Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Kama ulikua msomaji wa simulizi za namna hii tangu utotoni, hakika utapata utamu wake. Kuna aina ya picha inakuja kichwani, inakufikilisha maisha ya Afrika ya zamani, maisha ya nyikani, enzi za wanyama wa kila namna katika mbuga na nyanda zilizo na miti, vichaka na mbuga zenye nyasi. Ni simulizi ambazo hata lugha yake haichoshi machoni na masikioni. Hakika nyakati hizo zimepita na hazitarudi tena.
 
Kweli kabisa watunzi wa zamani walikua wanajua sana..!
 
Dah, had mtu unajikuta unasisimka
 
Kadri nisomavyo simulizi za namna hii ama kuangalia filamu za kufanana na simulizi hizi, nawiwa kusema pengine hakuna kipindi ambacho wanyama waliwindwa kama karne ya 19 na 20. Maana sidhani kama hata sheria za kikoloni ziliweka mipaka katika uwindaji.
 
Daaah, hii kitu ni kali wakuu [emoji119] [emoji119]
 
Kweli kabisa nadhani matajiri wengi wakibongo wametokea huko
 
Maji ! Maji ! Maji ..... kwenye maisha unaweza kufurahishwa na jambo dogo kulingana na ugumu unaopitia. Hakika ni funzo
 
SURA YA KUMI NA MBILI


Ilikuwa bahati yetu kuwa Infadus na wakubwa wale walivijua vema vinjia katika mji, na kwa hivyo ingawa ilikuwa giza tuliweza kwenda upesi.

Kwa muda wa saa moja hivi tulikwenda, mpaka mwezi ulianza kutoa mwangaza wake tena.

Tukautazama na mara tuliona mshale wa nuru unatoka na kuangaza, na baada ya dakika tano nyota zikaanza kutoweka tena na mwangaza ulitosha kutuwezesha kuona mahali tulipo.

Tukajiona kuwa tumekwisha toka mjini na sasa tunakaribia kilima ambacho juu yake ni sawa sawa kama meza. Kilikwenda juu yapata futi mia mbili hivi, na juu yake palikuwa na nafasi kwa kambi la skari wengi sana.

Tukaambiwa kuwa kwa kawaida vikosi vitatu vinafanya kambi hapa, lakini nafasi iliyopo inatosha kwa vikosi vingine pia. Tukakipanda kilima, tukaona kuwa vikosi vingine vipo tayari.

Tukaona watu wamesongana, wameamshwa katika usingizi na sasa wanatetemeka kwa hofu. Tukapita katikati bila kusema neno, tukafika kwenye nyumba moja, na hapa tulistaajabu, maana watu wawili walikuwa wakitungojea wamekisha leta vitu tulivyoviacha tulipotoka mjini.


Infadus akasema, ‘Mimi nilipeleka watu wavichukue, na hata hivi vile vile.’ Akamwonyesha Bwana Good suruali yake.

Bwana Good akacheka sana na katika furaha yake akashika suruali yake akaivaa pale pale.

Infadus alijaribu kumshauri asiivae na kuficha miguu yake, lakini Bwana Good hakukubali.

Basi Infadus alitwambia kuwa ameamuru vikosi vikusanyike jua likitoka tu ili awaeleza askari sababu ya kumwasi mfalme na kuwaonyesha mfalme wao wa haki, Ignosi.

Basi jua lilipochomoza wakakusanyika watu wapatao ishirini elfu walio bora katika askari wa Kukuana, wakajipanga katika kiwanja kikubwa; tukaenda kuwatazama.

Sasa Infadus akawaita wakubwa na baada ya kukaa kimya kidogo akaanza kueleza habari zote, naye alikuwa msemaji hodari. Alieleza habari za baba yake Ignosi na namna alivyouawa bila haki na Twala aliye mfalme wa sasa, na namna mke wake na mtoto wake walivyofukuzwa, wafe kwa njaa.


Kisha akaeleza kuwa watu weupe waliotoka katika nyota waliitazama nchi hii kutoka kwao juu wakaona dhuluma na taabu zilizopo, basi wakaja kwa taabu nyingi wapate kuwasaidia watu wa nchi; na ya kuwa walimshika Ignosi mfalme wa haki wa Wakukuana wakamwongoza kutoka nchi ngeni alipokuwako na kumleta kuvuka milima.


Tena akaeleza kuwa walikuwa wamekwisha ona vitendo viovu vya Twala na kwa hivyo waliwaonyesha ishara wale wasiosadiki, wakamwokoa Yule mwanamwali, wakazima mwangaza wa mwezi na kumuua Skraga; na sasa wapo tayari kutusaidia katika vita vya kumwondoa Twala na kumweka Ignosi, aliye mfalme wa haki, katika mahali pake.


Infadus alipomaliza kusema maneno yake, Ignosi, akasimama mbele, na baada ya kusema tena yote aliyosema Infadus mjomba wake, akasema, ‘Ee wakubwa, askari, na watu wote, mmesikia maneno yangu.


Sasa lazima mchague baina ya mimi na yeye anayekaa sasa katika kiti cha enzi, Yule mjomba wangu aliyemuua ndugu yake akamfukuza mtoto wa ndugu yake ili afe katika baridi ya usiku.

Ni kweli kuwa mimi ni mfalme wa kweli, na hawa wakubwa wanaweza kuwaambieni kuwa wamekwisha ona nyoka aliyechanjwa kiunoni mwangu.
 
Kama mimi si mfalme, je, watu weupe hawa wangetetea upande wangu kwa nguvu za uwezo wao?

Msitetemeke, wakubwa na askari na watu wote! Lile giza mliloona usiku ambalo, lililetwa kusudi kumfadhaisha Twala, mmekwisha kulisahau?

Si liko mbele ya macho yenu hata sasa? Mimi ni mfalme.’ Akasimama akajinyosha akainua shoka lake la vita juu kichwani, akasema, ‘Kama yupo mtu mmoja asiyekubali,
Basi atoke mbele nami nitapigana naye sasa na damu yake itakuwa dalili ya kuwa nisemayo ni kweli.’

Akatikisa shoka likang’aa katika mwangaza wa jua. Lakini hapana mtu aliyetoka mbele, akaendelea tena akasema, ‘Mimi ni mfalme wa kweli, na wote watakaosimama upande wangu watafuatana nami kwa heshima na fahari kama tukishinda.

Nitawapa ng’ombe na wanawake, nanyi mtakuwa wa kwanza katika vikosi vyote; na ikiwa tutashindwa, basi na mimi nitashindwa pamoja nanyi.

Na tazameni, nitatoa ahadi ya kuwa nikiisha kukaa juu ya kiti cha enzi cha babu zangu, kumwaga damu ya bure kutakoma.

Watambuzi wa wachawi hawatatafuta tena watu na kuwaua. Hapana mtu atakayeuawa ila atakayekosa sheri zetu.

Miji na nyumba zenu hazitaingiliwa tena, na kila mtu atalala salama katika nyumba yake bila hofu, na haki itazagaa katika nchi yetu yote.

Je, mmekwisha kuchagua nyinyi wakubwa na askari na watu wote?
Wakaitikia, ‘Tumechagua, Ee mfalme.’

Akajibu, ‘Vema. Geukeni mtazame matarishi wa Twala wanavyotawanyika kwenda mashariki na magharibi na kaskazini na kusini ili kukusanya jeshi kubwa wapate kuniua mimi na nyinyi na hawa rafiki zangu na walinzi wangu.

Kesho au labda kesho kutwa atakuja pamoja na watu wake wote kupigana nasi. Ndipo nitakapoona kweli walio watu wangu, watu wale wasio na hofu kufa kwa ajili ya yale wanayoamini; nami nakwambieni ya kuwa hamtasahauliwa katika wakati wa ngawira.

Wakubwa na askari na watu wote sasa nendeni nyumbani mkajitayarishe kwa vita.’
Basi ikawa kimya mpaka mmoja wa wakubwa wale akainua mikono yake akaita neno lile la kumwamkia mfalme, ‘Koom,’ ikawa ishara ya kuwa askari wamemkubali Ignosi kuwa mfalme wao. Wakatoka kwa taratibu za kiaskari, wakaenda zao.

Baada ya nusu saa tukafanya mkutano wa vita na wakubwa wote wakahudhuria. Ikawa dhairi kuwa kabla ya kupita muda mwingi tutashambuliwa na askari wengi kupita hesabu tuliyo nayo. Maana tuliona majeshi ya askari wanakuja kutoka kila mahali, na matarishi wa mfalme wanakwenda pote.

Kwa upande wetu tulikuwa na askari kadiri ya ishirini elfu wa katika vikosi saba vilivyo hodari katika nchi.

Infadus aliniambia kuwa Twala atakuwa na askari kadiri ya thelathini au thelathini na tano elfu, akasema kuwa watakuwepo Loo tayari, na kabla ya kufika saa sita kesho ataweza kuhudhurisha elfu tano zaidi.

Ilikuwa dhahiri kuwa lazima tujiweke tayari tuwezavyo kufanya vita, maana wao walikuwa wakijiweka tayari, na hata sasa makundi ya askari walikuwa wakizunguka kilima kwa chini, na dalili nyinginezo za vita zilionekana.
 
Basi tulianza kufanya imara mahali petu jinsi tulivyoweza. Kila mtu alifanya kazi nyingi sana.

Vinjia vyote vya kupandia kilima tuliviziba kwa chungu za mawe, tukakusanya chungu za mawe makubwa sana tayari kuyaangushia adui wakijaribu kupanda kilima.

Jua lilipokaribia kushuka tulipumzika kidogo tukaona kundi dogo la watu wanatujia kutoka mji wa Loo na mmoja alikuwa amechukua jani mkononi ili iwe dalili ya kutufahamisha kuwa yeye ni tarishi aliyetumwa.

Alipokaribia Ignosi na Infadus na wakubwa wawili watatu walishuka kumlaki. Tarishi huyo alikuwa mtu mkubwa shujaa, amevaa ngozi ya chui. Alipofika karibu alisema, ‘Salamu za mfalme kwa wale wanaompiga vita. Salamu za simba kwa wale fisi wanaovitafuna visigino vyake.’

Nikasema, ‘Haya sema utakayo.’ Akaendelea, ‘Haya ni maneno ya mfalme; mjitoe katika mikono ya mfalme kabla hamjapatwa na maafa. Bega la fahali mweusi limekwisha pasuliwa, na mfalme anamtembeza kambini huku linatoka damu.’ (Desturi hii inafuatwa katika makabila mengine ya Afrika ikiwa ni mwanzo wa vita au mwanzo wa jambo kubwa jingine).

Nikamuuliza, ‘Je, na mapatano ya mfalme yatakuwaje.?’ Akajibu, ‘Mapatano ya mfalme ni ya huruma na rehema, yaliyo stahili mfalme Twala.

Haya ndiyo maneno ya Twala, Mwenye chongo, Mume wa wake elfu, Bwana wa Wakukuana, Mlinzi wa Njia Kuu, Mpenzi wa Wale Watatu wakaao kimya juu ya milima ile, Ndama wa Ng’ombe Mweusi, Ndovu ambaye akikanyaga nchi ardhi hutetemeka.


Kitisho cha watenda maovu, Mbuni ambaye miguu yake hula jangwa, Mkubwa, Mweusi, Mwenye busara, Mfalme kutoka karne hata karne!

Haya ndiyo maneno ya mfalme Twala: Nitakuonyesheni rehema, nitaridhika kwa damu kidogo tu.

Mmoja katika kila kumi atakufa, wengine watapata msamaha; lakini Yule mtu mweupe aliyemuua Skraga, Yule mtu mweusi mtumishi wake anayejidai mfalme, na Infadus ndugu yangu anayefitinisha watu wangu, hawa watakufa kwa maumivu na mateso, wawe sadaka ya Wale Watatu wakaao kimya. Haya ndiyo maneno ya huruma ya Twala.’

Basi nikazungumza kidogo na wenzangu, kisha nikasema, kwa sauti kubwa ili wale askari wote wasikie, nikasema. ‘Rudi kwa Twala, wewe mbwa, rudi kwa aliyekuleta, ukamwambie kuwa:

Sisi,na Ignosi mfalme wa kweli wa Wakukuana, na sisi watu weupe wenye hekima tuliotoka katika nyota, tutiao mwezi giza, na Infadus wa ukoo wa ufalme, na Wakubwa na askari na watu waliokusanyika hapa tunampa jawabu na kusema: hatutajitoa kabisa katika mikono ya Twala; na kabla jua halijashuka mara mbili, Twala atalala maiti mkavu mbele ya mlango wake wa ikulu, na Ignosi, ambaye baba yake aliuawa na Twala, atatawala katika mahali pake! Sasa nenda, tusije tukakufukuza kwa mijeledi, nawe uangalie sana usiinue mkono wako kupigana na watu kama sisi.’


Yule tarishi akacheka akasema, ‘Huwezi kunitisha kwa maneno makubwa yanayovuma sana. Mjionyeshe kuwa mashujaa kesho, nyinyi mnaotia giza mwezi. Muwe mashujaa, mpigane kwa furaha kabla kunguru hajachambueni nyama mbali na mifupa yenu, mpaka ikawa meupe kuliko sura zenu zilivyo.


Kwaherini; labda tutaonana tena vitani, nawaombeni msiruke kwenda juu katika nyota tena bila ya kuningojea mimi.’

Basi alipokwisha kusema maneno hayo ya kutudharau, akatoka akaenda zake, na punde jua lilishuka. Usiku ule tulikuwa na kazi nyingi, maana ingawa tulichoka mno ikawa lazima kutengeneza vitu vyote tayari kadiri tulivyoweza tusiache jambo hata moja, na matarishi walikuwa wakija na kutoka mahali petu pa mashauri.


Basi yapata saa tano usiku, mambo yote tuliyoweza kuyatengeneza yalikwisha kuwa tayari, na kambi ikawa kimya kabisa ila kwa sauti za watu ‘Yaliokuwa wakishika zamu.


Mimi na Bwana Henry tukashuka kilimani pamoja na Ignosi na mkubwa mmoja tukazunguka kila mahali pa mbele penye mlinzi, tukaona kuwa wote wapo macho. Kisha tukarudi tena tukipita katikati ya askari maelfu waliolala usingizi ambao wengi wanalala usingizi wa mwisho duniani.

Nikamwambia Bwana Henry, ‘Mimi nimo katika hali ya woga kabisa. Mimi nafikiri kuwa hapana mmoja katika sisi atakayekuwa mzima usiku wa kesho. Tunashambuliwa na askari wengi kabisa kupita askari wetu.’

Bwana Henry akasema, ‘Tutafanya jitihada. Tutaonyesha ushujaa wetu lakini mambo haya ni makubwa mno, na kweli si haki yetu kuingia katika shughuli hii, lakini tumekubali na kwa hivyo lazima tufanye tuwezavyo.

Mwenyewe nimechagua kufa katika vita kuliko kufa kwa namna nyingine, na sasa nimeona kuwa hatuwezi kumwona ndugu yangu tena, basi kufa kwangu si kugumu.

Lakini kila mara hutokea kuwa mashujaa wana bahati, na labda tutawashinda. Liwalo naliwe lakini vita vitakuwa vikali nasi lazima tuwe katikati kabisa ya vita.’

Alisema maneno haya kwa sauti ya huzuni kabisa, lakini niliona macho yake yaking’aa sana nikatambua kuwa Bwana Henry kwa kweli alipenda vita.

Baada ya haya tulilala usingizi muda wa saa mbili. Ilipokuwa karibu na mapambazuko tuliamshwa na Infadus aliyekuja kutuarifu kuwa kwa upande wa mji wa Loo kuna shughuli nyingi, naya kuwa askari wengine wa Twala wanawafukuza askari wetu waliowekwa mahali pa mbele kulinda.

Tukaondoka tukavaa tayari kwa vita, tukavaa zile nguo za chuma ndani ya nguo zetu za kila siku, tukashukuru sana kuwa nazo.

Tulipokwisha kuvaa tulikula kwa haraka tukatoka kutazama mambo yanavyoendelea. Mahali pamoja juu kilimani palikuwa mwamba mkubwa, tukafanya kuwa ngome yetu na mahali pa kutazamia chini pote.

Hapa tuliona Infadus amezungukwa na kikosi chake kilichoitwa Wajivu, na bila shaka askari hao walikuwa bora kupita wote katika jeshi la Wakukuana.

Kikosi hicho kilikuwa na askari elfu tatu na mia tano, nacho kiliwekwa hapa kuwa kama akiba, na askari walikuwa wamelala chini wakitazama askari wa Twala wakitoka mji wa Loo, wakitambaa kama siafu.

Ilikuwa kama kwamba mistari hiyo ya askari wa Twala haina mwisho, nayo ilikuwa mistari mitatu na kila mstari ulikuwa na askari kadiri ya elfu mbili.


Walipokwisha toka mjini walijipanga. Jeshi moja likachagua njia ya kulia, na jingine njia ya kushoto, na jingine njia ya katikati.

Basi Infadus akasema, ‘Ah! Watatushambulia kutokea pande tatu kwa mara moja.’
Hii ilikuwa habari mbaya, maana mahali petu pa juu ya kilima palikuwa kama duara na urefu wa duara ile ulikuwa hadiri ya mwendo wa saa nne, na kwa kuwa eneo lake lilikuwa refu na askari wetu ni wachache, ikawa lazima tusongane kadiri tulivyoweza.


Lakini kwa kuwa hatukuweza kutambua hasa namna watakavyo tushambulia ikawa lazima tufanye tuwezavyo, tukapeleka habari kwa vikosi vyote kila mtu awe tayari kujitetea katika mashambulio.
 
Asante sana chief tupo pamoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…