Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Ikawa shani ya kustajabisha kabisa. Wote walisimama kimya kabisa, na mwezi ukawaangaza wakawa kama mwitu wa mikuki, na manyoya yao ya vichwani yalipepea katika upepo.

Popote tulipotazama tuliona mistari kwa mistari ya mikuki inayong’aa.
Nikamwambia Infadus, ‘Jeshi zima limehudhuria?’ akajibu, ‘La, Makumazahn, hii ni theluthi tu. Maana ni theluthi tu huudhuria kwenye ngoma kuu kila mwaka.

Theluthi nyingine imewekwa nje tayari kukomesha matata ikiwa yatatokea wakianza mauaji, elfu kumi hulinda nje ya mji wa Loo, na waliobaki wametawanywa katika miji ya nchi.’

Bwana Good akasema, ‘Wamekaa kimya kabisa.’ Infadus akauliza, ‘Je, Bwana anasema nini?’ Nikamtafsiria, akajibu, ‘Wanaokabiliwa na mauti huwa kimya.’
Nikamuuliza, ‘Wengi watakufa?’ Akajibu, ‘Wengi sana.’

Nikawaambia wenzangu nao wakasikitika kabisa . Nikamuuliza Infadus, ‘Je, waonaje, tutakuwa katika hatari?’ Akajibu, ‘Sijui, mabwana zangu, lakini natumai mtakuwa salama. Maana askari wananung’unika juu ya mfalme.’

Basi wakati huo tulikuwa tukisogea tufike katikati ya nafasi tuliona viti vimewekwa tayari. Tulipokuwa karibu tuliona kuwa wengine wanatoka katika jumba la mfalme, na Infadus akasema, ‘Ni mfalme Twala na mwanawe Skraga na kizee Gagula; na pamoja nao ni wale wauaji.’

Akaonyesha kundi dogo la watu wakubwa sana wenye sura za ukali na ukatili, kila mtu ana mkuki katika mkono mmoja na rungu katika mkono wa pili. Mfalme akakaa katika kiti chake katikati, na Gagula akajikalisha chini penye miguu yake, na wengine walisimama nyuma.

Mfalme Twala akasema, ‘Karibuni, mabwana weupe, kaeni msipoteze wakati wenye thamani, usiku ni mfupi sana na kazi iliyo mbele yetu ni kubwa. Mmekuja wakati unaofaa sana, maana mtaona mambo mkuu sana.

Tazameni, mabwana, nyota zaweza kuwaonyesha shani kama hii? Tazameni namna wanavyotetemeka kwa uovu wao, wale wote wenye uovu katika mioyo yao wanaihofu hukumu ya mbinguni.’

Gagula akalia, ‘Anzeni! Anzeni! Fisi wanaona njaa, wanalilia chakula chao. Anzeni! Anzeni!’

Kwa muda kidogo ikawa kimya kabisa. Mfalme akainua mkuki wake na mara ile miguu ishirini elfu ikainuliwa kama mguu wa mtu mmoja, ikakanyaga chini tena kwa kishindo kimoja.

Mara tatu walifanya hivi, na nchi ilitetemeka kwa kishindo.
Ndipo mbali palipo watu sauti moja ikaanza kuimba wimbo kama wa kusikitika na wengine wakaitika.

Maneno ya wimbo yalikuwa haya: Nini ajali ya mtu azaliwaye…? Na sauti za wote zikaitikia, Mauti…?

Kwa taratibu wimbo huo ulishikwa na watu wote katika kila kikosi mpaka wote walikuwa wakiimba. Sikuweza kusikia maneno yote ya wimbo ila nadhani yalikuwa yakisimulia habari za mambo yanayowapata wanadamu, kama vile tama zao na hofu zao na furaha zao.

Kwanza yalionyesha mapenzi, halafu yakawa ya vita, halafu yakawa maneno ya kusikitikisha sana ya mauti.

Walipokwisha kuimba kukawa kimya tena, na mfalme akainua tena mkono wake, na mara tulisikia nyayo za watu wanakuja na katika kundi la watu tuliona watu wa kutisha sana wanatoka.

Walipotukaribia tuliona kuwa ni wanawake wazee na nywele zao nyeupe zilifungiwa vibofu vidogo vilivyotolewa katika matumbo ya samaki, vikipeperuka nyuma yao.

Nyuso zao zimetiwa rangi nyeupe na ya kimanjano; na nyuma walifunga ngozi za nyoka na kiunoni walijifunga mifupa ya wanadamu, na kila mtu alishika fimbo yenye meno matatu nchani mkononi mwake.

Jumla yao ilikuwa kumi, na mmoja wao alimwonyesha Gagula kwa mkono wake akasema, ‘Mama, mama mzee, tupo hapa.’ Yule Gagula akaitikia, ‘Vema! Vema! Vema! Macho yenu makali? Nyinyi watambuzi, nyinyi mnaweza kuona gizani?’ Wakajibu, ‘Mama, ‘Ni makali.’

Akasema, ‘Vema! Vema! Vema! Masikio yenu yamefumbuka, nyinyi watambuzi, nyinyi mnasikia maneno yasiyotamkwa kwa ulimi?

Wakajibu, ‘Mama, yamefumbuka.’ Akaitikia, ‘Vema! Vema! Vema! Pua zenu zinaweza kusikia harufu, nyinyi watambuzi? Mnaweza kusikia harufu ya damu, manaweza kusafisha nchi yetu kwa kuwaondoa wale wanaomfanyia maovu mfalme na jirani zao?

Mpotayari kuhukumu kwa haki za mbinguni? Nyinyi niliowafundisha, mliokula mkate wa busara zangu na kunywa maji ya uwezo wangu?’ Wakaitikia, ‘Mama, tunaweza.’
Basi akasema, ‘Vema, nendeni.

Msikawie, nyinyi tai; mwaona wauaji?’ (Akawaonyesha wale waliosimama tayari kuua.) ‘Haya fanyeni mikuki yao kuwa mikali; watu weupe waliotoka mbali wana hamu ya kuona, nendeni!’
 
Basi wale watu wakalia kwa sauti kuu wakatawanyika pote, na mifupa waliyofunga ikagongana walipokuwa wakienda ; wakaenda kila mahali katika kundi lile la watu.

Hatukuweza kuwatazama wote, basi tulimtazama Yule aliyekuwa karibu. Alipopita karibu na askari wale waliosimama, kisha akaanza kucheza na kuruka ruka, akizunguka zunguka kwa upesi sana, na akisema maneno kama haya:

‘'Nasikia harufu yake, mtenda maovu! Yu karibu, Yule aliyempa sumu mama yake! Nasikia mawazo maovu aliyemwazia mfalme!’'

Akazidi kucheza upesi upesi mpaka akawa kama mwenye wazimu na povu likamtoka kinywani na macho yakawa kama yanatoka kichwani, na mwili wake ulitetemeka. Mara akasimama akakaza mwili kama mbwa anayesikia harufu ya nyama porini, akanyosha fimbo yake na akaanza kuwaendea pole pole wale askari.

Na sisi tulimfuata kwa macho yetu kama tumepagawaa. Basi akafanya hivi mpaka alipofika mbele yao karibu, ndipo aliposimama akanyosha fimbo yake, akatambaa mbele kidogo tena. Mara mambo yalikwisha.

Kwa kilio kikuu aliruka akamgusa askari mmoja kwa fimbo yake. Mara Yule askari alishikwa na wenzake wawili akaletwa mbele ya mfalme. Hakufanya ukaidi, lakini tuliona kuwa walipokuwa wakimleta alikuwa kama amepooza, na vidole vilikuwa kama vidole vya maiti, na mkuki ulimponyoka.

Alipofika karibu, wauaji wawili wakatoka mbele, wakamtazama mfalme ili kupewa amri. Mfalme akasema, ‘Muueni!’
Na Gagula akalia, ‘Muue!’
Na yule Skraga akacheka akasema, ‘Muue!’

Basi kabla hawajamaliza kusema, mauaji yalikwisha tendeka. Mtu mmoja akamchoma mkuki wa moyo, na Yule mwingine akampiga rungu la kichwa. Mfalme Twala akahesabu, ‘Mmoja.’ Na maiti ilichukuliwa ikalazwa pale pale.

Mara tuliona mtu mwingine analetwa kama ng’ombe anayeletwa kuchinjwa. Mtu huyu alikuwa mwenye cheo, maana alikuwa kava ngozi ya chui. Tena tulisikia maneno yale yale ya kikatili na Yule mtu akaanguka amekufa. Mfalme akahesabu, ‘Wawili.’


Basi vivyo hivyo mchezo wao ukaendelea mpaka maiti mia moja walilazwa kwa safu. Mara moja tulisimama tukajaribu kumzuia mfalme, lakini alitukanya kwa ukali, akasema, ‘Acheni sheria iendelea, nyinyi watu weupe. Mbwa hawa ni wachawi na watenda maovu; kufa ni haki yao.


Ilipopata saa nne na nusu, mambo yakasita kidogo, na wale waliokuwa wakichagua wachawi wakajikusanya pamoja, tukafikiri kuwa wamechoka.

Lakini sivyo, maana tuliona ajabu Gagula alipojiinua akajikongoja kwa fimbo yake akaja katikati. Ikawa ajabu kumwona, Alikuwa karibu kupinda kabisa, lakini alipata nguvu akaanza kwenda mbio huku na huko kama walivyo fanya wanafunzi wake.


Haku na huko alikwenda mbio huku akiimba, mpaka akamrukia mtu mrefu aliyekuwa kasimama mbele ya kikosi kimoja, akamgusa. Alipofanya hivi, watu wakikosi chake wakaguna. Lakini wawili wao wakamshika wamlete mbele ya mfalme auawe.


Baadaye tulikuja kujua kuwa ni mwenye cheo kikubwa naye ni tajiri sana, tena ni mjukuu wa mfalme mwenyewe. Aliuawa, na mfalme akahesabu mia moja na tatu. Tena Gagula akaruka huku na huko, akaanza kutukaribia sisi.

Bwana Good akasema, ‘Lo! Nadhani anatujia sisi.’ Bwana Henry akasema, ‘Upuuzi! Hathubutu!’ na mimi nilipoona kuwa Yule afiriti anatukaribia, nilikata tamaa kabisa. Nikageuka nikatazama safu zile za maiti, nikatetemeka.


Gagula akakaribia, akakaribia zaidi na macho yake yakang’aa kwa uovu. Akaja karibu, karibu, na kila mtu hadharani alimkodolea macho.

Mwisho akasimama, akanyosha fimbo yake, na mara akamrukia Umbopa, yaani Ignosi, akamgusa begani, akasema, ‘Nasikia harufu yake.

Muue, muue, amejaa uovu; muue mgeni huyu kabla damu haijamwagika kwa ajili yake. Ee mfalme, muue!’

Hapo ikawa kimya kidogo, nami nikasimama nikasema, ‘Ewe mfalme, mtu huyu ni mtumishi wa wageni wako. Yeyote atakaye mwaga damu yake anamwaga damu yetu. Kwa ajili ya ukarimu wako, naomba asidhuriwe.’ Mfalme akasema, ‘Gagula, mama wa watambuzi wa wachawi, amemchagua; lazima afe.’


Nikajibu, ‘Hafi kabisa. Atakayejari kumgusu ndiye Atakayekufa.’
Twala akasema kwa sauti kubwa. ‘Haya, mkamateni’ Na wale wauaji waliopaka damu ya wale waliowaua, wakaja mbele, lakini walisita. Ignosi alishika mkuki wake, akawa tayari kupigania maisha yake.


Nikasema, ‘Rudini nyinyi! nyinyi, mbwa! Mkitaka kuona mwangaza wa jua kesho, rudini! Mkigusa hata unywele mmoja wa kichwa chake, basi mfalme wenu atakufa.’

Nikaelekeza bastola yangu kwa mfalme, Bwana Henry na Bwana Good vile vile wakatwaa bastola zao, na Bwana Henry akamwelekezea Yule muuaji wa mbele, na Bwana Good akamwelekezea Gagula Yule kizee.


Twala alipoona bastola imewekwa sawa na kifua chake akajikunja, nikasema, ‘Je, Twala, utafanya nini?’ Akasema, ‘Haya wekeni mianzi yenu ya ajabu, umeomba kwa ajili ya ukarimu na kwa ajili hiyo nitamwacha, wala si kwa kuhofu vitendo vyenu. Nendeni kwa amani.’


Nikajibu, ‘Vema, tumechoka kuona mauaji. Tunataka tukalale. Je, ngoma imekwisha?’
Twala akajibu, ‘Imekwisha,’ Akageuka akaonyesha maiti wale akasema, ‘Mizoga ya mbwa hawa itupiwe fisi na tai mwituni.’ Akainua mkuki wake.


Mara vikosi vikaanza kutoka kwa taratibu na kwa kimya kabisa, wachache tu walibaki ili kuchukua maiti. Tukaondoka tukamuuaga mfalme tukaenda nyumbani, naye hakutaka hata kututazama .


Tulipofika nyumbani tukawasha taa za Kikukuana, yaani, uzi kidogo uliowekwa kwenye mafuta ya kiboko, na Bwana Henry akasema, ‘Mimi naona kama nataka kutapika.’
Na Bwana Good akasema, ‘Kama nilikuwa na shaka katika shauri la kumsaidia Umbopa katika kumpiga vita Yule Twala, basi sasa limeondoka kabisa.

Nilijizuia kwa nguvu walipokuwa wakiwaua wale watu. Nilijaribu kufumba machoyangu, lakini ikawa kila mara nilipoyafumbua ukawa wakati usiofaa! Je, yupo wapi Umbopa.


Ehe rafiki yangu, nadhani yafaa kutushukuru sana, wewe ulikuwa karibu na kufa leo.’ Umbopa akajibu, ‘Ndiyo, kweli, nawashukuru sana.

Sitaweza kusahau mambo ya usiku huu. Infadus atakuja baadaye, lazima tumngojee.’ Basi tukatia tumbako katika viko vyetu, tukakaa tukivuta na kumngoja.
 
Aisee, daah. Salute mkuu blackstarline
 
Ee bwana [emoji119] [emoji119]
 
SURA YA KUMI NA MOJA


Kwa muda mrefu, kadiri ya saa mbili tulikaa kimya. Tulikuwa tumeshindwa kuondosha fikra za vitisho tulivyoviona usiku ule. Baadaye tuliona ni usiku sana tukafikiri kwenda kulala, na mara tulisikia kishindo cha miguu ya watu.

Tukasikia sauti ya mtu aliyekuwa akilinda zamu, na mara tukasikia nyayo zinakaribia; na baada ya muda kidogo Infadus akaingia ndani pamoja na watu warefu sita.

Infadus akasema, ‘Mabwana zangu, nimekuja kama nilivyoahidi. Mabwana zangu na Ignosi, mfalme wa haki wa Wakukuana, nimewaleta watu hawa walio wakubwa wetu, na kila mmoja ni mkubwa wa skari elfu tatu.

Askari hao huwatii kufanya wanavyoamrishwa chini ya mfalme. Nimewaeleza niliyoyaona na kusikia. Sasa waonyeshe nyoka mtukufu aliyochajwa kiunoni mwako, Ee Ignosi, wapate kukata shauri kama watakusaidia kupingana na Mfalme Twala.’

Ignosi akavuta tena ukanda wake akawaonyesha Yule nyoka aliyochanjwa kiunoni mwake. Kila mkubwa akamtazama kwa mwangaza wa taa, kisha bila ya kusema neno, kila mmoja akapita akasima kando.

Sasa Ignosi akavaa tena ukanda akawaeleza habari zile alizosimulia asubuhi.
Kisha, Infadus akasema, ‘Sasa nyinyi wakubwa mmesikia, mnasemaje? Mtamsaidia mtu huyu ajipatie ufalme wa baba yake?

Nchi inalalamika kwa sababu ya ukatili wa Twala, na damu za watu zinamwagika kama mto wakati wa masika. Mmeona usiku huu huu. Walikuwapo wawili wengine niliotaka kusema nao, na sasa wako wapi? Fisi wanapigania maiti zao sasa.

Na nyinyi mtakuwa kama walivyo wao msipojipigania upesi. Basi ndugu zangu chagueni.’
Yule mkubwa katika wale sita akasimama mbele akasema, ‘Infadus, maneno yako niya kweli; nchi inasikitika.

Ndugu yangu mimi ameuliwa usiku huu huu; lakini jambo hili ni kubwa mno nalo ni vigumu kuamini.

Tutajuaje ya kuwa tukipigana kwa ajili ya mtu huyu hatumpiganii mwongo? Nasema ni jambo kubwa na mwisho wake haujulikani.

Kwa hakika damu itamwagika kama mito kabla ya kumalizika jambo hilo; wengi watamfuata mfalme; na watu weupe hawa waliotoka katika nyota, kweli uwezo wao ni mkubwa, nao Ignosi yu chini ya ulinzi wao.


Ikiwa kweli ni mfalme wa haki, basi na watuonyeshe ishara, na watu waonyeshwe ishara ili wote waione. Hivyo watu wataambatana nasi wakijua kuwa nguvu za watu weupe ziko upande wetu.’

Nikajibu, ‘Mmeona ishara ya nyoka.’ Akasema, ‘Bwana wangu, haitoshi. Inawezekana kuwa ile alama ilichanjwa baada ya utoto wake. Tuonyesheni ishara, Hatuwezi kufanya kitu bila kupata ishara.’

Wale wengine wakasema hivyo hivyo, nikawa katika shida, nikawageukia Bwana Henry na Bwana Good nikawaeleza mambo yote.

Bwana Good akacheka, akasema, ‘Nadhani nimepata shauri la kufaa. Waambie watupe nafasi kidogo tupate kufikiri.’

Nikawaambia, wakajitenga mbali kidogo. Bwana Good akafungua kasha lake la dawa zake, akatoa kitabu chake chenye takwimu.(Yaani hesabu ya miezi na miaka na habari za mwezi na nyota.)

Akasema, ‘Sasa tazameni rafiki zangu, kesho ni siku ya nne katika mwezi wa Juni sivyo?’ Tulikuwa tukiweka hesabu kila siku, tukamwambia ndiyo. Akasema, ‘Vema, hapa imeandikwa kuwa siku ya nne katika mwezi wa June mwezi utapatwa kwenye saa mbili na robo.

Basi ndiyo ishara yetu. Waambie kuwa tutafanya mwezi kutoweka usiku wa kesho.’ Shauri likawa ni jema sana, na hatari iliyopo ni labda habari zilizoandikwa katika kitabu ya kuwa zitatokea si kweli.

Maana tukitangaza ishara ya namna hiyo nayo isipotokea, nguvu zetu mbele ya Wakukuana zitakwisha kabisa, na tena tutashindwa kumweka Ignosi katika kiti cha ufalme wa Wakukuana.
 
Basi tukafanya hesabu yetu, tukaona kuwa kwa mahali tulipo, mwezi utapatwa saa nne ya usiku wa kesho, nao utaachiliwa tena saa tisa na nusu.

Yaani kwa muda wa saa moja na nusu itakuwa giza tupu. Bwana Henry akasema, ‘Basi, afadhali tubahatishe.’

Nikamtuma Umbopa kuwaita wale Wakubwa, na walipokuja nikawaambia, ‘Watu wakubwa wa Wakukuana na wewe Infadus, sikilizeni. Hatupendi kabisa kuonyesha kabisa nguvu zetu, maana kufanya hivi kunaweza kubadili mwendo wa mambo ya asili, napengine kutia dunia katika hofu na fadhaa.


Lakini kwa kuwa ni jambo kubwa, na kwa kuwa tumemkasirikia Mfalme Twala kwa ajili ya mauaji tuliyoyaona, na kwa sababu ya vitendo vya Yule Gagula ambaye alitaka kumuua rafiki yetu Ignosi, tumenuia kuonyesha ishara ambayo watu wote wataiona. Njooni.’


Nikawaongoza mlangoni nikawaonyesha mwezi uliokuwa ukishuka, nikasema, ‘Mnaona nini huko juu?’ Wakajibu, ‘Twaona mwezi unaotua.’


Nikajibu, ‘Kweli. Na sasa niambieni, je, yuko mtu yeyote anayeweza kuushusha mwezi kabla haujafika wakati wa kushuka, na kufunikiza nchi yote kwa pazia la giza usiku?’ Yule mkubwa aliyekuwa msemaji wao akacheka kidogo akasema, ‘Hayupo, bwana wangu, hapana mtu anayeweza kufanya hivi.

Mwezi una nguvu nyinyi kuliko wale wanaoutazama, wala hauwezi kubadili majira yake.’
Nikajibu, ‘Wewe unasadiki hayo, lakini nakwambia ya kuwa usiku wa kesho saa nne tutafanya mwezi kuliwa kwa muda wa saa moja na nusu.


Ndiyo, giza tupu litafunika nchi na itakuwa ishara kuonyesha kuwa Ignosi ndiye mfalme halisi wa Wakukuana.

Tukifanya hivi mtaridhika?’ Yule mkubwa akajibu, ‘Ndiyo, bwana wangu, mkifanya hivi sisi tutaridhika kabisa.’

Nikajibu, ‘Vema, itafanyika; sisi watatu tumesema, nayo yatafanyika. Umesikia, Infadus?’
Infadus akasema, ‘Nasikia bwana wangu, lakini ni jambo la ajabu uliloahidi litafanyika, yaani kuzima mwangaza wa mwezi ulio mama wa dunia.’

Nikasema, ‘Ni ajabu kweli, lakini nakwambia kuwa tutafanya.’
Infadus akasema, ‘Vema, bwana wangu, kesho saa mbili baada ya kushuka jua, mfalme Twala atawaita nyinyi mabwana zangu ili mwende mkatazame ngoma ya wanawali, na baada ya saa moja kutoka kuanza ngoma, Yule mwanamwali anayedhaniwa na Twala kuwa mzuri kupita wenzake wote atauawa na Skraga, mwana wa mfalme, awesadaka ya Wale Watatu wanaokaa kimya wakiangalia milima.’


Akaonyesha vile vilele penye mwisho wa Njia Kuu ya Sulemani, ‘Basi, ndipo mabwana zangu watie mwezi giza na kuokoa maisha ya mwanamwali, na kweli ndipo watakaposadiki watu wote.’


Yule mzee akasema, ‘Ndiyo, kweli ndipo watakaposadiki watu wote. ‘ Akacheka kidogo. Infadus akaendelea akasema, ‘Mwendo wa nusu saa kutoka mji wa Loo upo mlima uliokaa mfano wa upinde au mwezi mpya, nao ni kama boma, ndipo vilipowekwa vikosi vitatu vyangu na vikosi vitatu vingine vya wakubwa hawa.

Kesho asubuhi tutafanya shauri la kupeleka vikosi viwili au vitatu vingine.


Na ikiwa nyinyi mabwana wangu mtafaulu kutia giza mwezi, basi tutaungana mikono na nitawaongoza kumpiga vita mfalme.’ Nikajibu, ‘Vema, na sasa tuache tupumzike kidogo tufanye tayari ishara yetu.’


Walipokwisha kwenda, Umbopa, yaani Ignosi, akasema, ‘Rafiki zangu, mnaweza kufanya jambo hilo la ajabu, au mlikuwa mnasema maneno ya bure?’

Nikajibu, ‘Tunadhani kuwa tunaweza kulifanya, Ignosi.’ Akasema, ‘Tukiwa hai baada ya mambo haya, hakika nitawalipa.’

Bwana Henry akasema, ‘Ignosi, nakutaka uahidi neno moja.’ Ignosi akacheka, akajibu, ‘Hata kabla sijasikia neno lenyewe nitaahahidi nini?’

Akajibu, ‘Ni hili: ukijaliwa kuwa mfalme, ahidi kuwa utakomesha desturi hii tuliyoona ya kuwafichua wachawi na kuwaua watu bila kuwahukumu kwa haki.’

Ignosi akafikiri kidogo kwanza na baadaye akasema, ‘’Desturi za watu weusi si kama za watu weupe. Lakini nitaahidi. Nikipata nguvu nitazuia wasifichue tena wachawi, tena watu hawatauawa bila kuhukumiwa kwa haki kwanza.’

Basi Bwana Henry akasema, ‘Basi sasa tumekwisha patana, tulale tupumzike.’
 
Basi Bwana Henry akasema, ‘Basi sasa tumekwisha patana, tulale tupumzike.’


Tulilala upesi sana, maana tulichoka sana, wala hatukuamka mpaka Ignosi alipotuamsha saa tano. Tuliondoka tukaoga tukala. Baadaye tulitoka nje tukatazama namna nyumba zilivyojengwa, na desturi za watu.

Halafu Bwana Henry akasema, ‘Natumaini kuwa kweli mwezi utapatwa usiku.’ Nikajibu, ‘Kama haupatwi basi tumekwisha kabisa, maana haikosi wakubwa wengine watamweleza mfalme habari zote na hatima yetu itatatufika upesi.’

Basi tukarudi nyumbani tukala chakula cha mchana tukakaa tukizungumza na watu waliokuja kutuamkia. Jua liliposhuka tulikaa muda wa saa mbili tukifikiri, na saa mbili na nusu tarishi akaja kutoka kwa mfalme Twala kutukaribisha kwenye ngoma ya wanawali usiku huo huo.

Tukafanya haraka tukavaa nguo zile za minyororo ya chuma chini ya nguo zetu, tukatwaa bunduki zetu na risasi ili tuwe tayari ikilazimu kukimbia mambo kama ya kienda ovyo. Tukatoka kama mashujaa, lakini katika mioyo yetu tulitetemeka kabisa.

Tulipofika katika kiwanja kile mbele ya jumba la mfalme, tuliona ni namna nyingine kabisa. Badala ya safu za askari, tuliona makundi ya wanawali, na kila mmoja amejipamba na amevaa maua kichwani, na katika mkono mmoja ameshika kuti kama lile la mtende, na katika mkono wa pili ameshika ua kubwa jeupe.

Katika nafasi ya katikati iliyoangazwa na mbalamwezi, mfalme Twala amekaa na Gagula amekaa kitako miguuni pake, na kijana Yule Skraga amesimama nyuma pamoja na askari kumi na mbili. Wakubwa ishirini walikuwapo, nikawatambua wale waliotujia usiku wa jana.

Twala alituamkia kwa urafiki lakini niliona kama alimtazama Umbopa kwa uchungu mwingi, akasema, ‘Karibuni, nyinyi watu weupe mliotoka katika nyota.

Leo mtaona mambo mengine si kama yale mliyoona usiku wa jana, lakini si mazuri kama yale ya jana. Wanawali ni wazuri mno nao wanafurahisha, maana wasingekuwepo na sisi tusingekuwepo; lakini wanaume ni bora. Maneno ya wanawake ni matamu naya kupendeza, lakini kishindo cha mikuki ya mashujaa na harufu ya damu ni tamu zaidi.


Lakini karibuni, mabwana, na wewe mtu mweusi, karibu; Kama Gagula angalifanikiwa alivyotaka, wewe ungali kuwa maiti sasa. Una bahati kuwa na wewe vile vile umetoka katika nyota. Ha!Ha!’

Ignosi akajibu kwa upole sana, ‘Nitakuua wewe kabla ya kuniua mimi, nawe utakuwa mkavu kabla viungo vyangu havijaacha kujimudu.’

Twala akashtuka akasema kwa sauti kali, ‘Maneno yako ni makubwa, wewe kijana, usinikasirishe zaidi.’ Umbopa akajibu, ‘anayesema kweli ana haki ya kusema maneno makubwa. Kweli ni mkuki mkali unaopiga shabaha kila mara. Hii ndiyo habari ninayokupa kutoka nyotani Ewe Mfalme.’

Twala akakunja uso wake asiseme neno. Halafu alisema, ‘Haya, ngoma ianze sasa.’
Na mara wale wanawali waliopambwa na maua waliondoka wakaanza kucheza, wakaimba nyimbo nzuri.

Wakacheza, wakacheza, pengine walizunguka wakakutana katikati, wakafanya mfano wa vita, tena wakaenda mbele na kurudi nyuma tena.

Ndipo alipotokea mmoja mzuri sana akacheza mbele yetu kwa namna ya ajabu. Alipokwisha akarudi nyuma na mwingine akaja mbele akacheza, hivyo hivyo.

Walipokwisha cheza hivyo, mfalme akainua mkono akasema, ‘Je nyinyi watu weupe, nani mzuri kupita wote?’ Mimi nikajibu bila kufikiri sana, nikasema, ‘Yule aliyekuja kwanza kucheza .’

Mara nikakumbuka alivyotwambia Infadus kuwa Yule mzuri kupita wote lazima auawe ili kuwa sadaka, nikasikitika na nikajuta kwa maneno yangu.

Basi mfalme akasema, ‘Unavyofikiri wewe, ndivyo ninavyofikiri mimi. Yeye ni mzuri; na hayo ni huzuni kwake maana lazima afe.’

Gagula akaitikia, ‘Ndiyo, lazima afe.’ Akamtazama Yule masikini mwanamwali aliyekuwa kasimama hajui ajali inayomngojea.

Nikajizuiya nilivyoweza, nikamuuliza, ‘Ewe mfalme, kwa nini afe, Yule mwanamwali aliyecheza vizuri akatupendeza sana? Tena ni mzuri mno; ni vibaya kumlipa kwa kumuua.’

Twala akacheka akajibu, ‘Ni desturi yetu, maana wale watatu wakaao huko lazima wapate haki yao.’ Akaonyesha penye vilele vile vya mlima. ‘Nisipomuua Yule msichana mzuri, kisirani kitaniangukia nyumbani kwangu.

Haya ndiyo yaliyobashiriwa zamani. Ikiwa mfalme ataacha kumuua mwanamwali aliye mzuri katika siku ya ngoma ya wanawali awe sadaka kwa Wale Watatu wakaao huko, basi ataanguka yeye na nyumba yake.

Tazameni, watu weupe, ndugu yangu aliyetangulia kutawala, hakutoa sadaka kwa sababu ya machozi ya mwanamke, basi akaanguka yeye na nyumba yake vile vile, nami nilishika utawala wake.
Yamekwisha, lazima afe!
 
Akawageukia askari akasema, ‘Haya, mlete hapa; na wewe Skraga, unoe tayari mkuki wako.’ Basi watu wawili wakaja mbele na walipomkaribia Yule mwanamwali, ndipo kwanza alipofahamu ajali yake, akalia sana, akageuka apate kukimbia. Lakini wale askari wawili walimshika wakamleta analia na kujaribu kuwatoka.


Gagula akamuuliza, ‘Jina lako nani, wewe mwali? Je, hutaki kunijibu? Je, mwana wa mfalme afanye kazi yake sasa?

Kusikia hayo, Skraga alionekana kuwa mwovu kupita kiasi, akajongea hatua moja, akainua mkuki wake, na mara niliona mkono wa Bwana Good unashika bastola, na Nuru ya bastola ilimpata machoni Yule mwali, akanyamaza kimya.

Akaacha kushindana, akafumbata mikono yake akasimama anatetemeka toka kichwa hata miguu.

Skraga akacheka, akasema, ‘Tazama anajikunyata kuona mchezo wangu, hata kabla hajaiona.’ Akapapasa mkuki wake. Nikamsikia Bwana Good anasema kimoyomoyo, ‘Lo! Nikipata nafasi utajuta maneno yako, Mbwa we!’

Basi, sasa Gagula akamfanyia dhihaka , akasema, ‘Sasa umekwisha tulia, tuambie jina lako nani? Mpenzi wangu. Haya sema, usiogope.’


Yule mwali akatetemeka, akajibu, ‘’Ewe mama, jina langu naitwa Foulata, na ukoo wangu ni Suko. Ewe mama, kwa nini sina budi kufa? Mimi sikufanya makosa au ubaya wowote!’


Gagula akajibu, ‘Usifadhaike, lazima ufe uwe sadaka kwa Wale Wazee wakaao huko, lakini ni afadhali kulala usiku kuliko kufanya kazi mchana; ni afadhali kulala usiku kuliko kufanya kazi mchana; ni afadhali kufa kuliko kuishi, nawe utakufa kwa mkono wa mwana wa mfalme.’


Yule mwali Foulata akajiuma vidole vyake kwa huzuni akalia, ‘Ole wangu, huu ndio ukatili kweli! Mimi ni kijana! Nimefanya nini nisipate kuona jua likitoka katika giza la usiku huu, nisione tena nyota zikifuata majira ya jioni, nisipate kuchuma maua katika umande wala kusikiliza nyimbo za mteremko wa maji?


Ole wangu, sipati tena kuona nyumba ya baba yangu, wala kuona tena mapenzi ya mama yangu, wala kuchunga wana wa kondoo! Ole wangu, sitapata mwanaume wakunipenda na wala sitazaa wana! Ukatili! Ukatili!’

Tena akajiuma vidole kwa huzuni akageuka akatazama juu na machozi yalionekana yakimtoka machoni, akawa wa kusikitisha kabisa hata kuleta huruma kwa mtu yeyote, ila wale mashetani waliokuwa wamekaa mbele yetu hawakujali kabisa.

Na wala haikuvuta huruma kwa Gagula, wala bwana wa Gagula, ila niliona dalili ya huruma na huzuni katika sura za walinzi wale, na katika sura za wale wakubwa waliokuwapo; na Bwana Good alijizuia kwa shida tu, akafanya kama anakwenda kumsaidia.


Basi kwa akili ya kike, Yule mwali alitambua fikira zake, na mara akaruka akajitupa mbele yake akamshika miguu akalia, ‘Ewe baba mweupe uliyetoka katika nyota, nifunike kwa nguo yako ya ulinzi, nitambae katika kivuli cha nguvu zako nipate kuokoka.


Niokoe katika mikono ya watu waovu hawa wasio na huruma!’ Bwana Good akamshika mkono akasema, ‘Vema, mimi nitakulinda.’ Akainama akamshika mkono akasema, ‘Haya ondoka, mwanangu.’


Twala akageuka akamwashiria mwanawe, naye akajongea mbele ameshika mkuki juu.
Bwana Henry akasema akinong’oneza, ‘Sasa huu ndiyo wakati unaofaa; unangoja nini? Nikajibu kwa sauti ndogo, ‘Mimi nangoja kuona dalili ya mwezi kupatwa kwanza.


Nimeutazama kwa nusu saa hivi, lakini sioni dalili ya kupatwa.’
Akajibu, ‘Sasa lazima tubahatishe au huyu mwanamwali atauawa, maana naona Twala anaanza kuchoka.’

Basi nikatambua kuwa asemavyo ni kweli, nikatazama mwezi mara moja tena nisione hata dalili ya kupatwa, nikajikaza nikasimama mbele, nikajongea katikati ya Skraga na yule mwanamwali, nikasema, ‘Mfalme jambo hili halitakuwa; sisi hatutavumilia jambo hili; mwanamwali na aende zake salama.’


Twala akaghadhibika mno, akasimama katika kushangaa kwake, na askari wake waliokuwapo na wanawali nao walishangaa.


Na mfalme Twala akasema, ‘Halitakuwa! Wewe mbwa mweupe aliaye mbele ya simba katika pango lake; halitakuwa! Wewe una wazimu? Angalia sana usije ukapatwa na ajali ya kifaranga huyo, na wale waliopo pamoja nawe vile vile.

Je, wawezaje kumwokoa au kujiokoa mwenyewe? Nani wewe ujitiaye katikati ya mimi na matakwa yangu? Kaa upande, na wewe Skraga muue!


Haya, askari wangu, washike watu hawa.’ Basi hapo askari wengi wakatoka kwa nyuma ya jumba walikofichwa. Bwana Henry na Bwana Good na Umbopa wakasogea karibu nami, wakaelekeza bunduki zao.


Nikasema kwa sauti kuu lakini moyo wangu haukwepo kabisa, ‘Acheni! Twacheni sisi watu weupe tuliotoka katika nyota, tunasema kuwa halitakuwa.

Mkikaribia hata hatua moja tu, tutauzima mwezi, na sisi tukaao katika nyumba yake tunaweza kufanya hivi, tutaitia nchi yote katika giza tupu, nanyi mtaonja uchungu wa nguvu zetu.’

Basi maneno yangu yaliwastua; watu wakasimama, na Skraga akasimama kimya mbele yetu, ameshika mkuki wake juu.

Gagula akasema, ‘Msikieni! Msikieni! Msikieni asemavyo uwongo. Basi na afanye anavyosema na mwanamwali ataachiliwa. Afanye au auawe pamoja na mwanamwali na wale walio pamoja naye.’


Nikatazama mwezi tena, na sasa: nilifurahi, maana niliona kuwa alama nyeusi inaanza kuonekana katika mwezi.

Ndipo nilipoinua mkono wangu kwa taratibu sana nikaonyesha juu mbinguni, na Bwana Henry na Bwana Good wakafanya vile vile, tukaanza kusema maneno yoyote tuliyoweza kuyakumbuka.

Pole pole na kwa tara-tibu, kivuli kilianza kufunika mwezi, na kilipozidi kuja nikasikia watu wanaanza kuvuta pumzi juu, nikasema,
‘Tazama, Ewe Mfalme! Tazama, Gagula!

Tazameni nyinyi wakubwa, na watu wote, mwone kama watu weupe waliotoka katika nyota wametimiza maneno yao au kama ni uwongo mtupu! Mwezi unafunikwa mbele ya macho yenu; na sasa hivi itakuwa giza tupu.

Mmeomba ishara nasi tumeifanya. Ee mwezi, ufunikwe uwe giza tupu! Uzime mwangaza wako, Ee wewe mtakatifu; ulete ule moyo wa kiburi hata mavumbini, Ee mwezi, ule dunia kwa vivuli vyako.’

Basi watu wote waliguna kwa hofu. Wengine walisimama kama wamegeuka mawe, na wengine walijitupa chini wakapiga magoti wakalia kwa sauti kubwa.


Na mfalme mwenyewe alikaa kimya, uso umembadilika.
Gagula tu hakunyamaza, akasema, ‘Giza litapita, nimeyaona kama haya zamani; hapana mtu anayeweza kuzima mwangaza wa mwezi; msiogope; mkae kimya na giza litapita.’


Nikasema, ‘Ngojeni mtaona. Ee Mwezi!Mwezi! Mwezi!’ na sisi wote watatu tukazidi kusema maneno ya ovyo ovyo tu! na kwa muda wa dakika kumi tukaendelea hivyo hivyo.

Giza likazidi, na watu wote walikodoa macho yao kutazama juu, na walikaa kimya kabisa. Sasa dunia ikaanza kujaa vivuli vya ajabu, na kila kitu kilikuwa kimya kama mauti.

Wakati ulipita na pamoja giza likazidi kushika mwezi. Ikawa ajabu mno, maana kwanza ikawa kama mwezi unakaribia dunia na kuzidi kuwa mkubwa.

Sasa uligeuka rangi ukawa mwekundu kama damu, na halafu tuliona alama zile zilizo katika mwezi zinang’aa katika wekundu wake.

Pole pole giza likatambaa; sasa limefika nusu ya ule wekundu kama damu. Likazidi kuenea hata hatukuweza kuona sura za watu waliokuwa karibu. Sasa kila mtu alikuwa kimya kabisa, nasi hatukusema neno.


Mara Yule kijana Skraga alilia kwa hofu, ‘Mwezi unakufa. Wachawi weupe hawa wameuwa mwezi. Tutaangamia katika giza.’ Naye alishikwa na wazimu kwa hofu akainua mkuki wake akampiga Bwana Henry kwa nguvu zake zote.

Lakini alikuwa amesahau habari za nguo zile za chuma alizotupa mfalme, na mkuki ukapinduka bila kuzipenya.


Kabla hajapata nafasi kupiga tena, Bwana Henry akashika ule mkuki akampiga kifuani. Skraga akaanguka maiti! Basi watu walipoona hivyo, na kwa sababu ya hofu waliyokuwa nayo kufikiri kuwa mwezi unakufa, wakaanza kutawanyika, wakapiga mbio na kulia.


Na hata mfalme na walinzi wake na Gagula wakaondoka mbio wakakimbilia majumbani, na baada ya dakika chache tukajiona tupo peke yetu pamoja na Foulata, Yule mwanamwali tuliyemwokoa, na Infadus, na wakubwa wengine waliotujia usiku, na maiti ya Skraga mwana wa mfalme.


Nikasema, ‘Wakubwa, tumewaonyesha ishara mliyotaka. Kama mmeridhika, basi twendeni upesi mahali mlipotaja. Hatuwezi sasa kukomesha kitendo chetu.

Giza litaendelea kwa muda wa saa moja na nusu. Haya, na tujifiche kwa giza hili.’
Infadus akasema, ‘Twendeni.’ Akageuka akaenda, na wakubwa wale walimfuata, na sisi na yule mwanamwali tulifuatana nao.


Kabla hatujalifia lango la mji, mwezi uliliwa kabisa na nyota nyingi zikaonekana katika mbingu nyeusi. Tukashikana mikono tukajikokota katika giza.
 
Taratiiibu nai'fyonza apa ndo nilale. Ishakua arosto hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…