Haji Manara punguza kuitaja Simba kwenye kila press na maongezi yako

Haji Manara punguza kuitaja Simba kwenye kila press na maongezi yako

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Binafsi nadhani kila mtu keshajuwa kwanini uko Yanga Sasa. Hakuna sababu ya kuendelea kuitaja Simba katika kila fursa ya kwenda hewani. Ubongo wa Binadamu una tabia ya kuchoshwa (fed up) na kitu kinachojirudiarudia kila wakati, hata harufu ya chooni inapotea puani kama utakaa chooni kwa muda mrefu.

Hebu jikite kwenye club yako mpya ya yanga Sasa wakati huu wa maandalizi ya kuanza msimu mwingine, uchaguzi na mabadiliko.

Kuendelea kuikosoa Simba ni njia nyingine ya wazi ya kuitaka Simba irekebishe makosa yake ili ifanye vizuri kuizidi Yanga, hii ndiyo sababu ya wahenga kusema aliyelala usimwamshe ukimuamsha utalala wewe.

Sisi Wanayanga tunadhani kuwa unafanya hivyo ili kuiamsha Simba iliyolala. Maana bado moyo wako uko Simba, siku Barbara na mo wakiondka Simba unaweza kurudi Simba.

Utani uwepo lakini sio wa kila saa 24/7 kwa 365. Mipango ya Yanga Wacha iwe Siri ya Yanga na Simba Wana mipango Yao usiibeze. Mfano, unaposema huwezi kujenga uwanja kwa mchango wa buku buku wewe unaumia nini? Who are you to challenge their plans? Yaani unauza kwa Simba mipango ya Yanga ya namna yao ya kujenga uwanja au una maana gani?

Kila kitu lazima kiwe na kiasi. Iko siku watu watakustukia Haji mwanangu kwa ukosoaji wako huo wa Simba kwa kufananisha na mipango ya Yanga kwenye kila jambo, unauza Siri za Yanga kwa Simba kwa jina la utani wa jadi, haitakubalika kwa wanayanga.
 
Binafsi nadhani kila mtu keshajuwa kwanini uko Yanga Sasa. Hakuna sababu ya kuendelea kuitaja Simba katika kila fursa ya kwenda hewani. Ubongo wa Binadamu una tabia ya kuchoshwa (fed up) na kitu kinachojirudiarudia kila wakati, hata harufu ya chooni inapotea puani kama utakaa chooni kwa muda mrefu...
Alalaye usimwamshe, ukimwamsha utalala wewe
 
Manara moyo wake bado upo Simba.....ameumizwa sana kuondoka Simba.....bado anatibu maumivu ya kufukuzwa Simba....hana njia nyingine ya kuifurahisha nafsi yake iliyokarahishwa zaidi ya kuitukana Simba.....

Hivyo ndivyo anavyojitibu nafsi yake....Hali hiyo itakwenda ikipotea taratibu....nadhani viongozi wa Simba wameshalijua Hilo na ndio maana wamekaa kimya....

Wamegundua kuwa nyuma ya kejeli na matusi dhidi ya Simba kuna manufaa kwa Manara.....wameamua kumuacha apone...... inshallah siku moja atapona na atarudi kuwa kawaida.........
 
Manara wapelekee moto 🎵🎶 wapelekee moto moto 🎶🎵 wapelekee moto makolo 🔥🔥🔥🔥

Ila simba huwa mnatuchekesha, hii kazi ya ushauri mmeanza lini, yani kuna kipindi mkaanza eti kutushauri mambo ya kombe, dadeki Yani mke ni wangu halafu unanishauri jinsi ya kumgegeda, 😂😂😂.

Muwe wapole tu, Na vile mlivyo na hasira kwamba mabingwa hawajavunja rekodi yenu ya kukaa misimu mitano mfululizo 2012 hadi 2017 bila kombe, daah 😂😂.

Mabingwa tunatembea vifua mbele, Hii ndio yanga aisee, ni mwendo wa kufumua mishono tu..

Tunasubiri kukwapua F.A., Azizi mlieshindwa kumnasa kwa dau dogo anakuja kwa mabingwa wenye mkwanja, 😂😂 Dewji kafunga kiwanda chake cha mkonge huko sasa nikianza kufikiria makolo wanavyotoa pesa kwenye michangonya kiwanja isije ikawa mnachangia fidia za hasara za watu wenye biashara zao 😂😂

Dah, alafu nikifikiria Simba imenunuliwa milele ndio nacheka hadi machozi 😂😂
 
Manara moyo wake bado upo Simba.....ameumizwa sana kuondoka Simba.....bado anatibu maumivu ya kufukuzwa Simba....hana njia nyingine ya kuifurahisha nafsi yake iliyokarahishwa zaidi ya kuitukana Simba..
Haji hakuwa Simba kwa bahati mbaya TU, bali ni urithi wa Babu yake mzaa mama yake ambae alikuwa kiongozi mkubwa wa Simba. Sio kwamba ni jambo la utaniutani kwa Haji kuwa Simba na kuondoka Simba.
 
Manara wapelekee moto makolo 🔥🔥🔥🔥

Ila simba huwa mnatuchekesha, hii kazi ya ushauri mmeanza lini, yani kuna kipindi mkaanza eti kutushauri mambo ya kombe, Yani mke ni wangu halafu unanishauri jinsi ya kumgege*a, 😂😂😂.

Muwe wapole tu, Na vile mlivyo na hasira kwamba mabingwa hawajavunja rekodi yenu ya kukaa misimu mitano bila kombe kwa mara ya pili, daah 😂😂.

Mabingwa tunatembea vifua mbele, Hii ndio yanga aisee..

Tunasubiri kukwapua F.A
Utani unajulikana na chuki inajulikana tuombe radhi we kolokocho. Haiwezekani kila press ya mambo ya Yanga iwe na mambo ya Simba. Kila jambo zuri la Yanga lilinganishwe na jambo hilohilo la Simba.
 
Utani unajulikana na chuki inajulikana tuombe radhi we kolokocho. Haiwezekani kila press ya mambo ya Yanga iwe na mambo ya Simba. Kila jambo zuri la Yanga lilinganishwe na jambo hilohilo la Simba.
Manara utamchukia akiwa timu pinzani, akiwa timu yako ni burudani tu.

Kipindi manara akiwa simba hata yanga walikuwa wanalalamika hivi hivi.

Jamaa linajua kukera hiloo , ile mineno sijui anatoaga wapi huyu kiumbe, eti jezi za simba ni kama shuka la kihadzabe😂😂
 
Kuna haja ya kufufua hii kesi.
 

Attachments

  • 20220614_071533.jpg
    20220614_071533.jpg
    26.6 KB · Views: 8
Nakumbuka alivyokuwa akiwahamasisha yanga wakati Yuko simba kwa kuwaambia kuwa hawawezi kujaza uwanja kama simba yake yanga wakawa wanajitokeza kwa wingi
Hicho ndicho ninachosema mm. Haji anatumia njia nyingine za kuiimarisha Simba indirectly. Anakwenda kwenye redio, press na kwingineko kuelezea mipango miziri ya Yanga ili Simba wasikie kile kinachofanywa na Yanga.
 
Hicho ndicho ninachosema mm. Haji anatumia njia nyingine za kuiimarisha Simba indirectly.
ataimarishaje klabu iliyonunuliwa milele na watu ambao walikuwa wanamlipa laki 7 na kumuonea wivu umaarufu wake 😂😂😂

Manara ana hasira sana na makolo ndio maana anawapelekea moto mtindo moja,, ni moto tu
 
Binafsi nadhani kila mtu keshajuwa kwanini uko Yanga Sasa. Hakuna sababu ya kuendelea kuitaja Simba katika kila fursa ya kwenda hewani. Ubongo wa Binadamu una tabia ya kuchoshwa (fed up) na kitu kinachojirudiarudia kila wakati, hata harufu ya chooni inapotea puani kama utakaa chooni kwa muda mrefu...

Ushauri kuntu kabisa. Mzee Sunday Manara yuko wapi kumpa darsa kijana wake, Haji anajipaka mavi akiamini kuwa anajipulizia perfume
 

Attachments

  • JamiiForums1731448287.jpeg
    JamiiForums1731448287.jpeg
    47.4 KB · Views: 7
  • FB_IMG_1643091812708.jpg
    FB_IMG_1643091812708.jpg
    20.2 KB · Views: 7
  • FB_IMG_1630232080690.jpg
    FB_IMG_1630232080690.jpg
    86.6 KB · Views: 9
Manara utamchukia akiwa timu pinzani, akiwa timu yako ni burudani tu.

Kipindi manara akiwa simba hata yanga walikuwa wanalalamika hivi hivi.

Jamaa linajua kukera hiloo , ile mineno sijui anatoaga wapi huyu kiumbe, eti jezi za simba ni kama shuka la kihadzabe😂😂
Hiyo kauli ilisababisha Simba wakatafuta wapi Yanga wanatoa jezi zao
 
Back
Top Bottom