Hadithi: Madam President

Hadithi: Madam President

MADAM PRESIDENT 09
Roda alikuja na tukasaidiana kumbeba dada mpaka nje kwenye Gari, roda alienda kuangalia ufunguo kwa bahati akaupata tukaenda hospital mbezi ambapo madaktari walifanikiwa kumrudisha katika Hali yake ya kawaida ..


Ingawa hakuongea chochote alikua akilia tu,


Nilitoka nje huku nivaa kofia na miwani yangu vizuri ili kuepuka kutambulika,

Majira ya saa 5 tulirudi nyumbani

"Dada haya Mambo hayana ukweli na baada ya hapa utasikia Mambo mengi zaidi Ila unanijua mdogo wako sijawahi kuwa mwizi na siwezi kuwa"

Nilisema Kisha nikaenda chumbani...nilichukua kile kibegi changu na vitu vyangu vya muhimu, mfukoni nilibaki Kama na elf 30 hivi nikaondoka!

Sikutaka kuendelea kukaa na sister pale

Nilitoka huku Nikiwa sijui naenda wapi lakini niliona nirudi mlandizi nikachukue pesa na kadi zangu za benki kabla hawajazifunga....


Nilifika mbezi standi na nilipata Gari la mizigo lilikokuwa linaelekea chalinze, niliwapa elfu tano nikapanda na Safari ikaanza jamaa walikua wakipiga story kuhusu Allan

"Aisee Yule dogo noma Sana, millioni 50 usawa huu hata ingekuwa Mimi ningesepa nazo"


Alisema dereva

"Sio milioni 50 unaambiwa dogo alipiga hamsini keshi, Kisha akapiga ishirini za kwenye makaratasi yaani hizo anaenda kuzitoa mbele kwa mbele halafu akapiga na computer Kama tano hivi za ofisi"


Aliongezea mwenzake...

Nilijikuta nilitabasamu tu
Huku nikiendelea kufuatilia hizo stori zao..


"Unaambiwa dogo alikua anawasomea ramani tuu ,unaambiwa dogo hayupo Tena Tanzania yaani"
Dereva aliendelea kuongea..

"Ah huwez kaa bongo aisee, lakini huwez kujua pengine yupo hapa hapa nchini"

Tuliendelea na Safari Hadi tukafika mlandizi nikashuka zangu tayari ilikua saa 9 kasoro nikaingia uchochoroni nikavaa zile nguo za kike na nikatupia wigi juu na Ile miwani nikampigia Simu Jose


"Oya Niko mlandizi njoo hapa kwa msebene chap"


Ni kweli baada ya Muda mfupi Jose alitokea akiwa anaangaza macho huko na huko alifika mpaka pale niliposimama huku akiendelea kutafuta mwishowe alikuja

"Samahani sista hakuna jamaa alikua hapa dakika chache zimepita?"

Aliuliza

"Acha uboya Jose "
Nilisema huku nikitoa lile wigi..


"Hahaha aisee we Ni noma ushafkia kujigeuza demu?"

Jose alisema akiangalia huko na huko, tuliongozana na kupita vichochoro Hadi kwa Jose

Story zilikua zile zile..

Kwa bahati Jose alikua na piki piki tukaenda Hadi kwenye nyumba yangu nikazama ndani na kuchukua kadi zangu za benki kwenye akaunti yangu ya mshahara ilikua na pesa ambazo nilikua nimeomba mkopo Kama milioni 9 hivi na laki 3 ambazo ziliingia Ile siku ya tukio

Nilikua na akaunti yangu nyingine ambayo ndio nilikua naweka akiba zangu pamoja na Kodi za nyumba pamoja na pesa alizokuwa ananipa Janet,


Tulienda kwenye atm nikatoa pesa kwa kiwango kilichowezekana Kisha nikazigawa nilimuachia Ile atm yangu

"Sikiliza utakuwa unatoa kila siku milioni moja mpaka hizi pesa ziishe maana wataifungia siku sio nyingi weka kwenye hii akaunti yangu nyingine na endapo ukatokea umeshikwa nayo waambie mi nilikuachia kitambo hii kadi ulikua unanisimamia ujenzi wa nyumba wakikuuliza nyumba ipi wapeleke Ile misufini Ile ndogo anayokaa Ima,...

Hakikisha hakuna anayejua kuhusu nyumba nyingine zilipo na kule wife alipo,....

Tumia pesa vizuri tutakua tunawasiliana "


Nitajua namna ya kusolve hii kesi,


Sasa kachukue lile box kule mtafute Jacob"

Mimi napotea Broo"

Nilisema huku nikirudishia Lile wigi

Niliingia kwenye uchochoro mmoja Kisha nikavua Lile wigi na zile nguo za kike nikaweka jeans yangu moja hivi na raba Kisha nikatoa wigi lingine ambalo Sasa lilikua na nywele fupi ambazo Ni nyeusi Kama mwanaume tu aliyefuga nywele zake vizuri... nikatupia na miwani nyingine ndogo ingawa sikujitazama kwenye kioo Ila nilijiambia bila shaka naonekana Kama mtalii fulani hivi kutoka Jamaica...

Sasa nilitembea bila Shida kuelekea stand kuu ya magari ilikua Ni saa kumi na moja na dakika kadhaa Pilika Pilika za Maisha zilishaanza

Nilifika stand na kukata tiketi ya kwenda Dar kwa bas la mapema kabisa,

Niliongea Kingereza kibovu Ila walau tuliweza kuelewana na hakika wengi walijua Mimi Ni mtalii kutoka nje ya nchi....


Tulipanda kwenye Basi safari kwenda Dar ikawadia


SAA mbili na nusu tulikuwa kimara kutokana na foleni kidogo saa 3 na dakika kadhaa tulifika ubungo,

Nilishuka haraka kutoka nje ya stendi nikaenda kujichanganya na wapita njia..


Nilifika wanapouza magazeti nikachukua matatu nikayakunja na kuweka kwenye begi...


Nilinunua kofia kadhaa nguo na raba pear nyingine...

Nilipanga kwenda kutafuta sehemu ya mbali kabisa nje ya jiji niishi kwa kuruka ruka mpaka nitakapohakikisha Jacob na Jose wamepata lile box...


*****************

Niliishi kwa siku tatu Huku nikilala sehemu tofauti tofauti..

Vyombo vya habari vilizidi kuripoti habari zangu..


Siku hiyo nikiwa kwenye katika nyumba moja ya kulala wageni nilimuona Janet akiwa anafungua kongamano la kipolisi Kanda maalum ya Dar es saalam katika hotuba yake alikua akiwashambulia polisi kwa kushindwa kukamata wahalifu,


"Mtu kaiba mamilioni ya pesa na vifaa vya ofisini , lakini Hadi Leo IGP hakuna taarifa zozote, huyu mtu Yuko wapi...hii Ni aibu kwa Jeshi la polisi"
Aliongezea Janet
Alisisitiza ndani ya siku tatu niwe nimepatikana..
Bila shaka Janet alikua Ana hofu baada ya Mimi kuwatoroka vijana wake, alikua na hofu kuu,

Lakini zaidi ya yote alikua na hasira ya "kunikosa"

Labda hii ndio lilikua linamuumiza Sana,

"Aliwazalo mjinga ndilo linalomtokea, soon Janet mama utajua mziki wangu"

Sikutaka kuwasiliana na Jose hata kidogo niliwaza pengine atanipa taarifa za mke wangu sikutaka kuonana na mke wangu katika hali hii..


Nilienda dukani na kununua lap top pamoja na modemu Kisha nikaweka Ile laini nyingine nikaanza kufungua jumbe zangu...


Nilipata ujumbe mwingine kutoka kwa mtu niliyehisi atakua Jacob,


"1/5"

Ujumbe ulikua na maandishi kidogo "moja juu ya 5?"

Nilijaribu kuwaza lakini sikuelewa chochote nikaamua kuendelea na kusoma habari mbali mbali na Sasa niliangalia namna nilivyokua nikisakwa na polisi
Hadi wakati nilishalala sehemu tofauti na zote niliingia kwa mawigi tofauti....

Hata hivyo nilijua hii haitadumu muda mrefu haswa Kama Jose akikamatwa au mke wangu akijulikana alipo...

Niliweka Mipango yangu sawa na hatimaye nikaenda benki Nikiwa na wigi langu ambalo nililipachika jina la kijamaika,


Niliangalia salio na kukuta pesa bado za kutosha na kwa Maisha Yale ningeweza kukaa Hata miezi mitatu, Hata hivyo niliona ili niwe huru zaidi nitafute nyumba na kwa akili za haraka nikaona nisiende nje ya mji Sana Ila nitafute uswazi kabisa lakini nyumba itakayokuwa na kila kitu ndani,

Changamoto ilitokea namna ya kupata nyumba,

Mara nilitabasamu baada ya kupata wazo mujarabu kabisa,

Nilitoka pale benki nikiwa na kiasi Cha pesa nilinunua vocha za kutosha nikatafuta gesti nikalala ...
Uzuri wa Dar watu Ni wengi Sana na Kila mmoja alikua na hamsini zake,

Hivyo nilifika na kuomba chumba kwa Kiswahili Cha kuunga unga nikalala huku nikisubiri usiku nifanye dili langu nililopanga...

Majira ya saa Nne na nusu nilivaa begi langu ambalo lilishaanza kuwa zito kutokana na kuendelea kuongeza mizigo..


Nilichukua boda boda mpaka buguruni.
Kisha nikatembea kuelekea wanakosimama madada poa,



Niliangalia angalia mwenye sifa ambazo nilikua nazitaka kutokana na kazi yangu tukapatana Bei nikachukua tax tukaondoka!


*****************

Anasimulia Aida,

Baada ya Jose kuondoka amani ilijereja na alituletea vitu vingi Sana kesho yake asubuhi tulijaribu kumpigia Tena Allan hakupatikana,

Tulimpigia simu Jose akasema tusiwe na wasi wasi,

Mary aligoma kula chakula Cha mchana kabisa na mwishowe aliamua kujifungia ndani,


Nilijikuta naishiwa pozi hatimaye ikafika usiku kwa bahati nzuri Mary alikua chumbani wakati wanatangaza kwenye taarifa ya habari, hivyo Mara baada ya kuona Ile habari, sikujua naanza vipi kumueleza Mary,


Kwa asilimia 50 niliamini zile habari kwanza kutokana na zile nyumba Allan alizokuwa akijenga lakini pia pesa alizokuwa nazo, ingawa Sasa sikujua Kwanini anifiche Jambo Kama Lile au amfiche mkewe,

Ni wakati nawaza ndipo mama Yake Mary akampigia Simu,


Mary alitoka haraka akaja Hadi sebuleni huku akilia..


"Wanamsingizia mume wangu! Wanamsingizia, Allan hawezi kufanya vile jamani..."

Aliendelea kulia

Alilia Sana na ndipo tukaelewa kwanini Jose alikua anatudanganya..
Nilijaribu kumtia moyo Mary

"Angalia kwanza afya yako mpenzi, Sasa hivi tayari Kuna tatizo hebu usiongeze tatizo lingine kwanza"
Nilimwambia,
Tuliendelea kujadili usiku kucha na Mary akakubali kujivika ujasiri..
 
MADAM PRESIDENT 10

Tulifika mpaka kwenye Ile gesti nikachukua ufunguo na Kuingia ndani,

Yule dada Alikua anapepesa macho huko na huko,

"First Money, brother,!"

Alisema kingereza chake Cha kuunga unga,

"Asubuhi utapata pesa yako"
Nilimwambia huku nikienda bafuni kuoga,


Niliacha kila kitu mezani na nilijaribu kumchungulia Kama atafanya chochote lakini niliona tu amekaa kwenye kiti vile vile akichezesha miguu yake,

Nilimaliza kuoga na kuvaa bukta kule kule bafuni, Kisha nikatoka,


"Kaoge na wewe"

Nilisema huku nikiweka sawa wigi langu kana kwamba Ni nywele zangu


alienda bafuni kuoga Kisha akarudi amejifunga Taulo tu..

"Ila Kaka yangu utaongeza pesa hatukupatana kulala"

Alisema Sasa akipanda kitandani...


Sikumjibu nilikaa kitandani nikatoa laptop yangu nikaendelea na kazi yangu ndogo Kisha nikamgeukia...

"Sijui unaitwa Nana Dada"

Nilisema kwa upole

"Jesca"

"Okay Jesca kwanza samahani lakini naomba uvae nguo zako hatutafanya chochote nataka Kuna Jambo tuongee"

Nilisema bila kumuangalia


"We mkaka vipi yaani unilete Hadi hapa ujue mi nipo kazini ,au unaionaje kwanza? Nakujazia watu hapa Sasa hivi!"
Aling'aka,



"Hahaha sikiliza Jesca tumepata elfu 20, Ila ukasema tukilala niongeze pesa nikasema elfu 30,

Sasa Mimi nitakupa elf 50 Ila kwanza unisikilize"


Nilisema Sasa nikimgeukia,


"Sitaki kujua kwanini unafanya hii biashara, Ila macho yako yanaonekana kabisa hutaki kuifanya hii biashara"

Nilianza hotuba yangu,

"Nimekuchagua wewe nikiamini utanisaidia kazi yangu ndogo"

"Hivi karibuni umesikiliza vyombo vya habari unaweza kumjua huyu jamaa?"
Nilisema nikimgeuzia picha yangu pale kwenye laptop

"Mmmh ndio Nani sijui mkurugenzi wa huko mlandizi aliyeiba milioni Mia sijui?"

Alisema Jesca,

"Yap, "
nilitabasamu Kisha nikatoa lile wigi na kutoa miwani

"Aah kumbe ndio wewe"

Alisema Jesca huku akionyesha kutokujali Sana..


"Okay Sasa iko hivi Mambo Ni tofauti na wanavyosema huko nje, sijaiba hizo pesa ingawa najua zilipo, Sasa Cha kwanza kabisa nataka ukubali kunisaidia au la nikupe pesa yako elfu 20 usepe na naamini hutamwambia yeyote, Kama ukikubali nitakuambia Jambo lenyewe"

Nilisema

"Okay niambia nione namna ya kukusaidia"
. alisema

"Kwanza nataka utafute nyumba uswazi Kama manzese, tandale, temeke au buguruni ya vyumba viwili au vitatu na sebule ukishapata nitakupa pesa ulipie miezi mitatu, Ila ionekane ni wewe unapanga, lakini rafiki zako au mtu yoyote asifahamu, ukishapata hiyo nyumba utanipigia kwenye namba hii 0688 990 975

Uniambie hivi
"Kuku wako tayari "
Nitakuambia tukutane wapi..


"Mmh Ila Kaka Yangu Mimi naogopa haya Mambo jamani Nina familia inanitegemea"
Alisema

"Jesca kwa mtazamo Wangu kazi hii unayofanya Ni ngumu zaidi ya hii"

Nilimwambia

Nilitoa elf 50 na kumpa Kisha nikamruhusu aondoke zake,


****************

Ilikua majira ya saa 10 baada ya siku tatu,

Jesca alinipigia kuwa kuku Yuko tayari manzese,.


Tulikutana manzese darajani nikiwa nimevaa vile vile Lile wigi kubwa kichwani tulitembea na kushuka vichochoro vya mitaa mpaka tukafika kwenye nyumba yenyewe

Ilikua nyumba ya vyumba vitatu na sebule niliangalia na kuikubali wakati nataka kutoa kiasi Cha pesa nimpe nilijjikuta nikitazamana na mitutu ya bunduki,

Askari walikua chumba Cha pili,

"Jesca umeshindwa kuniamini mama?"

Nilisema niking'ata meno kwa hasira

Jesca Sasa alianza kunionea huruma huku akijaribu kuniomba radhi kwa macho ..

Polisi waliniweka Kati Kati huku mmoja akiwasiliana na makao makuu kuwa wapo na Mimi,

Niligeuka Tena kumuangalia Jesca huku nikimtingishia kichwa...

Tulitoka kwenye Ile nyumba huku Polisi mmoja akiwa amebeba begi langu tayari walishanivalisha pingu mkononi,

Kwa mbali nilisikia Sauti za ving'ora na wakati tunatokea barabarani tayari magari ya polisi yalikua Kama utitiri, wananchi walikua wameshaanza kujitokeza barabarani na waandishi wa habari kibao,

Niliingizwa kwenye Gari ya polisi huku msafara ukianza kuelekea kituo Cha polisi magomeni,


Polisi walifanya kazi ya ziada kuzuia umati wa watu ambapo kila mmoja alikua anataka kuniona

Tuliingia kituo Cha polisi nikapelekwa moja kwa moja kwenye chumba Cha mahojiano,

Polisi walinitoa Lile wigi na miwani na mahojiano yakaanza Polisi walitaka kujua zilipo pesa nilizoiba
Milioni hamsini,


Niliwajua vizuri Polisi wetu wa Tanzania endapo ningekataa Basi wangenipiga Sana wakiamini Ni kweli najua pesa zilipo


"Nitawaeleza kila kitu lakini kabla ya yote Kuna ujumbe nataka ufike kwa Raisi moja kwa moja"

Nilisema

"Hahaha wewe mpuuzi huo muda hatuna, sema pesa iko wapi"

Alisema Yule Afande.

"Afande nilishakuahidi kukupa ushirikiano ,na wewe nipe ushirikiano!"
Nilisema kwa upole Yule Askari alitoka na Kama dakika kumi hivi alirejea..

"Haya lete huo ujumbe wako tuupeleke"

"Kwani wewe ndio Raisi?"

Hakunijibu kitu aliachia bonge la kibao mpaka nikaona Giza hivi,..

"Basi Afande utaniua bure tu, lakini pasipo ujumbe wangu kumfikia Raisi moja kwa moja sitaongea chochote"

Nilisema huku nikifumba macho ili kusubiria Kama kutakuwa na kipigo


Yule Askari alitoka na Kama dakika ishirini alikuja kunitoa na kunipeleka chumba kingine kulikua na Simu ya ofisini,


Baada ya muda Simu iliita na ikasadikika mheshimiwa Raisi yupo hewani,

Nilikua naijua Sauti ya Janet hivyo wasingenifanyia mchezo wowote wale Askari...

"Halo Una dakika mbili za kueleza Shida yako baada ya sekunde kumi kutoka Sasa Raisi ataongea na wewe,

Nilisubiri sekunde kumi na kweli Janet alienda Hewani.


"Hello bila shaka una Jambo la Msingi Allan"


Alisema Janet sauti yake ilijaa hofu

"Ni kweli tafadhali Sana kabla sijahukumiwa nilikuwa na kitu fulani ningependa kukupa haswa ikizingatia wewe Ni Raisi wa watu wote Kuna Jambo lipo nyuma ya hii kesi Kama Raisi nataka ulijue" nilianza.


"Allan kumbuka upo chini ya watu wa usalama hapo Ni vyema ukajikita Sasa kueleza hoja yako ya Msingi una dakika moja"

Alisema

"Tuma watu wako Sasa hivi waende pale Kimara darajani Kuna mtu anauza vitabu anaitwa bwana nditi, Kuna mzigo niliacha kwa ajili yako"

Nilisema Kisha Mimi ndio nikakata Simu!

Polisi waliangaliana tu, Kisha nikarudishwa kwenye chumba Cha mawasiliano..

Nakumbuka kila jioni nilifika kwa Bwana nditi pale Kimara na kuchukua kitabu kimoja nikatafuta gesti nikalala,

Kwa muda wa wiki nzima pale tayari nilishasoma vitabu vitano,

Nilijua lazima ipo siku nitakamatwa hivyo niliweka tahadhari
Nikachukua picha moja na barua moja ambayo alikua ameniandikia Janet nikaitoa nakala mbili Kisha nikaweka kwenye bahasha,


Nilifika siku hiyo baada ya kuchukua kitabu nilimwambia Bwana Nditi aweke hiyo bahasha siku yoyote Kuna watu watakuja kuichukua ,


"Kwahiyo pesa umeweka wapi?"

Nilishtuka kwenye dimbwi la mawazo na swali Hilo la polisi,


"Ni kweli nilichukua pesa Ila sio million hamsini"

Nilisema tu huku nilitabasamu

"Umechukua tsh ngap?"

Polisi aliuliza.


"Ni laki 2 na elfu kumi pesa ya posho ya safari"
Nilisema Tena


Yule polisi alicheka tu Kisha akaanza kunishushia kipigo mpaka damu zikaanza kunitoka,

Nilikua nawazuga nikijua muda wowote Janet atapata ujumbe wake niliomuandikia pamoja na Ile picha,


Yule Polisi baada ya kuridhika na kipigo alitoka nilikua najisikia maumivu kila sehemu na sikutegemea Kama ningeweza Tena kuvumilia ilikua Ni wakati namalizia kidato Cha sita Wakati Janet anaenda chuo kikuu tulikutana Korogwe Mara ya mwisho na tukapiga picha nyingi Sana za ukumbusho ,

Tofauti na picha nyingine hii tulipiga kitandani! Tena tukiwa na nguo chache tu mwilini...

Pamoja na barua yake ya upendo ambayo alinitumia alipokua chuo kikuu katika barua hiyo pia alikua amekumbushia mapenzi niliyompa siku Ile Korogwe kuwa hawezi kuyasahau....

"Janet tucheze hii game tuone"
Nilijisemea nikiwa pale kwenye kiti

Niliendelea waliniacha pale pale huku nikisikia majadiliano huko nje, ilikua wazi kulikua na kundi kubwa la waandishi na watu wengine waliotaka walau kuchukua picha,

Nilipiga mahesabu ya muda na kuona Sasa Janet atakua ameshika barua mkononi,

"Hizo Ni copies, hakuna barua yako Hata moja niliwahi kuichana, hakuna chochote ambacho umenifanyia kiwe kibaya au kizuri ambacho sijaweka ushahidi,

Nifutie kesi hii vinginevyo jambo lolote baya likinitokea hutakua salama, utachafuka Sana Janet,
Think about that"

Nilihitimisha katika barua hiyo fupi,


Na hicho ndicho ambacho kilikuwepo katika Lile boksi ambalo nililiweka kule kwenye nyumba yangu,

Katika maelezo hayo kulikuwa na sehemu maalumu ya kupeleka vitu hivyo, pamoja na hayo kulikua na email na nywila yangu , ili kupata taarifa nyingine muhimu juu ya mahusiano yetu...

"Sidhani Kama Janet atakubali Siri ifichuke"

Niliwaza.

***************

Sasa Ni zamu ya Jose kusimulia..


Niliamua kuzima Simu kabisa ili nisipatikane nilikua sina Majibu hususani baada ya Ile taarifa ya habari,


Nisingekua na Jambo la kumueleza Shemeji ..

Kwanza angenilaumu ,


Niliwaza kwenda kuchukua Hilo sanduku, lakini kwanza niliona nifanye mpango wa kuwasiliana nae,

Nilikwenda benki na kutoa zile pesa mpaka zikaisha zote ,

Nilichukua ndoo Kisha nikaweka Michele, halafu nikaziweka zile pesa Kisha nikaweka mchele mwingine juu yake na kupanga ndio nyingine ya mchele juu yake,

Baada ya siku chache ndio nikapata taarifa kuwa Allan amekamatwa manzese ,

Niliumia Sana, muda ule ule nikatafuta usafiri kwenda Dar,

Niliwaza haraka endapo kutakuwa na taratibu zozote za kisheria n.k,

Nilifika dar saa 11 na nusu jioni,

Haraka niliuliza mpaka nikafika magomeni hata hivyo kulikua na watu wengi nikashindwa kabisa kumuona...


Nilikaa pale nje na watu wengine tukiendelea kupiga stori,


Na kila Mara Polisi aliyetoka tulijaribu kusogea lakini hakukua na uwezekano wa kumuona,

Ilipofika saa mbili nikaona nifanye namna, nilimfuata Polisi mmoja na kumvuta pembeni ...


"Afande huyo jamaa Ni Broo wangu naomba Sana kujua kinachoendelea"

"Utaratibu utatorewa wewe kaenderee kusubiri"

Yule Afande alisema akinisukuma hivi..

Niliamua kurudi pale na kuendelea kukaa Mara ghafla tukasikia ambulance na tukatawanywa na polisi,

Ambulance ilipaki baada ya dakika kadhaa nilimuona Allan akiwa chini ya ulinzi mkali akaingia kwenye Ile ambulance na Gari za polisi zikaongoza

Nilitoka mbio na kujaribu kutafuta piki piki Ila sikupata kwa haraka
Wazo la haraka likanijia nikarudi kule ndani..
 
Changudoa na mteja hata iweje usiwaamini
Kukuuza kisa buku dkk sufuri😁
 
MADAM PRESIDENT 11

"Afande samahi Allan anapelekwa wapi?"

Niliuliza nikihema

"Hospitali ya Aga Khan, alipandwa na presha ghafla wakati wa mahojiano"

Alisema Yule Askari sikuchelewa nilitoka mbio nakuchukua boda boda mpaka hospitali,.
Kama kawaida tayari watu walikua wamejaa

Sasa sikuwa na namna isipokuwa kumpigia simu Aida,

Kwanza nilimueleza Hali yote Kisha akanipa namba za dadake Tatu ambaye nae alikua pale pale Dar

Nikampigia tukaelekezana sehemu ya kukutana..

**************
Anasimulia Tena Allan,


Nikiwa pale ndani nilitegemea kwa haraka Janet angefanya mambo lakini baadae nilipata wazo la kuepukana na maumivu nilijiangusha kwenye kiti pale na kulala chini,.

Kwakuwa damu zilikua zinatoka Polisi alipoingia haraka Sana aliita wenzake Kisha wakanitoa zile pingu na kunifuta zile damu nikapewa maji na nikajifanya kufungua macho,

Polisi walizidi kuhaha na Mkuu wa Kituo alionyesha kuchanganyikiwa tayari tukio langu lilishavuta umakini wa watu na kuanza kufuatiliwa..


Hivyo niliongozwa pole pole kuelekea kwenye ambulance iliyokua nje,

Sikuelewa tunapoelekea Hadi baadae niliposhushwa haraka na kupelekwa kwenye chumba maalum ambapo baadae wauguzi waliingia na kuanza kunipa huduma,

Nilikua nimevimba mdomoni, na upande mmoja wa jicho ulikua umevilia damu,

Nilitulia pale kitandani wakati nesi akifanya kazi yake ..

Nilibaki pale hospitali huku polisi wakiendelea kuranda Randa

"Bila shaka Janet amepuuzia " niliwaza nikijaribu kujigeuza,

Manesi walimaliza kunihudumia Kisha wakaniacha nilale,


Sikuweza kulala niliwaza mke wangu, niliwaza watoto wangu na vile vile niliwaza kuhusu dada Yangu nilijua kwa vyovyote vile lazima atakuwa amenifanya jitihada kuniona ikashindikana.

**************

Kesho yake chini ya ulinzi mkali nilipelekwa mahakamani kisutu na kusomewa mashtaka yangu sikutakiwa kujibu chochote,
Hivyo nikarudishwa Tena mahabusu,


Wakati tunatoka waandishi walikua wengi na nilijua mahali fulani dada Yangu atakuwa ananitazama,


Wakati napanda kwenye Gari huku nikijua tayari waandishi wanafuatilia

Nilipaza Sauti..

"Muulizeni Raisi Kwanini anataka kunifunga? Muulizeni?"

Sauti ilisikika vizuri na niliona waandishi wakihaha Hata hivyo tayari ujumbe ulikua umefika na kile nilichokusudia kilifika,

Nilirudishwa mahabusu na kuendelea kukaa kwenye kile chumba,


Baadae kidogo nilikuja kutolewa na Askari mmoja na kuelezwa kuwa yupo mgeni wangu anataka kuonana na Mimi,


Niliingizwa kwenye chumba kingine na kumuona dada mmoja hivi amevaa suruali nyeusi na koti la rangi ya kijivu hivi ,

Alitabasamu huku akinionyeshea sehemu ya kukaa


"Pole Sana Allan,

Ah nataka tuongee kidogo Naitwa Isabela Michael"

Alianza

"Okay "
Nilijibu kifupi

"Aaah nimekuwa nikifuatilia kesi yako Tangu mwanzo na kusema kweli dada yako Tatu Ni rafiki yangu Sana, ndio maana nikaamua kujitolea msaada wa kisheria katika kesi yako hii"

Alisema

"Nitaaminije?"
Niliongea kwa msisitizo.


"Kwa Sasa Sina chochote Cha kufanya zaidi ya kusema tu naomba uniamini"

Aliongea kifupi huku akijaribu kutoa notebook yake.


"Sasa sikiliza kamwambie Janet kuwa kila kitu kitakuwa wazi , mwambie soon ,

Mwambie mapenzi hayalazimishwi!"

Nilisema nikinyanyuka na kumfuata Yule Askari..


Isabela alisimama kunikimbilia

"No Allan hold on, tafadhali niamini... tafadhali.."

Alijaribu kunisihi lakini hata hivyo niliondoka zangu,.

Na kurudi kwenye kile chumba,


Sikujua kitu gani kilitokea lakini Polisi hawakunihoji Tena na zaidi walinipa chakula kizuri na Sasa niliwekewa godoro kubwa kabisa na kuletewa magazeti ya kusoma,


"Ajabu sana hii"
Niliwaza.

Baada ya siku mbili niliitwa Tena kuwa Kuna mgeni ,

Nilitoka na kwenda kwenye chumba Tena sikuamini macho Yangu safari hii alikua Ni Mr Shija mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri yetu na Ni Bosi wangu,..

Nilijishauri Kama nimsikilize au nimtemee mate nirudi zangu mahabusu,


Tangu nimuone kwenye TV sikutaka kabisa kumuona Tena katika maisha Yangu,


Nilijishauri baadae nikakaa kumsikiliza,


"Pole sana young Broo, maisha hayawezi kusimama jitie Moyo"


"Sema Shida yako Broo, sidhani umetoka kote huko kuniambia hivi"
Nilisema nikiwa nimekasirika.

"Mke wako amejifungua, Ila kwa bahati mbaya mtoto amefariki na Hali ya mama si nzuri Sana tunafanya kila liwezekanalo apone"


"Whaaaat, "
Nilijikuta nasema kwa sauti

"Pole mdogo wangu this too shall pass"

Alisema akinyanyuka na kuondoka

Nilibaki pale pale kwenye kiti na nikiwa nimeishiwa nguvu kabisa,

Ina maana mke wangu alizidiwa ikabidi apelekwe hospital mpaka Hawa mabwege wamefahamu,

Pole mke wangu pole Sana Aida,

Jose come on,
Do something...
Njoo Basi hapa kituoni ..


Nilijikuta mawazo yananijia tu
"******************************

Anasimulia Jose,

Dada Tatu alifika muda muda mfupi na kutokana na mazingira yaliyokuwepo tuliona Ni Bora tukaingie kwenye Gari ili tuongee zaidi,


Sikuwa na jinsi nilimueleza kila kitu nilichojua kuhusu Allan na madam Janet,

Alipigwa na mshangao tu,


"Allan mdogo wangu unadate na Raisi? Huogopi mdogo wangu? Jaman Allan, !"

Aliongea kwa uchungu Sana,

Tulijaribu kwenda kule polisi kuomba Tena lakini walikataa kata kata,

Mwishowe polisi mmoja alitushauri tutafute wakili labda anaweza kuingia ndani kuonana nae,


Haraka Sana dada Tatu alimpigia Simu kwa mtu mmoja waliongea kifupi Kisha akamuomba kukutana,

Tuliondoka kuelekea kinondoni ambapo ndipo alipoishi huyo mtu aliniambia anaitwa Isabella,


Tulifika na wakapiga stori zao za wanawake kidogo Kisha maongezi yakaanza


"Isabella Kama nilivyokuambia ,

Mdogo wangu yupo ndani tunaomba msaada wako Isabella tutakupa chochote akitoka"

Alianza dada Tatu,


"Tatu Bwana unajua siwezi kuchukua pesa kwako, Allan Ni mdogo wangu pia, nitamsaidia bila masharti yoyote, hebu Sasa mniambie mnayoyajua, na huyu Ni Nani?"

Isabella alisema,
"Huyu ni rafiki yake anaitwa Jose anajua kila kitu"

Alisema tatu,

Ilibidi kueleza kila kitu ingawa bila kuelewa Mambo ya sanduku na nyumba zake sikusema,

Baadae alitingisha kichwa tu Isabela akiandika andika kwenye daftari lake ndogo,
"Dada Tatu kesi hii isingekua na mkono wa Raisi Ni kesi ya kutoka asubuhi Sana, tunashinda, hakuna Shida kubwa hapa niliyoiona maana kwa kiasi Cha pesa walichotaja lazima Kuna vielelezo mfano Hundi ya izo pesa, benki walizotoa, mazingira ya upoteaji n.k kesho tutaenda kumuona

***************

Kesho yake tulifika mahabusu lakini tukakataliwa Tena, ikabidi Isabella afanye juhudi za kisheria ikiwemo kuomba kibali Cha kisheria , kibali chake Cha kazi na makorokoro mengine Hadi jioni Isabella aliruhusiwa kwenda kumuona,
Tulibaki nje tukimsubiri baada ya dakika 40 alirejea akiwa na huzuni kiasi,

Alisema Allan alikataa kata kata kuongea nae akimtuhumu kuwa ametumwa na Raisi kumpeleleza...

Hata hivyo alisema kesho tutaenda Tena!
 
MADAM PRESIDENT 12

Anasimulia Aida,


Tukiwa bado tunawaza hili na Lile, Mara ghafla Mary alianza kulalamika tumbo,

Alikua akilia Kama mtoto mdogo, nilitoka nje Kama mwehu na kukimbia barabarani kuangalia usafiri nilikosa, nilijaribu kumpigia Jose akasema yupo Dar,

Nilibaki najiuliza Jambo la kufanya nilimwagiza Stella amuandae Mary aandae pia mizigo yake ya muhimu tunakwenda hospital nitoka Tena na kukimbia nje huko na huko,...
Hatimaye bila kuelewa nilijikuta kwenye nyumba ya Jirani Yetu mmoja mama Aika,

Nilimweleza hali halisi na kwa bahati alimpigia mume wake simu akafika akiwa na Gari yake ndogo,
Tulienda kumpakia Mary na mama Aika alikubali kuongozana na Mimi Hadi hospitali,
Tulifika hospital na kwa haraka Mary aliingizwa kwenye chumba Cha upasuaji kujaribu kumuokoa mtoto,

Tulibaki nje na mama Aika,.
Tuliendelea kukaa pale nje lakini Mara kwa Mara walikua wakiingia watu walionekana kama waserikali hivi hii Ni kutokana na magari yao waliokuwa wamekuja nayo,

Mwishowe alikuja mtu mmoja akajitambulisha kuwa Ni mkurugenzi mtendaji wa halmashauri,

"Poleni Sana samahani Nani anamhudumia mke wa Allan?"

Aliuliza

"Mimi hapa"

Nilimjibu Kisha nikasimama kumfuata.

"Bila shaka unafahamu kilichotokea kuhusu Allan, alianza kuongea huku akiangalia huko na huko kana kwamba hakutaka mtu yoyote asijue"

"Naitwa Bwana Shija, Allan Ni Kama mdogo wangu..."

Ndipo Sasa sura yake ikanijia, nilimkumbuka huyu ndie alikua ametangaza kwenye Televisheni siku Ile kuwa Allan ameiba pesa"

Nilishangaa Sana alivyokua anaongea

"Bwana mkurugenzi, wewe si ndi ulitangaza Allan kaiba pesa?"

Nilimuuliza Sasa huku nikiangalia mlangoni kule Kama daktari anatokea

"Dada Yangu Ni stori ndefu, usione hizi ofisi tunakalia wakati mwingine unalazimika kufuata maagizo tu, Sasa tuachane nayo,

Muda si mrefu watakuja polisi hapa kukuhoji,

Wape ushirikiano, lakini Kama Kuna mengine ambayo unahisi ukisema yanaweza kuwa hatari kwa Allan usiseme,

Kuhusu utaratibu wa hospital Kama kutakuwa na malipo ya ziada nitakuja kulipa, kwasasa chukua hii pesa iwasadie ndani ya siku hizi, kukiwa na chochote nipigie"
Alisema huku akitoa laki 2 na kunipa...

Nilibaki nimeshikilia zile pesa kwa mshangao Kisha nikarudi kule kwa mama Aika,..

Baada ya muda mfupi daktari alitokea na kutuita ndani
Daktari alisema mtoto alifariki na Hali ya Mary ilikua si nzuri Sana lakini madaktari walikua wanaendelea na jitihada za kuhakikisha wanaokoa maisha yake...
Tulibaki tukiomba Mungu Mimi na mama Aika ili Jambo baya lisitokee kwa upande wa Mary,
Nilimpata Jose na kumuleza Hali halisi alisema yeye akasema bado hajafanikiwa kumuona Allan,.


*********************

Anaendelea Allan.
Nilifika kule mahabusu huku nikiwa nimejawa mawazo tele kuhusu mke wangu,

Lakini pia nilizidi kuwaza kitu kilichotokea mpaka Janet ashindwe kufanya Kama nilivyomuagiza
Ni wakati naachukua Gazeti la MBONGO

Niliona habari iliyonivutia


"KESI YA WIZI WA MAMILIONI , WANASIASA WAINGILIA KATI"

nilijaribu kuisoma Ile habari,
"Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania mama Devota Limo amesema kwamba kesi inayomkabili afisa michezo Wilaya ya Pwani, Bwana Allan, imegubikwa na utata mkubwa,

Namnukuu

"Bila shaka Kuna Jambo linafichwa, mtuhumiwa alimtaja Raisi wazi wazi kuwa anajua kila kitu kuhusu Ile kesi, lakini tuliona pia Raisi wakati akiongea na makamanda wa polisi aliingilia Kati na kusema Bwana Allan akamatwe ndani ya siku chache,
Lakini pia tunajiuliza huyu mtu anawezaje kuiba kiasi Cha pesa kama hicho? Ni kwamba hizo pesa zilikua mezani?"
Alisema mama Devota wakati alipohojiwa na gazeti hili,

Hata hivyo msemaji wa serikali Bwana David ,

Akijibu tuhuma hizo alisema kwamba Raisi alitumia mamlaka yake kisheria kuagiza Allan akamatwe ajibu tuhuma na sio akamatwe afungwe, na ndio maana yupo mahabusu na sio Gerezani mpaka Sasa, Ni wakati wa mama Devota kuungana na serikali katika kupambana na uhalifu badala ya kutetea uhalifu kila Mara"

Alimalizia,

Hata hivyo kiongozi wa chama Cha TAC, Bwana Ahamad alisema polisi walitumia nguvu kubwa kumhoji Allan na ndio maana inaona aibu kumpeleka mahakamani

"Wamemvunja mkono, na kumuumiza sehemu ya kichwa na mgongo wakati wa kumhoji, walimpiga Sana"

Alisema Bwana Ahamadi,

Bwana Allan anatuhumiwa kuiba fedha taslimu shilingi million 50 , pamoja na kufanya ubadhirifu wa million 20, na kuiba komputa za ofisi,

Kesi hiyo itaendelea Tena siku ya ijumaa wiki hii"

Niliweka lile gazeti pembeni Kisha nikaangalia lingine...
Sasa nilipata picha,
Huko nje kulikua na mvutano tayari Janet anatafuta namna , kesi hii imeshaingia masikioni mwa watu...



Vipi Yule wakili,

"Isabella, ooh shit,"

nilijikuta nang'ata meno kwa Hasira,

Wakati namuona Jana sura yake haikuwa ngeni Sana,

Sasa nilimkumbuka Isabella, alikuja na Dada Tatu katika Harusi yangu miaka michache iliyopita,

Bila shaka ametumwa na dada Tatu,

"Dah Nasikitika sijampa ushirikiano"

Niliwaza nikijaribu kulala
 
MADAM PRESIDENT 13

Kesho yake niliitwa Tena na Askari kuwa mgeni wangu amefika,

Safari hii nilisimama haraka nilifikiri bila shaka angekuwa Isabella,
Ni kweli Isabella alikua akinisubiri na Mara alivyoniona alisimama kunifuata,
Sikutaka kuonyesha Kama namfahamu nilikaa kwenye kiti na kuanza kumsikiliza

"Allan we are going to get you out of this mess"

Alisema huku akitoa notebook yake ndogo bila shaka alikua akikimbizana na muda,

Alijaribu kunihoji vitu vingi ikiwemo namna nilivyoishi na wakuu wangu wa idara, na Kama niliwahi kukabidhiwa pesa yoyote kwa maandishi na vitu vingine ambavyo kwangu sikuona Kama vina maana,

"Unaweza kukumbuka vitu ulivyokuwa navyo siku unakamatwa Kwenye begi lako?" Aliniuliza..

"Yeah, naweza kukumbuka vingi Kama sio vyote,

Kulikua na laptop Dell vostro, 6300 series, Simu Motorola na line, modem, suruali tatu za jeans, madela mawili, mawigi matatu, Tisheti mbili na laki 8 na elf 10, "

"Haya madela na hivi vitu vya kike Ni vya Nini"

Aliniuliza kwa upole Sasa nikajikuta najiuma Uma,

Siku zote wanasema usimdanganye wakili wako...

Kwakuwa hakuuliza Mambo yoyote kuhusu bifu langu na Madam Janet niliona ugumu wa kumueleza uhusiano wa hivi vitu,

"Allan, kuwa mkweli usinifiche kitu"

Aliongea akinitazama usoni.

Niliangalia pembeni kwa aibu
"Ni story ndefu Isabella"
Nilisema

"Usijali niambie"
Alisema
Sikua na namna nilimueleza kwa ufupi kuhusu tulivyoanza uhusiano wetu na Janet mpaka nilivyomtembelea mwezi uliopita Pesa alizonipa na Mambo aliyotaka nifanye..

Jambo la Ajabu Isabella hakuonekana kustuka aliandika andika tu kwenye daftari lake Kisha akaendelea...

"Kwanza tutafuata kanuni na taratibu za kisheria kuhusu hii kesi kukutoa hatiani kwanza Mambo mengine tutawasiliana,

Kesho kutwa kesi itasomwa na wao wataleta ushahidi na mashahidi wao na mwishowe sisi tutaleta ushahidi wetu Kama ujuavyo kwenye sheria Ni jukumu la mshtaki kuthibitisha kuwa umetenda kosa, na sio wewe kuthibitisha kuwa hujatenda kosa"

Aliongea huku akitabasamu,

"Dada yako Tatu na Jose wanakusalimia Sana!" Alisema Isabella...

Aliondoka Isabella na Mimi nikarudi mahabusu huku nikitamani kesho kutwa ifike mapema,
Kesho Yale alhamis tulipanga kukutana na Isabella aje kunipa muongozo kuhusu mwenendo wa kesi,
Hata hivyo siku nzima ilipita na hakukua na dalili za Isabela kutokea...

Mpaka usiku nilikata tamaa ya kumuona Isabella hata hivyo niliona itakuwa amepata dharula na hivyo tungekutana mahakamani tu!

Ijumaa tulipanda kwenye Gari ya wafungwa na polisi kadhaa kuelekea kisutu ambapo kesi yangu itatajwa kwa mwara ya pili,


Nilijaribu kuangaza macho yangu huku na huko sikumuona dada Tatu , Jose Wala Isabella,

Nilidhani watakuwa kwenye chumba fulani pale mahakamani,

Hata hivyo mpaka kesi yangu inasomwa na mwendesha mashtaka,

Sikumuona Isabella!
Nilirudishwa mahabusu Tena na nilifka moja kwa moja na kuchukua gazeti la siku Ile..

"WAKILI AUWAWA KIKATILI DAR"

maiti yake yaokotwa ikiwa uchi"

Kilikua ni kichwa Cha gazeti za Mbongo ambalo nilikua napenda Sana kulisoma nilijikuta nikitetemeka baada ya kuona picha ya Isabella pembeni ambaye Sasa alikua Ni marehemu!

Nilikaa chini huku nikiwa nimeshikilia Lile gazeti huku nikitetemeka,

Mwanzoni nilichukulia Kama Jambo la kawaida tu ,

Nilimchukulia Janet kwa juu juu tu,

Sikutegemea angefikia uamuzi huu wa kumuua Isabella,

"Lengo Ni kunikomoa Mimi tu ama Kuna Jambo lingine?"

Niliwaza ,

"Ndio maana hajatokea mahakamani, maskini Isabella, vipi kuhusu Jose na mke wangu??" Nilijiuliza maswali mengi sana ,


Kesi Yangu upelelezi bado ulikua unaendelea na kwa jinsi nilivyoona Ni Kama Janet alitaka kunikomoa, nikae mahabusu tu muda mrefu nilijaribu kuwaza na kuwazua...


Sikuwa na uhalifu Mwingine katika maisha zaidi ya huo wa "kutembea na Janet"
Kuna haja Sasa niwe mhalifu kabisa...
Niliwaza.
Kwa siku chache nilizokaa pale niliweza kuzoeana na baadhi ya askari hususani chakula kilichokua kinaletwa, nilidhani Ni Janet alikua anaagiza nihudumiwe vizuri lakini baadae nilikuja kugundua mwishoni kabisa mtu aliyekuwa ananihudumia kwa chakula na magazeti....

Kwa mazoea pale mahabusu walitengwa vyumba kadhaa na kwa bahati Mimi nilipewa chumba Cha peke yangu...

Wakati Mwingine baada ya kula chakula Askari nilipiga nao story za hapa na pale, Yule mmoja aliyenihoji na kunipiga sikumuona tena,
Kwa mazoea ya pale endapo mahabusu angeugua usiku polisi mmoja angemsindikiza mgonjwa hospital kwenye Gari la wagonjwa na Kisha Askari wengine zaidi wangefuatia kule hospitali,
Ili kusudi Askari wengine wabaki kituoni...
Nilikaa na kumaliza kuchora ramani zangu zote na nikapanga siku ya jumapili nitekeleze mpango wangu huo...


*************

Jumapili iliwadia niliamka mapema huku nikifanya mazoezi Kama siku zote baadae nikasoma Hadithi ya "ordeal" Kisha nikalala, niliomba Mungu kwa kadri iwezekenavyo nipate usingizi ili kusudi nifanye Jambo langu usiku,.

Ni kweli nilistuliwa na sauti ya Afande kuhusu chakula,
Nilienda kula chakula Kisha nikarudi na kitandani, kwa kawaida Askari alipita Kati ya saa 7 au 8 hivi usiku na kuuliza Hali ya kila mmoja na endapo mahabusu asingeitika Basi Askari angeingia ,

Nilitulia huku nikisubiri muda ufike,

Ilipotimu saa 6 dk 40 nilisikia Askari akipita kwenye vyumba vingine na Ni Kama alitaka kupita kwenye chumba changu nilikua nimeshajiandaa kufanya nilichokusudia kwani Askari kwa kawaida hutumia dakika 18 Hadi 22 hivi kuzunguuka kwenye nyumba vyote na Mara nyingi walimaliza pale kwangu maana ndio kilikua chumba Cha mwisho karibu na kaunta,

Hivyo niliposikia tu Askari anaanza kuita niliamka haraka na kuanza kupiga push up nyingi Sana,

Nilipiga huku nikivuta pumzi na kuhema kwa nguvu jasho lilianza kutoka kwa nguvu niliendelea mpaka Askari alipokuja kuita kwenye chumba changu sikuitikia...

Nilijitupa sakafuni na kuanza kugala gala,
Huku nikipumua kwa nguvu ,

Askari alipoona Ile Hali haraka alimuita mwenzake ambaye nae alishangaa

"Itakuwa malaria Kali"

Mmoja alisema huku nikijifanya kulegea mwili kabisa..
 
Mtu kweli utafutwe nchi nzima Halaf umuamini kahaba umpe 50 anyamaze pesa ndogo sana
 
Back
Top Bottom