blackstarline
JF-Expert Member
- Sep 19, 2016
- 3,278
- 7,966
- Thread starter
-
- #101
Ikawa shani ya kustajabisha kabisa. Wote walisimama kimya kabisa, na mwezi ukawaangaza wakawa kama mwitu wa mikuki, na manyoya yao ya vichwani yalipepea katika upepo.
Popote tulipotazama tuliona mistari kwa mistari ya mikuki inayong’aa.
Nikamwambia Infadus, ‘Jeshi zima limehudhuria?’ akajibu, ‘La, Makumazahn, hii ni theluthi tu. Maana ni theluthi tu huudhuria kwenye ngoma kuu kila mwaka.
Theluthi nyingine imewekwa nje tayari kukomesha matata ikiwa yatatokea wakianza mauaji, elfu kumi hulinda nje ya mji wa Loo, na waliobaki wametawanywa katika miji ya nchi.’
Bwana Good akasema, ‘Wamekaa kimya kabisa.’ Infadus akauliza, ‘Je, Bwana anasema nini?’ Nikamtafsiria, akajibu, ‘Wanaokabiliwa na mauti huwa kimya.’
Nikamuuliza, ‘Wengi watakufa?’ Akajibu, ‘Wengi sana.’
Nikawaambia wenzangu nao wakasikitika kabisa . Nikamuuliza Infadus, ‘Je, waonaje, tutakuwa katika hatari?’ Akajibu, ‘Sijui, mabwana zangu, lakini natumai mtakuwa salama. Maana askari wananung’unika juu ya mfalme.’
Basi wakati huo tulikuwa tukisogea tufike katikati ya nafasi tuliona viti vimewekwa tayari. Tulipokuwa karibu tuliona kuwa wengine wanatoka katika jumba la mfalme, na Infadus akasema, ‘Ni mfalme Twala na mwanawe Skraga na kizee Gagula; na pamoja nao ni wale wauaji.’
Akaonyesha kundi dogo la watu wakubwa sana wenye sura za ukali na ukatili, kila mtu ana mkuki katika mkono mmoja na rungu katika mkono wa pili. Mfalme akakaa katika kiti chake katikati, na Gagula akajikalisha chini penye miguu yake, na wengine walisimama nyuma.
Mfalme Twala akasema, ‘Karibuni, mabwana weupe, kaeni msipoteze wakati wenye thamani, usiku ni mfupi sana na kazi iliyo mbele yetu ni kubwa. Mmekuja wakati unaofaa sana, maana mtaona mambo mkuu sana.
Tazameni, mabwana, nyota zaweza kuwaonyesha shani kama hii? Tazameni namna wanavyotetemeka kwa uovu wao, wale wote wenye uovu katika mioyo yao wanaihofu hukumu ya mbinguni.’
Gagula akalia, ‘Anzeni! Anzeni! Fisi wanaona njaa, wanalilia chakula chao. Anzeni! Anzeni!’
Kwa muda kidogo ikawa kimya kabisa. Mfalme akainua mkuki wake na mara ile miguu ishirini elfu ikainuliwa kama mguu wa mtu mmoja, ikakanyaga chini tena kwa kishindo kimoja.
Mara tatu walifanya hivi, na nchi ilitetemeka kwa kishindo.
Ndipo mbali palipo watu sauti moja ikaanza kuimba wimbo kama wa kusikitika na wengine wakaitika.
Maneno ya wimbo yalikuwa haya: Nini ajali ya mtu azaliwaye…? Na sauti za wote zikaitikia, Mauti…?
Kwa taratibu wimbo huo ulishikwa na watu wote katika kila kikosi mpaka wote walikuwa wakiimba. Sikuweza kusikia maneno yote ya wimbo ila nadhani yalikuwa yakisimulia habari za mambo yanayowapata wanadamu, kama vile tama zao na hofu zao na furaha zao.
Kwanza yalionyesha mapenzi, halafu yakawa ya vita, halafu yakawa maneno ya kusikitikisha sana ya mauti.
Walipokwisha kuimba kukawa kimya tena, na mfalme akainua tena mkono wake, na mara tulisikia nyayo za watu wanakuja na katika kundi la watu tuliona watu wa kutisha sana wanatoka.
Walipotukaribia tuliona kuwa ni wanawake wazee na nywele zao nyeupe zilifungiwa vibofu vidogo vilivyotolewa katika matumbo ya samaki, vikipeperuka nyuma yao.
Nyuso zao zimetiwa rangi nyeupe na ya kimanjano; na nyuma walifunga ngozi za nyoka na kiunoni walijifunga mifupa ya wanadamu, na kila mtu alishika fimbo yenye meno matatu nchani mkononi mwake.
Jumla yao ilikuwa kumi, na mmoja wao alimwonyesha Gagula kwa mkono wake akasema, ‘Mama, mama mzee, tupo hapa.’ Yule Gagula akaitikia, ‘Vema! Vema! Vema! Macho yenu makali? Nyinyi watambuzi, nyinyi mnaweza kuona gizani?’ Wakajibu, ‘Mama, ‘Ni makali.’
Akasema, ‘Vema! Vema! Vema! Masikio yenu yamefumbuka, nyinyi watambuzi, nyinyi mnasikia maneno yasiyotamkwa kwa ulimi?
Wakajibu, ‘Mama, yamefumbuka.’ Akaitikia, ‘Vema! Vema! Vema! Pua zenu zinaweza kusikia harufu, nyinyi watambuzi? Mnaweza kusikia harufu ya damu, manaweza kusafisha nchi yetu kwa kuwaondoa wale wanaomfanyia maovu mfalme na jirani zao?
Mpotayari kuhukumu kwa haki za mbinguni? Nyinyi niliowafundisha, mliokula mkate wa busara zangu na kunywa maji ya uwezo wangu?’ Wakaitikia, ‘Mama, tunaweza.’
Basi akasema, ‘Vema, nendeni.
Msikawie, nyinyi tai; mwaona wauaji?’ (Akawaonyesha wale waliosimama tayari kuua.) ‘Haya fanyeni mikuki yao kuwa mikali; watu weupe waliotoka mbali wana hamu ya kuona, nendeni!’
Popote tulipotazama tuliona mistari kwa mistari ya mikuki inayong’aa.
Nikamwambia Infadus, ‘Jeshi zima limehudhuria?’ akajibu, ‘La, Makumazahn, hii ni theluthi tu. Maana ni theluthi tu huudhuria kwenye ngoma kuu kila mwaka.
Theluthi nyingine imewekwa nje tayari kukomesha matata ikiwa yatatokea wakianza mauaji, elfu kumi hulinda nje ya mji wa Loo, na waliobaki wametawanywa katika miji ya nchi.’
Bwana Good akasema, ‘Wamekaa kimya kabisa.’ Infadus akauliza, ‘Je, Bwana anasema nini?’ Nikamtafsiria, akajibu, ‘Wanaokabiliwa na mauti huwa kimya.’
Nikamuuliza, ‘Wengi watakufa?’ Akajibu, ‘Wengi sana.’
Nikawaambia wenzangu nao wakasikitika kabisa . Nikamuuliza Infadus, ‘Je, waonaje, tutakuwa katika hatari?’ Akajibu, ‘Sijui, mabwana zangu, lakini natumai mtakuwa salama. Maana askari wananung’unika juu ya mfalme.’
Basi wakati huo tulikuwa tukisogea tufike katikati ya nafasi tuliona viti vimewekwa tayari. Tulipokuwa karibu tuliona kuwa wengine wanatoka katika jumba la mfalme, na Infadus akasema, ‘Ni mfalme Twala na mwanawe Skraga na kizee Gagula; na pamoja nao ni wale wauaji.’
Akaonyesha kundi dogo la watu wakubwa sana wenye sura za ukali na ukatili, kila mtu ana mkuki katika mkono mmoja na rungu katika mkono wa pili. Mfalme akakaa katika kiti chake katikati, na Gagula akajikalisha chini penye miguu yake, na wengine walisimama nyuma.
Mfalme Twala akasema, ‘Karibuni, mabwana weupe, kaeni msipoteze wakati wenye thamani, usiku ni mfupi sana na kazi iliyo mbele yetu ni kubwa. Mmekuja wakati unaofaa sana, maana mtaona mambo mkuu sana.
Tazameni, mabwana, nyota zaweza kuwaonyesha shani kama hii? Tazameni namna wanavyotetemeka kwa uovu wao, wale wote wenye uovu katika mioyo yao wanaihofu hukumu ya mbinguni.’
Gagula akalia, ‘Anzeni! Anzeni! Fisi wanaona njaa, wanalilia chakula chao. Anzeni! Anzeni!’
Kwa muda kidogo ikawa kimya kabisa. Mfalme akainua mkuki wake na mara ile miguu ishirini elfu ikainuliwa kama mguu wa mtu mmoja, ikakanyaga chini tena kwa kishindo kimoja.
Mara tatu walifanya hivi, na nchi ilitetemeka kwa kishindo.
Ndipo mbali palipo watu sauti moja ikaanza kuimba wimbo kama wa kusikitika na wengine wakaitika.
Maneno ya wimbo yalikuwa haya: Nini ajali ya mtu azaliwaye…? Na sauti za wote zikaitikia, Mauti…?
Kwa taratibu wimbo huo ulishikwa na watu wote katika kila kikosi mpaka wote walikuwa wakiimba. Sikuweza kusikia maneno yote ya wimbo ila nadhani yalikuwa yakisimulia habari za mambo yanayowapata wanadamu, kama vile tama zao na hofu zao na furaha zao.
Kwanza yalionyesha mapenzi, halafu yakawa ya vita, halafu yakawa maneno ya kusikitikisha sana ya mauti.
Walipokwisha kuimba kukawa kimya tena, na mfalme akainua tena mkono wake, na mara tulisikia nyayo za watu wanakuja na katika kundi la watu tuliona watu wa kutisha sana wanatoka.
Walipotukaribia tuliona kuwa ni wanawake wazee na nywele zao nyeupe zilifungiwa vibofu vidogo vilivyotolewa katika matumbo ya samaki, vikipeperuka nyuma yao.
Nyuso zao zimetiwa rangi nyeupe na ya kimanjano; na nyuma walifunga ngozi za nyoka na kiunoni walijifunga mifupa ya wanadamu, na kila mtu alishika fimbo yenye meno matatu nchani mkononi mwake.
Jumla yao ilikuwa kumi, na mmoja wao alimwonyesha Gagula kwa mkono wake akasema, ‘Mama, mama mzee, tupo hapa.’ Yule Gagula akaitikia, ‘Vema! Vema! Vema! Macho yenu makali? Nyinyi watambuzi, nyinyi mnaweza kuona gizani?’ Wakajibu, ‘Mama, ‘Ni makali.’
Akasema, ‘Vema! Vema! Vema! Masikio yenu yamefumbuka, nyinyi watambuzi, nyinyi mnasikia maneno yasiyotamkwa kwa ulimi?
Wakajibu, ‘Mama, yamefumbuka.’ Akaitikia, ‘Vema! Vema! Vema! Pua zenu zinaweza kusikia harufu, nyinyi watambuzi? Mnaweza kusikia harufu ya damu, manaweza kusafisha nchi yetu kwa kuwaondoa wale wanaomfanyia maovu mfalme na jirani zao?
Mpotayari kuhukumu kwa haki za mbinguni? Nyinyi niliowafundisha, mliokula mkate wa busara zangu na kunywa maji ya uwezo wangu?’ Wakaitikia, ‘Mama, tunaweza.’
Basi akasema, ‘Vema, nendeni.
Msikawie, nyinyi tai; mwaona wauaji?’ (Akawaonyesha wale waliosimama tayari kuua.) ‘Haya fanyeni mikuki yao kuwa mikali; watu weupe waliotoka mbali wana hamu ya kuona, nendeni!’