Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
Pia unaweza kuisoma hadithi hii na nyingine nyingi bure ndani ya maktaba app(by pictus). install toka playstore.
MIMI ni Kinyozi na nina ndugu sita. Hiki ni kisa cha ndugu yangu wa tano, Alnacha. Katika siku alizokuwa hai baba yetu, Alnacha alikuwa mvivu sana, hata kule kufanya kazi ya kujipatia chakula chake mwenyewe kulimshinda ikawa kila jioni kuomba, na vile alivyokuwa akipewa alikuwa akiviweka ili ale siku ya pili yake. Hata baba yetu alipokufa kwa uzee, aliacha reale mia saba, tukagawana, na kila mtoto alıpata mia mia. Alnacha, ambaye katika maisha yake yote hakupata kuwa na fedha nyingi kama zile, akawa anahangaika nazo asijue la kuzifanya. Mwishowe akaona ni afadhali anunue vioo, na chupa, na vitu vinginevyo vya namna kama hiyo.
Alipokwisha kununua vitu vyake akatoka kwenda kutafuta duka dogo lililo zuri, akakaa kitako mbele ya mlango wa duka lake ila vyombo vyake ameviweka ndani ya kapu wazi mbele yake akingojea wanunuzi wanaopita njia.
Basi akakaa katika hali hiyo huku amelikodolea macho lile kapu, lakini mawazo yake yalikuwa mbali kabisa. Na bila ya kufahamu mwenyewe akaanza kusema kwa sauti kuu, hata yule mshoni alayekuwa na duka mlango wa pili wa duka lake, alimsikia waziwazi aliyokuwa akisema. Alinacha alisema hivi: Kapu hili limenigharimu reale 100, na hizo ndizo zote nilizokuwa nazo. Na maadam sasa nauza rejareja hivi vilivyomo kapuni huenda nikapata reale 200, na katika hizi mia mbili nitanunua tena vioo ambavyo vitanizalia reale 400, na kwa njia hii muda wa siku chache nitakuwa na reale 4000 ambazo zitajiongeza zenyewe mara mbili kwa urahisi. Hata hapo nitakapopata reale 10,000 (elfu Kumi), nitaacha biashara ya vioo niwe mwuzaji wa jonari, na wakati wangu wote utakuwa katika biashara za lulu na almasi na mawe mengineyo ya thamani.
Mwisho, kama nikishatosheka na utajiri wangu, nitanunua nyumba nzuri sana ya shamba, kisha ninunue na farasi wengi halafu nitaishi Maisha ya raha na kuwakaribisha rafiki zangu katika karamu zangu zote nitawaita wapigaji vinanda na pia wachezaji kutoka miji ya karibu, ili waje kuwafurahisha Rafiki zangu. Walakini sitaitupa kazi ya biashara mpaka nipate mali nyingi kama reale laki moja za fedha, na hapo niwapo mtu wa kuheshimiwa sana nitamposa binti ya waziri mkuu nitamwambia babaake kuwa nimesikia habari zinazopendeza juu ya sifa za uzuri na akili ya binti yake. Na kwa hivyo siku ya harusi yetu nitakuwa tayari kulipa reale elfu za dhahabu na kama waziri akiyakataa haya ninayokusudia (lakini naona haitakua vigumu) nitamshika ndevu zake nimvute mpaka nyumbani kwangu.
KISA CHA NDUGUYE KINYOZI WA TANO
MIMI ni Kinyozi na nina ndugu sita. Hiki ni kisa cha ndugu yangu wa tano, Alnacha. Katika siku alizokuwa hai baba yetu, Alnacha alikuwa mvivu sana, hata kule kufanya kazi ya kujipatia chakula chake mwenyewe kulimshinda ikawa kila jioni kuomba, na vile alivyokuwa akipewa alikuwa akiviweka ili ale siku ya pili yake. Hata baba yetu alipokufa kwa uzee, aliacha reale mia saba, tukagawana, na kila mtoto alıpata mia mia. Alnacha, ambaye katika maisha yake yote hakupata kuwa na fedha nyingi kama zile, akawa anahangaika nazo asijue la kuzifanya. Mwishowe akaona ni afadhali anunue vioo, na chupa, na vitu vinginevyo vya namna kama hiyo.
Alipokwisha kununua vitu vyake akatoka kwenda kutafuta duka dogo lililo zuri, akakaa kitako mbele ya mlango wa duka lake ila vyombo vyake ameviweka ndani ya kapu wazi mbele yake akingojea wanunuzi wanaopita njia.
Basi akakaa katika hali hiyo huku amelikodolea macho lile kapu, lakini mawazo yake yalikuwa mbali kabisa. Na bila ya kufahamu mwenyewe akaanza kusema kwa sauti kuu, hata yule mshoni alayekuwa na duka mlango wa pili wa duka lake, alimsikia waziwazi aliyokuwa akisema. Alinacha alisema hivi: Kapu hili limenigharimu reale 100, na hizo ndizo zote nilizokuwa nazo. Na maadam sasa nauza rejareja hivi vilivyomo kapuni huenda nikapata reale 200, na katika hizi mia mbili nitanunua tena vioo ambavyo vitanizalia reale 400, na kwa njia hii muda wa siku chache nitakuwa na reale 4000 ambazo zitajiongeza zenyewe mara mbili kwa urahisi. Hata hapo nitakapopata reale 10,000 (elfu Kumi), nitaacha biashara ya vioo niwe mwuzaji wa jonari, na wakati wangu wote utakuwa katika biashara za lulu na almasi na mawe mengineyo ya thamani.
Mwisho, kama nikishatosheka na utajiri wangu, nitanunua nyumba nzuri sana ya shamba, kisha ninunue na farasi wengi halafu nitaishi Maisha ya raha na kuwakaribisha rafiki zangu katika karamu zangu zote nitawaita wapigaji vinanda na pia wachezaji kutoka miji ya karibu, ili waje kuwafurahisha Rafiki zangu. Walakini sitaitupa kazi ya biashara mpaka nipate mali nyingi kama reale laki moja za fedha, na hapo niwapo mtu wa kuheshimiwa sana nitamposa binti ya waziri mkuu nitamwambia babaake kuwa nimesikia habari zinazopendeza juu ya sifa za uzuri na akili ya binti yake. Na kwa hivyo siku ya harusi yetu nitakuwa tayari kulipa reale elfu za dhahabu na kama waziri akiyakataa haya ninayokusudia (lakini naona haitakua vigumu) nitamshika ndevu zake nimvute mpaka nyumbani kwangu.