakama kwanza, kupitia maombi (application) maalumu, chini ya vifungu vya 99(13), 128(2), na
392A(1)2) vya Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai.

Haya maombi ya ridhaa ndiyo yaliyo mahakamani mpaka sasa na si jinai dhidi ya Makonda. Maana yake Kubenea anaomba ridhaa yeye kama yeye ili aweze kumshitaki Makonda.

Hiki ndicho kilicho mahakamanı. Kwa hiyo Kubenea anaweza akakubaliwa kumshitaki Makonda yeye kama yeye bila DPP ama akakataliwa. Na hiyo ni mpaka hapo hiyo Mahakama ya Kinondoni yalipo hayo maombi 1takapotoa uamuzi kuhusu
hilo.

Katika maombi hayo utamualika DCI, utamualika DPP na utamualika yule unayetaka kumshitaki, ambao nao kila mmoja kwa nafasi yake anaweza kujibu maombi kwa kupinga ama kukubali.

Na kwa haya maombi ya Kubenea, DCI na DPP tayarı wamejitokeza na kupinga asishitaki yeye kama yeye. Makonda hajajitokeza kujibu lakini kwa kuwa haya ni maombi tu (application), basi halazimishwi. Wanaruhusiwa kuendelea tu bila yeye kujibu ama kuwapo (exparte).

Ikiwa Kubenea atakubaliwa kumshitaki Makonda yeye kama yeye bila kupitia kwa DPP, basi hapo ndipo kesi ya jinai dhidi ya Makonda itaanza, na hapo sasa ni lazima Makonda kufika mahakamani atake asitake, na akikosa.

Kwa hiyo tuelewane kuwa mpaka sasa Makonda hana kesi yoyote ya jinai katika mahakama yoyote, wala hatafutwi kukamatwa.

------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Source: Jamhuri

View attachment 2143035
Asante kwa ufafanuzi.
Jaji ni yule Tiganga?
 
Sakata la Mkuu wa Mkoa wa zamani wa Dar es Salaam, Paul Makonda lililopo Mahakamani limekuwa likiwatatiza wengi hasa baada ya awali kuonekana kwa wengi ni kama anaipotezea Mahakama kabla ya kujitokeza hivi karibuni kupitia mwanasheria wake.

Kupitia Kolamu ya Yakub Na Sheria inayoandikwa na Bashir Yakub, leo Jumanne Machi 8, 2022 anafafanua uhalisia wa nini kinachoendelea katika sakata hilo lilipo fika hadi sasa:

--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Hadi sasa Makonda hajashitakiwa popote

Kesi iliyo mahakamani dhidi ya Makonda si mashtaka ya jinai. Kilicho mahakamani mpaka sasa ni maombi tu ya Saed Ahmed Kubenea.

Wala Makonda hatafutwi kukamatwa na mahakama yoyote, wala taasisi nyingine ikiwamo Polisi. Nimeona hadi magazeti
yanayoheshimika yakisema Makonda ana jinai za kujibu mahakamani, mara anatafutwa kukamatwa, si kweli.

Ni hivi, Saed Ahmed Kubenea anaomba ridhaa ya kumshitaki Makonda. Kawaida ya sheria ni kuwa DPP (Mwendesha Mashtaka wa Serikali) ndiye mwenye mamlaka ya kushitaki na kuendesha kesi ya mtu yeyote aliyeonewa katika jinai
zote.

Anaendesha kesi za jinai kwa iaba ya raia au mtuu aliyeonewa ama aliyekosewa (aliyeibiwa, aliyeumizwa,
aliyebakwa nk).

Hata hivyo mtu binafsi anaweza pia kushitaki na kuendesha kesi yake ya Jinai mwenyewe bila kupitia kwa DPP.

Lakini ikiwa mtu binafsi atataka kuendesha kesi yake mwenyewe bila kupitia kwa DPP, basi anatakiwa
kuomba ridhaa ya Mahakama kwanza, kupitia maombi (application) maalumu, chini ya vifungu vya 99(13), 128(2), na
392A(1)2) vya Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai.

Haya maombi ya ridhaa ndiyo yaliyo mahakamani mpaka sasa na si jinai dhidi ya Makonda. Maana yake Kubenea anaomba ridhaa yeye kama yeye ili aweze kumshitaki Makonda.

Hiki ndicho kilicho mahakamanı. Kwa hiyo Kubenea anaweza akakubaliwa kumshitaki Makonda yeye kama yeye bila DPP ama akakataliwa. Na hiyo ni mpaka hapo hiyo Mahakama ya Kinondoni yalipo hayo maombi 1takapotoa uamuzi kuhusu
hilo.

Katika maombi hayo utamualika DCI, utamualika DPP na utamualika yule unayetaka kumshitaki, ambao nao kila mmoja kwa nafasi yake anaweza kujibu maombi kwa kupinga ama kukubali.

Na kwa haya maombi ya Kubenea, DCI na DPP tayarı wamejitokeza na kupinga asishitaki yeye kama yeye. Makonda hajajitokeza kujibu lakini kwa kuwa haya ni maombi tu (application), basi halazimishwi. Wanaruhusiwa kuendelea tu bila yeye kujibu ama kuwapo (exparte).

Ikiwa Kubenea atakubaliwa kumshitaki Makonda yeye kama yeye bila kupitia kwa DPP, basi hapo ndipo kesi ya jinai dhidi ya Makonda itaanza, na hapo sasa ni lazima Makonda kufika mahakamani atake asitake, na akikosa.

Kwa hiyo tuelewane kuwa mpaka sasa Makonda hana kesi yoyote ya jinai katika mahakama yoyote, wala hatafutwi kukamatwa.

------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Source: Jamhuri

View attachment 2143035

Paul Makonda aiomba Mahakama siku 21 ili ajibu hoja za Kubenea
 
Police na mahakama wameufyata wanamuogopa makonda,
 
Aombe muumba wake ili DPP asionyeshe nia kwa jambo hili pia DCI na yeye asitoe ushirikiano - vinginevyo aisee wahenga walishasemaga, mchwa kashambulia kamba......
Wasukuma hawawezi tupana
 
Ni jambo la wakati,, tutajua mbivu na mbichi..
 
Ila Makonda analiingiza kwenye mtego kama Sabaya alipoenda Clouds na kuropoka hivyo hivyo wajanja wa Msoga wamesha mlengesha Serikali itamuhoji hapo kesi zitaanza kesha jiingiza kwenye box
 
konda boy enzi hizo akiwa mmoja wa chawa wa dogo janja , bila shaka amesamehewa maana walitoka naye mbali sana....konda boy akiwa hana kitu kabisa apeche alolo mjini, dogo janja & family walimbeba sana aisee kama mwanafamilia vile..

japo konda boy anajua siri nyingi za dogo janja toka zama zile za unovice kwenye game, usenior mpaka utycoon..

shida ya Konda boy ni speed na kuingia kwenye mtego wa gangs na kujiside bila kujua kiasi cha kutumika na some gangs na yeye kunogewa akiamini God father will stay forever.
 
Back
Top Bottom