Haji Manara kulipwa mshahara laki 7 ni aibu na unyonyaji, arekebishiwe

Haji Manara kulipwa mshahara laki 7 ni aibu na unyonyaji, arekebishiwe

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
1626956524606.png



Najaribu tu kuwaza,kwamba Klabu ya simba inalipa wachezaji, benchi la ufundi, n.k mamilioni ya pesa,ina mdhamini wake ni tajiri kabisa hapa Afrika lakini leo nimepigwa na bumbuwazi bada ya mambo kuwa wazi kwamba msemaji mkuu wa simba analipwa hela ndogo ambayo hailingani na hadhi na mchango wake ndani ya klabu, kumlipa manara laki 7 si haki hata kidogo.

semeni yoote lakini manara amekuwa wa faida sana simba, ameipambisha sana hiyo timu yenu na kuwatia moyo hata wakati mlipokuwa mnakata tamaa. kwahiyo mshahara kama ndio huo mnampa jueni anajitolea tu hapo. kuweni na utu. ondoeni mtu huyo mmuweke mwingine muone kama ataleta hamasa kama anazoleta huyo kwenye klab ya simba.


Nadhani hii ilikuwa ni kama bakora pale manara alipokataa kusaini mkataba wa milioni kuwa rasmi mwajiriwa wa simba, Ila manara hakuwa kichaa kuuacha huu mkataba, aliuacha mkataba kwasababu ungemfunga asipate dili kutoka makapuni mengine, Ikumbkwe kwa sasa licha ya manara kupokea hio laki 7 kutoka simba, bado ana mikataba minono kutoka gsm, bakhresa, asas, n.k hii mikataba imemfanikisha mpaka ana nyumba yake na gari zake, kiufupi hii mikataba inamlipa vizuri sana, Hio milioni 4 ya simba ilikuwa ni ofa nzuri lakini kitendo cha kumfunga manara asitoke nje ya simba hicho kipengere kingempunguzia manara mapato.


Hata simba inapocheza wengi huwa wanafatilia manara kasema nini wenye press confrence, mitandao ya jamii, n.k. wengine hata page za simba hawafatilii wao wanafata page ya manara wa updates zote za simba, manara ana followers weng kuzidi hata page za simba.mbaya zaidi simba ikifungwa iwe ni mtani ama klabu nyingine basi mtu wa kwanza kushambuliwa na hizo timu huwa ni manara, maana ni kama kitovu kikuu cha brand ya simba, hatashambuliwa mo, hatashambuliwa mchezaji, hatashambuliwa kocha, hatashambuliwa babra, ni manara ambae anashambuliwa.

Kinachoonekana wazi ni kuwa, viongozi wa Simba wakiongozwa na MO na Babra, hawapendezwi na Manara kufanya kazi na makampuni ya nje, wanataka manara afanye kazi za simba tu na kama mnavyojua simba mfadhili ni MO kwahio wanataka kumtega manara atangaze kampuni zinazotengeneza bodhaa za MO, hawataki manara afanye kazi kwa makampuni mengine kama kuwa balozi wa gsm, azam au asas, kwahio wakaamua kuutumia huo mshahara wa laki 7 kama bakora ya kukaidi ofa ya kitumwa.

Na hicho ndicho kimemponza.

anamapungufu yake lakini kazi anayofanya ni kubwa kwakweli......he deserves more
 
Sote tunaujua mchango wa manara katika soka letu la hapa nchini...
Fvck this shit of manara kailetea simba mahudhurio. Kipindi kile cha mtani jembe alikua anajaza uwanja nani? Simba yenyewe ikifanya vizuri inavuta mashabiki sio ishu ya manara. Tena sasa hivi kuna mitandao ya kijamii sio ishu tena, ukiingia page za timu tu inashawishika. Manara aache ujinga wa kujifanya kabla yake simba haikuwapo. Nimemjua manara baada ya kuja simba.

Suala la malipo manara kawekewa mkataba mezani wa zaidi ya hiyo laki saba mpaka leo hajausaini sababu akiamini anastahili zaidi, kaamua kwenda na huo wa posho laki saba na kisha atumie kama kigezo cha anajitolea simba.

Hii ya kumchimba biti boss kachemka sana eti utaondoka simba, umenikuta...who the fvck is he? Kesho atamvimbimbia try again, magori au hata Mo.
 
Sote tunaujua mchango wa manara katika soka letu la hapa nchini.

Ni mtu mwenye taaluma na kipaji cha aina yake kinachofanya simba ipige hatua hasa linapokuja swala la kuhudhuria michezo uwanjani, kunogesha ushabiki, kuchangamsha derby, n.k

Sasa kweli mtu kama huyu analipwaje laki 7 aisee, hivi ni vituko kwakweli.
Muachien timu haji manara alaf mlipen milion 10 alaf wachezaj sajili wa lak saba saba ,muone kama mutapga iyo hatua, munaacha muwasifu wanaiofanya simba ipge hatua munawapa sifa wengine ,

shabik akimua aende uwanjan mara nyng anaenda akiamua na sana ikiwa timu inafanya vzur sio kwa ajir ya haji na aya maneno yenu ndio yanamjaza kichwa anazalau wenzio inawezekana vp taasisi kama ya simba kusitokee mgongano suhala ni kumalza pasipo kutokea kama aya sasa kila ktu anaenda mtandaon mwsho wake nn ata kama analipwa lak anastahili mbona asem na posho zake na babra sio mlipaj

Hiyo mishahara yeye ni mtendaj anafanya aliyoagizwa na bodi manara anafanya kaz uyu ceo wa tatu je kama wote walikua wanampa iyo lak saba ambayo anaona ndogo aliamua nn ,au babra ndio kashusha mshahara wake ,ana mtuhumu ceo ampend kisa anamuhusisha kuhujum timu ,ukiangalia pia kuna ukwel fikiria una siku 3 kwenda ktk mechi tena final na sio final tu ni ya watan alaf unaleta jambo kama ili watu watakuelewaje ,yote kwa yote migogoro ya ya wafanyakaz inamalzwa na viongoz ikishindikana unaacha kaz ukianza kuchafua watu bas ww ndio una shida
 
Siku mishahara Yanga iwekwe hadharani Dah titatafutana akiyanani
Acha kuhamisha magoli! Mada inamuongelea Haji Manara, Msemaji Mkuu wa Simba kulipwa mshahara wa laki 7 kwa mwezi!

Toa maoni yako kama huu mshahara unamtosha, au la! Binafsi naona unamtosha sana!!

Ndiyo maana frustrations hazimuishi! Kila anayemuona mbele yake, anataka tu kumparamia!! Kwa huku vijijini, laki 7 ni nyingi sana! Ila kwa Dar, nadhani hiyo ni hela ya mboga tu! Bado chakula, maji, kodi, ada ya watoto, nk.
 
Acha kuhamisha magoli! Mada inamuongelea Haji Manara, Msemaji Mkuu wa Simba kulipwa mshahara wa laki 7 kwa mwezi!

Toa maoni yako kama huu mshahara unamtosha, au la! Binafsi naona unamtosha sana!!

Ndiyo maana frustrations hazimuishi! Kila anayemuona mbele yake, anataka tu kumparamia!! Kwa huku vijijini, laki 7 ni nyingi sana! Ila kwa Dar, nadhani hiyo ni hela ya mboga tu! Bado chakula, maji, kodi, ada ya watoto, nk.

Kwanza hakuna mshahara unaotosha. Pili yeye anajua hio Ndio stahili inaomfaa. Hivi ana diploma kweli au ana piga domodomo apate kwenda msalani.
Sasa anaondoka Simba aone kama hajaachwa tena na mke huyu.
 
Back
Top Bottom