Abtali mwerevu
JF-Expert Member
- May 5, 2013
- 665
- 515
Na: Mwalimu Makoba
"NI hadithi kama hadithi za sungura na fisi. Haihusiani na tukio lolote halisi."
Sehemu ya Kwanza
Hapo zamani za kale watu kutoka mbali waliwavamia Wenyeji. Watu hawa waliwachukua na kuwauza kama anavyouzwa mbuzi mnadani. Ili kujihakikishia Wananchi hawafurukuti au kuanzisha matata, walifungwa minyororo, uhuru kwisha! Jambo hili liliitwa utumwa.
Inasemekana wale walionunuliwa na wavamizi kutoka mashariki ya mbali walihasiwa pengine ndiyo sababu mbegu ya Wenyeji haionekani vyema huko!
Wenyeji walifanya kila juhudi kujinasua na msiba huu ulioitwa utumwa, lakini hawakufua dafu. Ilitokea bahati, wanyang’anyi wa upande mwingine kuona sasa waachane na unyang’anyi huu wafanye unyang’anyi ule. Basi Wenyeji wakanusurika baada ya kuwa wameteseka kwa mamia ya miaka.
Furaha haikudumu kwa muda mrefu, Wenyeji wakavamiwa na watu kutoka Magharibi na kufanywa watumwa katika nchi yao.
Mungu hamtupi mja wake, Wenyeji wakapata bahati, akazaliwa Kanyere.
Inasimuliwa mkasa wa kuzaliwa kwake unastaajabisha. Alizaliwa akiwa na meno yote tena kichwa chake kikiwa na nywele nyeupe peee! Alivyoendelea kukua nywele zikabadilika rangi na kuwa nyeusi.
Inaelezwa siku aliyozaliwa, mkunga na watu wengine waliokuwepo walipomtolea macho alifoka, “Mnashangaa nini? Nisafisheni hamuoni nimetoka tumboni mwa Mama yangu?”
Mama alipoletewa Makande, kichanga hiki kiliyarukia kikisema, “Niache nile mimi mpya, wewe umekula siku nyingi!” Na kweli kikayala makande chungu kizima.
Inaaminika kwamba siku ileile kaliomba kaletewe Wazee wote. Walipofika kakasema, “Nimekuja kwa kazi moja tu, kuwarudishia uhuru, hakikisheni mnanilinda nisije nikauawa kabla sijatimiza jambo hili. Atakayenijaribu, mchapeni.”
Inaelezwa wazee walielewana mno na kichanga hiki cha ajabu. Wakati wengine wakishangaa wazee walisema, “Imetimia, mkombozi kazaliwa.”
Tangu kilipokuwa kitoto kiliitwa Kanyere, hakuna ajuaye tafsiri ya jina hili kwani kilijipa chenyewe, kilipozaliwa tu kilisema, “Jina langu Kanyere!” kilipoulizwa nini maana ya jina hili kilijibu, “Acha umbea!”
Soma: Mfumo wa Maombi wa Ajira za Serikali Unavyoweza Kukupa Kazi
"NI hadithi kama hadithi za sungura na fisi. Haihusiani na tukio lolote halisi."
Sehemu ya Kwanza
Hapo zamani za kale watu kutoka mbali waliwavamia Wenyeji. Watu hawa waliwachukua na kuwauza kama anavyouzwa mbuzi mnadani. Ili kujihakikishia Wananchi hawafurukuti au kuanzisha matata, walifungwa minyororo, uhuru kwisha! Jambo hili liliitwa utumwa.
Inasemekana wale walionunuliwa na wavamizi kutoka mashariki ya mbali walihasiwa pengine ndiyo sababu mbegu ya Wenyeji haionekani vyema huko!
Wenyeji walifanya kila juhudi kujinasua na msiba huu ulioitwa utumwa, lakini hawakufua dafu. Ilitokea bahati, wanyang’anyi wa upande mwingine kuona sasa waachane na unyang’anyi huu wafanye unyang’anyi ule. Basi Wenyeji wakanusurika baada ya kuwa wameteseka kwa mamia ya miaka.
Furaha haikudumu kwa muda mrefu, Wenyeji wakavamiwa na watu kutoka Magharibi na kufanywa watumwa katika nchi yao.
Mungu hamtupi mja wake, Wenyeji wakapata bahati, akazaliwa Kanyere.
Inasimuliwa mkasa wa kuzaliwa kwake unastaajabisha. Alizaliwa akiwa na meno yote tena kichwa chake kikiwa na nywele nyeupe peee! Alivyoendelea kukua nywele zikabadilika rangi na kuwa nyeusi.
Inaelezwa siku aliyozaliwa, mkunga na watu wengine waliokuwepo walipomtolea macho alifoka, “Mnashangaa nini? Nisafisheni hamuoni nimetoka tumboni mwa Mama yangu?”
Mama alipoletewa Makande, kichanga hiki kiliyarukia kikisema, “Niache nile mimi mpya, wewe umekula siku nyingi!” Na kweli kikayala makande chungu kizima.
Inaaminika kwamba siku ileile kaliomba kaletewe Wazee wote. Walipofika kakasema, “Nimekuja kwa kazi moja tu, kuwarudishia uhuru, hakikisheni mnanilinda nisije nikauawa kabla sijatimiza jambo hili. Atakayenijaribu, mchapeni.”
Inaelezwa wazee walielewana mno na kichanga hiki cha ajabu. Wakati wengine wakishangaa wazee walisema, “Imetimia, mkombozi kazaliwa.”
Tangu kilipokuwa kitoto kiliitwa Kanyere, hakuna ajuaye tafsiri ya jina hili kwani kilijipa chenyewe, kilipozaliwa tu kilisema, “Jina langu Kanyere!” kilipoulizwa nini maana ya jina hili kilijibu, “Acha umbea!”
Soma: Mfumo wa Maombi wa Ajira za Serikali Unavyoweza Kukupa Kazi