Haijawahi tokea, Mwana FA na AY kulipwa bil 2 tshs na Tigo

Haijawahi tokea, Mwana FA na AY kulipwa bil 2 tshs na Tigo

Daaah!!!! itakuwaje kwa ma DJ katika kumbi za starehe na sherehe maana nao wanaingiza faida, nauliza tu
 
Okay, hakukuwa na contract, kwa hiyo unaamua kucharge kiasi chochote?

Bila kuangalia hasara iliyosababishwa?
wizi ni wizi tuu..ndio maana mwizi wa kuku anapigwa mawe mpaka kufa kwa kosa kiduchuuu..mwizi wako akiingia anga zako unaweza kumchezea unavyotaka..hapa kuna charges nyingi sana za production wanaweza kuchomeka..coz hakukua na mkataba na tigo hawajui ni charges kiasi gani wasanii hao walitumia ku-produce miziki yao..
 
Dah wewe jamaa unampenda sana Diamond.. Huu sio ushabiki haya ni mahaba.

Kwani unaujua utajiri wa AY wewe? Akiongeza hiyo B? Punguza mahaba mkuu wewe mtoto wa kiume, watu tunamkubali Chibu ila sio kiivyo.
Hivi hata anajua AY na mwana FA wamekuwa kwenye hili game kwa muda gani? Wengine walikuja na kuondoka, wao wanafanya yao
 
sasa tusubir tigo watakavyotukata salio na vifurush vitazid kupanda da maana tg ni wez balaaa
 
Hivi hata anajua AY na mwana FA wamekuwa kwenye hili game kwa muda gani? Wengine walikuja na kuondoka, wao wanafanya yao
note.. kuwa kwenye game muda mrefu sio kigezo cha kua tajiri mkubwa.. kuna matajiri wengi vijana wamelipuka ghafla kama mmiliki wa facebook etc.. kuwa tajiri ni ubunifu na akili lukuki, kubwa na pana.. kama za huyu SIMBA(diamond) alivyowanyonga hao wakongwe..
 
note.. kuwa kwenye game muda mrefu sio kigezo cha kua tajiri mkubwa.. kuna matajiri wengi vijana wamelipuka ghafla kama mmiliki wa facebook etc.. kuwa tajiri ni ubunifu na akili lukuki, kubwa na pana.. kama za huyu SIMBA(diamond) alivyowanyonga hao wakongwe..
Wewe Wasema.
 
Hio billion 2 kwa tigo ndogo sana,,, tigo wana Wateja kama milioni 5 nchi nzima ...kila mtu akiingiza jero ndo hela itayotumika kuwalipa kina ay then siku ya pili mambo yanaendelea
 
Okay, hakukuwa na contract, kwa hiyo unaamua kucharge kiasi chochote?

Bila kuangalia hasara iliyosababishwa?
Hasara iliyosababishwa ni sawa na hicho kiasi 2.18b wanazodai hao jamaa, tena nadhani hicho kiasi kinaweza kuwa kidogo sana.
 
Usitegemee mambo kuisha kirahisi hivyo yangeshaisha mbona. Albert Msando mwanasheria wao yupo vizuri alimtoa knock out Lissu mchana kweupee.
Umeongea vizuri ila umemaliza kikanjanja,toka lini Msando alimtoa Lissu kwa Knock out mchana,Msando alikua anamsimamia Zitto asivuliwe uanachama wa Chadema,na Lissu alisimama upande wa CDM,na mwisho wa siku nani alishinda ile kesi?,CHADEMA chini ya Lissu walishinda kesi ndio maana Zitto alivuliwa uanachama,sasa unaleta ukapuku hapa wa kudanganya watu kwa taarifa zako za kuungaunga toka kwenye vikaratasi vya vidaftari vya mistari mikubwa na midogo hapa,acha uongo!
 
Ina maana watu hamjasoma kuwa tigo imekata rufaa?
 
Back
Top Bottom