Hai: Aliyekuwa Diwani wa CHADEMA aachiwa huru kwa tuhuma za kumbaka Mwanafunzi baada ya DNA kuonesha Mtoto aliyezaliwa sio wake

Hai: Aliyekuwa Diwani wa CHADEMA aachiwa huru kwa tuhuma za kumbaka Mwanafunzi baada ya DNA kuonesha Mtoto aliyezaliwa sio wake

Mahakama ya Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, imemwachia huru diwani wa zamani wa Masama Mashariki (CHADEMA), John Munisi, ambaye alikuwa akikabiliwa na kesi ya kubaka na kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari Marire.

Akisoma hukumu hiyo Leo, Hakimu Mkazi wa Wilaya hiyo, Jasmin Abdul amesema mahakama hiyo haijamtia hatiani mshtakiwa huyo katika makosa mawili yanayomkabili, kwa kuwa vipimo vya sampuli za vinasaba (DNA), kuonyesha mtoto aliyezaliwa, hakuwa mtoto wa mshtakiwa.

Aidha, hakimu huyo amesema kwa kuwa mtoto aliyezaliwa si wa mshtakiwa, mahakama hiyo haioni sababu ya kuamini kwamba mshtakiwa alimbaka mwanafunzi huyo, hivyo inamwachia huru.

Awali, ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Lebulu Mbise, kuwa mshtakiwa alitenda makosa hayo kwa nyakati tofauti.

Anadaiwa alitenda kosa la kwanza katika Kijiji cha Ngira, Wilaya ya Hai, kwa kumbaka mwanafunzi huyo Aprili 4, mwaka 2019, kosa alilotenda akijua ni kinyume cha sheria.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo, kinyume na kifungu 130 (1) (2) na kifungu 131 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura 16 ya Sheria iliyofanyiwa Marejeo Mwaka 2000.

Aidha, ilidaiwa pia mahakamani hapo kwamba, mshtakiwa alitenda kosa la pili katika kijiji hicho hicho, kwa kumpa ujauzito mwanafunzi huyo Aprili, kinyume na Sheria ya Elimu, kifungu cha 60 (A) (2) na (3) iliyofanyiwa Marejeo Mwaka 2002.

Katika ushahidi wa shahidi muhimu wa kesi hiyo ambaye ni mwanafunzi, alidai mahakamani hapo wakati akitoa ushahidi wake kwamba, hakuwahi kufanya ngono na mtu mwingine yoyote maishani mwake, tofauti na mshtakiwa huyo.

Wakati mshtakiwa Munisi, akitoa utetezi wake akiongozwa na Wakili Elia Kiwia, alidai hakuwahi kuwa na uhusiano wowote wa kimapenzi na mwanafunzi huyo, wala hakuwahi kufanya ngono naye.

Mshtakiwa huyo alijitetea kwamba alibambikiziwa kesi hiyo, baada ya kiongozi mmoja, kumlazimisha ajiunge na Chama Cha Mapinduzi (CCM) alipokataa, ndipo akambambikizia kesi hiyo namba 127 ya mwaka 2019.

Chanzo: IPP MEDIA
Hizi chuki na visasi vya kisiasa vinaondoa utu na ubinaadamu wetu kama watanzania, hapo lazima mwanaccm alikua injinia wa huo mchezo
 
Mungu ameamua kuliponya taifa kwa udhalimu huu yaani siasa hizihizi zinatesa watu hivi, tuome sana toba ukatili na kuoneana ni kitu kibaya sana , nakumbuka wale wanaume waliolawitiwa kwa nguvu huku wamelekezewa mitutu ya bunduki Zanzibar hizi zooote ni laana tombe sana toba
 
Inamaana mwanafunzi aliyebakwa hatapata haki yake?

Si mwanafunzi kabakwa?

Japo hajabakwa na mtajwa hapo awali ila yupo aliyembaka,atafutwa basi.

Kwa maelezo ya mbakwaji ni kuwa hajawahi shiriki ngono na mtu mwingine zaidi ya mtuhumiwa, sasa hapo unataka asakwe mtu hewa?!
 
Baada ya kufanya unyama huu MATAGA wakamwita shujaa wa Africa
 
Mnaosema jamaa alibambikiwa kesi mnataka kusema alitafutwa binti mwenye mimba ambaye ni underage spesho kwa ajili ya hili tukio?

Mnajua ni ngumu kiasi gani ubambikaji kua deal ya wengi hivyo?

Mimi naamini jamaa kamega. Isipokua kama ubambikaji basi ulifanywa baada ya kujulikana kwamba kamega. Hata hivyo inaonyesha binti ana attitude ya umri ni namba tu so alianza shows mapema.
Kwa maelezo ya huyo binti kwa mujibu wa taarifa hii ni kuwa aliieleza mahakama hajawahi shiriki ngono na mtu mwingine tofauti na mshitakiwa maishani mwake, kwa maelezo hayo logically ni kuwa kama DNA results zinakataa kuwa huyo si baba wa mtoto basi na kosa la ubakaji automatically linakufa.
 
Alibaka au alifanya tu kwa makubaliano ila ndio ikawa hivyo

Kubaka mtu yeyote au kufanya kwa makubaliano na underage, mwanafunzi wa shule ya msingi au sekondari ni kosa kwa mujibu wa sheria mkuu,
Hii ishu inafikirisha Sana inanikumbusha ishu ya akina babu seya inawezekana na wao walibambikiwa ile kesi yao ushahidi ukatengenezwa kutumia wale watoto Ila nayo ni ngumu Sana kuukubali kwa umriwa wale watoto.
Suala la kubambikiwa mimba /watoto kitaa lipo Sana.
Ila hizi roho za kuamua kuwasingizia watu kesi za uongo ni hatari tuombeane Mungu tu haya maisha sikuhizi yamekuwa hatarishi lolote linaweza kukutokea katika maisha ukabaki unashangaa.
 
Yes... Adai fidia itakayotoa fundisho kwa Mataga! Mwendazake angekua hai Mwamba Angeozea Kisongo!
Sasaiv haki zitapatikana, maana waliyekuwa wanamuogopa kama Mungu mpaka wananyima watu haki zao ili wamfurahishe yupo futi 6 chini kimyaaa
 
Kwa maelezo ya huyo binti kwa mujibu wa taarifa hii ni kuwa aliieleza mahakama hajawahi shiriki ngono na mtu mwingine tofauti na mshitakiwa maishani mwake, kwa maelezo hayo logically ni kuwa kama DNA results zinakataa kuwa huyo si baba wa mtoto basi na kosa la ubakaji automatically linakufa.
Unaweza ukambaka mtu na usimpe ujauzito mkuu.
Ila kwenye hii kesi inaonyesha mahakama waliamua kuweka burden of proof kwenye mimba./mtoto ( kupima dna akizaliwa) na sio kwenye kitendo Cha ubakaji kutokana na masuala ya muda
Inawezekana labda ni kweli huyo diwani alikuwa anatembea na huyo binti pamoja na watu wengine na huyo binti akapewa ujauzito na mtu mwingine sio diwani.
Maelezo ya binti kwamba hakuwahi kutembea na mtu mwingine zaidi ya diwani ninayatilia Shaka.
Mkemia mkuu wa serikali alihojiwaga akasema uhakika wa vipimo vya dna vya ofisi yake majibu yake ni sahihi kwa asilimia 99 na matokeo yao hayajawahi kutofautiana hata wakirudia.
 
Upinzani umepitia magumu sana kwenye utawala huu, hivi wale waliokua wanajiona miungu watu baada ya kufariki mtukufu wao watakua kwenye khali gani sasa🤔🤔
 
Katika ushahidi wa shahidi muhimu wa kesi hiyo ambaye ni mwanafunzi, alidai mahakamani hapo wakati akitoa ushahidi wake kwamba, hakuwahi kufanya ngono na mtu mwingine yoyote maishani mwake, tofauti na mshtakiwa huyo.
Kwahiyo walikuwa wakifanya ngono na si kubakana
 
Tanzania ilipita katika kipindi kibovu kuliko wakati wowote.
 
Mahakama ya Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, imemwachia huru diwani wa zamani wa Masama Mashariki (CHADEMA), John Munisi, ambaye alikuwa akikabiliwa na kesi ya kubaka na kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari Marire.

Akisoma hukumu hiyo Leo, Hakimu Mkazi wa Wilaya hiyo, Jasmin Abdul amesema mahakama hiyo haijamtia hatiani mshtakiwa huyo katika makosa mawili yanayomkabili, kwa kuwa vipimo vya sampuli za vinasaba (DNA), kuonyesha mtoto aliyezaliwa, hakuwa mtoto wa mshtakiwa.

Aidha, hakimu huyo amesema kwa kuwa mtoto aliyezaliwa si wa mshtakiwa, mahakama hiyo haioni sababu ya kuamini kwamba mshtakiwa alimbaka mwanafunzi huyo, hivyo inamwachia huru.

Awali, ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Lebulu Mbise, kuwa mshtakiwa alitenda makosa hayo kwa nyakati tofauti.

Anadaiwa alitenda kosa la kwanza katika Kijiji cha Ngira, Wilaya ya Hai, kwa kumbaka mwanafunzi huyo Aprili 4, mwaka 2019, kosa alilotenda akijua ni kinyume cha sheria.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo, kinyume na kifungu 130 (1) (2) na kifungu 131 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura 16 ya Sheria iliyofanyiwa Marejeo Mwaka 2000.

Aidha, ilidaiwa pia mahakamani hapo kwamba, mshtakiwa alitenda kosa la pili katika kijiji hicho hicho, kwa kumpa ujauzito mwanafunzi huyo Aprili, kinyume na Sheria ya Elimu, kifungu cha 60 (A) (2) na (3) iliyofanyiwa Marejeo Mwaka 2002.

Katika ushahidi wa shahidi muhimu wa kesi hiyo ambaye ni mwanafunzi, alidai mahakamani hapo wakati akitoa ushahidi wake kwamba, hakuwahi kufanya ngono na mtu mwingine yoyote maishani mwake, tofauti na mshtakiwa huyo.

Wakati mshtakiwa Munisi, akitoa utetezi wake akiongozwa na Wakili Elia Kiwia, alidai hakuwahi kuwa na uhusiano wowote wa kimapenzi na mwanafunzi huyo, wala hakuwahi kufanya ngono naye.

Mshtakiwa huyo alijitetea kwamba alibambikiziwa kesi hiyo, baada ya kiongozi mmoja, kumlazimisha ajiunge na Chama Cha Mapinduzi (CCM) alipokataa, ndipo akambambikizia kesi hiyo namba 127 ya mwaka 2019.

Chanzo: IPP MEDIA
Kwa ushauri wangu, tuungane tuishauri serikali kuangalia upya sheria zetu za jinai ili watuhumiwa wanaobambikiwa makosa kwa sababu binafsi ikithibitika mahakamani bila mashaka yoyote kuwa mtuhumiwa kabambikiwa kosa x na y, basi sheria iseme kosa hilo linaenda (kama lilivyo) kwa mtu aliyebambikia (y) na ndiye atakayetumikia adhabu ya kosa hilo. Kwa maoni yangu, kufanya hivi kutaleta haki zaidi katika utoaji haki.
 
hiyo mimba ilitoka wapi sasa na wakati hajawahi kufanya mapenzi na mtu yoyote?
Je wewe unaamimi au una ushahidi wowote wa uhakika kuwa kweli huyo binti hajawahi kufanya mapenzi na mtu mwingine yeyote zaidi ya huyo mshtakiwa??!!
 
Sidhani kama Mwendazake atakaribia hata geti la mbinguni. Wale wote aliokuwa akiwatumia kutesa wapinzani kina Ole Sabaya na Gumbo wamebaki hawajui kesho yao maana ngao waliyoitegemea haipo tena.
 
Alibaka au alifanya tu kwa makubaliano ila ndio ikawa hivyo
Kasomi au Kajinga? Vile kabisa tuseme hujui maana ya kubaka inapohusu watoto? Mtu chini ya miaka 18 ni mtoto. Anawaza, kunena na kutenda kitoto. Hata kama amekutongoza yeye umebaka!
Kwa dhana hiyo miaka 30 inakuhusu. Yule jamaa aliyesema majaji wetu wanakopi na kupeisti naye alikuwa mbumbumbu wa hiyo dhana. Isipokuwa kiaina. Fataki wale miaka jela. Mabinti wasirudi shule. Hasomeshi wazazi bure. Fataki alibaka kwa dhana ya mtoto. Mzazi wa mimba za utotoni alitaka mwenyewe kwa ujinga wa Kasomi! Hapo chacha(sio mura!).
 
Back
Top Bottom