Kichaa Msafi
JF-Expert Member
- Dec 26, 2017
- 1,087
- 2,134
mkuu hongera sana na shukrani kwa kutuletea hii simulizi ya kale nilikuwa nipita kimya kimya lakini leo nikaona nikupe heshima yako hongera sana
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Navuta picha ya gagula wa filamu ya Shaka Zulu, maana yataka moyo kumkabili.Gagula umemwona?
Ahsante mkuu blackstarlineBasi tulianza kufanya imara mahali petu jinsi tulivyoweza. Kila mtu alifanya kazi nyingi sana.
Vinjia vyote vya kupandia kilima tuliviziba kwa chungu za mawe, tukakusanya chungu za mawe makubwa sana tayari kuyaangushia adui wakijaribu kupanda kilima.
Jua lilipokaribia kushuka tulipumzika kidogo tukaona kundi dogo la watu wanatujia kutoka mji wa Loo na mmoja alikuwa amechukua jani mkononi ili iwe dalili ya kutufahamisha kuwa yeye ni tarishi aliyetumwa.
Alipokaribia Ignosi na Infadus na wakubwa wawili watatu walishuka kumlaki. Tarishi huyo alikuwa mtu mkubwa shujaa, amevaa ngozi ya chui. Alipofika karibu alisema, ‘Salamu za mfalme kwa wale wanaompiga vita. Salamu za simba kwa wale fisi wanaovitafuna visigino vyake.’
Nikasema, ‘Haya sema utakayo.’ Akaendelea, ‘Haya ni maneno ya mfalme; mjitoe katika mikono ya mfalme kabla hamjapatwa na maafa. Bega la fahali mweusi limekwisha pasuliwa, na mfalme anamtembeza kambini huku linatoka damu.’ (Desturi hii inafuatwa katika makabila mengine ya Afrika ikiwa ni mwanzo wa vita au mwanzo wa jambo kubwa jingine).
Nikamuuliza, ‘Je, na mapatano ya mfalme yatakuwaje.?’ Akajibu, ‘Mapatano ya mfalme ni ya huruma na rehema, yaliyo stahili mfalme Twala.
Haya ndiyo maneno ya Twala, Mwenye chongo, Mume wa wake elfu, Bwana wa Wakukuana, Mlinzi wa Njia Kuu, Mpenzi wa Wale Watatu wakaao kimya juu ya milima ile, Ndama wa Ng’ombe Mweusi, Ndovu ambaye akikanyaga nchi ardhi hutetemeka.
Kitisho cha watenda maovu, Mbuni ambaye miguu yake hula jangwa, Mkubwa, Mweusi, Mwenye busara, Mfalme kutoka karne hata karne!
Haya ndiyo maneno ya mfalme Twala: Nitakuonyesheni rehema, nitaridhika kwa damu kidogo tu.
Mmoja katika kila kumi atakufa, wengine watapata msamaha; lakini Yule mtu mweupe aliyemuua Skraga, Yule mtu mweusi mtumishi wake anayejidai mfalme, na Infadus ndugu yangu anayefitinisha watu wangu, hawa watakufa kwa maumivu na mateso, wawe sadaka ya Wale Watatu wakaao kimya. Haya ndiyo maneno ya huruma ya Twala.’
Basi nikazungumza kidogo na wenzangu, kisha nikasema, kwa sauti kubwa ili wale askari wote wasikie, nikasema. ‘Rudi kwa Twala, wewe mbwa, rudi kwa aliyekuleta, ukamwambie kuwa:
Sisi,na Ignosi mfalme wa kweli wa Wakukuana, na sisi watu weupe wenye hekima tuliotoka katika nyota, tutiao mwezi giza, na Infadus wa ukoo wa ufalme, na Wakubwa na askari na watu waliokusanyika hapa tunampa jawabu na kusema: hatutajitoa kabisa katika mikono ya Twala; na kabla jua halijashuka mara mbili, Twala atalala maiti mkavu mbele ya mlango wake wa ikulu, na Ignosi, ambaye baba yake aliuawa na Twala, atatawala katika mahali pake! Sasa nenda, tusije tukakufukuza kwa mijeledi, nawe uangalie sana usiinue mkono wako kupigana na watu kama sisi.’
Yule tarishi akacheka akasema, ‘Huwezi kunitisha kwa maneno makubwa yanayovuma sana. Mjionyeshe kuwa mashujaa kesho, nyinyi mnaotia giza mwezi. Muwe mashujaa, mpigane kwa furaha kabla kunguru hajachambueni nyama mbali na mifupa yenu, mpaka ikawa meupe kuliko sura zenu zilivyo.
Kwaherini; labda tutaonana tena vitani, nawaombeni msiruke kwenda juu katika nyota tena bila ya kuningojea mimi.’
Basi alipokwisha kusema maneno hayo ya kutudharau, akatoka akaenda zake, na punde jua lilishuka. Usiku ule tulikuwa na kazi nyingi, maana ingawa tulichoka mno ikawa lazima kutengeneza vitu vyote tayari kadiri tulivyoweza tusiache jambo hata moja, na matarishi walikuwa wakija na kutoka mahali petu pa mashauri.
Basi yapata saa tano usiku, mambo yote tuliyoweza kuyatengeneza yalikwisha kuwa tayari, na kambi ikawa kimya kabisa ila kwa sauti za watu ‘Yaliokuwa wakishika zamu.
Mimi na Bwana Henry tukashuka kilimani pamoja na Ignosi na mkubwa mmoja tukazunguka kila mahali pa mbele penye mlinzi, tukaona kuwa wote wapo macho. Kisha tukarudi tena tukipita katikati ya askari maelfu waliolala usingizi ambao wengi wanalala usingizi wa mwisho duniani.
Nikamwambia Bwana Henry, ‘Mimi nimo katika hali ya woga kabisa. Mimi nafikiri kuwa hapana mmoja katika sisi atakayekuwa mzima usiku wa kesho. Tunashambuliwa na askari wengi kabisa kupita askari wetu.’
Bwana Henry akasema, ‘Tutafanya jitihada. Tutaonyesha ushujaa wetu lakini mambo haya ni makubwa mno, na kweli si haki yetu kuingia katika shughuli hii, lakini tumekubali na kwa hivyo lazima tufanye tuwezavyo.
Mwenyewe nimechagua kufa katika vita kuliko kufa kwa namna nyingine, na sasa nimeona kuwa hatuwezi kumwona ndugu yangu tena, basi kufa kwangu si kugumu.
Lakini kila mara hutokea kuwa mashujaa wana bahati, na labda tutawashinda. Liwalo naliwe lakini vita vitakuwa vikali nasi lazima tuwe katikati kabisa ya vita.’
Alisema maneno haya kwa sauti ya huzuni kabisa, lakini niliona macho yake yaking’aa sana nikatambua kuwa Bwana Henry kwa kweli alipenda vita.
Baada ya haya tulilala usingizi muda wa saa mbili. Ilipokuwa karibu na mapambazuko tuliamshwa na Infadus aliyekuja kutuarifu kuwa kwa upande wa mji wa Loo kuna shughuli nyingi, naya kuwa askari wengine wa Twala wanawafukuza askari wetu waliowekwa mahali pa mbele kulinda.
Tukaondoka tukavaa tayari kwa vita, tukavaa zile nguo za chuma ndani ya nguo zetu za kila siku, tukashukuru sana kuwa nazo.
Tulipokwisha kuvaa tulikula kwa haraka tukatoka kutazama mambo yanavyoendelea. Mahali pamoja juu kilimani palikuwa mwamba mkubwa, tukafanya kuwa ngome yetu na mahali pa kutazamia chini pote.
Hapa tuliona Infadus amezungukwa na kikosi chake kilichoitwa Wajivu, na bila shaka askari hao walikuwa bora kupita wote katika jeshi la Wakukuana.
Kikosi hicho kilikuwa na askari elfu tatu na mia tano, nacho kiliwekwa hapa kuwa kama akiba, na askari walikuwa wamelala chini wakitazama askari wa Twala wakitoka mji wa Loo, wakitambaa kama siafu.
Ilikuwa kama kwamba mistari hiyo ya askari wa Twala haina mwisho, nayo ilikuwa mistari mitatu na kila mstari ulikuwa na askari kadiri ya elfu mbili.
Walipokwisha toka mjini walijipanga. Jeshi moja likachagua njia ya kulia, na jingine njia ya kushoto, na jingine njia ya katikati.
Basi Infadus akasema, ‘Ah! Watatushambulia kutokea pande tatu kwa mara moja.’
Hii ilikuwa habari mbaya, maana mahali petu pa juu ya kilima palikuwa kama duara na urefu wa duara ile ulikuwa hadiri ya mwendo wa saa nne, na kwa kuwa eneo lake lilikuwa refu na askari wetu ni wachache, ikawa lazima tusongane kadiri tulivyoweza.
Lakini kwa kuwa hatukuweza kutambua hasa namna watakavyo tushambulia ikawa lazima tufanye tuwezavyo, tukapeleka habari kwa vikosi vyote kila mtu awe tayari kujitetea katika mashambulio.
Pamoja sana mkuu
Mambo ni moto[emoji39]Basi tuliondoka hapo kwa haraka tukapita upande wa pili wa kilima, tukamwona Bwana Henry ameshika shoka lake la vita mkononi, na Ignosi na Infadus na wakubwa wachache wengine wanasemezana na kushauriana.
Bwana Henry akasema, ‘Ah, nimefurahi umekuja. Ignosi anataka kufanya mambo nami sifahamu maneno yake.
Nadhani kuwa ingawa tumekwisha kuwashinda maadui kwa sasa, lakini askari wengine wengi wanaletwa kumsaidia Twala, naye anadhani anawaweka watuzunguke ili tusipate chakula, na Infadus anasema kuwa maji yetu yapo karibuni kuisha.’
Infadus akasema, ‘Ndiyo, kweli. Chemchem haitoki maji ya kutosha watu wengi, na sasa yanapungua. Kabla ya kuingia usiku, wote tutaona kiu. Sikiliza, Makumazahn, wewe ndiye mwenye akili, pengine umeona vita vingi katika nchi nyingine, yaani ikiwa wanafanya vita katika nyota.
Twambie tufanye nini? Twala ameleta watu wengi kuchukua mahali pa wale waliokufa. Twala amekwisha pata akili.
Mwewe hakufikiri kukuta kuku tayari! Lakini tumekwisha muuma kifua; ana hofu kutupiga tena. Lakini hata na sisi tumejeruhiwa naye atangoja hapo mpaka tufe; atatuzunguka kama anavyofanya chatu anapokamata swala. Naye atapigana vita vya kusubiri tu.’
Nikasema, ‘Vema nimekusikia.’
Basi akaendelea, akasema, ‘Basi Makumazahn, waona sisi hapa hatuna maji, na chakula tulichonacho ni kidogo tu, nasi lazima tuchague kukaa na kufa kama simba anayekufa katika pango lake kwa njaa, au kujaribu kutoka kwa njia ya kaskazini au tumrukie Twala na kumshambulia kwa nguvu zetu zote.
Ndovu (yaani Bwana Henry ) ni shujaa, maana leo amepigana kama nyati aliyetegwa, na askari wa Twala walianguka mbele yake kama mtama mchanga unaopigwa na mvua yam awe; yeye asema ni afadhali tuwarukie; lakini ni desturi ya ndovu kushambulia.
Je, wewe Makumazahn, wasemaje? Wewe sungura mwerevu aliyekwisha ona mambo mengi na kupenda kumumiza adui kutoka kwa nyuma. Shauri la mwisho ni Ignosi aliye mfalme, maana ni hiari ya mfalme kupigana vita, lakini na tusikilize shauri lako, Ee Makumazahn.
Na vile tusikilize shauri la Bougwan, yeye mwenye jicho linalong’aa’. (Maana hilo ni jina walilomwita Bwana Good.)
Nikamuuliza Ignosi, ‘Je, Ignosi, wasemaje?’ lakini yeye, ambaye alikuwa mtumishi wetu lakini sasa amevaa kiaskari na kuonekana kuwa mfalme kabisa, akajibu, ‘Hapana, tafadhali wewe sema, nami niliye mtoto tu kwako kwa akili zangu, nitasikiliza maneno yako.’
Basi kuombwa hivyo, nikashauriana na Bwana Henry na Bwana Good, kisha nikawapa kauli yangu. Ikawa ya kuwa sisi tumekwisha tiwa mtegoni, na tena maji yanatupungukia, ni afadhali tuwashambulie askari wa Twala.
Tena nikashauri kuwa yafaa kuanza shambulio mara moja kabla ya kukauka majeraha yetu, na tena kabla askari wetu hawajakata tamaa kwa kuona wingi wa askari wa Twala.
Nikasema kuwa tukingoja, huenda wakubwa wengine wa upande wetu wakaghairi na kwenda kufanya suluhu na Twala, na hata kututia katika mikono yake.
Basi kauli yangu ikapokewa kwa furaha; na Wakukuana walipendezwa sana na shauri langu. Lakini neno la mwisho likawa kwa Ignosi aliye mfalme, tukamgeukia tusikilize asemavyo.
Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu kidogo akifikiri , alisema, ‘Rafiki zangu watu weupe; na Infadus mjomba wangu, na wakubwa wangu; nimekaza moyo wangu. Nitampiga Twala leo hivi na kubahatisha nguvu zetu.
Sikilizeni, hivi ndivyo namna nitakavyowapiga. Sasa ni saa sita na watu wote wanakula na kupumzika baada ya vita. Baadaye kidogo jua linapoanza kushuka, wewe mjomba wangu pamoja na jeshi lako uende pamoja na jeshi lingine hata pale penye mteremko, na mara Twala atakapowaoneni ataleta jeshi lake kupigana.
Lakini njia hii nyembamba na kwa hivyo jeshi linaweza kuja kikosi kikosi; na kwa hivyo wataangamizwa kikosi kikosi, na macho ya askari wote wa Twala yatakuwa yanatazama vita hivi vikali.
Na rafiki yangu Ndovu (yaani Bwana Henry) atafuatana nawe, na Twala akiona shoka lake kubwa linang’aa na kumeremeta katika safu ya kwanza ya Wajivu, moyo wake utafifia.
Mimi nitafuatana na jeshi la pili litakalokufuata wewe, yaani, ikiwa wewe utaangamizwa , basi mfalme atabaki, na watu watapigana kwa ajili yake. Na Makumazahn ataandamana pamoja na mimi.’
Infadus akasema, ‘Vema, Ewe Mfalme.’ Ignosi akaendelea tena akasema, ‘Na hapo askari wote wa Twala wanapotazama vita vikali, nataka jeshi la tatu lililobaki ligawanyike sehemu tatu.
Sehemu moja itatambaa kwenda kwa upande wa kushoto wa adui na kuwarukia, na sehemu ya pili watatambaa kwenda upande wa kulia, nami nikiona kuwa askari wa pande zote mbili wako tayari kuwarukia watu wa Twala, basi mimi nitashambulia kwa katikati, na tukiwa na bahati, tutashinda.
Nasi kabla jua halijashuka kabisa tutakuwa tumekaa kwa amani na raha katika mji wa Loo.
Na sasa tule tujiweke tayari, na wewe, Infadus, utengeneze mambo yote tusije tukasahau hata kitu kimoja, na Bougwan (yaani Bwana Good) yeye na aandamane na wale watakaokwenda kwa upande wa kulia apate kuwatia wakubwa nguvu kwa jicho lake linalong’aa.’
Basi matengenezo hayo yote yakafuatwa kwa upesi sana, yakaonyesha ustadi wa uaskari wa Wakukuana. Katika muda wa saa moja, watu wote walikuwa wamekwisha kula na majeshi yaligawanyika tayari.
Baadaye kidogo Bwana Good akatujia mimi na Bwana Henry akasema, ‘Kwaherini, rafiki zangu. Mimi nakwenda kwa upande wa kulia, na sasa nimekuja ili tupeane mikono maana labda hatutaonana tena.’ Basi tukapeana mikono kwa kimya sana na uzuni.