Episode Five
Siku iliyofuata nilifunga safari hadi Nanenane ili kutazama kama Jane alikuwa bado yupo pale na yupo salama katika upande wa Afya. Masikini Jane, alijuta kwanini alijuana na mimi. Nilijuta kwanini nimemzoea binti wa watu na kumweka katika wakati mgumu.
Kwanza alikuwa amepigwa hasa maeneo ya kichwani, kibanda ambacho walikuwa wanaishi wote watatu kilibomolewa huku mbira yake ikiharibiwa. Yote haya yalifanywa na Judy, kibaya ni kwamba Jane aliponiona hakuwa hata na hamu na mimi. Alinichukia na alikuwa na hasira ambazo zilipelekea hadi kunishikia kisu, alitaka kuniua. Alinifukuza kwa ishara akitaka nitoke huku akilia kabisa.
“Sio mimi Jane! Sijafanya haya lakini” nilijaribu kujilalamisha ila nani wakunitetea ikiwa Mama yake mlezi haoni labda angenitetea, ndugu yake ni bubu hakuwa na uwezo wa kuongea hata yeye mwenyewe alikuwa ni Kiziwi ambaye hata kuongea kulikuwa na shida.
Nilibaki nikidondosha machozi, niliumia moyoni hadi mwilini. Nikashikwa hasira dhidi ya Judy, niliona napaswa kwenda kumkalipia. Nakumbuka niliondoka pale nikiwa nimempatia Tsh laki mbili lakini aliitupa chini na kusigina. Hasira zilimuongoza, nami sikuikotoka ile hela. Niliamua kuiacha nikiimani kuwa angeiokota.
Safari yangu ilitua hadi Ikulu ambapo nilikuta kukiwa na kikao cha familia kimekaa yaani Baba, Mama, Mama Judy pamoja na Rais. Niliingia moja kwa moja katika kikao na kumchomoa Judy, kwa hasira.
“Ebu njoo kwanza unieleze”
“Niachie Jack”
“Sikuachi hadi uje useme nani ambaye alikuambia kuvunja kile kibanda” hili lilikuwa ni kosa kwangu, my daddy and mommy walikuja juu. Walikuja juu na kuanza kuniwakia.
“Huna akili wewe? Unakili nakuuliza?”
“Baba! Sio kwamba sina akili lakini Judy amevunja mbira ya Jane, anategemeaje?”
“Unadhani napenda unavyonitesa kihisia?”
“Lakini wote hawa ambao waliopo hapa wanajua ukweli kuwa sikupendi”
“Unipendi si ndio?”
“Ndio sikupendi na sina hata hisia na wewe, ni vile baba na Mama waliamua kutufanya tuwe pamoja lakini sio kweli kwamba nakupend—”
“Mtoto mjinga sana wewe” Baba alinipiga kofi nzito huku akinitusi, nilimtazama Baba kwa hasira kisha niliondoka na kuelekea chumbani kwangu nikiwa nimefuraha kwa hasira.
Huu ndio ukawa mwanzo wa Mimi kususa kila kitu katika Ikulu, kwanza nilishikwa na hasira. Hakuna mtu ambaye alidiliki kuniongesha kwa zaidi ya siku mbili. Nilikuwa nawaza kwanini naishi maisha yake? Kwanini namfanya Jane anateseka ikiwa sijui anaishi katika nini?
Siku ya tatu nilimuita Judy na kuzungumza naye, ilikuwa ni chumbani kwake ambapo yeye alikaa kwenye kiti huku mimi nikiwa nimekaa katika sofa.
“Unamtesa mwenzako, unadhani bado una mapenzi ya dhati?”
“Nawe unanitesa mimi unategemea nini?”
“Sikupendi, kwani unanilazimisha?”
“Mbona hukusema mapema nikatafuta mzungu wangu huko marekani nikaishi vizuri?”
“Waliokuwa nyuma yako wanajua nini kinaendelea”
“Basi nawe utajua nini kitaendelea jifanye kuwa mbishi. Nina nguvu, nina mamlaka na baba yangu ni Rais, lolote lile ambalo naamua basi lazima litimie” Judy alisisitiza.
Taarifa za sintofahamu yetu ilimfikia Rais ambaye alishikwa na hasira sana, basi jioni moja aliniita. Nami nilienda kumsikiliza.
“Mwenzako anateseka na tulikubaliana kwa kila kitu”
“Ni kweli Mtukufu Rais lakini kwa sasa nimebadilisha maamuzi, nampenda mtu mwingine”
“Unadhani upo sahihi?”
“Hata kama utaniona sipo sahihi lakini niheshimiwe kwa hili”
“Binafsi sitataka kukuona ukiishi Ikulu, utatafuta makazi mengine hadi pale ambapo utaamua kurudi kwa mwanangu”
“Ahsante na samahani kwa makosa haya” Nilikuwa tayari kutoka katika jengo ambalo linaheshimiwa mchini lakini yote yakiwa ni sehemu ya mapenzi kwa Jane.
Basi taarifa hii ilifika kwa Baba pamoja na Mama, hawa walinijia juu. Walikuwa tayari kunipa radhi, walikuwa wamechukia sana. Baba hakuacha kufoka, nami kama kawaida yangu. Alipofoka basi nilijinunisha, nikitaka kuondoka katika lile jengo lakini wao hawakuacha kunisisitiza nimuoe Judy.
Baba ilifika hatua alikuwa ananipiga vibao mbele ya Anna ambaye hakuwahi kuniona nikipigwa. Nilipatwa na hasira, damu yangu mwilini ilichemka maana sikuwa napenda dharau kama hizi. Nilimtazama Baba huku nikiwa nimekunja ngumi, naye alisisitiza kwa kusema.
“Nipige si unanipangia ngumi, nipige sasa” Nilimuomba sana Mungu kupoza hasira zangu, kwa bahati nzuri hasira zilipoa. Kwakuwa nilichukia basi niliamua kuondoka katika eneo lile, nilienda kubeba vitu vyangu ikiwemo begi na kutoka nalo nje.
Nilienda kuweka katika gari tayari kwa kuondoka lakini Mama na Baba walikuja na kuchukua funguo wakisema.
“Umeshakuwa na una uwezo wa kufanya maamuzi yako binafsi bila kutumia mali zetu, nenda. Acha hizi mali, hazikuhusu” Mwanaume ambaye ni baba yangu ndio alitoa maamuzi haya. Kwakuwa nilikuwa na hasira, niliamua kuondoka na sikutaka kurudi tena.
Lakini nyuma Judy alilia sababu alikuwa ananipenda, aliona kabisa anaenda kumpoteza mwanaume wa ndoto zake yaani kuolewa na mimi. Kila mmoja katika Ikulu alidhani kwamba nimerogwa, kila mmoja aliniona mjinga lakini binafsi niliweka msimamo wangu.
Niliimani kuwa chaguo langu alikuwa ni Jane na kile ambacho amefanyiwa hakikuwa kitu cha kiungwana, napaswa akuwajibika kama sehemu ya watu waliomsababishia matatizo. Nakumbuka niliondoka nyumbani huku mvua inanyesha, nilitembea kwa miguu hadi nilipofika Nanenane ambako huko mvua ilikuwa kubwa mno.
Nilikuta kina Jane wakiwa wamepanga miti na kuweka turubai juu. Walikuwa akiishi kwenye kibanda kidogo ambacho hata hakikuwekwa hata udongo wala fito kwa chini. Hapa ndipo walikuwa wakifanya nyumba ya kulala. Hawakuwa na makazi tena tangu walipobombolewa, nilijaribu kuongea na Jane lakini bado msimamo wake ulikuwa ule ule kwamba hayupo tayari kwa lolote. Alinifukuza kwa mara ya pili.
Mwisho nikaamua kuchukua maamuzi kama mwanaume, nilichukua panga na kuingia msituni ambako nilitafuta miti ili niweze kujenga kibanda nao wapate