Hadithi ya umslopagaas

Hadithi ya umslopagaas

SURA YA PILI


Baada ya muda, mambo yalipokuwa tayari, tulitoka Lamu, na baada ya kusafiri siku kumi na kukutana na mambo mengi, ambayo hapana haja kuyataja hapa tulifika mahali paitwapo Chara, kando ya mto Tana.

Katika mambo tuliyoyaona ni magofu ya miji ya zamani, nayo ni mengi katika pwani hizi. Kwa kadiri ya magofu ya misikiti na nyumba za mawe yaliyopo, miji hii ilikuwa na watu wengi sana zamani. Miji hiyo ni ya zamani sana.

Nimeambiwa ya kuwa ilikuwa maarufu hata katika wakati wa Agano la Kale, na watu waliokaa. Humo walikuwa wakifanya biashara na watu wa Uhindi na wa nchi nyinginezo.


Lakini utukufu wake umetoweka biashara ya watumwa imeumaliza na mahali pale waliposimama zamani matajiri wa kutoka nchi zilizostarabika wakati ule, wakishindania bei katika masoko yaliyojaa watu, sasa simba huja na kufanya baraza zao usiku, na badala ya mazungumzo ya watumwa na sauti za bidii za watu waliokuwa wakiwanadi, mlio wa simba hulialia katika magofu.


Huko Chara tuligombana sana na mnyapara wa wapagazi tuliowaajiri kufuatana nasi mpaka hapo, maana alitaka kututoza fedha nyingi kuliko ile tulivyopatana. Mwishowe alijaribu kututisha, ya kuwa atawapeleka Wajivuni kutushambulia.


Usiku ule yeye pamoja na wapagazi wote walitoroka pamoja na mizigo waliyoichukua. Kwa bahati hawakuziiba banduki wala risasi wala nguo zetu; si kwa sababu hawakuzitaka, ila kwa sababu zililindwa na wale askari watano wa Kikazi.


Basi, hapa tuliona dhahiri ya kuwa hatuwezi kuvumilia matata mengine ya wapagazi, na kwa kweli hatukubaki na vitu vingi vya kuchukuliwa. Lakini kama hatuna Wapagazi, tutaweza kuendelea namna gani?


Bwana Good ndiye aliyetoa shauri la kufaa. Alituonyesha mto, akasema, ‘’Hapa pana maji, na jana niliona wenyeji wengine katika mitumbwi wanawinda viboko.

Nadhani mahali anapokaa Bwana Mackenzie ni kando ya mto Tana. Je, kwa nini tusipate mitumbwi na kuiendesha mpaka kufika kwake?’’

Shauri hili zuri lilipokewa kwa furaha, na mara ile nilianza kufanya shauri la kununua mitumbwi inayofaa, kwa wenyeji wa karibu.

Baada ya kujaribu siku tatu niliweza kununua miwili mikubwa, kila mmoja uliweza kuchukua watu sita pamoja na mizigo mingine. Bei ya mitumbwi hiyo ilikuwa karibu kuimaliza bidhaa yetu yote, tena tukatoa na vitu vingine pia.

Basi, siku iliyofuata ile tuliyonunua mitumbwi, tulianza safari yetu tena. Katika mtumbwi wa kwanza mlikuwamo Bwana Good, Sir Henry na Wakazi watatu, katika ule wa pili, mimi, Umslopogaas na Wakazi wawili.

Kwa kuwa tulikuwa tukipanda mtoni, ilitupasa kuvuta kafi nne katika kila mtumbwi; ikawa kazi ngumu sana. Baada ya siku ya kwanza Bwana Good aliweza kusimamisha mlingoti katika kila mtumbwi, akatengeneza matanga, na kazi ilikuwa rahisi zaidi.


Lakini mkondo wa maji ulikuwa na nguvu, nasi hatukuweza kwenda zaidi ya maili ishirini kutwa.

Desturi yetu ilikuwa kuondoka asubuhi na mapema na kupiga kafi mpaka saa nne na nusu, ndipo jua linapokuwa kali zaidi. Basi, tulifunga mitumbwi kando ya mto tukala chakula kidogo kisha tulilala au kujizungumzisha mpaka saa tisa.

Saa tisa tulianza tena kuvuta kafi mpaka saa kumi na moja hivi, ndipo tulishuka kando ya mto kufanya kambi, na Bwana Good alianza kujenga boma la miiba na kukoka moto kwa msaada wa askari wetu.


Mimi pamoja na Sir Henry na Umslopogaas tulikwenda kuwinda tupate nyama kwa kitoweo chetu.

Kwa desturi hatukuona shida kupata mnyama, maana wanyama wa kila namna wapo kando ya mto Tana. Siku moja jioni Sir Henry alipiga twiga mchanga wa kike, na ubongo na mifupa yake ulikuwa mtamu sana.


Siku nyingine nilipiga kuro wawili, mmoja upande wa kushoto, na mmoja upande wa kuume, na siku moja Umslopogaas, ambaye kama Wazulu wote walivyo, hana shabaha, aliwahi kupiga pofu mnono kwa bunduki niliyomwazima.


Pengine tulibadili namna ya chakula chetu kwa kupiga kanga au ndege wengine waliokuwa wengi, kwa risasi, au kwa kuvua namna ya samaki wazuri waliokuwamo tele katika mto Tana.

Siku tatu baada ya kuondoka, jambo baya lilitokea.

Tulikuwa tunakaribia kando ya mto ili kufunga mitumbwi yetu na kupanga kambi tayari kwa usiku, tukaona mtu amesimama juu ya kilima kidogo mwendo wa yadi arobaini toka hapo tulipokuwapo, naye alikuwa anatuangalia sana. Kumtazama tu, mara nilitambua ya kuwa ni askari wa Kijivuni.


Na hata kama ningalikuwa na shaka kulitambua kabila lake ningalijuwa mara ile, maana Wakazi walinong’ona kwa hofu, ‘’Mjivuni!’’
 
Jinsi alivyotisha alipokuwa amesimama hivyo, amevaa mavazi yake ya vita! Nimezoea sana watu wa makabila mengi maisha yangu yote, lakini nadhani sijaona mmoja aliyekuwa wa kutisha zaidi ya huyo.


Kwanza alikuwa mrefu sana, nakisia alikuwa mrefu kama Umslopogaas, tena umbo lake zuri mno ila labda jembamba kidogo.

Lakini uso wake ulikuwa mwovu sana. Alikuwa ameshika mkuki mrefu kadiri ya futi tano na nusu katika mkono wake wa kuume, na bamba lake lilikuwa na urefu wa futi mbili na nusu, na uoana wake inchi tatu, na mwisho wa kipini chake ulikuwa na ncha ya chuma urefu wa futi moja au zaidi.


Kwa mkono wake wa kushoto alikuwa ameshika ngao ya ngozi ya nyati iliyotiwa alama alama.

Alikuwa amevaa vazi la manyoya ya mwewe begani, na kuzunguka shingo yake alivaa kipande kirefu cha kitambaa kadiri ya futi kumi na saba, na upana wake ulikuwa futi moja na nusu; kina mstari wa rangi katikati yake kwa marefu.


Ngozi ya mbuzi iliyokuwa mavazi yake ya siku za amani ilifungwa kiunoni kwa mkanda, na katika mkanda amechomeka sime upande wa kuume na rungu upande wa kushoto lakini labda vazi lililonivuta macho zaidi lilikuwa manyoya ya mbuni yaliyo fungwa kuuzunguka uso wake.

Duara hii ya manyoya ilifungwa chini ya kidevu chake, ikapita kichwani ikawa kama duara inayouzunguka uso wake mwovu.

Katika visigino vya miguu alikuwa amevaa manyoya meusi, na kwa juu ya machavu ya miguu amevaa vishungi vya manyoya ya mbega.

Basi, hayo ndiyo mavazi ya Yule Mjivuni, aliyesimama akituangalia tulipokuwa tukikaribia katika mitumbwi yetu, lakini kueleza tu hakufai, lazima mtu amwone ndio atambue namna alivyokuwa.

Kweli sikuweza kuona sehemu zote za mavazi yake kwa mara ile, ila nilipata nafasi nyingi baadaye kuziona.

Tulipokuwa tukisita na kufikiri shauri la kufanya, Yule Mjivuni alijinyosha wima kwa madaha, akautisa mkuki wake kutuelekea, kisha, aligeuka akateremka upande wa pili wa kilima.

Sir Henry aliita kutoka mtumbini mwake, akasema, ‘’Ati! Yule mnyapara amelishikilia neno lake na kutuletea Wajivuni.

Je, waonaje, itakuwa salama kuteremka kando ya mto?’’

Mimi sikufikiri ya kuwa itakuwa salama, lakini hata hivyo hatukuweza kupika katika mitumbwi yetu, wala hatukuwa na chakula kilichoweza kuliwa bila kupikwa, kwa hivi ilikuwa vigumu kujua shauri la kufanya.

Mwishowe, Umslopogaas alitoa shauri, yaani yeye aende kupeleleza, akatambaa katika kichaka kama nyoka, nasi tulikaa katikati ya mto tukingoja, Baada ya kupita nusu saa alirudi, akatuambia kuwa hakuona hata Mjivuni mmoja karibu.

Lakini aliona mahali walipokuwa wamefanya kambi karibuni, naye alifikiri ya kuwa waliondoka kadiri ya saa moja tu na Yule mtu tuliyemwona hakosi alipelekwa kupeleleza habari zetu.


Basi, hapo tulishuka, tukaweka mtu wa kushika zamu, tukaendelea kupika chakula na kukila. Kisha, tulifanyashauri juu ya hali yetu.

Kwetu yakini, iliwezekana kuwa Yule Mjivuni hana shughuli na sisi, ila labda ni mmoja wa kikosi cha Wajivuni waliokuwa wakienda kuwashambulia watu wa kabila jingine.

Rafiki yetu Yule Bwana Balozi wa Lamu alituambia kuwa vikosi vya namna hiyo vinatembea tembea.

Lakini tulipojikumbusha maneno ya Yule mnyapara, na kufikiri namna Yule Mjivuni alivyotutikisia mkuki wake, tuliona ya kuwa jambo hilo halikuendelea bali lilielekea ya kuwa wanatufuata wakingojea wakati unaofaa kutushambulia.

Basi, kama ni hivi, yapo mashauri mawili yanayowezekana, la kwanza tuendelee mbele, na la pili turudi nyuma.

Lile la pili lilikataliwa mara ile, maana ilikuwa dhahiri kwamba tukirudi tutapambana na hatari zilezile tutakazo pambana nazo kama tukiendelea, tena tulikuwa tumekaza nia kwenda mbele kwa vyovyote.

Lakini tuliona kuwa si salama kupiga kambi na kulala usingizi nchi kavu, kwa hivi tuliingia katika mitumbwi yetu, tukaipeleka katikati ya mto, ambayo haukuwa mpana sana, tukatia nanga, yaani mawe makubwa yaliyofungiwa kamba ya mnazi.

Hapa tulikuwa karibu kabisa kuliwa na mbu, na jambo hili pamoja na fikra za hali yetu ilinizuia nisilale usingizi kama wenzangu, ingawa wanashambuliwa na mbu.
 
Basi nilikaa nikivuta tumbako na kuwaza juu ya mambo mengi na hatari ipo ya kupatwa na homa kwa kulala mahali kama hapa, tena mguu wangu wa kuume umekufa ganzi kwa kukaa hali umekunjwa katika mtumbwi, lakini nilianza kuufurahia uzuri wa usiku.

Miali ya mbalamwezi ilichezacheza juu ya uso wa maji yanayopita kasi kuendea baharini, kama maisha ya wanadamu yapitavyo kuendea kaburini, mpaka yakang’aa kama utando mpana wa fedha, yaani mahali pa wazi pasipo fikiwa na vivuli vya miti.

Lakini karibu na kando ya mto palikuwa giza sana na upepo ulivuma katika matete, ukafanya sauti ya kuhuzunisha.


Upande wa kushoto, ng’ambo ya mto, palikuwapo namna ya ghuba ndogo yenye mchanga pasipo na miti, na hapo niliweza kuona vivuli vya wanyama wengi waliokuja kunywa maji, mpaka kwa ghafla nilisikia ngurumo ya kutisha sana, na mara ile wote wakatimka.

Baadaye kidogo, niliona umbo kubwa la simba akija kunywa maji baada ya kula kwake.

Halafu aliondoka, ndipo niliposikia kishindo katika matete kadiri ya yadi hamsini kutoka hapo tulipokuwapo, na baada ya dakika chache kitu kikubwa cheusi kiliibuka katika maji.

Kumbe, ni kichwa cha kiboko. Kikazama tena bila kufanya sauti, kikaibuka tena karibu, yaani kadiri ya yadi tano tu kutoka mahali tulipo.

Hapo niliona ya kuwa yupo karibu sana, na kwa hivi sikuona raha, na hasa kwa kuwa alionekana kama atakaye kujua mitumbwi yetu ni kitu gani.

Alikifunua kinywa chake kipana, labda apige miayo tu, nikayaona meno yake, nikafikiri jinsi anavyoweza kuusagilia mbali mtumbwi wetu mdogo kwa dhoruba moja.

Nilianza kufikiri labda itafaa nimpige risasi, lakini nilipofikiri zaidi, niliazimu kumwacha kama asipojaribu kuushambulia mtumbwi. Halafu alizama tena bila kufanya sauti hata kidogo, wala sikumwona tena.

Papo hapo nilitupa macho ng’ambo ya kuume, nikawa kama ninaweza kuona kitu cheusi kinapita katika mashina ya miti.

Macho yangu ni makali sana, nami nadhani niliona kitu kwa hakika, lakini kama ni ndege, au mnyama, au mtu sikuwa na hakika.

Lakini papo hapo wingu jeusi lilipita mbele ya mwezi, kwa hiyo sikukiona kilekitu tena. Tena, papo hapo nilisikia mlio kama wa bundi akilia mfulilizo, baadaye kukawa kimya kabisa isipokuwa sauti za kuchakacha katika miti na matete, wakati upepo ulipoyatikisa.

Lakini kwa jinsi isiyoelekezeka, sasa nilianza kushuku hatari za kuona hofu,hapakuwapo wala sababu ya dhahiri ya kunitia hofu hivyo zaidi ya zile zinazomzunguka msafiri yeyote katika nchi ya Afrika, lakini hata hivyo, bila shaka niliona hofu.

Lakini nilikaza nia nisishindwe na hofu, ingawa jasho baridi lilinitoka pajini mwa uso. Wala sikukubali kuwaamsha wenzangu.

Hali yangu ilizidi kuwa mbaya, na moyo wangu ulinipigapiga kama moyo wa mtu anayekaribia kufa. Na mishipa yangu ilinichezacheza kana kwamba kitisho kiovu kiko karibu. Watu waliopata kuota jinamizi, watafahamunamna hali yangu ilivyokuwa.
 
Lakini hata hivyo nilijikaza nikakaa kimya, nikageuza uso wangu tu kumtazama Umslopogaas na Wakazi wale wawili waliokuwa wamelala kando yake.

Nilisikia kishindo kidogo cha kiboko mbali, na Yule bundi alilia tena, na upepo ulianza kuvuma katika miti na kufanya sauti ya kuhuzunisha iliyopoozesha moyo. Baadaye nilipata kujua kuwa Wajivuni huitana kwa kuiga sauti ya bundi.

Juu niliona wingu jeusi, na chini maji meusi yalikuwa yakipita kasi, nikaona kama kwamba mimi na mauti tupo katika yake. Niliona ukiwa kabisa.


Mara damu yangu ilikuwa kama imevia katika mishipa yangu, na moyo wangu kusimama kimya. Je, ni ndoto tu ama ndio mwendo?

Niliyageuza macho yangu kuutazama mtumbwi wa pili uliokuwa ukielea kando yetu, nisiuone, ila badala yake niliona mkono mweusi mwembamba umeinuliwa juu ya ubavu mwa mtumbwi.

Hakika ni jinamizi! Lakini mara ile uso mwovu ulitokea juu kama kwamba umetoka majini, ndipo mtumbwi ulipoinama, kisu kikang’aa ghafla, na Mkazi mmoja aliyekuwa amelala kando yangu akapiga ukelele na kitu cha moto kilichuzurika usoni pangu.

Mara ile kuduwaa kwangu kukakoma, nikatambua kwamba si jinamizi, ila tumeshambuliwa na Wajivuni wanaogelea majini.

Nikashika silaha ya kwanza niliyoweza kuipata ikatokea kuwa ni shoka la vita la Umslopogaas, nikapiga kwa nguvu zangu zote pale nilipokuwa nimekiona kisu kinang’aa .
Pigo liliangukia juu ya mkono wa mtu likaugandamiza juu ya ubavu mnene wa mtumbwi, na kuukata kisiginoni.

Yule mtu asifanye sauti hata kidogo akatoweka kama kivuli, alikuja kama kivuli na akaondoka kama kivuli. Ameacha nyuma yake ule mkono wake wenye damu ungali umeshika sime ile iliyokuwa imechomwa katika moyo wa mtumishi wetu msikini.


Mara kulikuwa ghasia na fujo, nikadhani, sijui ni kweli au je, nikaona vichwa vyeusi vingine vikielea majini kuendea ng’ambo ya kuume, ambako mtumbwi wetu uliendea kasi kwa sababu kamba ile iliyokuwa na nanga ya jiwe imekatwa kwa kisu.


Mara nilipotambua hivyo, nilifahamu pia ya kuwa shauri lao ni kuikata kamba ili mtumbwi uchukuliwe na maji ili kuiendea ile ng’ambo ya kuume; na huko bila shaka Wajivuni wanangojea kutuchoma kwa mikuki yao.

Basi, nilishika kafi moja mwenyewe, nikamwambia Umslopogaas aishike nyingine, maana wale Wakazi walikuwa wameduwaa kwa hofu hata kushindwa kuhema, tukapiga kafi kwa nguvu kurejea tena katikati ya mto.

Wala hatukufanya hivyo kwa haraka zaidi kuliko ilivyopasa, maana katika dakika nyingine tungali kwamba na bila shaka ingalikuwa ndiyo mwisho wetu.

Mara tulipofika katikati ya mto tena, tulianza kupiga kafi kupaendea pale ulipokuwapo ule mtumbwi mwingine umetiwa nanga nayo ilikuwa kazi ngumu na hatari pia, kwa sababu hakuna la kutuongoza ila sauti ya Good, maana alipiga kelele mara kwa mara.

Mwishowe tuliufikia mtumbwi, tukashukuru tulipoona ya kuwa hawakushambuliwa.

Haikosi ule mkono ulioikata kamba ya mtumbwi wetu ungaliikata yao, na Yule mtu asingalivutwa na tamaa ya kuua na jambo hilo, ingawa lilitupotezea maisha ya mtu mmoja na Yule Mjivuni mkono wake, lakini pia lilituokoa sote wengine tusiangamizwe.

Kukosa kukiona kile kitisho kiovu kikitokea juu ya ubavu wa mtumbwi, kitisho ambacho sitakisahau mpaka siku ya kufa kwangu. Mtumbwi wetu ungalichukuliwa kando ya mto kabla sijatambua umepatwa na nini, na habari hizi hazingaliandikwa nami.
 
MAAJABU YALIYOWAPATA ALLAN QUATERMAIN NA WENZAKE
HADITHI YA UMSLOPAGAAS

SURA YA KWANZA


SIKU saba zilikuwa, zimepita tangu mwana wangu mpenzi alipozikwa na jioni ilipofika, nilikuwa Nikitembea huko na huko chumbani mwangu nikifikiri, mara mlango unabishwa, Nikaenda nikaufungua mlango mwenyewe, Kumbe rafiki zangu wa zamani Sir Henry Curts na Bwana John Good wapo nje.

Niliwakaribisha ndani wakaingiaa chumbani. Wakakaa mbele ya moto uliokuwa ukiwaka humo.

‘’Mmefanya vyema kuja kunitazama.’’

Hawakujibu neno, ila Sir Henry alishindilia tumbako katika kiko chake akakiwasha kwa kaa alilolitoa motoni, Alipokuwa akiinama mbele kufanya hivyo moto, uliwaka zaidi ukaangaza chumbani, nikafikiri jinsi alivyo mtu mzuri mno.

Uso wake mtulivu wenye nguvu, sura yake thabiti, macho yake makubwa ya kijivu ndevu na nywele zake rangi ya manjano.

Sura yake yote ilikuwa ya mtu aliye bora, tena umbo lake halikuwa kinyume cha uso wake, Sijapata kuona mabega mapana, zaidi wala kifua kinene kama chake.

Umbo la Sir Henry ni pana, ingawa ni mrefu wa futi sita na inchi mbili lakini haonekani kuwa mrefu nilipokuwa nikimtazama hivi, sikuweza kujizuia nisifiri namna mimi nilivyo mwembamba mfupi na namna nilivyohitilafiana na uso wake mzuri, na umbo lake bora.

Embu wazeni basi juu ya mtu mfupi aliyesinyaa, mwenye uso wa rangi ya manjano na umri wa miaka sitini na mitatu mwenye mikono membamba, macho makubwa ya kahawia, kichwa kimefunikwa na nywele zinazoingia mvi na kusimama wima kama brashi iliyotumika, kiasi uzani wake pamoja na mavazi aliyovaa ratili mia moja thelathini na mbili tu.

Basi hapo ndipo mtakapofahamu namna alivyo Allan Quatermain, ambaye kwa desturi huitwa Mwindaji Quatermain, na Waafrika humwita ‘’Makumazahn,’’ maana yake akeshaye usiku, yaani mtu mwerevu asiyedanganyika.


Tena, yupo Bwana Good ambaye hafanani na Sir Henry wala na mimi maana ni mfupi, mweusi kidogo, mnene mnene sana ana macho meusi yang’aayo na katika jicho moja siku zote huvaa rodi, yaani miwani ya jicho moja.


Nilisema yeye ni mnene, lakini neno hilo halitoshi kueleza namna alivyo mnene. Sir Henry humwambia ya kuwa amenenepa hivi kwa sababu yu mvivu, tena anakula sana, ingawa Bwana Good hapendezwi kwa maneno yake , lakini hawezi kuyakana.

Tulikaa kwa muda mfupi, kisha niilichuka kiberiti ili niiwashe taa, kwa sababu niiona giza linachosha, maana ndivyo inavyoelekea hasa ikiwa muda wa siku saba tu umepita tangu mtu alipozika tumaini la maisha yake.


Huku nyuma Sir Henry na Bwana Good walikuwa wamekaa kimya, wakiona nadhani, ya kuwa hawana la kusema linaloweza kunifariji, wakaridhika kunifariji kwa kuwapo kwao ni rambirambi zao za kimya.


Ni kweli ya kuwa twapata tumaini na faraja katika saa za majonzi kwa kuwapo wengine, wala si kwa maongezi yao ambayo huelekea kutuudhi tu. Wakakaa wakivuta tumbako, na mimi nilisimama mbele ya moto nikivuta tumbako pia na kuwaangalia.


Halafu kidogo nilisema, ‘’Je rafiki zangu wa zamani, tangu tuliporudi toka nchi ya Ukukuana hata leo, miaka mingapi imepita? ‘’Bwana Good akasema, ‘’Miaka mitatu. Kwa nini unauliza?’’.

Nikajibu, ‘’Nauliza kwa sababu nafikiri ya kuwa muda niiokaa pamoja na watu mijini umenitosha kabisa, Nitarudi mwituni tena.’’

Hapa Sir Henry alikipeleka nyuma kichwa chake, akacheka mcheko wake wa kindani, akasema, ‘’Ama ni ajabu sana, sivyo Good?’’

Bwana Good akaniangalia, na huku anacheka katika rodi yake, kama kwamba anaficha siri, akasema, ‘’Ndiyo, ajabu sana ajabu kweli kweli.’’

Mimi ni mtu asiyependa mafumbo na mambo ya sirisiri, basi niliwatazama mmoja mmoja, kishanikasema, ‘’Siwezi kufahamu vizuri,’’

Sir Henry akasema, ‘’Hufahamu? Basi, nitaeleza. Good na Mimi tulipokuwa tukija hapa tuliongea.’’

Nikayakatiza maneno yake kwa ukali kidogo, nikasema, ‘’Nadhali kama Good alikuwapo, hamkosi mliongea maana Good ni mtu apendaye sana maongezi. Je, mliongea habari gani?’’

Sir Henry, akauliza, ‘’Ee wafikiri tuliongea habari gani?’’
Nikatikisa kichwa changu.

Haiwezekani nikajua Good aliongea nini, maana mara nyingi huongea habari za mambo mengi.

Sir Henry akasema, ‘’Tuliongea juu ya shauri dogo nililoliwaza yaani kama wewe utakubali tutafunga mizigo yetu na kuiendea nchi ya Afrika kufanya safari nyingine,’’

Nilipoyasikia maneno yake, nilishtuka sana, nikasema, ‘’Ni kweli usemayo?’’ akajibu, ‘’Ni kweli, na Good naye amekubali pia, sivyo Good?’’
Na yeye akaitikia, ‘’Ndiyo.’’

Basi, Sir Henry akaendelea, na sauti yake ilionyesha namna anavyoona hamu, akasema, ‘’Nami pia nimechoka kukaa bure kiubwana katika nchi iliyokinai mabwana.

Kwa muda wa mwaka mzima na zaidi nimekuwa nikitukutika kama tembo mzee anusaye batari.

Kila mara ninaota ndoto za nchi ya Ukukuana, na bibi kichawi Gagula, na Mashimo ya Mfalme Sulemani. Nakuambia ya kuwa nimenaswa na hamu nisiyoweza kuieleza.
Wacha nianze kuirarua taratibu

Shukran mkuu blackstarline
 
MAAJABU YALIYOWAPATA ALLAN QUATERMAIN NA WENZAKE
HADITHI YA UMSLOPAGAAS

SURA YA KWANZA


SIKU saba zilikuwa, zimepita tangu mwana wangu mpenzi alipozikwa na jioni ilipofika, nilikuwa Nikitembea huko na huko chumbani mwangu nikifikiri, mara mlango unabishwa, Nikaenda nikaufungua mlango mwenyewe, Kumbe rafiki zangu wa zamani Sir Henry Curts na Bwana John Good wapo nje.

Niliwakaribisha ndani wakaingiaa chumbani. Wakakaa mbele ya moto uliokuwa ukiwaka humo.

‘’Mmefanya vyema kuja kunitazama.’’

Hawakujibu neno, ila Sir Henry alishindilia tumbako katika kiko chake akakiwasha kwa kaa alilolitoa motoni, Alipokuwa akiinama mbele kufanya hivyo moto, uliwaka zaidi ukaangaza chumbani, nikafikiri jinsi alivyo mtu mzuri mno.

Uso wake mtulivu wenye nguvu, sura yake thabiti, macho yake makubwa ya kijivu ndevu na nywele zake rangi ya manjano.

Sura yake yote ilikuwa ya mtu aliye bora, tena umbo lake halikuwa kinyume cha uso wake, Sijapata kuona mabega mapana, zaidi wala kifua kinene kama chake.

Umbo la Sir Henry ni pana, ingawa ni mrefu wa futi sita na inchi mbili lakini haonekani kuwa mrefu nilipokuwa nikimtazama hivi, sikuweza kujizuia nisifiri namna mimi nilivyo mwembamba mfupi na namna nilivyohitilafiana na uso wake mzuri, na umbo lake bora.

Embu wazeni basi juu ya mtu mfupi aliyesinyaa, mwenye uso wa rangi ya manjano na umri wa miaka sitini na mitatu mwenye mikono membamba, macho makubwa ya kahawia, kichwa kimefunikwa na nywele zinazoingia mvi na kusimama wima kama brashi iliyotumika, kiasi uzani wake pamoja na mavazi aliyovaa ratili mia moja thelathini na mbili tu.

Basi hapo ndipo mtakapofahamu namna alivyo Allan Quatermain, ambaye kwa desturi huitwa Mwindaji Quatermain, na Waafrika humwita ‘’Makumazahn,’’ maana yake akeshaye usiku, yaani mtu mwerevu asiyedanganyika.


Tena, yupo Bwana Good ambaye hafanani na Sir Henry wala na mimi maana ni mfupi, mweusi kidogo, mnene mnene sana ana macho meusi yang’aayo na katika jicho moja siku zote huvaa rodi, yaani miwani ya jicho moja.


Nilisema yeye ni mnene, lakini neno hilo halitoshi kueleza namna alivyo mnene. Sir Henry humwambia ya kuwa amenenepa hivi kwa sababu yu mvivu, tena anakula sana, ingawa Bwana Good hapendezwi kwa maneno yake , lakini hawezi kuyakana.

Tulikaa kwa muda mfupi, kisha niilichuka kiberiti ili niiwashe taa, kwa sababu niiona giza linachosha, maana ndivyo inavyoelekea hasa ikiwa muda wa siku saba tu umepita tangu mtu alipozika tumaini la maisha yake.


Huku nyuma Sir Henry na Bwana Good walikuwa wamekaa kimya, wakiona nadhani, ya kuwa hawana la kusema linaloweza kunifariji, wakaridhika kunifariji kwa kuwapo kwao ni rambirambi zao za kimya.


Ni kweli ya kuwa twapata tumaini na faraja katika saa za majonzi kwa kuwapo wengine, wala si kwa maongezi yao ambayo huelekea kutuudhi tu. Wakakaa wakivuta tumbako, na mimi nilisimama mbele ya moto nikivuta tumbako pia na kuwaangalia.


Halafu kidogo nilisema, ‘’Je rafiki zangu wa zamani, tangu tuliporudi toka nchi ya Ukukuana hata leo, miaka mingapi imepita? ‘’Bwana Good akasema, ‘’Miaka mitatu. Kwa nini unauliza?’’.

Nikajibu, ‘’Nauliza kwa sababu nafikiri ya kuwa muda niiokaa pamoja na watu mijini umenitosha kabisa, Nitarudi mwituni tena.’’

Hapa Sir Henry alikipeleka nyuma kichwa chake, akacheka mcheko wake wa kindani, akasema, ‘’Ama ni ajabu sana, sivyo Good?’’

Bwana Good akaniangalia, na huku anacheka katika rodi yake, kama kwamba anaficha siri, akasema, ‘’Ndiyo, ajabu sana ajabu kweli kweli.’’

Mimi ni mtu asiyependa mafumbo na mambo ya sirisiri, basi niliwatazama mmoja mmoja, kishanikasema, ‘’Siwezi kufahamu vizuri,’’

Sir Henry akasema, ‘’Hufahamu? Basi, nitaeleza. Good na Mimi tulipokuwa tukija hapa tuliongea.’’

Nikayakatiza maneno yake kwa ukali kidogo, nikasema, ‘’Nadhali kama Good alikuwapo, hamkosi mliongea maana Good ni mtu apendaye sana maongezi. Je, mliongea habari gani?’’

Sir Henry, akauliza, ‘’Ee wafikiri tuliongea habari gani?’’
Nikatikisa kichwa changu.

Haiwezekani nikajua Good aliongea nini, maana mara nyingi huongea habari za mambo mengi.

Sir Henry akasema, ‘’Tuliongea juu ya shauri dogo nililoliwaza yaani kama wewe utakubali tutafunga mizigo yetu na kuiendea nchi ya Afrika kufanya safari nyingine,’’

Nilipoyasikia maneno yake, nilishtuka sana, nikasema, ‘’Ni kweli usemayo?’’ akajibu, ‘’Ni kweli, na Good naye amekubali pia, sivyo Good?’’
Na yeye akaitikia, ‘’Ndiyo.’’

Basi, Sir Henry akaendelea, na sauti yake ilionyesha namna anavyoona hamu, akasema, ‘’Nami pia nimechoka kukaa bure kiubwana katika nchi iliyokinai mabwana.

Kwa muda wa mwaka mzima na zaidi nimekuwa nikitukutika kama tembo mzee anusaye batari.

Kila mara ninaota ndoto za nchi ya Ukukuana, na bibi kichawi Gagula, na Mashimo ya Mfalme Sulemani. Nakuambia ya kuwa nimenaswa na hamu nisiyoweza kuieleza.
Aisee, kumbe ma legend wote wapo ndani [emoji39] [emoji39]

Team imetimia
 
Nimechoka kupiga kanga na kwale, na sasa nataka kuwinda wanyama wakubwa. Mwaka ule mmoja tuliokaa pamoja katika nchi ya Ukukuana huonekana kama kwamba thamani yake inapita thamani ya jumla ya miaka yote ya maisha yangu.

Labda ni mpumbavu kwa hamu ninayoiona, lakini sina nguvu kuishinda, natamani kwenda, tena sina budi kwenda.’’ Basi alisita kidogo, kisha akaendelea..

‘’Tena, kwa nini nisiende? Sina mke wala baba, wala mama, wala mtoto wakunizuia nisiende. Nikipatikana na ajali, cheo changu na Mali itarithiwa na ndugu yangu George na mwanawe, nao watairithi kwa vyovyote.

Mimi si kitu kwa mtu yeyote.’’ Akasema,
‘’Ah! Nilifikiri utasema hayo. Na wewe Good, mbona wewe unataka kusafiri, unayo sababu?’’

Bwana Good, akasema na huku anajizuia asicheke, ‘’Ndiyo, ninayo sababu. Mimi sifanyi neno bila kuwa na sababu. Lakini ukitaka kujua sababu ya kweli, nitakwambia, ingawa sipendi kukuambia. Ninaanza kuwa mnene zaidi!’’


Basi, nilitia moto kikoni, maana ulikuwa umezimika, ndipo niliposema tena, nikauliza, ‘’Ninyi mmepata kusikia habari za mlima Kenya?’’

Bwana Good akajibu, ‘’Sipajui mahali hapo.’’
Nikauliza tena, ‘’Mmepata kusikia habari za kisiwa kiitwacho Lamu?’’
Bwana Good akajibu, ‘’La.

Ngoja si mahali palipo kaskazini ya Unguja kadiri ya maili mia tatu?’’
Nikasema, ‘’Ndipo. Sikilizeni. Shauri langu ni hili.

Twendeni Lamu, na kutoka huko tutasafiri ndani ya nchi kadiri ya maili mia mbili na hamsini mpaka mlima Kenya. Kutoka mlima Kenya tuendelee mbele tena kusikia habari zake. Kumbuka Mashimo ya Mfalme Sulemani.’’


Kadiri ya majuma kumi na manne yamepita tangu tulipoongea hivyo, na sasa habari hizi zinatokea katika mahali pa namna nyingine kabisa.

Baada ya kufikiri na kuhojiana sana habari, tuliona ya kuwa itafaa kuianza safari yetu kuuendea mlima Kenya mahali karibu na mlango wa mto Tana, wala si Mombasa.

Basi, ikatokea ya kuwa tulipofika Lamu, tuliteremka pwani pamoja na vitu vyetu vyote, na kwa kuwa hatukujua mahali pa kwenda, tulikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Bwana Balozi wa Serikali ya Kiingereza, tukapokewa kwa ukarimu.


Lamu ni mahali pageni kabisa, lakini mambo yanayodumu katika fikira zangu hata leo ni uchafu wake na uvundo wake. Hasa uvundo wake ni mno. Mbele ya jumba la Bwana Balozi ni pwani, au tuseme fungu la matope liitwalo pwani.


Maji ya bahari yapwaapo huacha nafasi wazi , ndipo mahali panapotupwa taka zote za mji. Pia, hapo wanawake huja wakafukia nazi katika matope na kuziacha humo mpaka makumbi yaoze, ndipo huja kuyafukua na kuzitumia nyuzinyuzi zake, yaani usumba, kutengenezea busati na vitu vinginevyo.


Kwa kuwa mambo hayo yameendelea kwa vizazi na vizazi, ni heri hali ya pwani hiyo ilivyo iwaziwe tu kuliko kuelezwa. Katika siku za maisha yangu nimepata kunusa harufu mbaya nyingi, lakini harufu kali iliyotoka pwani ya Lamu tulipokuwa tumekaa juu ya gorofa ya Bwana Balozi inazifanya zote ziwe kama si kitu kabisa.

Si ajabu ya kuwa watu hushikwa na homa Lamu. Lakini hata hivyo mahali hapo pana uzuri wa namna yake ingawa labda utamchosha mtu upesi.

Basi, tulipokwisha kula, tulikaa tukavuta tumbako, na rafiki yetu Balozi mkarimu aliuliza, ‘’Je, ninyi mabwana mnakwenda wapi?’’

Sir Henry akajibu, ‘’Tumekusudia kuuendea mlima Kenya, kisha, kuendelea mbele mpaka mlima Lekakisera. Quatermain amesikia hadithi ya kuwa liko taifa la watu weupe wanaokaa katika nchi za mbali zisizojulikana bado, kupita huko.’’

Bwana Balozi aliyatega masikio yake, akajibu ya kuwa hata na yeye amepata kusikia habari kama hizo.

Nikamuuliza, ‘’je, umesikia nini?’’ Akajibu, ‘’Si nyingi, ila najua ya kuwa zamani, kadiri ya mwaka mmoja, nilipata barua kwa Bwana Mackenzie, mtu wa misioni anayekaa mahali mwisho wa mto Tana panapofikiwa na mitumbwi, naye alitaja habari hizo.’’

Nikamuuliza, ‘’Je, unayo barua hiyo?’’

Akasema, ‘’La, niliitatua; lakini nakumbuka alisema ya kuwa mtu mmoja alifika kwake akasema kwamba alikwenda mbali kadiri ya safari ya miezi miwili kupita mlima Lekakisera, ambao hapana mtu mweupe aliyeufikia yaani kwa kadiri nijuavyo mimi akavumbua huko ziwa liitwalo Laga.

Kisha akaendelea upande wa mashariki ya kaskazi, safari ya mwezi mzima kuvuka jangwa na mbuga na milima mirefu, mpaka alipofika nchi wanapokaa watu weupe wakaao katika nyumba za mawe.

Huko alipokewa kwa ukarimu akakaa kwa muda, mpaka makuhani wa nchi ile walipo chochea habari ya kuwa yeye ni shetani, basi watu wakamfukuza, akasafiri muda wa miezi minane hata akafika mahali alipomkuta Bwana Meckenzie anakufa.
Mbona na hii inaonekana ni kali sana? Safi
 
Back
Top Bottom