KESI YA MZEE MNYOKA- MWISHO WA MWISHO (
Kwa udhamini wa mkuu
Gily )
Baada ya wiki moja
Oscar alikua amejilaza kwenye sofa huku akiangalia vipindi mbali mbali kwenye televisheni yalikua ni matangazo ya moja kwa moja kutoka chuo kikuu cha dar es salaam ambapo waziri mkuu alikua akiwatunukia shahada ya uzamivu wanafunzi waliohitimu mafunzo maalum ya mifumo ya komputa , hawakuwa wengi sana, na kutokana na kozi yenyewe,
Na wanafunzi hao kuitwa mmoja mmoja,
‘Na huyu ni mwanafunzi aliyefanya vizuri zaidi na kupata GPA 4.9 anaitwa JOYCE TITUS KILIBIKA!
Alisema mc wa shughuli hiyo
“whaaaaat!” alisema oscar akiruka pale kwenye kochi na kuvaa haraka haraka kisha akawasha gari na kuwahi mwenge. Mlimani..
Kama bahati alikuta sherehe bado hazijakamilika na wahitimu bado walikua ndani
Ndugu jamaa na marafiki walikua wamezunguuka nje na zawadi zao huku wakisubiri kwa hamu wapendwa wao watoke nje!
Naam hatimaye walianza kutoka mmoja baada ya mwingine wakiwa na majoho yao,
Oscar alijitahidi kujipenyeza hadi akafanikiwa kuwa karibu na mlangoni kabisa, kwanza hakua na zawadi yoyote! Hivyo ilikua ni rahisi kufika mbele kabisa,
Hatimaye mtu wake alitoka! Oscar kama mshale alichomoka na kwenda kumkumbatia Joyce! Joyce nae hakuamini macho yake, machozi yalimtoka kwa furaha,
Bila kujali macho ya watu oscar alimbeba Joyce na kutokomea nae kwenye gari…..
‘oscar tunaenda wapi? Ujue ndugu zangu nimewaacha na mshangao wa haja” alisema Joyce huku akivua joho la kubaki na suruali na tisheti nyepesi , oscar hakujibu chochote alizidi kukanyaga mafuta kuelekea Tegeta,
Baada ya safari ya kutokuamini hatimaye walifika , oscar alishuka na kwenda kufungua geti na kuingiza gari ndani kisha akafunga tena geti na kumbeba tena joyce hadi ndani na kumtua kwenye sofa!
“oscar. Oscar..”
“shhhhh!” oscar aliweka kidole mdomoni kumuashiria asiseme kitu Joyce kisha akamsogeza karibu na kuanza kumtomasa na kumvua nguo moja baada ya nyingine mwishowe walijikuta katika mapenzi mazito hapo hapo sebuleni, na hivyo kuamua kuhamia chumbani na shughuli ikaanza upya,
Saa mbili Usiku walirudi sebuleni na joyce alikimbilia simu yake,
“yaani wamepiga mpaka wamekoma, nimetafutwa sana!’ alisema Joyce
“vipi nikupeleke !” aliluliza Oscar
“ah keshoo njaa inauma hatari’ alisema Joyce akitafuta jiko lilipo oscar nae alimfuata akiwa na bukta .
Kesho yake walienda hadi gereza la keko kumtembelea mzee Tito,
oscar alibeba kitabu cha hadithi kilichoitwa “MPANGAJI” ili kumpa mzee Tito asome akiwa lupango..
“hakika maisha ni hadithi ndefu sana” alisema Joyce wakiwa njiani kurudi,
“nakuachia binti yangu, muangalie, nakuamini Oscar, asije kulia machozi yanayotokana na wewe!” oscar alikumbuka maneno ya mzee Tito muda mfupi uliopita na kujikuta machozi yakimtoka,
Hakupendezwa na hali hii ya kuishi na Joyce wakti baba yake akiwa gerezani lakini hakuwa na namna yoyote,
Maisha lazima yaendelee
Aliwaza akikanyaga mafuta kurudi tegeta.
MWISHO.
Namba zangu ni 0746 mia mbili sitini na sita mia mbili sitini na Saba
Niwashukuru sana wadau,
Asanteni kwa support yenu!
Mpaka wakati mwingine kwenye "MPANGAJI AU MZAHA WA DAMU"