Hadithi: Madam President

Hadithi: Madam President

Asantee baby gal Antonnia 😘😘😘
Where is Tayukwa jamani, muda sijaposhana naye. Hizi simulizi watazimaliza kweli ama?
Poker katuacha kwenye mataa, Umu ana Ban... mmh!!!
Tayukwa mi mwenyewe hata simuoni kabisa sikuhizi sijui kajifichia wapi au ametingwa na kazi!! Ankali Tayukwa werayyuuuuuuuu🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️
 
Asantee baby gal Antonnia 😘😘😘
Where is Tayukwa jamani, muda sijaposhana naye. Hizi simulizi watazimaliza kweli ama?
Poker katuacha kwenye mataa, Umu ana Ban... mmh!!!
Kuna muda mwili unakataa kabisa kufanya kazi zake kwa ufanisi lakini baada ya kuitwa tu najihisi kila kiungo kimekuwa kipya na madhubuti kabisa.
Huwezi kuitwa au kumisiwa na hii Bantu halafu mwili wako na stress zako zisipotee..
Ahsante sana mbantu mwenye kubantua nyoyo za wakwere much respect Bantu Lady.. Nipo my best majukumu tu ila kukumbukana kama hivi unasababisha mchafuko wa damu upotee mwilini mwangu
 
Tayukwa mi mwenyewe hata simuoni kabisa sikuhizi sijui kajifichia wapi au ametingwa na kazi!! Ankali Tayukwa werayyuuuuuuuu🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️
Am coming my real ankali majukumu tu yananipelekesha ili nami niwe na uwezo wa kuingia popote na KUKUAGIZIA CHOCHOTE bila kuuliza bei ya hicho kitu ankali..
Thanks for your # to me
Antonnia
 
Kuna muda mwili unakataa kabisa kufanya kazi zake kwa ufanisi lakini baada ya kuitwa tu najihisi kila kiungo kimekuwa kipya na madhubuti kabisa.
Huwezi kuitwa au kumisiwa na hii Bantu halafu mwili wako na stress zako zisipotee..
Ahsante sana mbantu mwenye kubantua nyoyo za wakwere much respect Bantu Lady.. Nipo my best majukumu tu ila kukumbukana kama hivi unasababisha mchafuko wa damu upotee mwilini mwangu
Karibu best tuko pamoja na pole na uchovu.
 
Ukiwa jobless shida sana, yani kila siku unapewa story mpya usome. Unakuta mtu umezipanga foleni stories kama 10 hivi, na zote unahitaji kuzisoma. Me kuna muda mpaka nachanganya characters, mara yunge, violin, allan, old ceo...am tired lakin siachi
 
MADAM PRESIDENT 04

Nilipita kwenye bustani ndogo ya maua Kisha nikaendelea mbele ambapo alitokea mlinzi mmoja akanikaribisha Kisha akachukua begi langu dogo akaniongoza njia, tulienda sehemu Nyingine ambapo tulipita kwenye ofisi Nyingine Kisha nikaambiwa nisubiri hapo,

Kwa kila namna Sasa nilianza kujisikia vibaya kukaguliwa Mara kupitishwa kwenye vidude gani nilitamani kugeuza kurudi....
Ni Kama Yale yote yalikuwa madogo..

Ni wakati nimekaa hapo nikikunja kunja vidole na kuangaza macho huko na huko akatokea mzee mmoja hivi ambaye alinisalimia kwa tabasamu Kisha akafungua mlango uliokuwa mbele yake akaniita ,

Hakuwa na maneno mengi akaniashiria nikae kwenye kiti ambacho Kiko mbele yake Kisha akafungua kabati na kutoa vifaa Kama vya kidaktari hivi....
"Aah mzee achana na Mimi aisee"

Nilijikuta Sasa uvumilivu unanishinda,

"Hahaha Tulia bhana Kijana mbona saa ulivaa? Tunamalizia tu zoezi dogo" alisema huku akichukua kidole changu na kukitoboa kidogo kwa sindano Kisha akachukua damu na kuipachika kwenye kidude Kama saa,

Alinipigisha Hadithi ambazo hazikuwa na kichwa Wala miguu nilishaelewa kuwa anasubiri vipimo vyake hivyo sikumjibu kitu na hatimaye akaacha kuongea baada ya kuona nimekasirika ...

Baada ya dakika Kama nane hivi alikichukua kile kidude na kukiingiza Tena kwenye kitu mfano wa saa ambapo alibinya binya namba fulani Kisha akatabasamu...

"Haya twende"

Alisema Kisha tukatoka Tena na kupanda ngazi ambapo aliniacha kwenye chumba kingine akaondoka zake...

Ni baada ya dakika tatu alitokea madam Janet akiwa na walinzi wawili nilisimama na tukasalimiana wale walinzi hawakunisalimia walinikodolea macho mpaka nikaishiwa pozi..

Tuliongozana na madam tukipiga stori mbili tatu mpaka kwenye chumba kingine kikubwa ambacho walinzi walibaki nje ..

"Aisee siwezi kurudi Tena hapa"
Nilisema wakati nikikaa vizuri kwenye sofa
"Haha pole hata hapo bado Kuna step tumekanyaga kanuni zinasema uje hapa wiki moja kabla, "

Alisema Janet kana kwamba haikuwa Shida kubwa...

Aliniuliza habari za kazi na Mipango mingine ya maisha

Sikuwa na maneno mengi kwanza sikuwa najisikia vizuri...

"Nimekumisi Sana wewe mwanaume yaani hapa ofisini hapakaliki mpaka navurugana na mawaziri yaani sijui Hilo dudu lako likoje yaani"
Alisema Janet huku akicheka,
"Ah mzee si yupo nilimuona siku Ile ya kuapishwa"

Nilisema
"Wee bado mgeni kwenye hii nchi ndugu? Mimi Janet niwe na mzee Kama Yule na watoto hao niwapate lini?"

Hahahaa hata hivyo wapo hapa kama utataka kuwaona! "

Janet aliongea Kish akanishika mkono...

"Sikia tunaingia kwenye chumba ambacho hatuonekani kuwa na amani mpenzi wangu"

Alisema Janet akinivuta nami nikaingia chumbani na kazi ikaanza....

Ni Kama alikua amenipania hata hivyo shughuli aliipata na mwishowe akapitiwa na usingizi nilienda bafuni kuoga Kisha nikachukua begi langu ambalo lililetwa nikavaa suti nyingine niliangalia saa yangu ilikua saa 12 jioni, njaa iliniuma Sana, nilimwamsha Janet ambaye alistuka kuniona nimevaa nguo nyingine.

"Vipi? "

Alisema akijifinyanga macho

"Madam siwez kulala hapa, halafu hapa Ni nyumbani kwako"

Nilisema huku nikionyesha dalili za kukasirika..


"Okay nashukuru hata hivyo nitajua namna ya kufanya najua una njaa Ila Sasa chakula Cha hapa Ni hakiivi Sasa hivi na ningependa ule chakula Cha Raisi leo"

Alisema janet Kisha akasimama vile vile na kunibusu..


Nitafanya mpango wiki mbili zijazo tuinjoy zaidi

Alivaa nguo zake Kisha akanitoa nje ambapo mlinzi mmoja alinifikisha kwenye chumba kingine ambacho nilimkuta dada mmoja ambaye alininipa begi langu Pamoja na bahasha nyingine nilitoka nje ya geti nikapiga ishara ya msalaba kutoka salama mle ndani....


"Siwezi kurudi Tena hapa kwakweli" nilijikuta nasema moyoni huku nikichanganya miguu .....

Niliangalia Ile bahasha na kukuta kiasi Cha pesa na zilikua Ni Dola za kimarekani..

Nilitafuta mgahawa mzuri nikapata chakula Kisha nikarudi zangu mlandizi,

Nikiwa kwenye Basi nilifikiri mengi Sana niliwaza mwisho wa Jambo hili utakuwaje,
Vipi Raisi akijua kuhusu familia yangu? Vipi ikijulikana natembea na Raisi?
Ni wakati natoa Simu yangu niliangusha kitambaa changu kwa bahati mbaya nikainama kukiokota wakati nanyanyua uso macho yangu yakagongana na huyu abiria mmoja aliyekaa upande wa nyuma,

Nilijaribu kumuangalia lakini kwa haraka Sana akaendelea kubonyeza Simu yake kana kwamba hakuniona,
Sikutilia maanani ingawa nilijikuta tu namuwaza na Sasa akili yangu ikakumbuka, wakati naingia pale rock mall kupata chakula alikuwa nyuma yangu na wakati nakula yeye alikua anakunywa maji

Ni wakati gani alipanda kwenye Basi sikutilia maanani...
"Au labda namfananisha" nilijisemea
Tulifika mlandizi majira ya saa tatu na robo usiku, moyoni nilikua najisikia huzuni kubwa na nilikua nikijihisi aibu kurudi nyumbani kwa mke wangu usiku ule,
Nilishuka na kuvaa begi langu Kisha nikasogea mpaka kwenye kijiwe Cha boda boda, ndipo yule jamaa nae kwa mbali niliona akiwa anashuka kwenye Basi wakati naongea na boda nilipogeuka sikumuona tena!

"Twende misongeni kwa mzee kivu"


Nilisema nikichukua boda boda,

"Wapi Ile ya juu au kule madukani"

Boda aliuliza

"Ya juu"

Nilisema nikikaa kwenye piki piki.
Nilifika nyumbani kwangu na mke wangu alikua ananisubiri Kama ilivyokuwa kawaida yake,
Nilitoa uongo tu kuhusu kazi na bla bla ikaisha...


Hata hivyo nilijiambia Mara hii siwezi kutoka Tena na Madam President potelea pote,


"Aniue tu, Kama mbwai na iwe mbwai"

Nilijisemea huku nikipanda kitandani.



*****************

Katikati ya usiku wa manane nilihisi Kama Kuna mtu anapita sebuleni,
Halafu Tena nikahisi Kama amekuja chumbani kwetu na kusimama baadae sikukumbuka Tena kilichotokea tulikuja kuamshwa na dada wa kazi Stella saa 4 asubuhi kwa ajili ya chai!
"Mimi nilijua leo hamuendi kazini"

Alisema Stella akiwa mlangoni, nilijaribu kunyanyuka lakini mwili ulikua mzito, mke wangu pia nae alijihisi uchovu...

Ndipo fahamu zangu zilirejea

"Mama tumevamiwa, wezi bila shaka wametupulizia dawa ya usingizi"

Nilisema Sasa nikisimama kutoka kitandani
Nilipitia mpaka sebuleni ambapo Kila kitu kilikua sawa , nilirudi Tena chumbani ambako niliangalia kabati lilikua sawa Ni Kama Kila kitu kilikua sawa...

Nilichukua Simu yangu na kumpigia Mkuu wa idara kumueleza Hali yote iliyotokea na Polisi walifika muda mfupi, walijaribu kuangalia sehemu kadhaa na kutuhoji ,

Daktari alifika pia na kutupima na alithibitisha kuwa dawa Kali ya usingizi ilikuwa imepulizwa


*****************

Ni wiki moja baada ya tukio sikuwa na mawasiliano yoyote na Janet kitu ambacho niliona kizuri sana,
Nikiwa ofisini baada ya kazi kupungua niliingia kwenye akaunti ya Yahoo ili nisome baadhi ya jumbe kutoka kwa marafiki,
Lakini kipekee tu nilidhani ningepata Hata meseji moja kutoka kwa Jacob,

Maana ilishapita miezi sita hatujawasiliana,
Ni wakati nafungua nilikuta meseji ambayo ilitumwa siku kadhaa zilizopita na mtu ambaye hakutaja jina lake Wala anuani yake haikuonekana,

"Unavuka barabara na ukiwa na mke wako na watoto angalia hiyo Gari inayokuja Kasi,
Jitahidi uvuke kwa spidi au urudi nyuma"

Ujumbe uliishia hapo, nilijaribu kuelewa lakini sikuambulia chochote hatimaye niliamua kumtumia Jacob Ile ujumbe huku nikiomba msaada wake,
Hata hivyo sikuelewa Jacob Anaweza kunijibu lini...
Ghafla wazo lilinijia,
Niliona Tena sio salama kukaa mazingira yale tayari mke wangu alikua mjamzito wa mtoto wetu wa pili, na tayari alishachukua likizo ya kwenda kujifungua,
Nilitoka ofisini haraka na kuchukua boda boda mpaka kwangu,
"Dear jiandae taratibu funga mizigo yako ya muhimu taratibu, Stella atakusaidia kwenye usiku tutaondoka hapa sitaki tukae mazingira haya kwa kipindi hiki"
Nilimuelewesha Kisha nikarudi kazini,
Nilitoa Simu Yangu na kumpigia jose,
"Kaka naomba unipeleke sehemu Leo usiku "

Nilisema baada ya simu kupokelewa
"Ha Kaka usiku Tena, vipi kwema"
Jose aliongea,
Huyu alikua Ni dereva pale stendi na Mara nyingi alikua ananibebea mizigo yangu wakati wa ujenzi wa nyumba zangu...
Tulikubaliana Kisha nikampigia gogo aliyekuwepo huko misufini ambako nilitegemea kumpeleka mke wangu,
Haikuwa mbali Sana na mjini lakini ilikua Ni sehemu nzuri sana kwa kutulia ama kujificha Kama nilivyowaza,

**************

Saa mbili usiku tulianza safari na ndani ya masaa matatu na nusu tulishafika na kushusha mizigo,

Nyumba ilikua kubwa na nzuri Sana,..

Tulishusha mizigo kwa kusaidiana na Yule kijana ambaye nilimuacha kama mlinzi, Mimi na Jose tulirudi Tena kumalizia mizigo iliyobaki...


"Kaka usiniambie ule mjengo Ni wako"


Nilitabasamu tu Kisha nikamwambia Jose kwa msisitizo..

"Jose wewe Ni Rafiki yangu, nimekuchagua kwenye hii kazi kwakuwa nakuamini,


Siku sio nyingi pengine Kuna Mambo mabaya yanaweza kunipata, naomba mtu yoyote asijue kuwa mke wangu anakaa katika Ile nyumba ndio maana tumehamia usiku,

Jose alisimamisha Gari ghafla na kutoka nje..
"We jamaa unaumwa? Mbona unongea ujinga hivi?" Eti Nini?
Jose alihamaki akitweta...

"Jose sikiliza bhana sijasema nitakufa! Nimesema naweza kupatwa na jambo baya kwa tahadhari tu sitaki mke wangu aguswe tutaongea zaidi hebu tumalize kazi kwanza tukachukue mizigo iliyobaki....

Ilikua Ni Kama saa Saba usiku na tulikuwa tunakaribia kufika kwangu ndipo kwa mbali nikaona piki piki imeegeshwa nje kwangu,

"Jose ona kule!"

Nilisema nikinyoosha kidole

"Aisee huyu fala anaweza kuegesha kabisa piki piki nje kwa mtu saa hizi?"

Jose alisema akiongeza Mwendo..
"Sikiliza usipaki pale home fanya Kama unapita hiyo nyumba tumsome kwanza huyo boya" nilisema
 
MADAM PRESIDENT 05

Tulipita pale kwangu kwenda mbele kidogo Kisha tukasimama,

Tulitazama kana kwamba kila mmoja anasubiri mwenzake atoe wazo Kisha kama tumeambizana tukashuka wote kwenye Gari na kuelekea nyumbani kwangu..

Taa zilikua zinawaka na tuliingia na kukuta milango yote ikiwa wazi na Ile piki piki ilikua pale nje,...
Hatukuwa na silaha yoyote kwahiyo tuliingia ndani moja kwa moja.
Ilikua Ni nyumba ya serikali lakini nilikabidhiwa Mimi kukaa na tayari nilishakaa zaidi ya miaka mitatu kwenye hii nyumba lakini leo nilijikuta nakuwa muoga kabisa,

Jose aliingia kwenye baadhi ya vyumba na Kisha tukatoka sebuleni Kama Tuendelee na zoezi la kupakia mizigo ama la..
Wakati tunashaurina mlango wa mbele ulifunguliwa kwa Kasi ya ajabu na mtu mmoja aliyejifunga kitambaa usoni akaruka akiwa na bastola mkononi,
Wakati tunakaa sawa mwingine akaingia akiwa na bastola na kutuweka chini ya ulinzi....
"Shit!!!!" Nilijisemea nikikubali kupiga magoti...
Jose alinitazama Kama anayeuliza maswali nami nilimuangalia Kama mtu anayesema "hiki ndio nilikua nakuambia"

"Nyie Ni Akina Nani na mnataka Nini kwangu?"

Nilisema Sasa nikifoka,
"Sisi Ni rafiki zako tumekuja kukusaidia"
"Kunisaidia?"

Niliuliza nikitweta

Mmoja alisogea na kumnong'oneza mwenzake kitu Kisha wakaangaliana tulieni hivyo hivyo na ole wake mtu ageuke...

Tulibaki tumetulia na ukimya ulitawala kwa dakika kadhaa hivi nikaamua kunyanyuka..
Hakukuwa na mtu, Jose nae alisimama na kwenda mlango ambapo hatukuona mtu, Ile piki ilibaki pale pale nje...

Ndipo Sasa wazo lilinijia

Bila shaka Hawa watu walikuja Kama wageni wa kawaida usiku ule kwangu lakini walipoona hatupo wakaamua kubaki kusubiri kwa kuvizia Kama hivi...
"Ila Sasa wanataka Nini mbwa Hawa?"


Niliwaza bila kupata jibu...
Jose alikua ananitazama Kama mtu Mwenye maswali mengi...

"Kaka hebu niambie kunani ujue Mimi Mambo ya bunduki bunduki nayaona kwenye picha tu!"

Jose aliongea..


"Jose tupakie mizigo kwanza...hii sio inshu ya dakika mbili hata hivyo itabidi tuhakikishe hakuna anayetufuata...


Familia yangu ikishakaa salama Basi nitakuambia Kaka"


Nilisema Kisha tukamalizia mizigo iyobaki Safari ikaanza tulikwenda pole pole na kuhakikisha hakuna mtu Wala Gari linatufuata wakati mwingine tulishuka kabisa na kuangaza macho huko na huko Kisha safari ikaendelea...

Tulifika saa kumi na moja kasoro asubuhi, na kupakia mizigo


Nilitamani kumwambia mke wangu Mambo yote kuanzia mwanzo Hadi mwisho lakini niliogopa kutokana na Hali yake ya ujauzito..


Tulipanga mizigo yote ikiwemo kuweka vitu sawa ikiwemo televisheni na vitu vingine vya muhimu chumbani, tulilazimika kufanya wenyewe baadhi ya Mambo ili kuepusha watu wengi kujua ninapoishi..

Tulimaliza kazi saa 9 mchana tukapata chakula Kisha tukapumzika kidogo ili usiku tuanze safari ya kurudi mjini Mimi na Jose..



Kwa kawaida mwezi wa 4 Hadi wa 6 kila mwaka nakuwa na shughuli nyingi za umiseta wilaya na mkoa na taifa na wakati huu nakuwa na majukumu mengi ya kusafiri Sana pamoja na kuwa mashindano haya kwa mwaka ule yalifanyika pale pale wilayani kwangu nilitumia fursa hii kumdanganya mke wangu kuwa nitasafiri kikazi kwa mwezi mzima


"Mahitaji yote atakuwa analeta Jose, halafu Kuna Shemeji yangu mke wa rafiki mmoja nitamuomba aje akae na wewe kwa miezi hii miwili,


Hatuna haja ya kumsumbua mama safari hii"

Nilisema Kisha tukaagana Mimi na Jose tukarudi mjini...
Niliweka wastani wa mwezi mmoja nimalizane na Janet


"Jose kiuhalisia nahisi tu Kuna Mambo mabaya yanaweza kunitokea Sasa si unajua Ile nyumba yangu kule mabatini ambayo tulipeleka bomba kipindi kile?"


Niliongea Sasa nikiwa Sina utani Tena..


"Yeah nakumbuka," Jose alisema..



"Okay ikitokea chochote labda nimepotea ghafla au chochote yaani...."

Jose alinikatisha..


"Unajua we jamaa sikuelewi ulikua unasema Kama hivyo tukakuta watu kule sijui majambazi sijui usalama sijui Nini...


Mwanangu mi mtu wako bhana niambie Basi sikuelewi ujue"

Jose alinitazama

Kaka Ni stori ndefu kidogo Ila usijali kwakuwa wewe Ni mtu wangu nitakueleza kila kitu..


"Wakati nikiwa kidato Cha tano pale mombo sekondari tulikwenda tanga kwenye umiseta........."


Pamoja na kuwa Jose alikua sio ndugu yangu lakini katika harakati za maisha hususani baada ya Jacob "kupotea" katika mazingira ya kustaajabisha nilimchukulia huyu Kama rafiki yangu mwingine ...
Hivyo nilijikuta namueleza kila kitu wakati namaliza kusimulia ndio niligundua kuwa machozi yalikua yanatoka


"Kaka Pole,

Ujue kumgonga madam si mchezo ujue, Sasa nakuelewa kaka, Hawa wajinga lazima wakutafute....niambie kaka tunatokaje Sasa"

Jacob aliniuliza huku akiwa amesimamisha Gari...


"Kwasasa nitaenda kumshawishi Aida , aende kukaa na wife kwa kipindi chote, mpaka atakapojifungua.. Mimi nitaendelea kuishi Kama popo nikijigeuza geuza"

Nilisema kwa upole..


"Ulisema kuhusu kule kwenye nyumba yako mabatini kuna Nini "


Aliniuliza

"Sikiliza Jacob, ukiwa unaenda bafuni Kuna malu malu ambayo yako tofauti ukiangalia tu mwenyewe utaona zipo Kama tiles nane 8 hivi utazitoa ..


Utaona box moja la Chuma , pembeni yake Kuna chupa ya soda ambayo Ina bahasha yenye maelezo yote,

Lakini hii Ni endapo tu utakuwa umejihakikishia kuwa hutaniona Tena, lakini sambamba na Hilo Hakikisha unamtafuta Jacob Lota, ikibidi hata kwenye magazeti umkabidhi Hilo box kabla ya kulifungua, ukimkosa Jacob Kama nae atakuwa amekufa kwa bahati Basi ulifungue Hilo sanduku wewe mwenyewe"


Sasa twende zetu mjini!

Nilisema huku tukiendelea na Safari...


"Mimi nahisi Jacob yupo Tanzania na ndio atakuwa kakutumia ule ujumbe kuhusu kuvuka barabara na familia"

Jose alisema...


"Aisee Jose itakuwa kweli umenikumbusha kitu, ngoja nikaangalie Ile email Tena kesho asubuhi"


Tulifika salama kwenye majira ya saa nne usiku na sikutaka kwenda kwenye Ile nyumba Tena,
Niliagana na Jose baada ya kumpatia kiasi Cha pesa Kisha nikatafuta gesti ya karibu nikalala.

*************

Nilifika ofisini kesho yake na wengi walinipa pole kwa kuvamiwa na kuuliza kuhusu kuibiwa chochote...


Nilienda ofisini kwangu na moja kwa moja nilifungua computer na kuingia kwenye barua Pepe yangu...


Niliangalia Tena Ile barua Pepe na kisha nikatabasamu!

Naam Ni kweli ujumbe ule ukitoka kwa Jacob, nilijilaumu Sana kutokuelewa mapema,


Kwa kawaida Jacob alikua anapenda kuchanganya Walau Herufi moja kubwa au ndogo katika jumbe zake Lau Mara kadhaa angemalizia na nukta mbili mwishoni.


Hivyo nilivyoona nukta mbili mwishoni nikajua moja kwa moja Ni Jacob alikua anataka kunionya kuhusu kinachoendelea .

Ni wakati natoka kwenda kwenye kikao Cha bajeti ya umiseta mke wangu alinipigia kuwa Kuna picha yetu kubwa ya ndoa pamoja na Cheti Cha ndoa hajaviona katika Ile mizigo yote tuliyobeba..

Nilimsihi aangalie au amuulize Stela lakini alisema alishakagua sehemu zote hakuna kitu, hivyo alinitaka kuangalia Kama nimesahau kule kwenye Ile nyumba...

"Okay nikitoka nitaenda kuangalia itakuwa tumesahau kule " nilisema huku nikienda kwenye kikao...
******************
Nilifika kwenye Ile nyumba na kukuta Ile piki piki ikiwa vile vile pamoja na ufunguo wake ukining'inia..
Niliingia ndani na kutafuta kila sehemu sikuona picha Wala Cheti hicho Cha ndoa...
Sasa nilikaa kwenye kiti pale sebuleni na kutafakari ndipo nikagundua mahali vitu hivyo vilipo...
 
Back
Top Bottom