Jackal
JF-Expert Member
- Apr 10, 2012
- 9,971
- 13,608
- Thread starter
-
- #21
NITAKUPA TU
SEHEMU YA 018
Yalikuwa mateke mazito kwake,
mateke ambayo yalipigwa katika aina
ya kushtukiza. Alianguka kama furushi
la mahindi. Hakuweza kuinuka. Alikuwa
ametulia akionyesha kupotewa na
fahamu. Masimba hakusubiri, alimfuata
pale chini kisha kumpekua. Vitendo
vyote hivyo vilitendeka katika muda
mfupi tu. Alichukua bastola ambayo
aliikuta kwenye mavazi ya binti yule,
akaondoka akimuacha amelala
sambamba na bunduki yake. Kwa kuwa
alikuwa analitambua jengo lile, na kwa
vile alishawahi kupita katika majengo
yanamna ile. Haikuwa kazi ngumu
kuzikwepq camera za usalama ndani
ya jengo lile. Safari hii aliubadilisha
mwelekeo, aliubadilisha mwelekeo
sababu hakutaka kuua ama kukutana
na wanausalama wasiolijua tatizo.
Alitaka kuondoka bila kumwaga damu
ya mtu isipokuwa pale itakapobidi
kufanya hivyo. Akachepuka hapa na
kutokea pale, mpaka alipofika karibu
na lango la kutokea baharini ndipo
aliposikia king'ora cha hatari. Hapo
akahisi kwamba alikuwa hatarini.
Akaondoka akiongeza kasi kuwahi
kutoka ndani ya jengo. Hakutaka
kukamatwa tena, hakutaka kurudi tena
mikononi mwa watu wa usalama wa
taifa. Alitaka kwenda kuwafikishia
ujumbe wale waliomsingizia. Wale
waliomuwekea mtego na kusababisha
yeye kukamatwa..
******
Muda ulikuwa unakwenda lakini bado
hakumuona Masimba, alikuwa
amezoea kutokumuona masimba
akiwa nje ya nyumba, lakini hili la leo
lilimshangaza na kumtia wasiwasi.
Matukio ya muda mfupi uliopita, kisha
kutokufika kwa masimba mpaka muda
ule, ni kitu ambacho kilimpa wasiwasi.
Akaendelea kuivuta subira huku muda
wote macho yake yakiitizama saa
iliokuwa ukutani. Muda uliendelea
kusogea, hakumuona Masimba,
hakuiona ishara kwamba masimba
atarudi. Hilo likaufanya usingizi wake
upae, hakuiona sababu ya kulala. Kwa
mara ya kwanza alikuwa akimuhitaji
Masimba kuliko siku yoyote nyingine.
Angelalaje wakati masimba hakurudi.
Angelalaje wakati amegeukwa na watu
aliowaamini? Akainuka kutoka
kitandani kwa mara nyingine.
Hakuuona usalama wa kuendelea
kuwepo pale. Akayapitia mavazi yake
sambamba na bastola zake mbili.
Akazivuta hatua kuliacha jumba lao.
Wakati anamaliza kufunga mlango wa
nje akausikia mngurumo wa magari,
magari zaidi ya moja, michuno ya
matairi ndio kitu pekee kilichomfanya
Teddy ahisi uhatari. Uhatari ambao
alianza kuuona pale watu waliovalia
suti nyeusi wakipaa angani na kutua
ndani katika namna inayovutia, namna
ambayo ingekuwa burudani kama
ungekuwa ukiitizama. Teddy hakuwa
mgeni na kikundi hiki, kikundi maalum
cha kulinda viongozi wa taifa hili.
Kuwaona wakitua pale katika aina ile,
lilikuwa jibu kuwa Masimba
ameshageukwa, masimba
ameshaharibu. Kutua kwa watu wale
kukafuatiwa na kitendo ambacho
kilimuacha Teddy akiwaangalia.
Walipotua kwa ndani kila mmoja
alikuwa akichupa katika namna yake
na kwa upande wake, hata
walipomkaribia Teddy hawakuonyesha
kutaka utani. Midomo ya bastola
ilielekezwa kwake, macho ya watu
yakimtizama katika aina ya kumuuliza
maswali. Ni katika maswali hayo
kupitia macho yao Teddy alipohisi kitu.
Kitu ambacho hakikuwa cha kawaida.
Masimba hakufika, watu kuivamia
nyumba yao, gari yao kulipuliwa na
sasa kuvamiwa na kikosi maalum cha
kumlinda Rais ni suala zito sana. Aliiona
siku ile haikuwa nzuri kwako, haikuwa
nzuri kwa kilichotokea. Macho
yalikuwa yakimuangalia yeye kwa aina
ya maswali. Naye akajibu kwa aina ya
sijui kwa kutumia macho. Hawakutaka
kumsikiliza, wawili wakapita huku
wangine wakiendelea kumuweka kati.
Hazi kupita sekunde hata ishirini
walikwisha toka wakiwa na baadhi vitu
mikononi mwao. Hawakuongea tena
na mwanamke yule zaidi ya kumpita
na kuondoka wakimuacha
amesumama. Muda huo huo akayasikia
magari yakiondolewa kwa kasi. Bado
Teddy alikuwa ameduwaa, bado teddy
alikuwa akisafiri mbali kimawazo.
Kupotea kwa madawa ya kulevya,
kushikiwa bastola na washirika
wenzake haikuwa picha nzuri kwake.
Alijua kutakuwa na msukumo kutoka
sehemu moja kwenda sehemu
nyingine. Lakini bado hakulipata
jawabu, nani amelazimisha hili?
Masimba atakuwa wapi muda huu?
Kwa nini Kikosi maalum cha kumlinda
Rais kiwe kwenye hili suala la
kumtafuta masimba? Hayo na maswali
mengine mengi ndio yaliomchanganya
teddy.
Hakuona sababu ya kuendelea kubaki
pale. Aliondoka usiku ule ule akiamua
kwenda nyumbani kwa Jimmy
Lambert. Aliamua kwenda huko kwa
kuwa alitaka kuujua ukweli kuhusu hiki
kinachoendelea kutokea. Pia alitaka
kujua ni nani ambao walikuja
nyumbani kwake. Ilikuwa safari
ambayo alihisi ingekuwa ya Hatari.
Wakati akiwa juu ya usafiri akielekea
nyumbani kwa Jimmy, akamuona mtu,
hakumtilia manani pale alipomuona
mara ya kwanza, lakini akajikuta
akimuangalia yule mtu ambaye sasa
alikuwa akitembea kama mlevi. Macho
yake yakavutika kumuangalia mtu yule
tena na tena. "Masimba!? Yalikuwa
maneno pekee kutoka kinywani
kwake. Kilichofuata ni kuufungua
mlango ili kushuka,lakini ya kufanya
hivyo akaliona gari, gari ambalo hapo
mwanzo aliliona karibu na nyumbani
kwake. Hapo akagundua alikuwa
akifuatiliwa. Mawazo yakumfuatilia
yule mtu mlevi yakaisha. Alimtambua
kuwa mtu yule ni Masimba.
Alimtambua kwa urahisi kwa kuwa
alimjua masimba.
******
Aliendesha gari mpaka maeneo ya
Ambience club, akaipaki gari na
kushuka kisha kuongoza moja kwa
moja mpaka ndani ya ukumbi.
Akatafuta sehemu nzuri ya kukaa.
Katika kuangaza kwake akaiona meza
moja ikiwa tupu. Akasogea hapo,
akavuta kiti nakukaa. Baada ya kukaa
hapo, mhudumu akasogea na
kumuuliza kinywaji gani ambacho
angetaka kutumia. Teddy akamjibu na
baada ya hapo akaendelea kutulia
akiwaza na kuwazua kile alichokiona
kule njiani. Masimba akiyumba njiani,
masimba akitembea katika aina hii ya
ulevi? Kuna nini kimemtokea Masimba?
Kuna nini kimetokea nyuma ya hiki
anachokifanya masimba? Ina maana
kuna hili tu ama kuna kingine nyuma?
Mawazo yake hayo yakakatizwa na
mtu aliyemuona akiingia. Huyu alihisi
kumuona mahala, wakati akiendelea
kuangalia hilo akamuona mtu
mwingine akiingia. Huyu alikuwa
amejibadilisha sana. Licha kujibadilisha
huko lakini alimjua licha ya
kujibadilisha kwake. HUYU ALIKUWA
MASIMBA
SEHEMU YA 018
Yalikuwa mateke mazito kwake,
mateke ambayo yalipigwa katika aina
ya kushtukiza. Alianguka kama furushi
la mahindi. Hakuweza kuinuka. Alikuwa
ametulia akionyesha kupotewa na
fahamu. Masimba hakusubiri, alimfuata
pale chini kisha kumpekua. Vitendo
vyote hivyo vilitendeka katika muda
mfupi tu. Alichukua bastola ambayo
aliikuta kwenye mavazi ya binti yule,
akaondoka akimuacha amelala
sambamba na bunduki yake. Kwa kuwa
alikuwa analitambua jengo lile, na kwa
vile alishawahi kupita katika majengo
yanamna ile. Haikuwa kazi ngumu
kuzikwepq camera za usalama ndani
ya jengo lile. Safari hii aliubadilisha
mwelekeo, aliubadilisha mwelekeo
sababu hakutaka kuua ama kukutana
na wanausalama wasiolijua tatizo.
Alitaka kuondoka bila kumwaga damu
ya mtu isipokuwa pale itakapobidi
kufanya hivyo. Akachepuka hapa na
kutokea pale, mpaka alipofika karibu
na lango la kutokea baharini ndipo
aliposikia king'ora cha hatari. Hapo
akahisi kwamba alikuwa hatarini.
Akaondoka akiongeza kasi kuwahi
kutoka ndani ya jengo. Hakutaka
kukamatwa tena, hakutaka kurudi tena
mikononi mwa watu wa usalama wa
taifa. Alitaka kwenda kuwafikishia
ujumbe wale waliomsingizia. Wale
waliomuwekea mtego na kusababisha
yeye kukamatwa..
******
Muda ulikuwa unakwenda lakini bado
hakumuona Masimba, alikuwa
amezoea kutokumuona masimba
akiwa nje ya nyumba, lakini hili la leo
lilimshangaza na kumtia wasiwasi.
Matukio ya muda mfupi uliopita, kisha
kutokufika kwa masimba mpaka muda
ule, ni kitu ambacho kilimpa wasiwasi.
Akaendelea kuivuta subira huku muda
wote macho yake yakiitizama saa
iliokuwa ukutani. Muda uliendelea
kusogea, hakumuona Masimba,
hakuiona ishara kwamba masimba
atarudi. Hilo likaufanya usingizi wake
upae, hakuiona sababu ya kulala. Kwa
mara ya kwanza alikuwa akimuhitaji
Masimba kuliko siku yoyote nyingine.
Angelalaje wakati masimba hakurudi.
Angelalaje wakati amegeukwa na watu
aliowaamini? Akainuka kutoka
kitandani kwa mara nyingine.
Hakuuona usalama wa kuendelea
kuwepo pale. Akayapitia mavazi yake
sambamba na bastola zake mbili.
Akazivuta hatua kuliacha jumba lao.
Wakati anamaliza kufunga mlango wa
nje akausikia mngurumo wa magari,
magari zaidi ya moja, michuno ya
matairi ndio kitu pekee kilichomfanya
Teddy ahisi uhatari. Uhatari ambao
alianza kuuona pale watu waliovalia
suti nyeusi wakipaa angani na kutua
ndani katika namna inayovutia, namna
ambayo ingekuwa burudani kama
ungekuwa ukiitizama. Teddy hakuwa
mgeni na kikundi hiki, kikundi maalum
cha kulinda viongozi wa taifa hili.
Kuwaona wakitua pale katika aina ile,
lilikuwa jibu kuwa Masimba
ameshageukwa, masimba
ameshaharibu. Kutua kwa watu wale
kukafuatiwa na kitendo ambacho
kilimuacha Teddy akiwaangalia.
Walipotua kwa ndani kila mmoja
alikuwa akichupa katika namna yake
na kwa upande wake, hata
walipomkaribia Teddy hawakuonyesha
kutaka utani. Midomo ya bastola
ilielekezwa kwake, macho ya watu
yakimtizama katika aina ya kumuuliza
maswali. Ni katika maswali hayo
kupitia macho yao Teddy alipohisi kitu.
Kitu ambacho hakikuwa cha kawaida.
Masimba hakufika, watu kuivamia
nyumba yao, gari yao kulipuliwa na
sasa kuvamiwa na kikosi maalum cha
kumlinda Rais ni suala zito sana. Aliiona
siku ile haikuwa nzuri kwako, haikuwa
nzuri kwa kilichotokea. Macho
yalikuwa yakimuangalia yeye kwa aina
ya maswali. Naye akajibu kwa aina ya
sijui kwa kutumia macho. Hawakutaka
kumsikiliza, wawili wakapita huku
wangine wakiendelea kumuweka kati.
Hazi kupita sekunde hata ishirini
walikwisha toka wakiwa na baadhi vitu
mikononi mwao. Hawakuongea tena
na mwanamke yule zaidi ya kumpita
na kuondoka wakimuacha
amesumama. Muda huo huo akayasikia
magari yakiondolewa kwa kasi. Bado
Teddy alikuwa ameduwaa, bado teddy
alikuwa akisafiri mbali kimawazo.
Kupotea kwa madawa ya kulevya,
kushikiwa bastola na washirika
wenzake haikuwa picha nzuri kwake.
Alijua kutakuwa na msukumo kutoka
sehemu moja kwenda sehemu
nyingine. Lakini bado hakulipata
jawabu, nani amelazimisha hili?
Masimba atakuwa wapi muda huu?
Kwa nini Kikosi maalum cha kumlinda
Rais kiwe kwenye hili suala la
kumtafuta masimba? Hayo na maswali
mengine mengi ndio yaliomchanganya
teddy.
Hakuona sababu ya kuendelea kubaki
pale. Aliondoka usiku ule ule akiamua
kwenda nyumbani kwa Jimmy
Lambert. Aliamua kwenda huko kwa
kuwa alitaka kuujua ukweli kuhusu hiki
kinachoendelea kutokea. Pia alitaka
kujua ni nani ambao walikuja
nyumbani kwake. Ilikuwa safari
ambayo alihisi ingekuwa ya Hatari.
Wakati akiwa juu ya usafiri akielekea
nyumbani kwa Jimmy, akamuona mtu,
hakumtilia manani pale alipomuona
mara ya kwanza, lakini akajikuta
akimuangalia yule mtu ambaye sasa
alikuwa akitembea kama mlevi. Macho
yake yakavutika kumuangalia mtu yule
tena na tena. "Masimba!? Yalikuwa
maneno pekee kutoka kinywani
kwake. Kilichofuata ni kuufungua
mlango ili kushuka,lakini ya kufanya
hivyo akaliona gari, gari ambalo hapo
mwanzo aliliona karibu na nyumbani
kwake. Hapo akagundua alikuwa
akifuatiliwa. Mawazo yakumfuatilia
yule mtu mlevi yakaisha. Alimtambua
kuwa mtu yule ni Masimba.
Alimtambua kwa urahisi kwa kuwa
alimjua masimba.
******
Aliendesha gari mpaka maeneo ya
Ambience club, akaipaki gari na
kushuka kisha kuongoza moja kwa
moja mpaka ndani ya ukumbi.
Akatafuta sehemu nzuri ya kukaa.
Katika kuangaza kwake akaiona meza
moja ikiwa tupu. Akasogea hapo,
akavuta kiti nakukaa. Baada ya kukaa
hapo, mhudumu akasogea na
kumuuliza kinywaji gani ambacho
angetaka kutumia. Teddy akamjibu na
baada ya hapo akaendelea kutulia
akiwaza na kuwazua kile alichokiona
kule njiani. Masimba akiyumba njiani,
masimba akitembea katika aina hii ya
ulevi? Kuna nini kimemtokea Masimba?
Kuna nini kimetokea nyuma ya hiki
anachokifanya masimba? Ina maana
kuna hili tu ama kuna kingine nyuma?
Mawazo yake hayo yakakatizwa na
mtu aliyemuona akiingia. Huyu alihisi
kumuona mahala, wakati akiendelea
kuangalia hilo akamuona mtu
mwingine akiingia. Huyu alikuwa
amejibadilisha sana. Licha kujibadilisha
huko lakini alimjua licha ya
kujibadilisha kwake. HUYU ALIKUWA
MASIMBA