blackstarline
JF-Expert Member
- Sep 19, 2016
- 3,278
- 7,966
- Thread starter
- #121
Badaye kama kawaidaMzee baba shisha nondo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Badaye kama kawaidaMzee baba shisha nondo
Ukuwepo miaka ya semanini
Kama ulikua msomaji wa simulizi za namna hii tangu utotoni, hakika utapata utamu wake. Kuna aina ya picha inakuja kichwani, inakufikilisha maisha ya Afrika ya zamani, maisha ya nyikani, enzi za wanyama wa kila namna katika mbuga na nyanda zilizo na miti, vichaka na mbuga zenye nyasi. Ni simulizi ambazo hata lugha yake haichoshi machoni na masikioni. Hakika nyakati hizo zimepita na hazitarudi tena.UTANGULIZI
Hadithi hii ilipigwa chapa kwa lugha ya Kiingereza katika mwaka 1885. Katika mwaka 1905 Bwana H. Rider Haggard aliandika maneno haya: 'Sasa katika mwaka 1905 naweza kuzidisha maneno yangu kwa kusema ya kuwa nimefurahishwa sana kuona hadithi yangu inadumu kuwapendeza wasomaji wengi. Hayo yaliyobuniwa yamedhibitishwa kuwa ni kweli: Mashimo ya Malme Sulemani niliyokuwa nikiyafikiri sasa yamegunduliwa nayo sasa yanatoa dhahabu tena, na kwa habari zilizotoka hivi karibuni hata almasi pia hutoka.'
MASHIMO YA MFALME SULEIMAN
SURA YA KWANZA
Kukutana na Bwana Henry Curtis
Ni ajabu sana kwa mtu aliyefika umri wangu, yaani miaka hamsini na tano, kushika kalamu na kuanza kuandika kitabu, kama hivi ‘nifanyavyo mimi sasa. Sijui habari hizi zitakuwaje nikiisha kuzitunga, yaani nikijaliwa kufika mwisho wa safari yangu salama, maana ingawa nimefanya mambo mengi katika maisha yangu, lakini sijawahi kujaribu kuandika kitabu. Tokea utoto wangu nimeshughulika na kazi ya biashara na kuwinda, kupigana na kuchimba dhahabu, na tangu kupata utajiri huu nilionao ni miezi minane tu.
Sasa nina mali nyingi sana, hata jumla yake siijui, lakini nadhani nisingekubali kuvumilia tena hayo yote niliyoyavumilia katika miezi kumi na tano iliyopita hata kama ningejua kwa hakika kuwa nitatoka salama pamoja na mali nyingi pia. Mimi ni mtu mtaratibu, sipendi ghasia, na tena nimechoka kabisa kusafirisafiri na kupambana na mambo ya ajabu. Sijui kwa nini naandika kitabu hiki, maana uandishi si kazi yangu. Mimi si mwana chuoni ingawa napenda sana kusoma vitabu. Hebu kwanza nijaribu kuandika sababu zangu za kutunga kitabu hiki, ili muone kama kweli ninazo sababu.
Sababu ya kwanza ni kuwa Bwana Henry Curtis na Bwana Good wameniomba nikitunge. Sababu ya pili ni kuwa nimebaki hapa Durban kwa kuwa mguu wangu wa kushoto waniuma sana. Tangu nilipoumwa na simba ninapata maumivu, na hasa siku hizi yanazidi, hata siwezi kwenda vizuri. Nadhani haikosi meno ya simba yana sumu na kama sivyo majeraha yangeisha pona kabisa na yasinge rudi tena, na hasa ajabu ni kuwa yanarejea mwezi ule ule niliyong’atwa. Ni ajabu sana kuwa baada ya kuua simba sitini na tano na labda zaidi, Yule wa sitini na sita aliniuma mguu. Jambo hili limeharibu mipango yangu ya desturi yote, na kwa kuwa mimi ni mtu wa kufuata taratibu na mipango naona dhiki kabisa. Lakini hayo hayamo katika habari za kitabu hiki.
Sababu ya tatu ni kuwa nataka mwanangu Harry anaesoma katika chuo cha utabibu, awe na mazungumzo ya kumfurahisha na kumpendeza. Asifanye upumbavu. Kusomea utabibu si kazi rahisi, na kazi ya kuvumbua habari za mwili vile vile inachosha. Habari zilizomo katika kitabu hiki si kama zile zinazotokea kila siku, kwa hivyo labda zitamfurahisha kwa muda kidogo.
Sababu ya nne na ilivyo ya mwisho ni kuwa nataka kusimulia hadithi ya ajabu kupita zote ninazozijua. Labda itakuwa ajabu kweli kwa kuwa hapana mwanamke aliyetajwa katika hadithi hii, ila Foulata. Lakini ngoja kwanza! Nilitaka kumsahau Gagula, lakini sina hakika kama alikuwa mwanamke au shetani. Lakini kwa umri wake ulizidi miaka mia moja na kwa kuwa: haoleki, basi simhesabu kuwa mwanamke. Basi afadhali nijifunge kibwebwe. Kazi ni ngumu nami naona kama nimekwisha yavulia nguo maji. Lakini kama wasemavyo wajuzi, ‘Pole pole ndio mwendo,’ Basi sasa naanza.
‘Mimi Alan Quatermain, mzaliwa wa Durban, Natal, naapa na kusema …’Hii ndiyo namna nilivyoanza kusema mbele ya kadhi nilipokuwa natoa habari za kufa kwa Khiva na Ventvogel, lakini naona kuwa hii siyo namna ya kuanza kutunga kitabu. Basi, je, mimi ni muungwana? Muungwana ni nini? Sijui hakika. Maisha yangu yote nilikuwa nikifanya kazi ya biashara na kuwinda tu. Nimejaribu daima kuwa muungwana, basi wewe usomaye utanihukumu. Mungu ajua kuwa nimejaribu. Ama kweli katika maisha yangu nimeua watu wengi, lakini sikuu mtu bure wala sikuua mtu asiye na hatia, ila kwa kujilinda mwenyewe tu. Mwenyezi Mungu alitupa maisha, nadhani nia yake ni kwamba tujilinde, nami siku zote nimeshikilia hivyo ; natumaini kwamba hayo hayatanitia hatiani siku ya kuhukumiwa itakapowadia.
Lakini dunia ina ukali na maovu, na ingawa mimi ni mtu taratibu na mwoga kidogo nimeona mauaji mengi. Lakini naweza kusema kuwa sijaiba, ingawa mara moja nilimdanganya mtu mmoja nikachukua kundi la ng’ombe wake. Lakini yeye alikuwa amenifanyia mambo mabaya kabisa na hata hivyo, tangu siku ile ninajuta kwa vitendo vyangu nilivyovifanya.
Toka nilipokutana na Bwana Henry Curtis na Bwana Good mara ya kwanza, imepita miezi kumi na nane, na namna tulivyokutana ilikuwa hivi: Nilikwenda kupita Bamangwato ili kuwinda ndovu. Nikawa na bahati mbaya sana katika safari hiyo, na juu ya hayo nilishikwa na homa kali. Nilipopona nikasafiri mpaka kunakochimbwa almasi, nikauza pembe zangu zote nilizokuwa nazo pamoja na gari la ng’ombe, nikawapa ruhusa wawindaji wangu, na mimi mwenyewe nikapanda gari niende Captown. Baada ya kukaa Captown kwa muda wa jumaa moja niliona kuwa gharama za hoteli zinazidi sana, tena nilikuwa nimekwisha ona yote niliyoyataka kuyaona, basi nikanuia kurudi Natal kwa meli iitwayo Edinburg Castle inayotoka Ulaya.
Basi nikaenda kukata tiketi nikaingia melini, na jioni ile ile meli ikang’oa nanga tukasafiri. Katika abiria walioingia melini niliona wawili niliowatazama sana. Mmoja alikuwa mtu mwenye umri kadiri ya miaka thelathini, kifua kipana na mikono mirefu kushinda watu wote niliowahi kuwaona. Nywele zake zilikuwa za rangi ya kimanjano na alikuwa na ndevu nyingi za rangi ile ile, na macho yake yalikuwa ya rangi ya kijivujivu tena yameingia ndani. Wala nilikuwa sikupata kuona mtu mzuri kumpita yeye. Halafu nikajua kuwa huyu ni Bwana Henry Curtis. Yule mtu mwingine aliyekuwa akiongea na Bwana Henry alikuwa mfupi tena mnene, kisha mweusi kidogo, na sura yake ilikuwa haikufanana hata kidogo na ile ya Bwana Henry. Halafu nikajua kuwa anaitwa Bwana Good.
Basi jioni nilipokuwako sitahani nilisikia sauti, mara nikageuka kuangalia, nikaona kuwa ni Yule Bwana Good. Hata tulipokwenda chini kula chakula tulimkuta Bwana Henry amekwisha kaa mezani, na mara tukaanza kuongea habari za kuwinda na mambo mengineyo. Akaniuliza maswali mengineyo. Akaniuliza maswali mengi sana, nami nikamjibu kadiri nilivyoweza. Halafu yake tukaanza kuongea habari za ndovu, na mtu mmoja aliyekuwa karibu yetu akasema, ‘Ee bwana, kama ukitaka mtu hasa anayeweza kukwambia kweli habari za ndovu, ni mwindaji Quatermain.’ Bwana Henry Curtis aliposikia hivi, akashtuka na akasema kwa sauti ya upole, ‘Niwie radhi bwana, jina lako wewe ni Allan Quatermain?’ Nikamwambia, ‘Ndiye mimi.’
Tulipokwisha kula, tukawa tunatoka mezani, na Bwana Henry akanijia kunikaribisha niende chumbani kwake tukavute tumbako, nami nikakubali. Mradi tulikuwa watu watatu, na mara Bwana Henry Curtis akasema, ‘Bwana Quatermain, nadhani miaka miwili iliyopita ulipata kuwako mahali panapoitwa Bamangwato katika nchi ya Transvaal,sivyo? Kusikia hivyo nikaona ajabu sana yeye kujua habari za safari zangu. Nikamwambia, ‘Ndiyo nilikuwako’, Bwana Good akauliza, ‘Ulikuwa ukifanya biashara sivyo?’ Nikajibu, ‘Ndiyo, nilichukua gari la bidhaa nikapiga kambi nje ya mji, nikakaa huko mpaka nilipokwisha kuuza zote .’ Bwana Henry aliyekuwa amekaa katika kiti kukabili kiti changu, akaniuliza, ‘Ulipata kukutana na mtu mmoja jina lake Neville?’ Nikajibu, ‘Ndiyo, tulipiga kambi zetu karibu kwa muda wa siku kumi na nne, na baada ya miezi michache nikapokea barua kutoka kwa Mwana Sheria ya kuniuliza habari zake kama namjua alipo, nami nikapeleka majibu kueleza habari zake kama nilivyoweza.’
Bwana Henry akasema, ‘Najua, maana barua yako ililetwa kwangu. Ulisema kwamba mtu aitwaye Neville alitoka Bamangwato mwanzo wa mwezi wa Mei akasafiri kwa gari pamoja na watu wake na mwindaji mtu mweusi mmoja jina lake Jim, naye alisema kuwa anakwenda mpaka Inyati ambao ndio mji wa mwisho katika nchi ya Mtabele ; akifika hapo atauza gari lake aende kwa miguu. Kisha ulisema kuwa kweli aliuza gari lake kwa sababu uliliona tena baada ya miezi sita, na mtu uliyemwona nalo alikuwa ni Mreno mfanya biashara aliyekwambia kuwa amelinunua Inyati kwa mtu mweupe mmoja, ambaye jina lake amelisahau ila anafikiri kuwa yeye pamoja na boi wake amekwenda mwituni kuwinda.’ Nikajibu, ‘Hayo ni kweli.’ Basi tukanyamaza kidogo, kisha, Bwana Henry Curtis akasema, ‘Naona ya kuwa hujui vema habari hizo. Huwezi kukisia sababu zake za kusafiri kwenda kaskazini na mahali gani alipokwenda?’ Nikamjibu, ‘Nilisikia kidogo.’
Na kwa kuwa sikutaka kusema naye zaidi juu ya habari hizi nikanyamaza kimya. Bwana Henry na Bwana Good wakatazamana, kisha Bwana Good akatikisa kichwa kwa kumfanyia ishara Bwana Henry, akasema, ‘Bwana Quatermain nitakusimulia hadithi yangu, halafu unipe shauri na msaada wako. Yule wakili wangu aliyeniletea barua yako aliniambia kuwa wewe ni mtu wa heshima sana na watu wote wanakustahi, na kwa hiyo naweza kukuamini. Basi nikainamisha kichwa kwa haya kwa vile nilivyosifiwa na Bwana Henry akaendelea kusema, ‘Huyo Bwana Neville ni ndugu yangu.’ Niliposikia hivi nikastuka sana, maana sasa nalifahamu sababu ya kumtazama sana nilimwona mara ya kwanza, kwa kuwa wamefanana sana.
Basi Bwana Henry akaendelea kusema, ‘Yeye ni mdogo wangu, na mpaka miaka mitano iliopita nadhani hatukupata kuachana hata kwamuda wa mwezi mmoja. Lakini katika mwaka ule wa mwisho tulioonana tulipatwa na msiba kama wanavyopatwa watu wote mara kwa mara. Maana tuligombana sana hata nilimtenda mambo yasiyo ya haki kwa ajili ya hasira zangu. Haikosi unajua kuwa mtu akifa na kama mali yake ni mashamba tu, wala naye hakuacha wosia wowote, kwa sheria ya Uingereza mrithi huwa ni Yule mtoto mwanaume mkubwa, yaani aliyezaliwa kwanza, ndiye anayechukua mali yote. Basi hivyo ndivyo ilivyokuwa. Na wakati ule tulipokuwa tukigombana baba yetu alifariki naye hakuwahi kuandika wosia. Basi kwa hivyo ilionekana kuwa mdogo wangu hakuwa na urithi.
Kusema kweli ilikuwa ni wajibu wangu kumsaidia na kumtunza, lakini kwa ule uchungu wa ugomvi jinsi ulivyokuwa mwingi sana, hata sasa naona aibu kukiri kuwa sikufanya jambo. Sikuwa na nia ya kumnyima haki yake, ila nilitaka yeye aje kwangu’ kuomba suluhu, naye hakuja. Nasikitika sana kukuudhi kwa habari hizi zangu, lakini naona sina budi kukueleza waziwazi mambo yote, sivyo Bwana Good?’ Bwana Good akajibu, ‘Ndivyo, nami najua kwa hakika kuwa Bwana Quatermain atayasitiri yote moyoni mwake.’ Nikajibu, ‘Vema,’ Maana mimi natafakari sana kuwa si mtu wa kupayuka.
Halafu Bwana Henry akasema, ‘Mdogo wangu alikuwa na fedha kidogo na bila kunishauri alitoa fedha zote alizokuwa nazo katika banki, na kuchukua jina lingine la Neville, akafunga safari kwenda kuchuma Afrika ya Kusini. Nikakaa kwa muda wa miaka mitatu bila kupata habari zake wala salamu zake, ingawa mimi nilimwandikia barua nyingi. Labda zilikuwa hazimfikii. Lakini baadaye nikaanza kuwa na wasiwasi, maana mtu haachi kumpenda ndugu yake.’
Nikasema, ‘Hayo ni ya kweli. ‘Maana nilikuwa nikimkumbuka mtoto wangu. Bwana Henry akawa anaendelea kusema, ‘Nikahisi kuwa hata nusu ya mali yangu yote nitatoa ili nipate kujua yaliyompata mdogo wangu, maana ni mmoja tu aliyebaki katika ukoo wangu. Basi siku zilipozidi kupita nami nikazidi kuwa na wasiwasi, nikatamani sana kupata habari zake. Ndipo nikaanza kuulizauliza, hata nikapata ile barua. Basi mpaka sasa habari ni nzuri, maana zaonyesha kuwa yu hai mpaka sasa. Na nilitia nia kwenda mwenyewe kumtafuta, na Bwana Good amenifurahisha sana kwa kufuatana nami.’ Basi Bwana Good akasema, ‘Ndiyo na sasa Bwana, labda utatwambia habari zote ujuazo za Yule mtu aitwaye Neville.’
SURA YA PILI
Basi kabla sijaanza kumjibu Bwana Good, nilitia tumbako katika kiko changu, na Bwana Henry akauliza, ‘ Ulisikia habari gani juu ya safari ya ndugu yangu ulipokuwako Bamangwato?’ Nikamjibu, ‘Nalisikia hivi, ya kuwa anakwenda kutafuta Mashimo ya Sulemani. Na tangu siku hiyo hata hivi leo, sijamwambia mtu habari hizo.’ Wote wawili wakauliza pamoja, ‘Mashimo ya Sulemani! Yapo wapi?’ Nikajibu, ‘Mimi sijui, lakini najua mahali ambapo watu husema kuwa yapo. Siku moja niliona vilele vya milima inayopakana nayo, lakini baina ya mahali hapo nilipokuwa mimi na milima hiyo palikuwa na jangwa la upana wa maili mia moja na thelathini, nami sijapata kusikia kuwa Mzungu yeyote amepata kuvuka jangwa hilo, isipokuwa mtu mmoja tu.
Lakini nadhani itakuwa vizuri zaidi nikisimulia habari hizo, yaani kama nilivyopokea kutoka kwa wenyeji, za Mashimo ya Sulemani kwa kadiri ninavyojua, ikiwa mtaahidi kuwa mtazisitiri mioyoni mwenu na kutomwambia mtu yeyote bila ya idhini yangu. Je, mtakubali sharti hilo?’ Bwana Henry akainamisha kichwa, na Bwana Good akaitikia, ‘Naam, naam.’ Basi, nikaanza kutoa hadithi yangu: ‘Kwa kawaida mwajua kuwa wawindaji wa ndovu ni watu wasiotamani anasa za dunia, wala hawashughuliki na mambo ila ya kweli ya dunia. Lakini pengine mwaweza kumkuta mtu mmoja mmoja anajitia katika mambo ya kuandika hadithi na kujaribu kutunga habari za zamani za watu wa kale. aliyeniambia maneno haya alikuwa ni mtu wa namna hiyo, na tangu aliponiambia maneno haya umepita muda wa miaka thelathini. Ilikuwa hivi: katika safari yangu ya kwanza nilikwenda kuwinda ndovukatika nchi ya Matabele. Mtu mmoja aliyeitwa Evans ndiye aliyeniambia maneno hayo, naye masikini aliuawana nyati mwaka wa pili yake, akazikwa mahali palipokuwa karibu na maporomoko ya maji yam to wa Zambezi. Nami nakumbuka sana kuwa siku moja nilikuwa nikizungumzia habari za kulungu na pofu katika mtaa mmoja wa Transvaal.’
Evans akasema, ‘Ndiyo, lakini mimi nitakutolea hadithi iliyo ya ajabu zaidi kupita habari za wanyama.’ Akaendelea kuhadithia jinsi alivyopata kuvumbua magofu ya mji wa zamani sana ambao aliamini kuwa ni mji ule uliokuwa ukiitwa Ophir uliotajwa katika Agano la Kale,na tangu siku hizo, watu wengi wenye maarifa kuliko yeye marehemu Evans wamesema hivyohivyo. Mimi nikakaa kusikiliza sana, maana wakati ule mimi nilikuwa bado kijana, na hadithi zile za kale zilinipendeza sana, na mara akasema, ‘je, mwanangu, umepata kusikia habari za milima ya Sulemani iliyo upande wa kaskazini wa nchi ya Mashukulumbwe?’’ , Nikamwambia, ‘Sijapata kusikia .’Akasema, ‘Basi, haidhuru, hapo ndipo mashimo ya Sulemani yalipo, yaani mashimo ya almasi.’ Nikamuuliza, ‘Je, wewe umejuaje?’ Akajibu, ‘Najuaje! Najua kwa jina lake lilivyo, na tena niliambiwa na mwanamke mmoja mchawi wa kabila la Isanusi katika nchi ya Manika. Alisema kwamba watu wanaokaa upande wa pili wa milima ile ni wa ukoo wa Amazulu, wanasema lugha inayofanana na Kizulu, ila wao ni wakubwa, tena wazuri zaidi ya Amazulu. Lakini kuna wachawi wenye nguvu nyingi wanaokaa humo na walikuwa na siri ya shimo la ajabu lenye mawe yale yanayong’aa.’ Nilicheka sana niliposikia hadithi hii, nikaipuuza, lakini ilinipendeza sana, maana wakati ule mashimo ya almasi yalikuwa bado hayajavumbuliwa. Lakini Yule marehemu Evans aliuawa, nami nikakaa muda wa miaka ishirini bila kufikiri tena jambo hili.
Baada ya miaka ishirini, na huo ni muda mrefu sana, maana mwindaji wa ndovu ana shida kuishi miaka ishirini katika kazi yake, nikasikia habari zaidi juu ya milima ya Sulemani na nchi iliyo upande wa pili yake. Hapo mimi nilikuwa katika nchi ya Manika, mahali paitwapo KwaSitanda, napo ni mahali pabaya sana, maana sikuweza kupata chakula wala wanyama hakuna. Nilishikwa na homa kali mno hata hali yangu ikawa dhaifu sana, na siku moja akafika Mreno mmoja pamoja na mwenziwe mmoja suriama. Tukaongea kidogo pamoja, maana yeye aliweza kusema Kiingereza kidogo, nami pia nilijua kusema Kireno kidogo, akaniambia kuwa jina lake ni Jose Silvestre, na tena ana shamba karibu na Delagoa Bay. Lakini siku ya pili yake aliondoka pamoja na mwenziwe. Katika kuniaga akasema ‘Bwana, tukionana tena natumai mimi nitakuwa tajiri kuliko watu wote duniani, nami nitakukumbuka.’ Nikacheka kidogo, maana nilikuwa mnyonge kwa homa na kwa hivyo sikuweza kucheka sana; nikamwona akienda kuvuka lile jangwa kwenda upande wa magharibi. Nikadhani kuwa ana wazimu, kwani anakwenda kutafuta nini huko? Baada ya juma moja, nikapona, na jioni nilipokuwa nimekaa nje ya hema langu dogo, nikitafuna paja la kuku wa mwisho niliyemnunua kwa mtu mmoja kwa bei ya kitambaa kimoja kilichonipatia kuku ishirini, nikitazama jua jinsi lilivyokuwa jekundu linavyoshuka nyuma ya jangwa hilo, mara nikaona kitu kama mzungu amevaa koti akiteremka mteremko uliokuwako kiasi hatua mia sita, mbele yangu.
Kwanza mtu huyo alitambaa kwa magoti na mikono, kisha akasimama na kupepesuka hatua chache mbele, tena akaanguka na kutambaa. Mradi nikaona kuwa ni mtu aliye taabani. Nikapeleka mmoja wa wawindaji wangu kwenda kumsaidia, na baadae kidogo akaja nae. Je, wadhani alikuwa ni nani? Alikuwa ni Yule Jose Silvetre, kwa kweli, mifupa yake ilikuwa dhaifu, tena alikuwa amekonda kabisa. Uso wake ulikuwa manjano, uking’aa kwa homa aliyokuwa nayo, nayale macho yake meusi makubwa yalionekana kama yaliyotokeza nje, maana alikuwa hana nyama kabisa .. Ngozi yake ilikuwa imekauka, na nywele zake zilikuwa zimegeuka rangi zikawa nyeupe, na mifupa imemtoka. Akawa anaugua huku akisema, ‘Nipeni maji! Jamani.
Nikaona kuwa midomo yake imepasuka na ulimi ulikuwa mweusi tena umevimba. Nikampa maji yaliyochanganyika na maziwa kidogo, akayabugia. Nikamzuia kusudi asinywe zaidi. Na mara homa ilimshika tena na kuanza kupayuka na kusema habari za milima ya Sulemani, na almasi na jangwa. Nikamchukua na kumweka hemani mwangu nikamtunza kama nilivyoweza; lakini nilijua kuwa atakufa. Kama saa tano ya usiku akatulia kidogo, nami ndipo nilipopata usingizi kidogo, nikalala. Kulipopambazuka nikaamka, nikamwona namna alivyokuwa amekonda sana amekaa na kulikodolea jangwa macho. Baadae kile kianga cha kwanza chajua kilionekana mawinguni, kikaangaza jangwa mpaka kufika kilele kirefu katika milima ya Sulemani, masafa ya maili mia moja na zaidi. Mara Yule mgonjwa akanyosha mkono wake mwembamba kuelekeza kileleni na huku akisema kwa Kireno, ‘Ndipo, ndipo papo hapo, lakini mimi sitawahi kupafikia kamwe. Wala hapana atakayepafikia kwamwe!’ Mara akakaa kimya kidogo kama mtu anayewaza jambo moyoni, halafu akanigeukia akasema, ‘Rafiki bado ungalipo? Ama sasa naona macho yangu yanaingia giza,’ Nikajibu, ‘Ndiyo, nipo hapa hapa.
Lakini sasa afadhali ulale upumzike.’ Akasema, ‘Ndiyo nitapumzika sasa hivi; tena nitakuwa na wasaa mwingi wa kupumzika, hata milele. Nisikilize, ninakufa! Wewe umenitendea mema. Nitakupa hati. Labda utaweza kupafikia ikiwa utaishi na kuvuka jangwa ambalo limemuua mtumishi wangu na mimi!’
Akapapasapapasa katika mfuko wake akatoa kitu nilichokidhania kuwa kikoba cha kuwekea tumbako kilichofanywa kwa ngozi ya mnyama. Kikoba hicho kilifungwa kwa uzi wa ngozi naye alijaribu kukifungua asiweze. Akanipa akisema, ‘Fungua.’Nikakifungua nikatoa kipande cha kitambaa kikuukuu cha katani kilichokuwa kimeandikwa maneno, na ndani ya kitambaa hicho mlikuwamo karatasi. Kisha akasema kwa sauti ya kufifia, maana alizidi kudhofu, akanena, ‘Juu ya hiyo karatasi kumeandikwa yote yaliyoshindikwa juu ya kitambaa na hivyo ilinibidi kufanya kazi miaka hata kuweza kuisoma. Sikiliza: Babu yangu ambaye ilimlazimu kuutoka mji wa Lisbon alikuwa katika Wareno hao wa kwanza waliofika katika nchi hii.
Aliandika maneno hayo wakati alipokuwa akifa katika milima ile ambayo hapana hata Mzungu mmoja aliyepata kuikanyaga kwa miguu yake mpaka hivi leo. Jina lake lilikuwa Jose da Silvestre, naye aliishi miaka mia tatu, nyuma. Mtumishi wake aliyekuwa akimngojea upande huu wa milima aliona kuwa amekwisha kufa, nae ndiye aliyeleta maandishi haya mpaka Delagoa. Na tokea wakati huo yametunzwa na warithi wake, lakini hapana aliyetaka kuyasoma, mpaka mimi nilipofaulu. Nami nimepoteza maisha yangu kwa ajili yake, lakini labda mtu mwingine ataweza kufaulu na kuwa tajiri kupita watu wote duniani. Lakini usimpe mtu mwingine bwana, wewe nenda mwenyewe!’ Akaanza kuugua tena, na baada ya saa moja akafa. Mungu amrehemu. Nilimzika katika kaburi la kwenda chini sana, nikaweka na mawe makubwa juu ili kusudi asifukuliwe na fisi. Kisha nikaondoka pale.
Bwana Henry akauliza, na sauti yake ilionyesha jinsi alivyokuwa akisikiliza maneno yangu, ‘Ehe, lakini hiyo hati iko wapi? Naye Bwana Good akaongeza, ‘Hati hiyo iko wapi sasa, iliandikwa habari gani?’ Nikasema, ‘Mkitaka nitawasimulia habari zake. Nami sijamwonyesha hata mtu mmoja ila Mreno mmoja mfanya biashara aliyekuwa amelewa wakati alipoitafsiri, tena hakosi’ kuwa alikuwa amekwisha sahau habari zake ulevi ulipomtoka. Hicho kitambaa chenyewe nimekiweka kwangu Durban pamoja na hiyo karatasi aliyoifasiri marehemu Jose, lakini hapa ninayo tafsiri ya Kiingereza na nakala ya ramani iliyokuwamo, nayo ni hii:’
Mimi Jose da Silvestre nipo hapa ninakufa kwa njaa ndani, ya pango dogo katika upande wa kaskazini mwa titi la mlima ulio upande wa kusini wa milima miwili ambayo nimeipa jina la Maziwa ya Sheba. Naandika haya kwa kipande cha mfupa na wino wa damu yangu mwenyewe katika mwaka 1590. Ikiwa mtumishi wangu atakuja na kuiona na kuichukua mpaka Delagoa, nataka rafiki yangu (Na hapo katika hati, jina lake limefutika.) ampashe habari mfalme ili alete jeshi la askari watakaoweza kuvuka jangwa hili na kuwashinda hawa Wakukuana walio majabali sana na wenye uchawi mwingi. Lakini kwa sababu ya hila na udanganyifu wa Mchawi Gagula sikuweza kuleta kitu cha ushahidi, tena hata maisha yangu nayo nimeyaokoa kwa shida nyingi. Na huyu atakayekuja na afuate ramani, apande theluji ya ziwa la kushoto la Sheba mpaka afike penye titi, ambapo kwa upande huo wa kaskazini pana njia kuu iliyotengenezwa na Sulemani. Kutoka hapo ni mwendo wa siku tatu kufikia jumba la Mlalme. Basi na amwue Gagula. Nawe niombe dua.
Kwaheri. Jose da Silvestre.
Nilipokwisha soma barua na kuonyesha ile nakala ya ramani iliyoandikwa na Yule mzee kwa damu ya mkono wake, wakanyamaza kimya kwa ajili ya kustaajabu kwao. Baadae Bwana Good akasema, ‘Lo! Nimezunguka dunia mara mbili, tena nimefika bandari nyingi lakini sijapata kusikia hadithi kama hii hata vitabuni.’ Bwana Henry akasema, ‘Ni hadithi ya ajabu Bwana Quatermain. Natumai unajaribu kutuhadaa! Najua kwamba watu hudhani kuwa si vibaya kumhadaa mjinga.’ Niliposikia hivi nikaudhika, nikatwaa karatasi nikaiweka mfukoni, maana sikupenda kudhaniwa kuwa ni mmoja wa wale wapendao kusimulia uwongo na kuwahadithia wageni habari za kuwinda na mambo mengine ambayo hayakutokea kamwe. Basi nikajibu, ‘Kama unafikiri hivyo basi mambo yaishe hapa hapa. Nikasimama nikataka kwenda zangu. Bwana Henry akaniwekea mkono wake begani pangu akasema, ‘ Kaa, Bwana Quatermain, niwie radhi, usiudhike; kwani naona kuwa hupendi kutuhadaa, lakini hadithi yenyewe ni ya ajabu mno hata kwanza niliona vigumu kuisadiki.’
Basi ndipo nilipoanza kutulia kidogo, maana nilipofikiri niliona kuwa si ajabu kuwa yeye hawezi kusadiki hadithi, nikamwambia, Tutakapojaliwa kufika Durban utaona ramani ya asili na maandishi yake. Lakini bado sijakwambia habari za ndugu yako. Nilimjua Yule Jim aliyekuwa pamoja naye. Yeye ni Mbechuana, mwindaji hodari, tena na mtu mwenye busara. Siku hiyo Bwana Neville alipoanza safari yake nilimwona Jim amesimama karibu na gari langu akisokota tumbako yake, nikasema, ‘Jim, safari hii unakwenda wapi? Kuwinda ndovu?’ Akajibu ‘La! Tunakwenda kutafuta kitu kinachotafutwa sana zaidi ya pembe za ndovu.’ Mimi nikazidi kumdadisi, nikamuuliza, ‘Je, kitu hicho chaweza kuwa nini? Ni dhahabu? Akacheka akajibu, ‘siyo Bwana, ni kitu kinachotakiwa zaidi ya dhahabu.’
Basi sikumuuliza neno tena, maana sikupenda kuonekana kuwa ni mdaku. Baada ya Jim kuisha kusokota tumbako yake, akasema ‘Bwana, sisi tunakwenda kutafuta almasi.’ Nikasema, ‘Almasi! Lakini mbona unafuata njia ambayo si njia ya kwendea huko; kwa nini hufuati njia inayoendelea kwenye mashimo?’ Akajibu, ‘ Bwana, umepata kusikia habari za mlima wa Sulemani?’ Nikamjibu, ‘Ndiyo.’ Akaniuliza, ‘Umesikia habari za almasi zilizoko huko?’ Nikwamwambia, ‘Ni upuuzi tu.’ Akanena, ‘Si upuuzi,? Wana maana, namjua mwanamke aliyetoka huko, naye alifika Natal pamoja na mtoto wake, akaniambia; lakiniamekufa sasa.’
Nikamjibu, ‘Wewe na bwana wako mkijaribu kufika nchi ya Sulemani, hamkosi mtaliwa na tai.’ Akacheka, akasema, ‘Labda, bwana . Mtu amezaliwa naye atakufa; nami ningependa kutembea katika nchi ngeni; maana ndovu wanakwisha katika nchi hii.’ Nikasema, ‘Haya, tutaona.’ Baada ya nusu saa nikaona gari la Neville likitoka. Na baadae kidogo Jim akarudi mbio akasema, ‘Kwaheri bwana, kwani sikupenda kuanza safari bila kuagana nawe. Ninaona labda umesema kweli ya kuwa hatutasafiri kwenda kusini tena.’ Nikamuuliza, ‘Je, Jim, wasema kweli? Bwana wako amesema kuwa anakwenda mlima wa Sulemani, au sivyo?’ Akasema, ‘Ni kweli bwana maana aliniambia kuwa imempasa ajaribu kuchuma mali kwa njia yoyote; basi ni afadhali ajaribu kutafuta hiyo almasi.’ Nikasema, ‘Vema Jim, lakini ngoja kwanza, nataka uchukue barua hii, lakini lazima uahidi kuwa hutampa mpaka nifike Inyati.’ Kufika Inyati ilikuwa ni mwendo wa maili kama mia. Basi akaahidi. Nami nikachukua karatasi nikaandika maneno haya: ‘Kwa huyo atakayekuja ..apande theluji ya ziwa la kushoto la Sheba mpaka afike penye titi, ambapo kwa upande huo wa kaskazini pana njia kuu iliyotengenezwa na Sulemani.’
Basi nikampa, kisha nikamwambia, ‘Sasa utakapompa bwana wako barua hii, mwambie afuate sana shauri lililomo. Wala usimpe sasa barua hii kwa sababu sipendi arudi kuja kuniuliza maswali mengi ambayo sitaweza kuyajibu. Haya nenda.’ Basi Jim akaitwaa barua akaenda zake. Na hayo ndiyo yote ninayoyajua juu ya ndugu yako, Bwana Henry; lakini nachelea sana ya kuwa.. ‘Bwana Henry akasema, ‘Tazama, Bwana Quatermain, mimi ninakwenda kumtafuta ndugu yangu; nitamtafuta hata mlima wa Sulemani, hata nitaupita ikiwa ni lazima, mpaka hapo nitakapomwona au mpaka hapo nitakapo hakikisha ya kuwa amekufa; je, utafuatana nami?’
Nimekwisha sema kuwa mimi ni mtu wa taratibu , kweli na pengine ni mwoga kidogo, na haya yalinitia hofu. Maana safari kama hiyo iliyokusudiwa nilibaini kuwa ni kufa tu. Na tena juu ya hivyo nina mtoto anaenitegemea mimi kwa hivi sipendi nife. Basi nilijibu, ‘Hapana bwana, ahsante sana lakini naona ni afadhali nisiende. Sasa mimi ni mzee siwezi kusafiri safari ya kubahatisha hivyo, na tena naona mwisho wetu utakuwa kama ule wa rafiki yetu Silvestre. Mtoto wangu ananitegemea mimi, basi kwa hivyo sina haki ya kujitia katika hatari.’
Basi hapo wote wawili, yaani Bwana Henry na Bwana Good wakahuzunika sana, na Bwana Henry alisema, ‘Bwana Quatermain, mimi ni tajiri sana, nami nimenuia kusafiri ili nimtafute ndugu yangu, na kadhalika waweza kutaja mshahara wowote uutakao nami nitakupa kabla ya kuanza safari. Tena nitausia kuwa tukipatikana na ajali, mtoto wako atazamwe. Mradi sasa naona kwa maneno hayo utaweza kutambua jinsi tunavyo kuhitaji wewe ufuatane pamoja nasi. Tena ikiwa kwa bahati tutavumbua mahali pale palipo na almasi, basi hizo zitakuwa shirika wewe na Bwana Good, mimi sizitaki. Vile vile ikiwa tutapata pembe za ndovu. Waweza kutoa shauri na kufanya mapatano yoyote yanayokupendeza, na tena gharama zote za safari ni juu yangu mwenyewe.’ Nikajibu, ‘Bwana Henry, maneno yako ni mema kweli kweli, lakini lazima niyafikiri kwanza, maana mimi sina mali nyingi, pili kwa sababu najua kuwa ni kazi kubwa sana, basi nipe nafasi nipate kuyafikiri zaidi. Nitakupa jibu kabla hatujafika Durban.’ Bwana Henry akasema, ‘Vema.’ Nikamwambia kwa heri, nikaenda kulala, na nilipolala nilimwota Yule marehemu Silvestre na almasi!
Itaendelea...
Kweli kabisa watunzi wa zamani walikua wanajua sana..!Kama ulikua msomaji wa simulizi za namna hii tangu utotoni, hakika utapata utamu wake. Kuna aina ya picha inakuja kichwani, inakufikilisha maisha ya Afrika ya zamani, maisha ya nyikani, enzi za wanyama wa kila namna katika mbuga na nyanda zilizo na miti, vichaka na mbuga zenye nyasi. Ni simulizi ambazo hata lugha yake haichoshi machoni na masikioni. Hakika nyakati hizo zimepita na hazitarudi tena.
Hahaah old is goldHadithi nzuri sana nilisoma nilipokuwa darasa la saba..
Ila hapa naisoma tena kwa umakini..
Niliipenda toka kipindi kile
Kweli chief teremsha mzigoHahaah old is gold
Dah, had mtu unajikuta unasisimkaBasi wale watu wakalia kwa sauti kuu wakatawanyika pote, na mifupa waliyofunga ikagongana walipokuwa wakienda ; wakaenda kila mahali katika kundi lile la watu.
Hatukuweza kuwatazama wote, basi tulimtazama Yule aliyekuwa karibu. Alipopita karibu na askari wale waliosimama, kisha akaanza kucheza na kuruka ruka, akizunguka zunguka kwa upesi sana, na akisema maneno kama haya:
‘'Nasikia harufu yake, mtenda maovu! Yu karibu, Yule aliyempa sumu mama yake! Nasikia mawazo maovu aliyemwazia mfalme!’'
Akazidi kucheza upesi upesi mpaka akawa kama mwenye wazimu na povu likamtoka kinywani na macho yakawa kama yanatoka kichwani, na mwili wake ulitetemeka. Mara akasimama akakaza mwili kama mbwa anayesikia harufu ya nyama porini, akanyosha fimbo yake na akaanza kuwaendea pole pole wale askari.
Na sisi tulimfuata kwa macho yetu kama tumepagawaa. Basi akafanya hivi mpaka alipofika mbele yao karibu, ndipo aliposimama akanyosha fimbo yake, akatambaa mbele kidogo tena. Mara mambo yalikwisha.
Kwa kilio kikuu aliruka akamgusa askari mmoja kwa fimbo yake. Mara Yule askari alishikwa na wenzake wawili akaletwa mbele ya mfalme. Hakufanya ukaidi, lakini tuliona kuwa walipokuwa wakimleta alikuwa kama amepooza, na vidole vilikuwa kama vidole vya maiti, na mkuki ulimponyoka.
Alipofika karibu, wauaji wawili wakatoka mbele, wakamtazama mfalme ili kupewa amri. Mfalme akasema, ‘Muueni!’
Na Gagula akalia, ‘Muue!’
Na yule Skraga akacheka akasema, ‘Muue!’
Basi kabla hawajamaliza kusema, mauaji yalikwisha tendeka. Mtu mmoja akamchoma mkuki wa moyo, na Yule mwingine akampiga rungu la kichwa. Mfalme Twala akahesabu, ‘Mmoja.’ Na maiti ilichukuliwa ikalazwa pale pale.
Mara tuliona mtu mwingine analetwa kama ng’ombe anayeletwa kuchinjwa. Mtu huyu alikuwa mwenye cheo, maana alikuwa kava ngozi ya chui. Tena tulisikia maneno yale yale ya kikatili na Yule mtu akaanguka amekufa. Mfalme akahesabu, ‘Wawili.’
Basi vivyo hivyo mchezo wao ukaendelea mpaka maiti mia moja walilazwa kwa safu. Mara moja tulisimama tukajaribu kumzuia mfalme, lakini alitukanya kwa ukali, akasema, ‘Acheni sheria iendelea, nyinyi watu weupe. Mbwa hawa ni wachawi na watenda maovu; kufa ni haki yao.
Ilipopata saa nne na nusu, mambo yakasita kidogo, na wale waliokuwa wakichagua wachawi wakajikusanya pamoja, tukafikiri kuwa wamechoka.
Lakini sivyo, maana tuliona ajabu Gagula alipojiinua akajikongoja kwa fimbo yake akaja katikati. Ikawa ajabu kumwona, Alikuwa karibu kupinda kabisa, lakini alipata nguvu akaanza kwenda mbio huku na huko kama walivyo fanya wanafunzi wake.
Haku na huko alikwenda mbio huku akiimba, mpaka akamrukia mtu mrefu aliyekuwa kasimama mbele ya kikosi kimoja, akamgusa. Alipofanya hivi, watu wakikosi chake wakaguna. Lakini wawili wao wakamshika wamlete mbele ya mfalme auawe.
Baadaye tulikuja kujua kuwa ni mwenye cheo kikubwa naye ni tajiri sana, tena ni mjukuu wa mfalme mwenyewe. Aliuawa, na mfalme akahesabu mia moja na tatu. Tena Gagula akaruka huku na huko, akaanza kutukaribia sisi.
Bwana Good akasema, ‘Lo! Nadhani anatujia sisi.’ Bwana Henry akasema, ‘Upuuzi! Hathubutu!’ na mimi nilipoona kuwa Yule afiriti anatukaribia, nilikata tamaa kabisa. Nikageuka nikatazama safu zile za maiti, nikatetemeka.
Gagula akakaribia, akakaribia zaidi na macho yake yakang’aa kwa uovu. Akaja karibu, karibu, na kila mtu hadharani alimkodolea macho.
Mwisho akasimama, akanyosha fimbo yake, na mara akamrukia Umbopa, yaani Ignosi, akamgusa begani, akasema, ‘Nasikia harufu yake.
Muue, muue, amejaa uovu; muue mgeni huyu kabla damu haijamwagika kwa ajili yake. Ee mfalme, muue!’
Hapo ikawa kimya kidogo, nami nikasimama nikasema, ‘Ewe mfalme, mtu huyu ni mtumishi wa wageni wako. Yeyote atakaye mwaga damu yake anamwaga damu yetu. Kwa ajili ya ukarimu wako, naomba asidhuriwe.’ Mfalme akasema, ‘Gagula, mama wa watambuzi wa wachawi, amemchagua; lazima afe.’
Nikajibu, ‘Hafi kabisa. Atakayejari kumgusu ndiye Atakayekufa.’
Twala akasema kwa sauti kubwa. ‘Haya, mkamateni’ Na wale wauaji waliopaka damu ya wale waliowaua, wakaja mbele, lakini walisita. Ignosi alishika mkuki wake, akawa tayari kupigania maisha yake.
Nikasema, ‘Rudini nyinyi! nyinyi, mbwa! Mkitaka kuona mwangaza wa jua kesho, rudini! Mkigusa hata unywele mmoja wa kichwa chake, basi mfalme wenu atakufa.’
Nikaelekeza bastola yangu kwa mfalme, Bwana Henry na Bwana Good vile vile wakatwaa bastola zao, na Bwana Henry akamwelekezea Yule muuaji wa mbele, na Bwana Good akamwelekezea Gagula Yule kizee.
Twala alipoona bastola imewekwa sawa na kifua chake akajikunja, nikasema, ‘Je, Twala, utafanya nini?’ Akasema, ‘Haya wekeni mianzi yenu ya ajabu, umeomba kwa ajili ya ukarimu na kwa ajili hiyo nitamwacha, wala si kwa kuhofu vitendo vyenu. Nendeni kwa amani.’
Nikajibu, ‘Vema, tumechoka kuona mauaji. Tunataka tukalale. Je, ngoma imekwisha?’
Twala akajibu, ‘Imekwisha,’ Akageuka akaonyesha maiti wale akasema, ‘Mizoga ya mbwa hawa itupiwe fisi na tai mwituni.’ Akainua mkuki wake.
Mara vikosi vikaanza kutoka kwa taratibu na kwa kimya kabisa, wachache tu walibaki ili kuchukua maiti. Tukaondoka tukamuuaga mfalme tukaenda nyumbani, naye hakutaka hata kututazama .
Tulipofika nyumbani tukawasha taa za Kikukuana, yaani, uzi kidogo uliowekwa kwenye mafuta ya kiboko, na Bwana Henry akasema, ‘Mimi naona kama nataka kutapika.’
Na Bwana Good akasema, ‘Kama nilikuwa na shaka katika shauri la kumsaidia Umbopa katika kumpiga vita Yule Twala, basi sasa limeondoka kabisa.
Nilijizuia kwa nguvu walipokuwa wakiwaua wale watu. Nilijaribu kufumba machoyangu, lakini ikawa kila mara nilipoyafumbua ukawa wakati usiofaa! Je, yupo wapi Umbopa.
Ehe rafiki yangu, nadhani yafaa kutushukuru sana, wewe ulikuwa karibu na kufa leo.’ Umbopa akajibu, ‘Ndiyo, kweli, nawashukuru sana.
Sitaweza kusahau mambo ya usiku huu. Infadus atakuja baadaye, lazima tumngojee.’ Basi tukatia tumbako katika viko vyetu, tukakaa tukivuta na kumngoja.
Daaah, hii kitu ni kali wakuu [emoji119] [emoji119]Akawageukia askari akasema, ‘Haya, mlete hapa; na wewe Skraga, unoe tayari mkuki wako.’ Basi watu wawili wakaja mbele na walipomkaribia Yule mwanamwali, ndipo kwanza alipofahamu ajali yake, akalia sana, akageuka apate kukimbia. Lakini wale askari wawili walimshika wakamleta analia na kujaribu kuwatoka.
Gagula akamuuliza, ‘Jina lako nani, wewe mwali? Je, hutaki kunijibu? Je, mwana wa mfalme afanye kazi yake sasa?
Kusikia hayo, Skraga alionekana kuwa mwovu kupita kiasi, akajongea hatua moja, akainua mkuki wake, na mara niliona mkono wa Bwana Good unashika bastola, na Nuru ya bastola ilimpata machoni Yule mwali, akanyamaza kimya.
Akaacha kushindana, akafumbata mikono yake akasimama anatetemeka toka kichwa hata miguu.
Skraga akacheka, akasema, ‘Tazama anajikunyata kuona mchezo wangu, hata kabla hajaiona.’ Akapapasa mkuki wake. Nikamsikia Bwana Good anasema kimoyomoyo, ‘Lo! Nikipata nafasi utajuta maneno yako, Mbwa we!’
Basi, sasa Gagula akamfanyia dhihaka , akasema, ‘Sasa umekwisha tulia, tuambie jina lako nani? Mpenzi wangu. Haya sema, usiogope.’
Yule mwali akatetemeka, akajibu, ‘’Ewe mama, jina langu naitwa Foulata, na ukoo wangu ni Suko. Ewe mama, kwa nini sina budi kufa? Mimi sikufanya makosa au ubaya wowote!’
Gagula akajibu, ‘Usifadhaike, lazima ufe uwe sadaka kwa Wale Wazee wakaao huko, lakini ni afadhali kulala usiku kuliko kufanya kazi mchana; ni afadhali kulala usiku kuliko kufanya kazi mchana; ni afadhali kufa kuliko kuishi, nawe utakufa kwa mkono wa mwana wa mfalme.’
Yule mwali Foulata akajiuma vidole vyake kwa huzuni akalia, ‘Ole wangu, huu ndio ukatili kweli! Mimi ni kijana! Nimefanya nini nisipate kuona jua likitoka katika giza la usiku huu, nisione tena nyota zikifuata majira ya jioni, nisipate kuchuma maua katika umande wala kusikiliza nyimbo za mteremko wa maji?
Ole wangu, sipati tena kuona nyumba ya baba yangu, wala kuona tena mapenzi ya mama yangu, wala kuchunga wana wa kondoo! Ole wangu, sitapata mwanaume wakunipenda na wala sitazaa wana! Ukatili! Ukatili!’
Tena akajiuma vidole kwa huzuni akageuka akatazama juu na machozi yalionekana yakimtoka machoni, akawa wa kusikitisha kabisa hata kuleta huruma kwa mtu yeyote, ila wale mashetani waliokuwa wamekaa mbele yetu hawakujali kabisa.
Na wala haikuvuta huruma kwa Gagula, wala bwana wa Gagula, ila niliona dalili ya huruma na huzuni katika sura za walinzi wale, na katika sura za wale wakubwa waliokuwapo; na Bwana Good alijizuia kwa shida tu, akafanya kama anakwenda kumsaidia.
Basi kwa akili ya kike, Yule mwali alitambua fikira zake, na mara akaruka akajitupa mbele yake akamshika miguu akalia, ‘Ewe baba mweupe uliyetoka katika nyota, nifunike kwa nguo yako ya ulinzi, nitambae katika kivuli cha nguvu zako nipate kuokoka.
Niokoe katika mikono ya watu waovu hawa wasio na huruma!’ Bwana Good akamshika mkono akasema, ‘Vema, mimi nitakulinda.’ Akainama akamshika mkono akasema, ‘Haya ondoka, mwanangu.’
Twala akageuka akamwashiria mwanawe, naye akajongea mbele ameshika mkuki juu.
Bwana Henry akasema akinong’oneza, ‘Sasa huu ndiyo wakati unaofaa; unangoja nini? Nikajibu kwa sauti ndogo, ‘Mimi nangoja kuona dalili ya mwezi kupatwa kwanza.
Nimeutazama kwa nusu saa hivi, lakini sioni dalili ya kupatwa.’
Akajibu, ‘Sasa lazima tubahatishe au huyu mwanamwali atauawa, maana naona Twala anaanza kuchoka.’
Basi nikatambua kuwa asemavyo ni kweli, nikatazama mwezi mara moja tena nisione hata dalili ya kupatwa, nikajikaza nikasimama mbele, nikajongea katikati ya Skraga na yule mwanamwali, nikasema, ‘Mfalme jambo hili halitakuwa; sisi hatutavumilia jambo hili; mwanamwali na aende zake salama.’
Twala akaghadhibika mno, akasimama katika kushangaa kwake, na askari wake waliokuwapo na wanawali nao walishangaa.
Na mfalme Twala akasema, ‘Halitakuwa! Wewe mbwa mweupe aliaye mbele ya simba katika pango lake; halitakuwa! Wewe una wazimu? Angalia sana usije ukapatwa na ajali ya kifaranga huyo, na wale waliopo pamoja nawe vile vile.
Je, wawezaje kumwokoa au kujiokoa mwenyewe? Nani wewe ujitiaye katikati ya mimi na matakwa yangu? Kaa upande, na wewe Skraga muue!
Haya, askari wangu, washike watu hawa.’ Basi hapo askari wengi wakatoka kwa nyuma ya jumba walikofichwa. Bwana Henry na Bwana Good na Umbopa wakasogea karibu nami, wakaelekeza bunduki zao.
Nikasema kwa sauti kuu lakini moyo wangu haukwepo kabisa, ‘Acheni! Twacheni sisi watu weupe tuliotoka katika nyota, tunasema kuwa halitakuwa.
Mkikaribia hata hatua moja tu, tutauzima mwezi, na sisi tukaao katika nyumba yake tunaweza kufanya hivi, tutaitia nchi yote katika giza tupu, nanyi mtaonja uchungu wa nguvu zetu.’
Basi maneno yangu yaliwastua; watu wakasimama, na Skraga akasimama kimya mbele yetu, ameshika mkuki wake juu.
Gagula akasema, ‘Msikieni! Msikieni! Msikieni asemavyo uwongo. Basi na afanye anavyosema na mwanamwali ataachiliwa. Afanye au auawe pamoja na mwanamwali na wale walio pamoja naye.’
Nikatazama mwezi tena, na sasa: nilifurahi, maana niliona kuwa alama nyeusi inaanza kuonekana katika mwezi.
Ndipo nilipoinua mkono wangu kwa taratibu sana nikaonyesha juu mbinguni, na Bwana Henry na Bwana Good wakafanya vile vile, tukaanza kusema maneno yoyote tuliyoweza kuyakumbuka.
Pole pole na kwa tara-tibu, kivuli kilianza kufunika mwezi, na kilipozidi kuja nikasikia watu wanaanza kuvuta pumzi juu, nikasema,
‘Tazama, Ewe Mfalme! Tazama, Gagula!
Tazameni nyinyi wakubwa, na watu wote, mwone kama watu weupe waliotoka katika nyota wametimiza maneno yao au kama ni uwongo mtupu! Mwezi unafunikwa mbele ya macho yenu; na sasa hivi itakuwa giza tupu.
Mmeomba ishara nasi tumeifanya. Ee mwezi, ufunikwe uwe giza tupu! Uzime mwangaza wako, Ee wewe mtakatifu; ulete ule moyo wa kiburi hata mavumbini, Ee mwezi, ule dunia kwa vivuli vyako.’
Basi watu wote waliguna kwa hofu. Wengine walisimama kama wamegeuka mawe, na wengine walijitupa chini wakapiga magoti wakalia kwa sauti kubwa.
Na mfalme mwenyewe alikaa kimya, uso umembadilika.
Gagula tu hakunyamaza, akasema, ‘Giza litapita, nimeyaona kama haya zamani; hapana mtu anayeweza kuzima mwangaza wa mwezi; msiogope; mkae kimya na giza litapita.’
Nikasema, ‘Ngojeni mtaona. Ee Mwezi!Mwezi! Mwezi!’ na sisi wote watatu tukazidi kusema maneno ya ovyo ovyo tu! na kwa muda wa dakika kumi tukaendelea hivyo hivyo.
Giza likazidi, na watu wote walikodoa macho yao kutazama juu, na walikaa kimya kabisa. Sasa dunia ikaanza kujaa vivuli vya ajabu, na kila kitu kilikuwa kimya kama mauti.
Wakati ulipita na pamoja giza likazidi kushika mwezi. Ikawa ajabu mno, maana kwanza ikawa kama mwezi unakaribia dunia na kuzidi kuwa mkubwa.
Sasa uligeuka rangi ukawa mwekundu kama damu, na halafu tuliona alama zile zilizo katika mwezi zinang’aa katika wekundu wake.
Pole pole giza likatambaa; sasa limefika nusu ya ule wekundu kama damu. Likazidi kuenea hata hatukuweza kuona sura za watu waliokuwa karibu. Sasa kila mtu alikuwa kimya kabisa, nasi hatukusema neno.
Mara Yule kijana Skraga alilia kwa hofu, ‘Mwezi unakufa. Wachawi weupe hawa wameuwa mwezi. Tutaangamia katika giza.’ Naye alishikwa na wazimu kwa hofu akainua mkuki wake akampiga Bwana Henry kwa nguvu zake zote.
Lakini alikuwa amesahau habari za nguo zile za chuma alizotupa mfalme, na mkuki ukapinduka bila kuzipenya.
Kabla hajapata nafasi kupiga tena, Bwana Henry akashika ule mkuki akampiga kifuani. Skraga akaanguka maiti! Basi watu walipoona hivyo, na kwa sababu ya hofu waliyokuwa nayo kufikiri kuwa mwezi unakufa, wakaanza kutawanyika, wakapiga mbio na kulia.
Na hata mfalme na walinzi wake na Gagula wakaondoka mbio wakakimbilia majumbani, na baada ya dakika chache tukajiona tupo peke yetu pamoja na Foulata, Yule mwanamwali tuliyemwokoa, na Infadus, na wakubwa wengine waliotujia usiku, na maiti ya Skraga mwana wa mfalme.
Nikasema, ‘Wakubwa, tumewaonyesha ishara mliyotaka. Kama mmeridhika, basi twendeni upesi mahali mlipotaja. Hatuwezi sasa kukomesha kitendo chetu.
Giza litaendelea kwa muda wa saa moja na nusu. Haya, na tujifiche kwa giza hili.’
Infadus akasema, ‘Twendeni.’ Akageuka akaenda, na wakubwa wale walimfuata, na sisi na yule mwanamwali tulifuatana nao.
Kabla hatujalifia lango la mji, mwezi uliliwa kabisa na nyota nyingi zikaonekana katika mbingu nyeusi. Tukashikana mikono tukajikokota katika giza.
Kweli kabisa nadhani matajiri wengi wakibongo wametokea hukoKadri nisomavyo simulizi za namna hii ama kuangalia filamu za kufanana na simulizi hizi, nawiwa kusema pengine hakuna kipindi ambacho wanyama waliwindwa kama karne ya 19 na 20. Maana sidhani kama hata sheria za kikoloni ziliweka mipaka katika uwindaji.
Hakika, hususani huu utajiri wa jamii ya wa Asia, mara nyingi sana utawakuta kwenye miji ya zamani katika bara la Afrika.Kweli kabisa nadhani matajiri wengi wakibongo wametokea huko
Asante sana chief tupo pamojaBasi tulianza kufanya imara mahali petu jinsi tulivyoweza. Kila mtu alifanya kazi nyingi sana.
Vinjia vyote vya kupandia kilima tuliviziba kwa chungu za mawe, tukakusanya chungu za mawe makubwa sana tayari kuyaangushia adui wakijaribu kupanda kilima.
Jua lilipokaribia kushuka tulipumzika kidogo tukaona kundi dogo la watu wanatujia kutoka mji wa Loo na mmoja alikuwa amechukua jani mkononi ili iwe dalili ya kutufahamisha kuwa yeye ni tarishi aliyetumwa.
Alipokaribia Ignosi na Infadus na wakubwa wawili watatu walishuka kumlaki. Tarishi huyo alikuwa mtu mkubwa shujaa, amevaa ngozi ya chui. Alipofika karibu alisema, ‘Salamu za mfalme kwa wale wanaompiga vita. Salamu za simba kwa wale fisi wanaovitafuna visigino vyake.’
Nikasema, ‘Haya sema utakayo.’ Akaendelea, ‘Haya ni maneno ya mfalme; mjitoe katika mikono ya mfalme kabla hamjapatwa na maafa. Bega la fahali mweusi limekwisha pasuliwa, na mfalme anamtembeza kambini huku linatoka damu.’ (Desturi hii inafuatwa katika makabila mengine ya Afrika ikiwa ni mwanzo wa vita au mwanzo wa jambo kubwa jingine).
Nikamuuliza, ‘Je, na mapatano ya mfalme yatakuwaje.?’ Akajibu, ‘Mapatano ya mfalme ni ya huruma na rehema, yaliyo stahili mfalme Twala.
Haya ndiyo maneno ya Twala, Mwenye chongo, Mume wa wake elfu, Bwana wa Wakukuana, Mlinzi wa Njia Kuu, Mpenzi wa Wale Watatu wakaao kimya juu ya milima ile, Ndama wa Ng’ombe Mweusi, Ndovu ambaye akikanyaga nchi ardhi hutetemeka.
Kitisho cha watenda maovu, Mbuni ambaye miguu yake hula jangwa, Mkubwa, Mweusi, Mwenye busara, Mfalme kutoka karne hata karne!
Haya ndiyo maneno ya mfalme Twala: Nitakuonyesheni rehema, nitaridhika kwa damu kidogo tu.
Mmoja katika kila kumi atakufa, wengine watapata msamaha; lakini Yule mtu mweupe aliyemuua Skraga, Yule mtu mweusi mtumishi wake anayejidai mfalme, na Infadus ndugu yangu anayefitinisha watu wangu, hawa watakufa kwa maumivu na mateso, wawe sadaka ya Wale Watatu wakaao kimya. Haya ndiyo maneno ya huruma ya Twala.’
Basi nikazungumza kidogo na wenzangu, kisha nikasema, kwa sauti kubwa ili wale askari wote wasikie, nikasema. ‘Rudi kwa Twala, wewe mbwa, rudi kwa aliyekuleta, ukamwambie kuwa:
Sisi,na Ignosi mfalme wa kweli wa Wakukuana, na sisi watu weupe wenye hekima tuliotoka katika nyota, tutiao mwezi giza, na Infadus wa ukoo wa ufalme, na Wakubwa na askari na watu waliokusanyika hapa tunampa jawabu na kusema: hatutajitoa kabisa katika mikono ya Twala; na kabla jua halijashuka mara mbili, Twala atalala maiti mkavu mbele ya mlango wake wa ikulu, na Ignosi, ambaye baba yake aliuawa na Twala, atatawala katika mahali pake! Sasa nenda, tusije tukakufukuza kwa mijeledi, nawe uangalie sana usiinue mkono wako kupigana na watu kama sisi.’
Yule tarishi akacheka akasema, ‘Huwezi kunitisha kwa maneno makubwa yanayovuma sana. Mjionyeshe kuwa mashujaa kesho, nyinyi mnaotia giza mwezi. Muwe mashujaa, mpigane kwa furaha kabla kunguru hajachambueni nyama mbali na mifupa yenu, mpaka ikawa meupe kuliko sura zenu zilivyo.
Kwaherini; labda tutaonana tena vitani, nawaombeni msiruke kwenda juu katika nyota tena bila ya kuningojea mimi.’
Basi alipokwisha kusema maneno hayo ya kutudharau, akatoka akaenda zake, na punde jua lilishuka. Usiku ule tulikuwa na kazi nyingi, maana ingawa tulichoka mno ikawa lazima kutengeneza vitu vyote tayari kadiri tulivyoweza tusiache jambo hata moja, na matarishi walikuwa wakija na kutoka mahali petu pa mashauri.
Basi yapata saa tano usiku, mambo yote tuliyoweza kuyatengeneza yalikwisha kuwa tayari, na kambi ikawa kimya kabisa ila kwa sauti za watu ‘Yaliokuwa wakishika zamu.
Mimi na Bwana Henry tukashuka kilimani pamoja na Ignosi na mkubwa mmoja tukazunguka kila mahali pa mbele penye mlinzi, tukaona kuwa wote wapo macho. Kisha tukarudi tena tukipita katikati ya askari maelfu waliolala usingizi ambao wengi wanalala usingizi wa mwisho duniani.
Nikamwambia Bwana Henry, ‘Mimi nimo katika hali ya woga kabisa. Mimi nafikiri kuwa hapana mmoja katika sisi atakayekuwa mzima usiku wa kesho. Tunashambuliwa na askari wengi kabisa kupita askari wetu.’
Bwana Henry akasema, ‘Tutafanya jitihada. Tutaonyesha ushujaa wetu lakini mambo haya ni makubwa mno, na kweli si haki yetu kuingia katika shughuli hii, lakini tumekubali na kwa hivyo lazima tufanye tuwezavyo.
Mwenyewe nimechagua kufa katika vita kuliko kufa kwa namna nyingine, na sasa nimeona kuwa hatuwezi kumwona ndugu yangu tena, basi kufa kwangu si kugumu.
Lakini kila mara hutokea kuwa mashujaa wana bahati, na labda tutawashinda. Liwalo naliwe lakini vita vitakuwa vikali nasi lazima tuwe katikati kabisa ya vita.’
Alisema maneno haya kwa sauti ya huzuni kabisa, lakini niliona macho yake yaking’aa sana nikatambua kuwa Bwana Henry kwa kweli alipenda vita.
Baada ya haya tulilala usingizi muda wa saa mbili. Ilipokuwa karibu na mapambazuko tuliamshwa na Infadus aliyekuja kutuarifu kuwa kwa upande wa mji wa Loo kuna shughuli nyingi, naya kuwa askari wengine wa Twala wanawafukuza askari wetu waliowekwa mahali pa mbele kulinda.
Tukaondoka tukavaa tayari kwa vita, tukavaa zile nguo za chuma ndani ya nguo zetu za kila siku, tukashukuru sana kuwa nazo.
Tulipokwisha kuvaa tulikula kwa haraka tukatoka kutazama mambo yanavyoendelea. Mahali pamoja juu kilimani palikuwa mwamba mkubwa, tukafanya kuwa ngome yetu na mahali pa kutazamia chini pote.
Hapa tuliona Infadus amezungukwa na kikosi chake kilichoitwa Wajivu, na bila shaka askari hao walikuwa bora kupita wote katika jeshi la Wakukuana.
Kikosi hicho kilikuwa na askari elfu tatu na mia tano, nacho kiliwekwa hapa kuwa kama akiba, na askari walikuwa wamelala chini wakitazama askari wa Twala wakitoka mji wa Loo, wakitambaa kama siafu.
Ilikuwa kama kwamba mistari hiyo ya askari wa Twala haina mwisho, nayo ilikuwa mistari mitatu na kila mstari ulikuwa na askari kadiri ya elfu mbili.
Walipokwisha toka mjini walijipanga. Jeshi moja likachagua njia ya kulia, na jingine njia ya kushoto, na jingine njia ya katikati.
Basi Infadus akasema, ‘Ah! Watatushambulia kutokea pande tatu kwa mara moja.’
Hii ilikuwa habari mbaya, maana mahali petu pa juu ya kilima palikuwa kama duara na urefu wa duara ile ulikuwa hadiri ya mwendo wa saa nne, na kwa kuwa eneo lake lilikuwa refu na askari wetu ni wachache, ikawa lazima tusongane kadiri tulivyoweza.
Lakini kwa kuwa hatukuweza kutambua hasa namna watakavyo tushambulia ikawa lazima tufanye tuwezavyo, tukapeleka habari kwa vikosi vyote kila mtu awe tayari kujitetea katika mashambulio.