Hadithi ya Kweli: Jini wa Daraja la Selander

Hadithi ya Kweli: Jini wa Daraja la Selander

JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.5.


ILIPOISHIA:
Kwa vile Brighton alikuwa amekwishaoga, Suzana naye alikwenda kuoga na kujumuika wote kitandani. Kama kawaida walisafiri katika meli ya wapendanao, safari ya kwanza ilianza vizuri kila mmoja alifurahia safari ile.
Baada ya safari ya kwanza kwisha, Suzana hamu ilikuwa bado haijamuisha, alitaka asafiri safari moja zaidi ndipo wapumzike.
Ajabu kila alipomgusa mwenzake, jogoo alikataa kuwika kitu kilichomshtua Suzana.
“Vipi mpenzi mbona hivi?”
“Hata mimi nashangaa.”
SASA ENDELEA...

“Au umeanzia kwa mwingine?”
“Lakini kwa nini kila linapotokea tatizo unanifikiria vibaya kuwa nilikuwa na wanawake? Siku hizi sina kazi, kazi yangu kutembea na wanawake,” Brighton alilalamika.
“Mbona leo imekuwa hivi?”

“Hata mimi nashangaa.”
Suzana alijitahidi kumkanda mpenzi wake kumrudisha kwenye hali ya kawaida lakini hakukuwa na mabadiliko, jogoo alikataa kuwika. Aliamua kumwacha ajipumzishe waendelee baadaye. Alijilaza pembeni ya Brighton aliyeonekana mwingi wa mawazo.

Suzana akiwa amejilaza alikuwa na yake aliyokuwa akiwaza, ghafla mazungumzo yake na Sharifa yalijaa kichwani na kuyakumbuka maneno aliyoelezwa juu ya tatizo la mume wake.

“Basi shoga, siku ile niliporudi nyumbani nilikutana kimwili na mume wangu kama kawaida mzunguko wa kwanza ulikwenda vizuri, ajabu wa pili hakuwa na nguvu kila alivyojitahidi, nguvu za kiume ziligoma.”

Sauti ile ilijirudia kichwani mwake na kumfanya atishike na kuamini huenda tatizo la Sharifa limempata na yeye. Bila kujielewa, alijikuta akikaa kitako na kumshtua Brighton aliyekuwa katika dimbwi la mawazo.
“Brighton,” alimwita kwa sauti ya juu japo alikuwa pembeni yake.
“Unasemaje?”

“Hali hii imekutokea mara ngapi?”
“Suzana swali gani hilo, toka niwe na wewe hali hii imeshanitokea?”
“Hapana, basi utakuwa na tatizo la muda mrefu.”

“Lakini siamini huenda ni uchovu ngoja nipumzike kidogo tutaendelea,” Brighton alimtoa hofu Suzana.
“Mmh! Sawa,” Suzana aliguna akiwa na wasiwasi na maneno aliyoelezwa na Sharifa ya mpenziwe kuwa amekufa nguvu za kiume.

Kila mmoja alilala upande wake, mchana waliamka na kwenda kupata chakula cha mchana. Wakiwa wamekaa wanakula, Brighton akamsifia Suzana kwa usafi aliofanya na kuifanya nyumba ipendeze.
“Mpenzi umetumia muda gani kufanya usafi ule?”
“Usafi gani?”

“Wa nyumba,” kauli ile ilimshtua Suzana na kuamini kabisa tayari nyumba yao imeingia kwenye tatizo lakini hakutaka kulikubali mara moja ili kuficha kila anachokiwaza, alijikuta akikubali pongezi zisizo zake.

Baada ya kupata chakula walirudi nyumbani kupumzika, kwa vile kila mmoja alikuwa na hamu na mwenzake baada ya kuoga walipanda kitandani kujiachia kwa raha zao. Lakini hali ilikuwa mbaya zaidi Brighton hakuwa na nguvu za kiume.
Hali ile ilizidi kumweka Suzana kwenye hali mbaya, hakukubaliana nayo, aliendelea kumsaidia mpenzi wake lakini hali ilikuwa ile ile.
Suzana alijikuta akiangua kilio kitu kilichomshtua Brighton na kuhoji:

“Suzana mbona unalia?”
“Brighton unajiona upo sawa?”
“Sijajua nikujibu nini?”
“Hujioni haupo sawa?”
“Hali ya leo inanishangaza hata mimi si kawaida yangu.”
“Inawezekana kuwa ndiyo yenyewe,” Suzana aliropoka.
“Yenyewe nini?”

“We acha tu, kesho nitakwenda kumweleza Sharifa.”
“Kumweleza nini?” Brighton alizidi kuyashangaa maneno ya mpenzi wake.

“Naomba leo tuachane na hilo.”
“Kwani umegundua nini kuhusu tatizo langu?”
“Brighton sijagundua lolote.”
“Mbona unasema utanijibu kesho?”
“Sijajua nini tatizo, linafanana na la Sharifa.”
“Sharifa ana tatizo gani?”
“Brighton tutazungumza kesho, naomba niondoke.”
“Si ulisema utalala?”

“Kwa hali hii siwezi kulala niache tu niwahi nyumbani.”
Brighton hakuwa na la kusema zaidi ya kumruhusu Suzana akalale kwao. Suzana akionekana amechanganyikiwa, aliwasha gari na kurejea kwake. Alijikuta akilia njia nzima juu ya hali ya mpenzi wake huku akijiuliza kama itakuwa hivyo mpenzi wake amekufa nguvu za kiume atafanya nini? Alipoingia ndani kwake alijitupa kitandani hata usingizi ulivyomchukua hakujua.

Suzana alishtuka siku ya pili, alijiandaa kwenda kazini huku akiwa na shauku ya kuonana na Sharifa kumwelezea yaliyomsibu kama yake. Alipofika kazini kiti alikiona cha moto, hakukaa, alikwenda moja kwa moja ofisini kwa Sharifa. Sharifa alipomuona alishtuka na kumkaribisha:

“Mmh! Dada mbona asubuhi asubuhi?”
“Wee acha tu, ukiona hivyo ujue kuna jambo.”
“Karibu, mi ndo naingia sasa hivi hata vumbi sijafuta kwenye kompyuta.”
“Yaani wee acha tu,” Suzana alisema huku akiketi kwenye kiti.
“Mh, kuna kipi kipya?”

“Kuna mapya! Yale yaliyokutokea yamefika na kwangu.”
“Yapi hayo tena?”
“Si yaliyomtokea mume wako.”
“Unamaanisha jogoo kushindwa kuwika?”
“Ndiyo.”
“Ehe!”

Suzana alimwelezea Sharifa yaliyomkuta, baada ya kumsikiliza alishusha pumzi na kusema:
“Unajua unaweza kuona nakutania .”
“Kwa kipi?”
“Jana usiku nilipokutana na mume wangu huwezi kuamini, nimefurahia tendo kama kawaida.”

“Wewee! Mara zote?”
“Tena ajabu lilikuwa penzi tamu ajabu hata asubuhi nimeamka nilihisi kama siku ya kwanza kuonana na mume wangu.”
 
JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.6.


ILIPOISHIA;
Suzana alimuelezea Sharifa yaliyomkuta, baada ya kumsikiliza alishusha pumzi na kusema:
“Unajua unaweza kuona nakutania!”
“Kwa kipi?”

“Jana usiku nilipokutana na mpenzi wangu huwezi kuamini nimefurahia tendo kama kawaida.”
“Wewee! Mara zote?”
“Tena ajabu lilikuwa penzi tamu ajabu hata asubuhi nimeamka nilihisi kama siku ya kwanza kuonana na mume wangu.”
“Usiniambie,” Suzana alishika mkono kwa mshtuko. SASA ENDELEA...

“Hata nashindwa kuelewa hali ya jana inatokana na nini?”?”Au alikwenda hospitali?”
“Walaa, hata yeye anashangaa.”
“Sasa kwangu imetokana na nini?”
“Hapo ndipo nashindwa kujua hali hii inatokana na nini.”

“Yaani nashindwa kuelewa na kubakia njia panda, niliamini lililonitokea jana ndilo lililokutokea wewe wiki moja iliyopita. Leo imekuwa tofauti kabisa uliponieleza hali imebadilika.”
“Suzana hebu nawe angalia kwa wiki tuone mabadiliko, huenda vyakula tunayokula vimesababisha upungufu wa nguvu za kiume.”

“Lakini Sharifa upungufu gani hata kunyanyuka kidogo.”
“Suzana hata kwangu ilikuwa hivyo hivyo, jana sikuamini, tena mume wangu ndiye aliyeniamsha usingizini.”
“Basi inawezekana tatizo hili limeingia, kwani hujawahi kusikia mwingine zaidi yetu mwenye tatizo kama hili?”?”Mmh! Sijawahi.”

“Kama lako limekwisha huenda langu bado nalo litakwisha.”
“Ondoa wasiwasi nina imani litakwisha.”
“Mmh! Sawa.”

Suzana alimuaga Sharifa na kurudi ofisini kwake, alipofika alijikuta akicheka peke yake na kuamini huenda tatizo lile huondoka bila dawa.
Siku hiyo Suzana alishinda akiwa bado yupo njia panda, baada ya kuamini alichokiona Daraja la Salenda ndicho kilichosababisha hali ile.

Lakini ilikuwa tofauti baada ya kukutana na Sharifa na kumueleza kuwa hali ya mumewe kukosa nguvu za kiume imekwisha. Pamoja na kusikia nguvu za mume wa Sharifa zimerudi katika hali yake bado alikuwa na maswali juu ya hali ile kuwatokea wanaume wawili tofauti ilitokana na nini?

Suzana naye alijipa moyo kuwepo na mabadiliko kwa mpenzi wake, lakini walipokutana zaidi ya mara tatu hakukuwa na mabadiliko yoyote. Bado alijipa moyo kwa vile wiki ilikuwa bado haijakatika. Akiwa ofisini kwake akiendelea na kazi alimuona Sharifa akiingia kwa mwendo wa kujivuta.

Alipomuona alishtuka na kumuuliza:
“Vipi shoga mbona hivyo?”
“Wee acha tu, hata sijui hili ni balaa gani?”
“Kwa nini? Hebu kaa kwanza.”

Baada ya kuketi Sharifa alishusha pumzi huku akiuma meno kuonesha kuna kitu kilimuuma sana.
“Vipi shoga kulikoni?”
“Mmh! Hata nashindwa nianzie wapi.”
“Kivipi tena Sharifa mbona unanitisha.”

“Hebu ngoja,” alisema huku akijiweka vizuri kwenye kiti.
Suzana alimuangalia Sharifa kwa huruma alivyokuwa akiugulia maumivu.
“Jamani Sharifa si uende hospitali?”
“Hata sielewi ugonjwa huu ni wa hospitali au vipi.”
“Kwa nini?”

“Hadithi bado inaendelea?”
“Hadithi gani tena Sharifa?”
“Si ile niliyokueleza.”
“Ya?”

“Kuhusu mume wangu na matatizo yake.”
“He! Yamerudi tena?”
“Tena sasa hivi hata kuielezea siwezi.”
“Sharifa mbona unanitisha au bado ni yale yale ya Daraja la Salenda?”

“Inaweza kuwa hivyo.”
“Mmh! Ehe, kwa hiyo tatizo limejirudia?”
“Hapana, ila limezuka lingine.”
“Lipi hilo?”

“Basi shoga siku ile baada ya kukueleza raha nilizipata kwa mume wangu usiku wake vilitokea vitu vya ajabu. Nilipokutana na mume wangu nilishangaa kuhisi maumivu makali kama vile maumbile yake yameongezeka hata kuingia ilikuwa shida.”
“Weweee!”

“Basi shoga wacha nipige kelele za maumivu ambazo zilimshtua mume wangu na kuniuliza hali ile imeanza lini la kuyaona maumbile yake yananiumiza. Nilivumilia lakini sikuona raha yoyote zaidi ya maumivu. Mpaka tunamaliza sikuwa na hamu tena sehemu za siri zilikuwa zikiniuma sana.

“Siku ya pili sikuwa tayari kuendelea kuumizwa, lakini mume wangu alikuwa akinishangaa na kusema mbona yupo kawaida. Siku ile tulifanya gizani, lakini jana tuliwasha taa na kuyaona ya kawaida. Hata tulipokuwa kwenye zoezi sikuhisi maumivu yoyote.

“Baada ya kufanya mapenzi na mume wangu kila mmoja aligeuka upande wake kulala, katikati ya usingizi niliota kuna mtu kaingiza mkono sehemu zangu za siri na kuanza kukoroga, kitu kile kilifanya nihisi maumivu makali sana chini ya tumboni.

Niliposhtuka usingizini nilishtuka kumuona mume wangu akiwa juu yangu, kutokana na maumivu niliyokuwa nikisikia nilimsukuma kwa miguu. Baada ya kumsukuma tumbo lilinikata kwa muda kisha lilitulia.”

“Jamani kama angekuwa na shida na wewe kwa nini usikuambie kuliko kukuingilia bila taarifa?” Suzana alichangia.
“Hata mimi nashangaa mume wangu toka anioe hajawahi kufanya vile.”
“Wewee!’” Suzana alishtuka kusikia vile.

“Hebu ona ajabu nyingine baada ya kumsukuma mume wangu na miguu na kuanguka upande wa pili, aliendelea na usingizi mzito na asubuhi nilipomuuliza alishangaa huku akiapa kwa miungu yote hakuniingilia usiku.”

“Weweee!”
“Yaani nilimueleza yote lakini alibisha na kusema labda nilikuwa naota.
Nilimueleza kuwa alikuwa juu yangu na hali niliyosikia, bado alikataa.

Basi shoga yangu tokea hapo nilishangaa kuiona damu yangu ya hedhi, ilikuwa ajabu kuingia hedhi mara mbili kwa mwezi. Hata kutembea sitakiwi kuharakisha, nikiharakisha chini ya kitovu pananivuta sana.”

“Sharifa unajua tunafanya uzembe, tukija shituka tumekwisha umia.”
“Na kweli hili jambo siwezi kuliacha lipite hivi hivi, sasa hivi mapenzi nayaogopa kwani yamekuwa mateso.”

“Si ulinieleza kuna mtu unayemfahamu tulifanyie kazi, nipo tayari kukusaidia
Mpaka hatua ya mwisho.”
“Nimekuelewa acha nikapumzike, kiuno chote kimenishika na mama amesema anikute nyumbani.”

Suzana na Sharifa waliagana, baada ya kutoka shoga yake Suzana alizidi kuchanganyikiwa. Alijiuliza ni kitu gani tena kilichomtokea Sharifa, alipanga amtafute mtu amuelezee matatizo ya mpenzi wake.
 
JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.7.

ILIPOISHIA;
“Nimekuelewa, acha nikapumzike nyumbani kwani kiuno chote kimenishika na mama amesema anikute.”
Suzana na Sharifa waliagana, baada ya kutoka, Suzana alizidi kuchanganyikiwa juu ya hali ya shoga yake. Alijiuliza ni kitu gani kilichomtokea Sharifa, alipanga amtafute mtu amwelezee matatizo ya mpenzi wake.
SASA ENDELEA...

Sharifa akiwa na maumivu makali ya chini ya tumbo, alitembea taratibu kurudi nyumbani. Suzana alipata wazo la kumsindikiza shoga yake ambaye aliamini kabisa alihitaji msaada wake. Alitoka haraka nje na kumkuta akimtafuta dereva wa kampuni ampeleke nyumbani.

“Sharifa acha nikupeleke mimi.”
“Suzana endelea na kazi, acha tu nitafika.”
“Haiwezekani, lazima nikusindikize.”
“Mmh! Sawa.”

Suzana alikimbilia kwenye gari lake na kuligeuza haraka kisha akasimamisha pembeni ya Sharifa na kumfungulia mlango. Sharifa aliingia na kufunga mlango. Alimpeleka kwake kupitia Barabara ya Ali Hassani Mwinyi. Ajabu walipokaribia Daraja la Salenda, Suzana alipunguza mwendo na kumfanya Sharifa aliyekuwa amejilaza kukaa kitako.

Wote walijikuta wakitupia macho maeneo ya baharini labda wataona kitu chochote lakini hawakuona kitu walichokikusudia zaidi ya kuwaona watu wakitembea juu ya mchanga baada ya bahari kupwa. Baada ya kila mmoja kuwa na uhakika hakuna kitu, Suzana aligeuza uso wake na kubadili gia ili waendelee na safari yao.

Sharifa alikuwa wa kwanza kushtuka na kupaza sauti yake...
“Suzana umemuona yule mwanamke pale pembeni ya barabara?”
Suzana aligeuza shingo tena kuangalia sehemu aliyooneshwa na rafiki yake, kweli alimuona mwanamke mmoja mrefu aliyekuwa amevalia gauni la rangi nyekundu na mtandio wake mwepesi ulioziacha nywele zake nje. Ajabu wakati huo gari lao lilizimika ghafla.

“Suzana vipi, mbona hivyo?”
“Hata mimi nashangaa gari limezimika ghafla.”
“Makubwa, sasa yule dada ni nani?”
“Hata najua, muone jinsi alivyo mzuri, tena anatuchekea labda anatujua.”

“Mmh! Lakini mbona sielewi, nausikia mwili wote ukinisisimka.”
“Siyo wewe tu, hata mimi nasikia nywele zikinisisimka.”
“Mmh! Inawezekana mtu yule si mzuri?”
“Na kweli Suzana, hebu yaone macho yake! Mbona siyaelewi... Mungu wangu! Ona miale inatoka machoni kwake, Suzana washa gari tuondoke.”

Suzana alijaribu kuwasha gari lake lakini liligoma kuwaka, walijikuta wakizidi kupagawa na kutamani kupiga kelele. Sharifa alishtuka kuona mabadiliko kwa yule mwanamke aliyekuwa bado amesimama sehemu ile ile chini ya mti.
“Suzana haya ni maajabu!”
“Ya nini?”

“Muone yule mwanamke, si alikuwa amevaa gauni jekundu na mtandio?”
Suzana alinyanyua uso kumuangalia yule mwanamke na kumuona akiwa na gauni lingine la rangi pinki lililokuwa limempendeza zaidi ya mwanzo, nywele zake zikiwa zimetengenezwa vizuri na kuongeza urembo wake.

“Mmh! Kweli! Kama sikosei alikuwa na gauni jekundu.”
“Unajua yule si kiumbe wa kawaida, huenda ni jini.”
“Jini?”

Kauli ile ilifanya wasikie msonyo mkali ambao ulifanya tumbo la Sharifa livurugike ghafla, baada ya muda lilitulia na kurudi katika hali ya kawaida. Yule mwanamke waliyekuwa wanamshangaa aliwapungia mkono kama anawafahamu, wakajikuta wote wakimpungia mkono, aligeuka na kuondoka kuelekea baharini.

Walijikuta wakimsindikiza kwa macho yule mwanamke aliyeanza kuelekea katikati ya bahari na kupotea machoni mwao.
“Mmh! Suzana hii nini?”
“Hata sijui.”

“Sasa yule atakuwa nani?”
“Yaani nazidi kuchanganyikiwa, ulisikia ule msonyo?”
“Nisiusikie vipi wakati umelifanya tumbo langu lingurume na kutulia.”

Ajabu nyingine, Suzana alipojaribu kuwasha gari liliwaka, wakaamua kuendelea na safari yao huku kila mmoja akijiuliza yule mwanamke mzuri aliyevalia gauni lenye mshono mzuri ambao hawakuwahi kuuona.
“Jamani haya ni maajabu, sasa yule mwanamke ni jini?”

“Lakini jini gani anavaa nguo nzuri kama zile tena za gharama?”
“Mmh! Makubwa, hata sielewi eneo hili lina nini. Kuna umuhimu wa kuulizia zaidi kwa watu ili tupate ufumbuzi.”

Suzana aliendesha gari mpaka nyumbani kwa Sharifa, bahati nzuri walimkuta mama yake ameshafika nyumbani kwake. Hali ya Sharifa ilikuwa tofauti na muda mfupi uliopita akiwa ofisini. Alishangaa kujiona akiwa mzima kabisa, wala hakutembea kwa kupinda mgongo kwa maumivu ya tumbo tena.

Hali ile ilimshangaza hata Suzana kumuona shoga yake yupo katika hali nzuri.
“Sharifa vipi maumivu yamekwisha?”
“Huwezi kuamini sasa hivi sijambo kabisa, siumwi chochote mwilini.”

“Mmh! Mbona mwaka huu wa maajabu, kila dakika kinazuka kitu kipya machoni mwangu.”

“Shoga karibu ndani umsalimie mama uwahi kazini.”
Suzana aliingia ndani kwa Sharifa kumsalimia mama yake. Alipoingia nusura akimbie kwa mshtuko, aliyeambiwa ni mama yake Sharifa alikuwa ni yule mwanamke mrembo waliyemuona maeneo ya Daraja la Salenda.

“Karibu mwanangu.”
“A..a..sante.”
Alishangaa kumuona akitabasamu lakini ajabu Sharifa hakuonesha mabadiliko yoyote zaidi ya kuendelea kumtambulisha kwa mama yake.
“Sharifa huyu ndiye mama yangu.”

Suzana alijiuliza iweje amshangae baharini lakini nyumbani amtambulishe kuwa ni mama yake. Tofauti yake ilikuwa vazi alilovaa, muda ule alivaa hijabu nyeusi na mtandio mwepesi.

Suzana aliaga na kutaka kuondoka baada ya kushindwa kumuelewa mama. Ghafla yule mama alibadilika na kuwa mtu wa makamo tofauti na mwanzo. Suzana aliaga ili aondoke baada ya kushindwa kuelewa alichokiona mbele yake.

Kila dakika imekuwa ikimshangaza Suzana, ni kweli aliyemuona mbele yake ni yule waliyemuona baharini na aligeuka na kuwa mtu mwingine?
 
JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.8.


ILIPOISHIA;
Alishangaa kumuona akitabasamu, lakini ajabu Sharifa hakuonesha mabadiliko yoyote zaidi ya kuendelea kumtambulisha kwa mama yake.
“Sharifa huyu ndiye mama yangu.”

Suzana alijiuliza iweje amshangae baharini lakini nyumbani amfahamishe ni mama yake. Tofauti yake ilikuwa vazi alilovaa muda ule lilikuwa hijabu nyeusi na mtandio mwepesi. Suzana aliaga ili aondoke baada ya kushindwa kumuelewa mama, lakini ghafla yule mama alibadilika na kuwa mtu wa makamo tofauti na mwanzo. Suzana alishindwa kuelewa alichokiona mbele yake. SASA ENDELEA...

Akiwa njiani alijiuliza maswali yasiyo na majibu juu ya mambo aliyokutana nayo ya kumuona mwanamke mzuri aliyebadilika nguo, pia kutambulishwa tena kuwa ndiye mama yake Sharifa. Alijikuta akijiuliza Sharifa huenda naye ni jini lakini wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kwa Sharifa, mtu aliyemfahamu muda mrefu hakuonesha kitu chochote cha kumfanya amdhanie kuwa si mtu wa kawaida.

Alijiuliza ilikuwaje amuone akifanana na mwanamke waliyemuona pembeni mwa Barabara ya Ali Hasani Mwinyi karibu na Daraja la Salenda na baadaye kumuona mtu tofauti. Aliamua kurudi ofisini kuendelea na kazi.

******
Jioni akiwa nyumbani alipigiwa simu na Sharifa, aliipokea na kuzungumza.
“Vipi shoga za muda?’
“Nzuri tu, vipi unaendeleaje?”
“Huwezi kuamini sijambo kabisa kama siyo mimi niliyekuja ofisini nikitembea kwa shida, kingine kilichonishangaza ni kukatika ghafla kwa damu yangu ya hedhi.”

“Wewee!”
“Yaani Suzy siamini kila dakika kwangu ni miujiza.”
“Mmh! Makubwa.”
“Halafu Suzy eti kuna kitu gani kisicho cha kawaida ulikiona tulipofika nyumbani?”
“Kitu gani?”
“Kisicho cha kawaida ambacho kilikutisha,” swali lile lilimshtua Suzy na kujiuliza kwa nini ameulizwa.

“Kwa nini umeniuliza swali hilo?”
“We nijibu kuna kitu nataka kukuambia.”
“Ni kweli, we umejuaje?”
“Hivi nd’o nimeingia toka kwa mtaalamu mama alinipeleka.”
“He ! Amesemaje?”
“Mmh! Shoga mazito si ya kuyazungumza kwenye simu.”
“Kwa hiyo?”

“Kama unaweza kuja nyumbani njoo, maana hapa nilipo niliyoelekezwa yamenichosha.”
“Mmh! Lazima nije?”
“Basi shoga njoo usikie mambo ya dunia.”
Taarifa zile zilimfanya Suzana ajiandae haraka haraka na kuingia ndani ya gari lake, tayari kwenda kwa Sharifa akiwa na shauku ya kutaka kujua kitu gani kilichomfanya aseme vile. Alimkuta Sharifa akimsubiri kwa hamu.

“Karibu shoga yangu.”
“Asante.”
“Naona ndiyo unatoka kuoga?’
“Wee acha mwili ulikuwa umechoka kila kona, karibu.”
“Asante,” Suzana alijibu huku akikaa kwenye kochi.
“Mh! Shoga lete habari,” Suzana alianzisha mazungumzo.

“Basi shoga baada ya kuondoka nilibakia na mama na kumueleza yote yaliyonitokea hata tukio la kuonana na yule mwanamke leo.”
“Ehe.”
“Mama alinieleza lazima yule atakuwa jini.”
“Ehe.”

“Basi alinichukua na kunipeleka kwa mzee mmoja mtaalam wa majini, tulipofika tulikaribishwa kwenye chumba kilichokuwa na mkeka na nyuma yake kulikuwa shuka nyekundu, pia kulikuwa na picha za kuchora za simba na viumbe visivyoeleweka.”
“Mmh.”

“Basi mganga huyo kijana akachukua kioo kidogo na kunitaka niweke mkono juu yake na kuniuliza matatizo yangu. Baada ya muda akatanitaka nitoe mkono na kunitaka nikitazame kile kioo kwa muda kisha alishusha pumzi.

“Huwezi kuamini wakati akikitazama kile kioo jasho lilianza kumvuja yule mganga kama kamwagiwa maji, kitu kilichonishtua sana. Baada ya kushusha pumzi alichukua kitambaa na kukifuta na kutuuliza.”

“Mnataka mtatuliwe matatizo yenu au unataka kujua sababu ya yote yaliyotokea?”
“Wewe utakavyoona inafaa,” Mama alijibu.
“Mama si huwa nasikia eti waganga wanajua kila kitu kilichotokea kabla ya kutibu?” Niliuliza.

“Ni kweli tunajua na yote nimeyaona hapa,” mganga alinijibu.
“Sasa si ungeniambia ili nijue natibiwa kitu gani?”
“Hakuna tatizo, kwa hiyo upo tayari kuyasikia yaliyokusibu?”
“Nipo tayari,” nilimjibu.

“Haya vizuri,” Baada ya kusema vile alichukua unga na kuumwaga mbele yake huku akisema maneno kwa sauti ya chini. Baada ya kusema vile alikichukua kioo na kuangalia tena kwa muda wa kama dakika kumi kisha alitugeukia na kusema:
“Kama nitakuwa nasema uongo naomba ukatae, sitaki nionekane nazungumza tofautina ukweli.”
“Sawa.”

“Unaitwa Sharifa, sawa?”
“Ndiyo”
“Umeolewa?”
“Ndiyo.”
“Ndani ya wiki tatu kumetokea matatizo ndani ya ndoa yako?’
“Ndiyo.”

“Wasiwasi wako ni tukio lililokutokea katika Daraja la Salenda?”
“Kweli.”
“Basi ni kweli tatizo lako lilitokana na tukio la darajani ambalo lilipelekea kukuingizia mgogoro ndani ya ndoa yako. Yule uliyekutana naye ni Jini Balikis, kazi yake kubwa ni kuvuruga ndoa za watu. Si wewe tu kuna watu wengi wamekumbwa na mgogoro huu hata kufikia hatua ya kuachana.

“Hata rafiki yako kipenzi ana tatizo hilo, tena yule ndiye chaguo la Jini Balkis kwa vile ni mwanadamu pekee aliyeshuhudia sherehe ya kuagwa kwake kuja duniani.

“ Tuachane na hayo ya shoga yako najua naye ana yake, ila tatizo la mumeo kukosa nguvu za kiume linatokana na kufanya mapenzi na Jini Balkis.
“Kila mnapofanya mapenzi, jini huyo hufika katika eneo la tukio hilo na kuziondoa nguvu za mumeo ili asiweze kukuridhisha vyema.

“Anafanya hivyo makusudi ili aweze kufanya naye mapenzi yeye wakati wa usiku mkiwa mmelala.
“Kama nasema uongo muulize mumeo kama huwa hafanyi mapenzi na mwanamke mzuri kiasi cha kufikia kukuona wewe hufai tena kwake.”

Huu ni mwanzo wa siri ya Jini la Daraja la Salenda. Nini kiliendelea?
 
JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.9.


ILIPOISHIA:
Kama nasema uongo muulize mumeo kama huwa hafanyi mapenzi na mwanamke mzuri usingizini hadi kufikia hatua ya kukuona hufai tena kwake.”
SASA ENDELEA...

Kauli ile kwa kweli ilinishtua sana, basi mganga akaendelea kuchimbua mambo na kusema:

“Baada ya kufanya vile kitu kile kilikutia wasiwasi kiasi cha kufikiria kutafuta ufumbuzi baada ya kupata tatizo kama hilo kumtokea shoga yako. Kumbuka mwanzo uliamini kabisa tatizo lile linatokana na mwenzako kutokuwa mwaminifu ndani ya ndoa yako kweli?”
“Kweli.”

“Baada ya kupanga mipango ya kutafuta ufumbuzi wa mumeo kupoteza nguvu za kiume na shoga’ako kukutwa kama mtu aliyekufa, pale shoga’ako kama wangechelewa alikuwa anabadilishwa kwa kuchukuliwa maiti yake ambayo ingepelekwa chini ya bahari na yeye Jini kukaa na mchumba wake.”

Kauli ile ilimshutua sana Suzana na kujikuta akishika mdomo kwa mshtuko.
“Mungu wangu, ina maana pale nilikuwa nakufa?” Suzana alimuuliza Sharifa.

“Shoga hebu tulia kwanza unisikilize utaniuliza maswali mwisho japo nina imani maelezo nitakayokupa hutahitaji kuniuliza swali.”
“Mmh! Inatisha sana, haya endelea.”
Basi mganga akaendelea kunieleza:

“Kilichomrudisha shoga yako duniani ni maombi yaliyofanywa na familia yake bila hivyo maisha yake yote yangekuwa chini ya bahari na jini yule kuishi na mpenzi wake kwa kuwa shida yake ilikuwa kusambaratisha ndoa za wanadamu au uhusiano wa watu waliopendana. Baada ya shoga yako kurudi katika hali yake ya kawaida na wewe mumeo akapoteza nguvu za kiume.

“Mlipokutana na kuhadithiana juu ya kilichotokea Daraja la Salenda na matukio yaliyowatokea. Alihamia kwa shoga yako kumtoa nguvu za kiume mpenzi wake. Mwanzo shoga yako hakuwa na imani kuwa kuna vitu kama hivyo vinatokea, vilipomtokea kama ulivyomuhadithia mumeo kutokewa na hali ile, hapo ndipo akaamini kabisa ni kweli tatizo lipo katika Daraja la Salenda.

“Jini Balkis aliwachezea akili kwa kumrudishia mumeo nguvu za kiume ili taarifa za shoga zako zipingane na ukweli ambao ungepata picha ya tukio la Daraja la Salenda.

Kumbuka usiku wa siku ile ulipokutana kimwili na mumeo kulikuwa na tofauti kubwa na siku zote tangu muoane, kweli au uongo?” Mganga aliniuliza.
“Kweli,” nilijibu huku nikiona aibu kutamka maneno yale mbele ya mama.
“Unajua ni kwa nini?” Aliniuliza.
“Hata sijui.”

“Majini wanapotaka kufanya mapenzi na wanadamu huwapaka mafuta sehemu za siri ili asipungukiwe nguvu za kiume ili waweze kumpa raha kwa muda mrefu. Hawapendi kukatishwa raha, huchukia sana. Mwanzo walikuwa wakifanya mapenzi na wanadamu bila kutumia kitu chochote.

“Lakini tatizo la nguvu za kiume ndilo lililowakasirisha na kutafuta njia ya kustarehe na mwanadamu kwa muda mrefu. Njia ilikuwa ni kutafuta dawa ya kumwezesha mwanaume awe na nguvu muda wote wa kufanya mapenzi chombo kisilale, nina imani umenielewa kusema chombo?” Mganga aliniuliza.

“Ndiyo nakuelewa endelea mzee wangu,” nilimjibu huku nikihisi mwili ukinisisimka kwa yale niliyoyasikia. Basi mzee akaendelea huku akiangalia kioo kama anasoma kitu.

“Basi baada ya kujua kesho yake shoga yako naye yamemtokea kama yako na kuamini kabisa mtaamini kilichotokea kinatokana na tukio la Darajani Salenda. Usiku mkiwa mmelala, Jini Balkis alikuja na kumpaka mafuta yale mumeo sehemu za siri ambayo yalizifanya sehemu zake zinyanyuke. Mumeo alikuamsha usingizini kutaka haki yake, kweli au si kweli?” Mganga aliniuliza.

“Kweli,” nilimjibu kwa aibu mbele ya mama aliyekuwa ametulia akisikiliza kwa makini.
“Najua hukuamini kuikuta hali yake tofauti na siku zilizopita za kukosa nguvu za kiume, ulishtuka, hukushtuka?”
“Nilishtuka.”

“Hata ulipokubali kufanya naye mapenzi bado hukumuamini, ulijua ni yale yale ya siku zote, lakini ilikuwa tofauti na siku zote. Pia kulikuwa na tofauti kubwa siku za nyuma ulipofanya mapenzi kwa muda mrefu ulikuwa unachoka sana lakini siku ile ilikuwa tofauti, kweli au si kweli?”

“Kweli.”
“Usijibu kwa kuniogopa, nijibu kwa uhakika siyo ukubali hata la uongo.”
“La uongo nitakuambia lakini yote unayosema ni kweli.”
“Najua asubuhi ulipoamka ulijishangaa kuwa na nguvu za ajabu huku ukikumbuka penzi tamu la mumeo ambalo hakuwahi kukupa tangu akuoe.”
“Ni kweli.”

“Ni kwa nini hukuchoka kama siku zote?”
“Hata sijui, nilifikiri labda kutokana na kukaa muda mrefu bila kukutana na mume wangu.”
“Unataka kuniambia kipindi hiki ndicho kirefu kuchelewa kukutana na mumeo?”
“Hapana.”

“Unajua sababu ya kufurahia penzi la siku hiyo na asubuhi kuamka na nguvu za ajabu hata kazi siku hiyo ulifanya ukiwa na furaha tele moyoni?”
“Hata sijui.”
“Nawe ulipakwa mafuta yale ambayo hutumia majini wa kike, kujipaka sehemu za siri ambayo huongeza raha ya mapenzi kiasi cha kumfanya mwanaume asikuchoke na yeye kusikia raha ya mapenzi.

Hata wewe hukuchoka na kusikia raha muda wote wa kufanya mapenzi na ulipoamka hukusikia uchovu wa mwili. Kwa kutumia mafuta yale unaweza kufanya mapenzi ya nguvu kila siku.”
“Mmh! Kumbe.”

“Wakati wewe unakula raha ndiyo siku hiyo shoga yako yalimtokea kama yaliyokutokea wewe siku za nyuma za mumeo kupoteza nguvu za kiume. Shoga yako alikuja kazini akiamini ungeungana naye kwenye tatizo lake lakini ilikuwa kinyume kitu kilichomchanganya mwenzako na kuwa njia panda tatizo la nguvu za kiume za mpenzi wake lilitokana na nini.

“Baada ya Jini Balkis kuwachanganya, wazo la kutafuta ufumbuzi wa tatizo lenu lilifutika. Hali ile mwenzako aliamini huenda itaisha kutokana wewe kumuhakikishia tatizo lake linaweza kwisha kama lako bila kwenda popote. Naye aliamini na kumpa nafasi Jini Balkis kufanya mapenzi na mpenzi wake usingizini hadi kufikia hatua ya kutokuwa na hamu naye.

Siri ya Jini Balkis imewekwa hadharani, je, ufumbuzi utapatikana au ndiyo kumwagia mafuta kwenye moto?
 
JINI WA DARAJA LA SALENDA......EP.10.


ILIPOISHIA;
“Nawe ulipakwa mafuta yale ambayo hutumia majini wa kike, kujipaka sehemu za siri ambayo huongeza raha ya mapenzi kiasi cha kumfanya mwanaume asikuchoke na yeye kusikia raha ya mapenzi. Hata wewe hukuchoka na kusikia raha muda wote wa kufanya mapenzi na ulipoamka hukusikia uchovu wa mwili. Kwa kutumia mafuta yale unaweza kufanya mapenzi kila siku bila kuchoka.”
“Mmh! Kumbe.”

“Wakati wewe unakula raha ndiyo siku hiyo shoga yako yalimtokea kama yaliyokutokea siku za nyuma za mumeo kupoteza nguvu za kiume. Shogayo alikuja kazini akiamini ungeungana naye kwenye tatizo lake, lakini ilikuwa kinyume kitu kilichomchanganya mwenzako na kuwa njia panda tatizo la nguvu za kiume za mpenzi wake lilitokana na nini.

“Baada ya jini Balkis kuwachanganya wazo la kutafuta ufumbuzi wa tatizo lenu lilifutika. Hali ile mwenzako aliamini huenda itaisha kutokana wewe kumhakikishia huenda tatizo lake likaisha kama lako bila kwenda popote. Naye aliamini na kumpa nafasi jini Balkis kufanya mapenzi na mpenziwe usingizini kufikia hatua ya kutokuwa na hamu naye. SASA ENDELEA...

“Baada ya kuweza kukuchanganyeni akili, penzi mlilofanya na mumeo lilirudisha mapenzi yaliyoanza kutoweka. Kitu kile kilimuudhi sana jini Balkis na kuamua kukukomoa. Najua alichokufanya nikikueleza utaogopa lakini kwa vile umetaka mwenyewe sina budi kukueleza,” kauli ya mganga ilinitisha lakini kwa vile maji nilikwisha yavulia nguo nilikuwa sina budi kuyaoga. Basi mganga akaendelea.

“Usiku mlipokuwa mkifanya mapenzi bila kuzima taa jini Balkis alishindwa kufanya kitu chochote, kosa kubwa mlilofanya japo msingeweza kujua madhara yake. Nina imani mapenzi uliyofanya wakati wa giza na mwanga kuna mabadiliko yalitokea ulipofanya mapenzi?”
“Ndiyo.”

“Mlipokuwa mkifanya mapenzi gizani ulihisi maumbile ya mumeo kuwa makubwa na kusababisha uumie sana badala ya raha ikawa maumivu.”
“Ni kweli kabisa.”

“Basi wakati mlipokuwa mkifanya mapenzi gizani, mumeo aliondolewa juu yako na jini Balkis aliingiza mguu wake uliokuwa na kwato kama mbuzi na kuanza kukusukumia ndani.”
Kauli ile ilinifanya nisijikie vibaya mpaka tumbo likaanza kunikata chini ya kitovu, nikiwa navuja jasho la hofu. Mganga aliendelea kunieleza maneno niliyohisi yananikata maini.

“Basi ulijikuta ukivumilia huku ukiumia, ilifikia hatua kutotamani tena kufanya mapenzi na mumeo kwa kuamini maumbile yake yameongezeka ukubwa. Lakini ulipowasha taa ulishangaa kuyaona ya kawaida uliyoyazoea, kweli si kweli?”

“Kweli,” nilijibu huku nikizidi kumuogopa mganga kuwa na uwezo wa ajabu kuyajua mambo ambayo hakuyaona lakini utafikiri alikuwepo.
“Ajabu hukumwambia mumeo, kwa nini?”
“Hata sijui,” nilimjibu.

“Baada ya kuamua kutofanya mapenzi na mumeo kuogopa kuumizwa badala ya kupewa raha, uliamua kutafuta visingizio ili usikutane naye kimwili, uongo kweli?”
“Kweli.”
“Jana kuna kitu cha ajabu kimekutokea ndiyo sababu ya kumpigia simu Bi mkubwa wako?”

“Ni kweli.”
“Basi, baada ya kuona hufanyi tena mapenzi na mumeo, jana ulipolala uliota ndoto kuna mtu anakuingiza mkono sehemu zako za siri na kuanza kukukoroga kama anavuta kitu toka sehemu zako cha siri na ulipoamka ulijikuta ukitoka damu ambazo uliamini ni za hedhi japo ulishangaa kutokwa na damu ya hedhi mara mbili kwa mwezi kitu ambacho hakikuwahi kukutokea maishani mwako.”
“Ni kweli.”

“Unajua madhara yake?”
“Hapana!.”
“Naomba uwe na moyo mgumu kwa vile alichokifanya kwa tiba ya kubabaisha hutapona milele.”
“Mungu wangu,” kauli ilitushtua mimi na mama na kujiuliza ni ugonjwa gani tena huo Yaillah.

“Baba ni ugonjwa gani tena huo?” Ilibidi mama aulize baada ya mimi kuwa katika wakati mgumu nilishika mikono kifuani, nilimuomba Mungu aniepushe na balaa linalotaka kunikumba.

“Jina Balkis alijiulaumu kwa kuamini alifanya kosa ambalo aliliona limempotezea mapenzi ya mumeo kwake,” mganga alimjibu mama.
“Mapenzi yapi hayo?” Mama aliendelea kuuliza.

“Kosa kubwa alilofanya ni kumpaka mafuta ya kuongeza ladha ya mapenzi mwanao, kumbuka maumbile ya jini na mwanadamu yanatofautiana, kwa vile yako ya kibinadamu baada ya kukupaka ilizidi raha mara dufu na thamani yake kwa mumeo ilishuka. Alichokifanya kilikuwa kukutoa kizazi kitu ambacho ndicho kitakacho vunja ndoa yenu. Katika ndoto ulichokiota ndicho kilichotendeka usiku wa jana. Jini Balkis alikutoa kizazi na sasa hivi huwezi kuzaa tena maishani mwako.”

“Mungu wangu,” kauli ya mganga ilinikata maini.
“Sasa baba utatusaidia vipi?” Mama bado alikuwa na ujasiri kutaka kujua nini hatima ya ukatiri wa jini Balkis kwangu.
“Mmh! Ndiyo maana nikasema ipo kazi tena kazi kubwa sana si ya kitoto na tukifanya mchezo tutapotea wote.”

“Jamani, tupotee kivipi?”
“Vita yake ni kubwa sana, kumdhibiti naweza lakini kama nitakufanyia kinga ya kukufunga huwezi kupona tena. Na kosa lolote linaweza kuhatarisha maisha yetu. Hawezi kukubali kuona anazuiwa kutimiza dhamira yake, kwa kutumia nguvu zake anaweza kututeketeza wote.”

“Unataka kutuambia kuna uwezekano wa kupona?”
“Upo, lakini ndiyo mzame sana.”
“Baba wewe huwezi?” Mama aliuliza tena kwa vile mimi nilikuwa nimechanganyikiwa kwa niliyoyasikia.

“Uongo mbaya, mimi siwezi kukirudisha kizazi chake, si yeye ni wanawake wengi wametolewa na yote kaenda kuiweka chini ya bahari kwenye mwamba wa maji yaliyotulia pia hayafikiwi na kitu chochote kitakachoweza kugusa kizazi kile. Kama utaenda hospitalini wanawake wengi wanasumbuliwa na maradhi ya tumbo na wengi maradhi yao kwa tiba ya kisasa hayaonekani lakini siri ni kwamba wengi wao wameondolewa kizazi na kingine sasa hivi matatizo ya nguvu za kiume yamekuwa mengi ambayo yameweka migogolo lakini mabwana hao wakifanya mapenzi ndotoni na mwanamke mzuri hujikuta hawana hamu na wake zao.”

“Ni kwa sababu gani?” Mama aliuliza.
“Hakuna sababu nyingine ni ya huyo huyo jini Balkis ambaye amekuja duniani kwa sababu ya kuharibu ndoa za watu pia kupata tiba ya tatizo lake la uzazi. Tatizo hili litakwisha akiisha maliza kazi yake ya kupata vizazi mia, ambao walipata bahati ya kutokutana naye. Lakini wengine wote ambao hawatapata tiba mapema ndiyo watakuwa tasa milele.”

Siri nzito za jini Balkis zinazidi kufunguka, nini hatma ya yote je kuna tiba sahihi ya tatizo hilo? Kuyajua yote hayo tukutane EPISODE 11. KESHOOO........
 
Back
Top Bottom