Timu za Tanzania ili zishinde zinahitaji mambo manne
1. Kocha mzuri wa kufundisha formation ambayo huonyeshwa kwenye screen ya Azam TV kabla ya mechi kuanza lakini wakishaanza kucheza wanajichanganya woote kukimbiza mpira hakuna tena zile 4-4-2 wala 1-1-2
2. Lazima awepo Tajiri au kundi la mapedeshee wenye hela zao ambao watakuwa wanawalipa wachezaji na kutoa fungu kwa kamati mbalimbali ikiwemo kamati ya ufundi na kamati ya kwakirimu marefa na fedha zinazopatikana kwenye viingilio na mashindano zikitafunwa na wajanja
3. Lazima kuwepo na kamati ya wanamalunde a.k.a Kamati ya ufundi ambapo huicheza mechi kabla haijechezwa na matokeo kujulikana. Hapa mchezaji atazingatia zaidi alichoambiwa na kupewa na kamati kuliko kocha wake ili apate ushindi. Iwe taulo sawa!!! iwe irizi twende kazi
4. Lazima awepo mtu wa kubwabwaja " msemaji" ambaye atakuwa ni mropokaji huyu na kujibizana kwa kejeli na wasemaji wa klabu nyingine. Hii hutia hamasa kwa wachezaji na mashabiki hujaa uwanyani kushuudia tambo za msemaji kama zinakuwa kweli.
Hali walionayo Yanga sasa hivi 1. Hawana pedeshee mwenye kutoa mamilioni baada ya pedeshee manji kujitoa 2.Hawana mropokaji mwenye uwezo wa kucheza vita ya maneno na akina MANARA, KIFARU , NA BWIRE. JERY MURO NDIO ALIKUWA KIBOKO WA MANARA. Sijui ni kwanini yanga walimtimua. Alikuwa na uwezo wa kutengeneza morali na ikawa kweli sasa Manara kabaki mwenyewe hana mpizani na timu inachukua tambo zake na kuimarika kisakolojia