CK Allan
JF-Expert Member
- Aug 14, 2013
- 2,781
- 6,139
- Thread starter
- #41
KESI YA MZEE MNYOKA 07
Aliwaza na kuwazua Kisha akapiga moyo konde,
"Liwalo na liwe Kama mbwai na iwe mbwai"
Alijisemea akielekea Nyumbani kwake,
Alifika na kujituliza Kwenye Kochi lake lililochakaa kidogo hivi, macho yake Sasa yalitazama juu ya dari ya nyumba yake , kulikua na michirizi yenye rangi Nyeusi iliyotokana na matone ya maji kulikua na tobo Kwenye bati ambalo lilisababisha kuvuja Mara kwa Mara mvua inaponyesha,
Mzee Mnyoka Sasa alijaribu kufumba macho,
Na kuvuta hisia kuhusu mpango wake huo ,
Alimfikiria Mzee Pembe ambaye Jana tu walikua wote,
Ni wazi kuwa usipotetea maisha yako Basi unanenepesha kifo chako,..
Mzee Mnyoka Sasa alihitimisha mpango wake kichwani na wakati wa kutekeleza Sasa umefika,
***********
Mama Monica nae Kama wanakijiji wengine alikua ameenda msibani,
Baada ya kurejea aliamua kupitiliza jikoni moja kwa moja na kuandaa chakula Cha jioni,
Ni wakati anaingia sebuleni ndipo akamuona Mzee Mnyoka akiwa ameanguka chini!
Huku akipumua kwa shida!
Mzee Mnyoka alikua alisumbuliwa na presha na muda mrefu ,
Lakini Ni mwaka mmoja na miezi mitatu Sasa Mzee Mnyoka hakuwahi kuanguka presha,.
Alijitahidi kufuata ushauri wa daktari ikiwemo kula chakula kisichokua na mafuta Sana,
Na kuhusu mazoezi Mzee Mnyoka aliamua kuwa "mzururaji" mzuri tu! Na ndio maana alipenda Sana kutembea tembea!
Kuna wakati Mzee Mnyoka alikua anawatania marafiki zake kuwa
Anaogopa kulala!
Ndio maana anarudi Nyumbani kwa kuchelewa ili "alale kidogo"
Kwa ufupi Mzee Mnyoka alijali Hali yake Sana na hata Mara ya mwisho aliporudi hospital kucheki afya yake daktari alimpongeza Sana,...
Mama Monica hakusubiri,
Alitoka nje haraka na kupiga kelele kuita majirani,
Ni nusu saa baadae Mzee Mnyoka alishafikishwa zahanati ya Kijiji na kuwekewa madripu ya maji,
Baadae Mganga wa Ile Zahanati alishauri Mzee Mnyoka apelekwe hospital kuu ya wilaya Kama mgonjwa wa rufaa na hivyo walipiga simu kwa ajili ya kuletewa ambulance,
Mzee Mnyoka alikua kitandani kimya tu hakujitingisha Wala kufumbua macho,
Mke wake Sasa alikua akilia tu,
Masaa matatu baadae Mzee Mnyoka , mkewe na Mzee Omari pamoja na manesi wawili walikuwa Kwenye ambulance wakikatisha mitaa kuelekea hospital ya wilaya,
"Atapona tu mumeo mama usilie"
Manesi walijaribu kumbembeleza mama Monica,
*****
SAA 5:50 usiku ,
Hospital ya wilaya Kiomboi
Mzee Mnyoka alipelekwa haraka Kwenye wodi ya wagonjwa mahututi, na kilichowangaza madaktari vipimo vyote vilionyesha Mzee Mnyoka hakuwa na tatizo lolote!
Hata hivyo mzee Mnyoka hakufumbua macho kabisa,
Ni wakati Sasa madaktari wakiwa wanashauriana
"Aitwe dokta Kimei"...
"Yeah, Mpigie"
"Ngoja nimfuate , hajafika mbali"
Madaktari Sasa walikua wanazungumza, na mwishowe walimpigia simu dk Kimei,..
Hayo yote Mzee Mnyoka aliyasikia,.
Na hicho ndicho alichokusudia,.
"Dokta Kimei"
Ndio,
Huyu alikua daktari wake Mzee Mnyoka, wakati wote aliokua anaumwa presha alikua Ni yeye alikua akimtibia,
Ilipelekea Sasa Mzee Mnyoka hata alipokua anakuja wilayani Kwenye vikao vya ushirika,
Hakuishia huko tu Bali alifika hospital kumtembelea dokta Kimei,
Na hivyo ilikua rahisi tu dokta Kimei kuweza kuja haraka kumuangalia Mgonjwa "wake"
"Ooh Mzee Mnyoka!
Vipi mama Mzee amekuwaje Tena"
Dokta Kimei aliongea baada ya Kumuona mama Monica
"Baba nilitoka msibani ndio nikamkuta katika Hali hiyo , mpaka Sasa alikua ameanguka sakafuni dokta msaidie"
Mama Monica alianza kusema huku machozi yakimlenga lenga
Dokta Kimei alisogea alipokua mgonjwa wake na kuanza kumkagua , alianza na mapigo ya moyo ,na kuangalia Mambo mengine ya kidaktari,
"Hebu nione faili lake"
Dokta Kimei alisema,
Alikagua faili la Mzee Mnyoka Kisha akaendelea na vipimo Ni wakati anaendelea na "kumkagua"
Mzee Mnyoka Sasa Dokta Kimei alijiridhisha kuwa Mzee Mnyoka hakuwa na ugonjwa wowote!
Sasa aliamua kufanya Jambo la kubahatisha!
"Hebu naomba mnipishe na huyu mgonjwa!"
Madaktari wenzake sasa walipigwa na butwaa!
Kisha Kama waliambizana wakatoka nje kwa pamoja!
Baada ya kutoka nje dokta Kimei Sasa aliamua kufunga mlango kabisa!
******
Miaka minne iliyopita
Dokta Kimei akiwa pale pale hospital aliletewa mgonjwa mmoja siku hiyo kwa dharula,
Tofauti na Mzee Mnyoka, mgonjwa wa siku hiyo alikua Ni mwanamke,
Walidai amezimia kwa ghafla,
Walifanya vipimo vyote na hakukua na ugonjwa wowote,
Ni wakati dokta Kimei amewatoa nje wauguzi ili amfanyie vipimo vya ziada ndipo yule mama akafumbua macho!
Dokta Kimei hakustuka Sana lakini baadae yule mgonjwa alimuita na kumueleza kila kitu,
Alisema wazi hakua akiumwa popote lakini alichoka maisha yake ya ndoa na mumewe , na ndugu zake hawakumuelewa na ameona Kama atajiua atakua hajawatendea haki watoto wake,
Na hivyo njia pekee aliona Ni kujifanya anaumwa ili apumzikie hospital!
Dokta Kimei Sasa alikumbuka kesi hiyo huku akirudi kitandani alipo Mzee Mnyoka..
"Haya Mzee Mnyoka niambie Sasa kuna inshu gani?"
Dokta Kimei aliongea akitabasamu na kukaa kitandani!
Itaendelea
Aliwaza na kuwazua Kisha akapiga moyo konde,
"Liwalo na liwe Kama mbwai na iwe mbwai"
Alijisemea akielekea Nyumbani kwake,
Alifika na kujituliza Kwenye Kochi lake lililochakaa kidogo hivi, macho yake Sasa yalitazama juu ya dari ya nyumba yake , kulikua na michirizi yenye rangi Nyeusi iliyotokana na matone ya maji kulikua na tobo Kwenye bati ambalo lilisababisha kuvuja Mara kwa Mara mvua inaponyesha,
Mzee Mnyoka Sasa alijaribu kufumba macho,
Na kuvuta hisia kuhusu mpango wake huo ,
Alimfikiria Mzee Pembe ambaye Jana tu walikua wote,
Ni wazi kuwa usipotetea maisha yako Basi unanenepesha kifo chako,..
Mzee Mnyoka Sasa alihitimisha mpango wake kichwani na wakati wa kutekeleza Sasa umefika,
***********
Mama Monica nae Kama wanakijiji wengine alikua ameenda msibani,
Baada ya kurejea aliamua kupitiliza jikoni moja kwa moja na kuandaa chakula Cha jioni,
Ni wakati anaingia sebuleni ndipo akamuona Mzee Mnyoka akiwa ameanguka chini!
Huku akipumua kwa shida!
Mzee Mnyoka alikua alisumbuliwa na presha na muda mrefu ,
Lakini Ni mwaka mmoja na miezi mitatu Sasa Mzee Mnyoka hakuwahi kuanguka presha,.
Alijitahidi kufuata ushauri wa daktari ikiwemo kula chakula kisichokua na mafuta Sana,
Na kuhusu mazoezi Mzee Mnyoka aliamua kuwa "mzururaji" mzuri tu! Na ndio maana alipenda Sana kutembea tembea!
Kuna wakati Mzee Mnyoka alikua anawatania marafiki zake kuwa
Anaogopa kulala!
Ndio maana anarudi Nyumbani kwa kuchelewa ili "alale kidogo"
Kwa ufupi Mzee Mnyoka alijali Hali yake Sana na hata Mara ya mwisho aliporudi hospital kucheki afya yake daktari alimpongeza Sana,...
Mama Monica hakusubiri,
Alitoka nje haraka na kupiga kelele kuita majirani,
Ni nusu saa baadae Mzee Mnyoka alishafikishwa zahanati ya Kijiji na kuwekewa madripu ya maji,
Baadae Mganga wa Ile Zahanati alishauri Mzee Mnyoka apelekwe hospital kuu ya wilaya Kama mgonjwa wa rufaa na hivyo walipiga simu kwa ajili ya kuletewa ambulance,
Mzee Mnyoka alikua kitandani kimya tu hakujitingisha Wala kufumbua macho,
Mke wake Sasa alikua akilia tu,
Masaa matatu baadae Mzee Mnyoka , mkewe na Mzee Omari pamoja na manesi wawili walikuwa Kwenye ambulance wakikatisha mitaa kuelekea hospital ya wilaya,
"Atapona tu mumeo mama usilie"
Manesi walijaribu kumbembeleza mama Monica,
*****
SAA 5:50 usiku ,
Hospital ya wilaya Kiomboi
Mzee Mnyoka alipelekwa haraka Kwenye wodi ya wagonjwa mahututi, na kilichowangaza madaktari vipimo vyote vilionyesha Mzee Mnyoka hakuwa na tatizo lolote!
Hata hivyo mzee Mnyoka hakufumbua macho kabisa,
Ni wakati Sasa madaktari wakiwa wanashauriana
"Aitwe dokta Kimei"...
"Yeah, Mpigie"
"Ngoja nimfuate , hajafika mbali"
Madaktari Sasa walikua wanazungumza, na mwishowe walimpigia simu dk Kimei,..
Hayo yote Mzee Mnyoka aliyasikia,.
Na hicho ndicho alichokusudia,.
"Dokta Kimei"
Ndio,
Huyu alikua daktari wake Mzee Mnyoka, wakati wote aliokua anaumwa presha alikua Ni yeye alikua akimtibia,
Ilipelekea Sasa Mzee Mnyoka hata alipokua anakuja wilayani Kwenye vikao vya ushirika,
Hakuishia huko tu Bali alifika hospital kumtembelea dokta Kimei,
Na hivyo ilikua rahisi tu dokta Kimei kuweza kuja haraka kumuangalia Mgonjwa "wake"
"Ooh Mzee Mnyoka!
Vipi mama Mzee amekuwaje Tena"
Dokta Kimei aliongea baada ya Kumuona mama Monica
"Baba nilitoka msibani ndio nikamkuta katika Hali hiyo , mpaka Sasa alikua ameanguka sakafuni dokta msaidie"
Mama Monica alianza kusema huku machozi yakimlenga lenga
Dokta Kimei alisogea alipokua mgonjwa wake na kuanza kumkagua , alianza na mapigo ya moyo ,na kuangalia Mambo mengine ya kidaktari,
"Hebu nione faili lake"
Dokta Kimei alisema,
Alikagua faili la Mzee Mnyoka Kisha akaendelea na vipimo Ni wakati anaendelea na "kumkagua"
Mzee Mnyoka Sasa Dokta Kimei alijiridhisha kuwa Mzee Mnyoka hakuwa na ugonjwa wowote!
Sasa aliamua kufanya Jambo la kubahatisha!
"Hebu naomba mnipishe na huyu mgonjwa!"
Madaktari wenzake sasa walipigwa na butwaa!
Kisha Kama waliambizana wakatoka nje kwa pamoja!
Baada ya kutoka nje dokta Kimei Sasa aliamua kufunga mlango kabisa!
******
Miaka minne iliyopita
Dokta Kimei akiwa pale pale hospital aliletewa mgonjwa mmoja siku hiyo kwa dharula,
Tofauti na Mzee Mnyoka, mgonjwa wa siku hiyo alikua Ni mwanamke,
Walidai amezimia kwa ghafla,
Walifanya vipimo vyote na hakukua na ugonjwa wowote,
Ni wakati dokta Kimei amewatoa nje wauguzi ili amfanyie vipimo vya ziada ndipo yule mama akafumbua macho!
Dokta Kimei hakustuka Sana lakini baadae yule mgonjwa alimuita na kumueleza kila kitu,
Alisema wazi hakua akiumwa popote lakini alichoka maisha yake ya ndoa na mumewe , na ndugu zake hawakumuelewa na ameona Kama atajiua atakua hajawatendea haki watoto wake,
Na hivyo njia pekee aliona Ni kujifanya anaumwa ili apumzikie hospital!
Dokta Kimei Sasa alikumbuka kesi hiyo huku akirudi kitandani alipo Mzee Mnyoka..
"Haya Mzee Mnyoka niambie Sasa kuna inshu gani?"
Dokta Kimei aliongea akitabasamu na kukaa kitandani!
Itaendelea