Kichaa Msafi
JF-Expert Member
- Dec 26, 2017
- 1,087
- 2,134
Riwaya za Zamani, Hadithi ya Allan Quatermain - JamiiForumsMkuu ni ipi unayo isemea?
Asante mkuuMkuu hongeraa sana
Wacha nianze kuirarua taratibuMAAJABU YALIYOWAPATA ALLAN QUATERMAIN NA WENZAKE
HADITHI YA UMSLOPAGAAS
SURA YA KWANZA
SIKU saba zilikuwa, zimepita tangu mwana wangu mpenzi alipozikwa na jioni ilipofika, nilikuwa Nikitembea huko na huko chumbani mwangu nikifikiri, mara mlango unabishwa, Nikaenda nikaufungua mlango mwenyewe, Kumbe rafiki zangu wa zamani Sir Henry Curts na Bwana John Good wapo nje.
Niliwakaribisha ndani wakaingiaa chumbani. Wakakaa mbele ya moto uliokuwa ukiwaka humo.
‘’Mmefanya vyema kuja kunitazama.’’
Hawakujibu neno, ila Sir Henry alishindilia tumbako katika kiko chake akakiwasha kwa kaa alilolitoa motoni, Alipokuwa akiinama mbele kufanya hivyo moto, uliwaka zaidi ukaangaza chumbani, nikafikiri jinsi alivyo mtu mzuri mno.
Uso wake mtulivu wenye nguvu, sura yake thabiti, macho yake makubwa ya kijivu ndevu na nywele zake rangi ya manjano.
Sura yake yote ilikuwa ya mtu aliye bora, tena umbo lake halikuwa kinyume cha uso wake, Sijapata kuona mabega mapana, zaidi wala kifua kinene kama chake.
Umbo la Sir Henry ni pana, ingawa ni mrefu wa futi sita na inchi mbili lakini haonekani kuwa mrefu nilipokuwa nikimtazama hivi, sikuweza kujizuia nisifiri namna mimi nilivyo mwembamba mfupi na namna nilivyohitilafiana na uso wake mzuri, na umbo lake bora.
Embu wazeni basi juu ya mtu mfupi aliyesinyaa, mwenye uso wa rangi ya manjano na umri wa miaka sitini na mitatu mwenye mikono membamba, macho makubwa ya kahawia, kichwa kimefunikwa na nywele zinazoingia mvi na kusimama wima kama brashi iliyotumika, kiasi uzani wake pamoja na mavazi aliyovaa ratili mia moja thelathini na mbili tu.
Basi hapo ndipo mtakapofahamu namna alivyo Allan Quatermain, ambaye kwa desturi huitwa Mwindaji Quatermain, na Waafrika humwita ‘’Makumazahn,’’ maana yake akeshaye usiku, yaani mtu mwerevu asiyedanganyika.
Tena, yupo Bwana Good ambaye hafanani na Sir Henry wala na mimi maana ni mfupi, mweusi kidogo, mnene mnene sana ana macho meusi yang’aayo na katika jicho moja siku zote huvaa rodi, yaani miwani ya jicho moja.
Nilisema yeye ni mnene, lakini neno hilo halitoshi kueleza namna alivyo mnene. Sir Henry humwambia ya kuwa amenenepa hivi kwa sababu yu mvivu, tena anakula sana, ingawa Bwana Good hapendezwi kwa maneno yake , lakini hawezi kuyakana.
Tulikaa kwa muda mfupi, kisha niilichuka kiberiti ili niiwashe taa, kwa sababu niiona giza linachosha, maana ndivyo inavyoelekea hasa ikiwa muda wa siku saba tu umepita tangu mtu alipozika tumaini la maisha yake.
Huku nyuma Sir Henry na Bwana Good walikuwa wamekaa kimya, wakiona nadhani, ya kuwa hawana la kusema linaloweza kunifariji, wakaridhika kunifariji kwa kuwapo kwao ni rambirambi zao za kimya.
Ni kweli ya kuwa twapata tumaini na faraja katika saa za majonzi kwa kuwapo wengine, wala si kwa maongezi yao ambayo huelekea kutuudhi tu. Wakakaa wakivuta tumbako, na mimi nilisimama mbele ya moto nikivuta tumbako pia na kuwaangalia.
Halafu kidogo nilisema, ‘’Je rafiki zangu wa zamani, tangu tuliporudi toka nchi ya Ukukuana hata leo, miaka mingapi imepita? ‘’Bwana Good akasema, ‘’Miaka mitatu. Kwa nini unauliza?’’.
Nikajibu, ‘’Nauliza kwa sababu nafikiri ya kuwa muda niiokaa pamoja na watu mijini umenitosha kabisa, Nitarudi mwituni tena.’’
Hapa Sir Henry alikipeleka nyuma kichwa chake, akacheka mcheko wake wa kindani, akasema, ‘’Ama ni ajabu sana, sivyo Good?’’
Bwana Good akaniangalia, na huku anacheka katika rodi yake, kama kwamba anaficha siri, akasema, ‘’Ndiyo, ajabu sana ajabu kweli kweli.’’
Mimi ni mtu asiyependa mafumbo na mambo ya sirisiri, basi niliwatazama mmoja mmoja, kishanikasema, ‘’Siwezi kufahamu vizuri,’’
Sir Henry akasema, ‘’Hufahamu? Basi, nitaeleza. Good na Mimi tulipokuwa tukija hapa tuliongea.’’
Nikayakatiza maneno yake kwa ukali kidogo, nikasema, ‘’Nadhali kama Good alikuwapo, hamkosi mliongea maana Good ni mtu apendaye sana maongezi. Je, mliongea habari gani?’’
Sir Henry, akauliza, ‘’Ee wafikiri tuliongea habari gani?’’
Nikatikisa kichwa changu.
Haiwezekani nikajua Good aliongea nini, maana mara nyingi huongea habari za mambo mengi.
Sir Henry akasema, ‘’Tuliongea juu ya shauri dogo nililoliwaza yaani kama wewe utakubali tutafunga mizigo yetu na kuiendea nchi ya Afrika kufanya safari nyingine,’’
Nilipoyasikia maneno yake, nilishtuka sana, nikasema, ‘’Ni kweli usemayo?’’ akajibu, ‘’Ni kweli, na Good naye amekubali pia, sivyo Good?’’
Na yeye akaitikia, ‘’Ndiyo.’’
Basi, Sir Henry akaendelea, na sauti yake ilionyesha namna anavyoona hamu, akasema, ‘’Nami pia nimechoka kukaa bure kiubwana katika nchi iliyokinai mabwana.
Kwa muda wa mwaka mzima na zaidi nimekuwa nikitukutika kama tembo mzee anusaye batari.
Kila mara ninaota ndoto za nchi ya Ukukuana, na bibi kichawi Gagula, na Mashimo ya Mfalme Sulemani. Nakuambia ya kuwa nimenaswa na hamu nisiyoweza kuieleza.
Aisee, kumbe ma legend wote wapo ndani [emoji39] [emoji39]MAAJABU YALIYOWAPATA ALLAN QUATERMAIN NA WENZAKE
HADITHI YA UMSLOPAGAAS
SURA YA KWANZA
SIKU saba zilikuwa, zimepita tangu mwana wangu mpenzi alipozikwa na jioni ilipofika, nilikuwa Nikitembea huko na huko chumbani mwangu nikifikiri, mara mlango unabishwa, Nikaenda nikaufungua mlango mwenyewe, Kumbe rafiki zangu wa zamani Sir Henry Curts na Bwana John Good wapo nje.
Niliwakaribisha ndani wakaingiaa chumbani. Wakakaa mbele ya moto uliokuwa ukiwaka humo.
‘’Mmefanya vyema kuja kunitazama.’’
Hawakujibu neno, ila Sir Henry alishindilia tumbako katika kiko chake akakiwasha kwa kaa alilolitoa motoni, Alipokuwa akiinama mbele kufanya hivyo moto, uliwaka zaidi ukaangaza chumbani, nikafikiri jinsi alivyo mtu mzuri mno.
Uso wake mtulivu wenye nguvu, sura yake thabiti, macho yake makubwa ya kijivu ndevu na nywele zake rangi ya manjano.
Sura yake yote ilikuwa ya mtu aliye bora, tena umbo lake halikuwa kinyume cha uso wake, Sijapata kuona mabega mapana, zaidi wala kifua kinene kama chake.
Umbo la Sir Henry ni pana, ingawa ni mrefu wa futi sita na inchi mbili lakini haonekani kuwa mrefu nilipokuwa nikimtazama hivi, sikuweza kujizuia nisifiri namna mimi nilivyo mwembamba mfupi na namna nilivyohitilafiana na uso wake mzuri, na umbo lake bora.
Embu wazeni basi juu ya mtu mfupi aliyesinyaa, mwenye uso wa rangi ya manjano na umri wa miaka sitini na mitatu mwenye mikono membamba, macho makubwa ya kahawia, kichwa kimefunikwa na nywele zinazoingia mvi na kusimama wima kama brashi iliyotumika, kiasi uzani wake pamoja na mavazi aliyovaa ratili mia moja thelathini na mbili tu.
Basi hapo ndipo mtakapofahamu namna alivyo Allan Quatermain, ambaye kwa desturi huitwa Mwindaji Quatermain, na Waafrika humwita ‘’Makumazahn,’’ maana yake akeshaye usiku, yaani mtu mwerevu asiyedanganyika.
Tena, yupo Bwana Good ambaye hafanani na Sir Henry wala na mimi maana ni mfupi, mweusi kidogo, mnene mnene sana ana macho meusi yang’aayo na katika jicho moja siku zote huvaa rodi, yaani miwani ya jicho moja.
Nilisema yeye ni mnene, lakini neno hilo halitoshi kueleza namna alivyo mnene. Sir Henry humwambia ya kuwa amenenepa hivi kwa sababu yu mvivu, tena anakula sana, ingawa Bwana Good hapendezwi kwa maneno yake , lakini hawezi kuyakana.
Tulikaa kwa muda mfupi, kisha niilichuka kiberiti ili niiwashe taa, kwa sababu niiona giza linachosha, maana ndivyo inavyoelekea hasa ikiwa muda wa siku saba tu umepita tangu mtu alipozika tumaini la maisha yake.
Huku nyuma Sir Henry na Bwana Good walikuwa wamekaa kimya, wakiona nadhani, ya kuwa hawana la kusema linaloweza kunifariji, wakaridhika kunifariji kwa kuwapo kwao ni rambirambi zao za kimya.
Ni kweli ya kuwa twapata tumaini na faraja katika saa za majonzi kwa kuwapo wengine, wala si kwa maongezi yao ambayo huelekea kutuudhi tu. Wakakaa wakivuta tumbako, na mimi nilisimama mbele ya moto nikivuta tumbako pia na kuwaangalia.
Halafu kidogo nilisema, ‘’Je rafiki zangu wa zamani, tangu tuliporudi toka nchi ya Ukukuana hata leo, miaka mingapi imepita? ‘’Bwana Good akasema, ‘’Miaka mitatu. Kwa nini unauliza?’’.
Nikajibu, ‘’Nauliza kwa sababu nafikiri ya kuwa muda niiokaa pamoja na watu mijini umenitosha kabisa, Nitarudi mwituni tena.’’
Hapa Sir Henry alikipeleka nyuma kichwa chake, akacheka mcheko wake wa kindani, akasema, ‘’Ama ni ajabu sana, sivyo Good?’’
Bwana Good akaniangalia, na huku anacheka katika rodi yake, kama kwamba anaficha siri, akasema, ‘’Ndiyo, ajabu sana ajabu kweli kweli.’’
Mimi ni mtu asiyependa mafumbo na mambo ya sirisiri, basi niliwatazama mmoja mmoja, kishanikasema, ‘’Siwezi kufahamu vizuri,’’
Sir Henry akasema, ‘’Hufahamu? Basi, nitaeleza. Good na Mimi tulipokuwa tukija hapa tuliongea.’’
Nikayakatiza maneno yake kwa ukali kidogo, nikasema, ‘’Nadhali kama Good alikuwapo, hamkosi mliongea maana Good ni mtu apendaye sana maongezi. Je, mliongea habari gani?’’
Sir Henry, akauliza, ‘’Ee wafikiri tuliongea habari gani?’’
Nikatikisa kichwa changu.
Haiwezekani nikajua Good aliongea nini, maana mara nyingi huongea habari za mambo mengi.
Sir Henry akasema, ‘’Tuliongea juu ya shauri dogo nililoliwaza yaani kama wewe utakubali tutafunga mizigo yetu na kuiendea nchi ya Afrika kufanya safari nyingine,’’
Nilipoyasikia maneno yake, nilishtuka sana, nikasema, ‘’Ni kweli usemayo?’’ akajibu, ‘’Ni kweli, na Good naye amekubali pia, sivyo Good?’’
Na yeye akaitikia, ‘’Ndiyo.’’
Basi, Sir Henry akaendelea, na sauti yake ilionyesha namna anavyoona hamu, akasema, ‘’Nami pia nimechoka kukaa bure kiubwana katika nchi iliyokinai mabwana.
Kwa muda wa mwaka mzima na zaidi nimekuwa nikitukutika kama tembo mzee anusaye batari.
Kila mara ninaota ndoto za nchi ya Ukukuana, na bibi kichawi Gagula, na Mashimo ya Mfalme Sulemani. Nakuambia ya kuwa nimenaswa na hamu nisiyoweza kuieleza.
Mbona na hii inaonekana ni kali sana? SafiNimechoka kupiga kanga na kwale, na sasa nataka kuwinda wanyama wakubwa. Mwaka ule mmoja tuliokaa pamoja katika nchi ya Ukukuana huonekana kama kwamba thamani yake inapita thamani ya jumla ya miaka yote ya maisha yangu.
Labda ni mpumbavu kwa hamu ninayoiona, lakini sina nguvu kuishinda, natamani kwenda, tena sina budi kwenda.’’ Basi alisita kidogo, kisha akaendelea..
‘’Tena, kwa nini nisiende? Sina mke wala baba, wala mama, wala mtoto wakunizuia nisiende. Nikipatikana na ajali, cheo changu na Mali itarithiwa na ndugu yangu George na mwanawe, nao watairithi kwa vyovyote.
Mimi si kitu kwa mtu yeyote.’’ Akasema,
‘’Ah! Nilifikiri utasema hayo. Na wewe Good, mbona wewe unataka kusafiri, unayo sababu?’’
Bwana Good, akasema na huku anajizuia asicheke, ‘’Ndiyo, ninayo sababu. Mimi sifanyi neno bila kuwa na sababu. Lakini ukitaka kujua sababu ya kweli, nitakwambia, ingawa sipendi kukuambia. Ninaanza kuwa mnene zaidi!’’
Basi, nilitia moto kikoni, maana ulikuwa umezimika, ndipo niliposema tena, nikauliza, ‘’Ninyi mmepata kusikia habari za mlima Kenya?’’
Bwana Good akajibu, ‘’Sipajui mahali hapo.’’
Nikauliza tena, ‘’Mmepata kusikia habari za kisiwa kiitwacho Lamu?’’
Bwana Good akajibu, ‘’La.
Ngoja si mahali palipo kaskazini ya Unguja kadiri ya maili mia tatu?’’
Nikasema, ‘’Ndipo. Sikilizeni. Shauri langu ni hili.
Twendeni Lamu, na kutoka huko tutasafiri ndani ya nchi kadiri ya maili mia mbili na hamsini mpaka mlima Kenya. Kutoka mlima Kenya tuendelee mbele tena kusikia habari zake. Kumbuka Mashimo ya Mfalme Sulemani.’’
Kadiri ya majuma kumi na manne yamepita tangu tulipoongea hivyo, na sasa habari hizi zinatokea katika mahali pa namna nyingine kabisa.
Baada ya kufikiri na kuhojiana sana habari, tuliona ya kuwa itafaa kuianza safari yetu kuuendea mlima Kenya mahali karibu na mlango wa mto Tana, wala si Mombasa.
Basi, ikatokea ya kuwa tulipofika Lamu, tuliteremka pwani pamoja na vitu vyetu vyote, na kwa kuwa hatukujua mahali pa kwenda, tulikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Bwana Balozi wa Serikali ya Kiingereza, tukapokewa kwa ukarimu.
Lamu ni mahali pageni kabisa, lakini mambo yanayodumu katika fikira zangu hata leo ni uchafu wake na uvundo wake. Hasa uvundo wake ni mno. Mbele ya jumba la Bwana Balozi ni pwani, au tuseme fungu la matope liitwalo pwani.
Maji ya bahari yapwaapo huacha nafasi wazi , ndipo mahali panapotupwa taka zote za mji. Pia, hapo wanawake huja wakafukia nazi katika matope na kuziacha humo mpaka makumbi yaoze, ndipo huja kuyafukua na kuzitumia nyuzinyuzi zake, yaani usumba, kutengenezea busati na vitu vinginevyo.
Kwa kuwa mambo hayo yameendelea kwa vizazi na vizazi, ni heri hali ya pwani hiyo ilivyo iwaziwe tu kuliko kuelezwa. Katika siku za maisha yangu nimepata kunusa harufu mbaya nyingi, lakini harufu kali iliyotoka pwani ya Lamu tulipokuwa tumekaa juu ya gorofa ya Bwana Balozi inazifanya zote ziwe kama si kitu kabisa.
Si ajabu ya kuwa watu hushikwa na homa Lamu. Lakini hata hivyo mahali hapo pana uzuri wa namna yake ingawa labda utamchosha mtu upesi.
Basi, tulipokwisha kula, tulikaa tukavuta tumbako, na rafiki yetu Balozi mkarimu aliuliza, ‘’Je, ninyi mabwana mnakwenda wapi?’’
Sir Henry akajibu, ‘’Tumekusudia kuuendea mlima Kenya, kisha, kuendelea mbele mpaka mlima Lekakisera. Quatermain amesikia hadithi ya kuwa liko taifa la watu weupe wanaokaa katika nchi za mbali zisizojulikana bado, kupita huko.’’
Bwana Balozi aliyatega masikio yake, akajibu ya kuwa hata na yeye amepata kusikia habari kama hizo.
Nikamuuliza, ‘’je, umesikia nini?’’ Akajibu, ‘’Si nyingi, ila najua ya kuwa zamani, kadiri ya mwaka mmoja, nilipata barua kwa Bwana Mackenzie, mtu wa misioni anayekaa mahali mwisho wa mto Tana panapofikiwa na mitumbwi, naye alitaja habari hizo.’’
Nikamuuliza, ‘’Je, unayo barua hiyo?’’
Akasema, ‘’La, niliitatua; lakini nakumbuka alisema ya kuwa mtu mmoja alifika kwake akasema kwamba alikwenda mbali kadiri ya safari ya miezi miwili kupita mlima Lekakisera, ambao hapana mtu mweupe aliyeufikia yaani kwa kadiri nijuavyo mimi akavumbua huko ziwa liitwalo Laga.
Kisha akaendelea upande wa mashariki ya kaskazi, safari ya mwezi mzima kuvuka jangwa na mbuga na milima mirefu, mpaka alipofika nchi wanapokaa watu weupe wakaao katika nyumba za mawe.
Huko alipokewa kwa ukarimu akakaa kwa muda, mpaka makuhani wa nchi ile walipo chochea habari ya kuwa yeye ni shetani, basi watu wakamfukuza, akasafiri muda wa miezi minane hata akafika mahali alipomkuta Bwana Meckenzie anakufa.
Umenena vema Bwana blackstarlineHakuna shida wewe iweke tu popote unapoona pana faa, nadhani itakuwa faida kwa watu wote wanao penda Hadithi napia ni akiba kwa vizazi vijazo. But usiwe lagai ukauzia watu.
Hahaah karibu sanaNgoja nivute kigoda hapa.
Hahaah hii ni hatari.Mbona na hii inaonekana ni kali sana? Safi
Gagula tu ndiyo hayupo!Aisee, kumbe ma legend wote wapo ndani [emoji39] [emoji39]
Team imetimia
Hasha, huyu kizee kichawi simkosi, Foulata pekee ndiye anayefanya moyo wangu kuwa mzito sana, umauti wake ulinitia ufa moyoni, ukaupasua katikati. [emoji29] [emoji29]Gagula tu ndiyo hayupo!