Haji Manara: "Simba ndio wa Kimataifa"

Haji Manara: "Simba ndio wa Kimataifa"

ngoja tumsubiri na huyo wa kimataifa aje.....hala hala tu.....uvumilivu unahitajika......hadj umesahau kuwa washabiki wenu mmewajenga kusikiliza zaidi POROJO kuliko FACTS Si ajabu hata ulichokizungumza hapo hakijaeleweka hata kwa hao washabiki maandazi.......nawasih nyote wawili muwe na uvumilivu
 
Hapa ni record za simba vs yanga.....Tp mazembe anaingiaje tena? Mnatafuta chaka?
Anajaribu tu kuonyesha kwama si sahihi kujifungia ndani sababu ya records bali ni wakati wa watu kutoka nje ya maboksi, yaani tuachane na tabia ya kuishi katika historia na tuanze kuuisgi uhalisia. Ni mzigo mkubwa kuishi na mzigo wa historia mabegani wakati haukusaidii chochote katika wakati tulio nao sas.

Ndiyo chanzo cha kuiongelea TP Mazembe ambayo haina kabisa huo mkeka wa historia
 
Katika Hali Isiyokuwa Ya Kawaida Msemaji Wa Klabu Ya Simba Haji Manara Leo Ameamua Kumpiga Vibaya Sana Kwa Knock Out Msemaji Wa Klabu Ya Yanga Jerry Muro Baada Ya Ubishani Mkubwa Wa Ni Timu Gani Kweli au Hakika Inastahili Kuitwa au Kujiita YA KIMATAIFA au WA KIMATAIFA Kutokana Na Rekodi Za KUTUKUKA Ilizonazo Hiyo Timu.

Hiki Ndicho Msemaji Wa Simba Alichokisema...........


Waungwana kila uchwao kwenye jiji hili na viunga vyake sambamba na maeneo mengi ya nchi, kuna neno wa ‘kimataifa’ hulisikia likiimbwa.

Waimbaji wakuu wa neno hilo ni mashabiki wa Yanga wakiongozwa na mpiga zumari wao aliyeacha kazi yake na kujigeuza muimbaji.

Kinyume chake hilo neno klabu ya Simba huitwa wa ‘mchangani’ au wa ‘matopeni’. Wengi wananilaumu kuwa kwa nini huwa sijibu neno lolote la ajabu kwa Yanga. Jibu langu ni jepesi tu, lazima tujitofautishe msemaji wa klabu na mropokaji wa klabu.

Mimi hupenda kuzungumzia issues sio porojo au lugha za uchochoroni. Haiwezekani nikawa kiongozi kisha nikaongea lugha za mashabiki ‘maandazi’.

Kwa hiyo mtaniwia radhi wapenzi wa mpira kwa kutokuwa muimbaji wa ngonjera za uchochoroni. Mara zote nitabaki msemaji wa klabu kubwa nchini na ntaongea facts kwa kadri zilivyo.

Wadau zisomeni sifa za kimataifa kwa klabu ya Simba nje ya nchi halafu zifananisheni na timu nyingine nchini.

Walau kama zitafikia nusu tunawaruhusu watafute tusi jipya. Ombi langu kwenu isambazeni taarifa hii katak kila mtandao wa kijamii kisha waseme wao wanaojiita wa kimataifa.

1. Simba ndiyo timu ya kwanza nchini kupanda ndege na hii ilikuwa mwaka 1963 tena wakati huo taifa la Tanzania halikuwa limeundwa, ilikwenda Ethiopia kwa mwaliko wa rais wa taifa hilo Haile Selassie

2. Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa jezi na hii ilikuwa 1938 ilipocheza na kombaini ya mabaharia wa meli zilizotia nanga kwenye bandari ya Dar es salaam.

3. Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa viatu nchini na hii ilikuwa1949 ilipocheza na kombaini ya jeshi la majini Navy ya Afrika Kusini.

4. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa na basi lake yenyewe na hili lilinuliwa mwaka1968.

5. Simba ndiyo timu ya kwanza kumiliki jengo lake lenyewe na hili lilizinduliwa 1971.

6. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa bingwa wa ligi kuu nchini1966.

7. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwakilisha nchi na hii ilikuwa 1967.

8. Simba klabu ya kwanza nchini kwenda Ulaya na hii ilikuwa 1974 ilipokwenda Poland

9. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa mabingwa wa Afrika Mashariki na kati na hii ilikuwa 1974.

10.Simba ndio mabingwa wa kihistoria wa Afrika Mashariki na Kati, ndiyo timu iliyochukua ubingwa mara nyingi kuliko klabu yeyote Afrika Mashariki na Kati (Champs off all time.)

11.Simba ndiyo timu pekee nchini iliyowahi kufika nusu fainali ya klabu bingwa Afrika na hii ilikuwa1974.

12.Simba ndiyo timu pekee nchini na Afrika Mashariki kufika fainali ya kombe la Caf na hii ilikuwa1993.

13.Simba ndio timu inayoshikilia rekodi Afrika kama si duniani kwa kufungwa na Mufurila Wonderers ya Zambia magoli 4-0 na kwenda kuibamiza 5-0 kwao, mbele ya rais wao Kenneth Kaunda. Hii haijafanywa na klabu yeyote Afrika na nina mashaka duniani, hii ilikuwa 1979.

14.Simba ilicheza katik hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika 2003 kwa mafanikio makubwa kulinganisha na timu yoyote nchini.

15.Simba ndiyo timu pekee kuivua ubingwa klabu bingwa Afrika nadi Zamalek hii ilikuwa pia 2003.

16.Simba ndiyo klabu pekee nchini kuzifunga timu zote za mataifa ya kiarabu kuanzia

· Waliowatoa mwaka jana Etoile du Sahel (Tunisia)

· Widad Casablanca (Morocco)

· El Setif (Algeria)

· El Harach (Algeria)

halaf tumezifunga timu zote kubwa za Misri Zamelek,Al Ahly, Arab Contractors, Ismailia, Mehala, Al kubra na timu nyingine mnajua huwa inafanywaje ikigusa kule.

Pia imeshaitoa El Merekh ya Sudan 1994 katak klabu bingwa ya Afrika. Simba pia imeshazifunga miamba ya Afrika Magharibi kuanzia Asec, Asante Kotoko, Hafia ya Guinea hata mabingwa wa kihistoria wa Zambia Nkana Red Devils.

17. Tukirudi juu Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa suti na hii ilikuwa 1974 ilipokwenda Poland.

18.Simba ndiyo klabu pekee nchini kujenga jengo lake yenyewe kwa nguvu za wanachama na mashabiki, wenzetu ni mkopo na msaada toka kwa mzee Karume100%, Simba ilipewa kiasi flan na mzee karume baada ya jengo kukamilika na hii ilikuwa mwanzoni mwa miaka ya 70.

19.Angalia idadi ya wachezaji wa Simba walioenda Ulaya kucheza soka la kulipwa.

· Nico Njohole

· Deo Njohole

· Kassim Matitu

· George Kulagwa

Huku ikiwa na makumi ya nyota wake kadhaa waliowahI kutapakaa sehemu mbalimbali duniani.

Nikutajie wachache.

· Khalid Abeid

· Haidar Abeid

· Martin Kikwa

· Athman Mambosasa

· Zamoyoni Mogella

· Hamis Gaga

· Lilla Shomari

· Iddi Pazi

· Kiwelu Mussa

· George Masatu

· Hussein masha na wengine wengi.bila kumsahau nguli wa sasa mbwana samata.mutoto ya msimbazi.

Na hapa kumbukumbu zikae vizuri wazee wangu mimi, Sunday na Kassim Manara wakati wanaenda kucheza Ulaya hawakuwa wachezaji wa Yanga, walikuwa wakicheza Pan African.

20. Nimalizie kwa kuwaambia FIFA ilizitaja timu bora za karne kwa kila nchi kwa Tanzania Simba ilitajwa ndio timu bora ya karne na wenye mpira wao FIFA. Nenda kwenye rekodi za Caf ndio utajua nani wa kimataifa baina ya cc na wao.

Porojo za mjini ntakuwa nimezimaliza sasa na anayebisha abishe kwa data. Wakoloni wetu walitufundisha hivi…No reaserch no data no right to speak.Tafsiri isiyo rasmi, hujafanya utafiti na huna takwimu funga bakuli lako.

Asanteni na nendeni mkawaambie.

Haji S Manara
Msemaji wa klabu bora ya muda wote Tanzania (best club of all time)
Ukiona errors zipotezee jadili issues na nnaruhusu challenges kama zipo
Porojo peleka kuleeeeeee.

Nimalizie Tu Kwa Kusema Msemaji Wa VYURA FC au Yanga Football Club Jerry Muro Anyamaze Tu Kwani Sasa Wanasimba Wameamua Kutembea Na Facts Hizi Ambapo Sasa Watakuwa Kama Wakimsikia Anaikashifu au Kuitukana Simba Sports Club Basi Na Wao Watamkabidhi Hizi Data Ili Kusudi Na Yeye Pia Atupatie Za Yanga Kama Zipo.


Shikamoo Msemaji Wa Simba Sports Club Haji Manara Hakika Leo Umemaliza Kila Kitu Huku Ukimtia Aibu Mtu Anayejitamba Kuwa Ana Masters Degree, Kaoa Mzungu Na Anaishi Mbezi Beach Mropokaji Wa Yanga Jerry Muro.

Na Mwisho Ningeshauri Sana Ewe Mwana Yanga Football Club Yoyote Utakayeiona Hii Na Kuisoma Basi Si Vibaya Ukaisambaza Kwa Wana Yanga FC Wenzio Popote Pale Walipo au Watakapokuwepo Ili KUMBUKUMBU Hii Muhimu Isije Ikawatoka AKILINI Mwenu. Kila Mwana Yanga Apate Copy Ya Hii Tafadhali.

Katika Hali Isiyokuwa Ya Kawaida Msemaji Wa Klabu Ya Simba Haji Manara Leo Ameamua Kumpiga Vibaya Sana Kwa Knock Out Msemaji Wa Klabu Ya Yanga Jerry Muro Baada Ya Ubishani Mkubwa Wa Ni Timu Gani Kweli au Hakika Inastahili Kuitwa au Kujiita YA KIMATAIFA au WA KIMATAIFA Kutokana Na Rekodi Za KUTUKUKA Ilizonazo Hiyo Timu.

Hiki Ndicho Msemaji Wa Simba Alichokisema...........


Waungwana kila uchwao kwenye jiji hili na viunga vyake sambamba na maeneo mengi ya nchi, kuna neno wa ‘kimataifa’ hulisikia likiimbwa.

Waimbaji wakuu wa neno hilo ni mashabiki wa Yanga wakiongozwa na mpiga zumari wao aliyeacha kazi yake na kujigeuza muimbaji.

Kinyume chake hilo neno klabu ya Simba huitwa wa ‘mchangani’ au wa ‘matopeni’. Wengi wananilaumu kuwa kwa nini huwa sijibu neno lolote la ajabu kwa Yanga. Jibu langu ni jepesi tu, lazima tujitofautishe msemaji wa klabu na mropokaji wa klabu.

Mimi hupenda kuzungumzia issues sio porojo au lugha za uchochoroni. Haiwezekani nikawa kiongozi kisha nikaongea lugha za mashabiki ‘maandazi’.

Kwa hiyo mtaniwia radhi wapenzi wa mpira kwa kutokuwa muimbaji wa ngonjera za uchochoroni. Mara zote nitabaki msemaji wa klabu kubwa nchini na ntaongea facts kwa kadri zilivyo.

Wadau zisomeni sifa za kimataifa kwa klabu ya Simba nje ya nchi halafu zifananisheni na timu nyingine nchini.

Walau kama zitafikia nusu tunawaruhusu watafute tusi jipya. Ombi langu kwenu isambazeni taarifa hii katak kila mtandao wa kijamii kisha waseme wao wanaojiita wa kimataifa.

1. Simba ndiyo timu ya kwanza nchini kupanda ndege na hii ilikuwa mwaka 1963 tena wakati huo taifa la Tanzania halikuwa limeundwa, ilikwenda Ethiopia kwa mwaliko wa rais wa taifa hilo Haile Selassie

2. Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa jezi na hii ilikuwa 1938 ilipocheza na kombaini ya mabaharia wa meli zilizotia nanga kwenye bandari ya Dar es salaam.

3. Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa viatu nchini na hii ilikuwa1949 ilipocheza na kombaini ya jeshi la majini Navy ya Afrika Kusini.

4. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa na basi lake yenyewe na hili lilinuliwa mwaka1968.

5. Simba ndiyo timu ya kwanza kumiliki jengo lake lenyewe na hili lilizinduliwa 1971.

6. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa bingwa wa ligi kuu nchini1966.

7. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwakilisha nchi na hii ilikuwa 1967.

8. Simba klabu ya kwanza nchini kwenda Ulaya na hii ilikuwa 1974 ilipokwenda Poland

9. Simba ndiyo timu ya kwanza kuwa mabingwa wa Afrika Mashariki na kati na hii ilikuwa 1974.

10.Simba ndio mabingwa wa kihistoria wa Afrika Mashariki na Kati, ndiyo timu iliyochukua ubingwa mara nyingi kuliko klabu yeyote Afrika Mashariki na Kati (Champs off all time.)

11.Simba ndiyo timu pekee nchini iliyowahi kufika nusu fainali ya klabu bingwa Afrika na hii ilikuwa1974.

12.Simba ndiyo timu pekee nchini na Afrika Mashariki kufika fainali ya kombe la Caf na hii ilikuwa1993.

13.Simba ndio timu inayoshikilia rekodi Afrika kama si duniani kwa kufungwa na Mufurila Wonderers ya Zambia magoli 4-0 na kwenda kuibamiza 5-0 kwao, mbele ya rais wao Kenneth Kaunda. Hii haijafanywa na klabu yeyote Afrika na nina mashaka duniani, hii ilikuwa 1979.

14.Simba ilicheza katik hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika 2003 kwa mafanikio makubwa kulinganisha na timu yoyote nchini.

15.Simba ndiyo timu pekee kuivua ubingwa klabu bingwa Afrika nadi Zamalek hii ilikuwa pia 2003.

16.Simba ndiyo klabu pekee nchini kuzifunga timu zote za mataifa ya kiarabu kuanzia

· Waliowatoa mwaka jana Etoile du Sahel (Tunisia)

· Widad Casablanca (Morocco)

· El Setif (Algeria)

· El Harach (Algeria)

halaf tumezifunga timu zote kubwa za Misri Zamelek,Al Ahly, Arab Contractors, Ismailia, Mehala, Al kubra na timu nyingine mnajua huwa inafanywaje ikigusa kule.

Pia imeshaitoa El Merekh ya Sudan 1994 katak klabu bingwa ya Afrika. Simba pia imeshazifunga miamba ya Afrika Magharibi kuanzia Asec, Asante Kotoko, Hafia ya Guinea hata mabingwa wa kihistoria wa Zambia Nkana Red Devils.

17. Tukirudi juu Simba ndiyo timu ya kwanza kuvaa suti na hii ilikuwa 1974 ilipokwenda Poland.

18.Simba ndiyo klabu pekee nchini kujenga jengo lake yenyewe kwa nguvu za wanachama na mashabiki, wenzetu ni mkopo na msaada toka kwa mzee Karume100%, Simba ilipewa kiasi flan na mzee karume baada ya jengo kukamilika na hii ilikuwa mwanzoni mwa miaka ya 70.

19.Angalia idadi ya wachezaji wa Simba walioenda Ulaya kucheza soka la kulipwa.

· Nico Njohole

· Deo Njohole

· Kassim Matitu

· George Kulagwa

Huku ikiwa na makumi ya nyota wake kadhaa waliowahI kutapakaa sehemu mbalimbali duniani.

Nikutajie wachache.

· Khalid Abeid

· Haidar Abeid

· Martin Kikwa

· Athman Mambosasa

· Zamoyoni Mogella

· Hamis Gaga

· Lilla Shomari

· Iddi Pazi

· Kiwelu Mussa

· George Masatu

· Hussein masha na wengine wengi.bila kumsahau nguli wa sasa mbwana samata.mutoto ya msimbazi.

Na hapa kumbukumbu zikae vizuri wazee wangu mimi, Sunday na Kassim Manara wakati wanaenda kucheza Ulaya hawakuwa wachezaji wa Yanga, walikuwa wakicheza Pan African.

20. Nimalizie kwa kuwaambia FIFA ilizitaja timu bora za karne kwa kila nchi kwa Tanzania Simba ilitajwa ndio timu bora ya karne na wenye mpira wao FIFA. Nenda kwenye rekodi za Caf ndio utajua nani wa kimataifa baina ya cc na wao.

Porojo za mjini ntakuwa nimezimaliza sasa na anayebisha abishe kwa data. Wakoloni wetu walitufundisha hivi…No reaserch no data no right to speak.Tafsiri isiyo rasmi, hujafanya utafiti na huna takwimu funga bakuli lako.

Asanteni na nendeni mkawaambie.

Haji S Manara
Msemaji wa klabu bora ya muda wote Tanzania (best club of all time)
Ukiona errors zipotezee jadili issues na nnaruhusu challenges kama zipo
Porojo peleka kuleeeeeee.

Nimalizie Tu Kwa Kusema Msemaji Wa VYURA FC au Yanga Football Club Jerry Muro Anyamaze Tu Kwani Sasa Wanasimba Wameamua Kutembea Na Facts Hizi Ambapo Sasa Watakuwa Kama Wakimsikia Anaikashifu au Kuitukana Simba Sports Club Basi Na Wao Watamkabidhi Hizi Data Ili Kusudi Na Yeye Pia Atupatie Za Yanga Kama Zipo.


Shikamoo Msemaji Wa Simba Sports Club Haji Manara Hakika Leo Umemaliza Kila Kitu Huku Ukimtia Aibu Mtu Anayejitamba Kuwa Ana Masters Degree, Kaoa Mzungu Na Anaishi Mbezi Beach Mropokaji Wa Yanga Jerry Muro.

Na Mwisho Ningeshauri Sana Ewe Mwana Yanga Football Club Yoyote Utakayeiona Hii Na Kuisoma Basi Si Vibaya Ukaisambaza Kwa Wana Yanga FC Wenzio Popote Pale Walipo au Watakapokuwepo Ili KUMBUKUMBU Hii Muhimu Isije Ikawatoka AKILINI Mwenu. Kila Mwana Yanga Apate Copy Ya Hii Tafadhali.
 
Hata mazuri na mafanikio wanayo yapata Tp mazembe ni record wanatengeneza......

Tukubali record zinawekwa ili zivunjwe kwa kuangalia mafanikio ya pande zote.
 
Kapigwa APR jana hapo kwao Rwanda wewe uko unawasubiri Prison ya Mbeya basi haina haja ya kusumbua akili Simba ni WAMCHANGANI najua inauma ila hakuna namna mkiweza jikwamueni.
 
Yanga hata rank za CAF haipo
 

Attachments

  • 1457857187371.jpg
    1457857187371.jpg
    28.5 KB · Views: 41
Siku zote hawezi kupiga hoja kwa matusi tu toa hoja zako ndiyo tukuamini mambo ya Manara yako sawa ili uyapinge weka record ya Yanga siyo matusi mbona nyie mnakuwa wapuzi kama msemaji wa Yanga pinga kwa topic za maana siyo matusi
 
atoto ebu njoo huku kwanza ule fact. Soma uzi wenye facts!
Vyura fc tupa kule, hapa ni MNYAMA aka SIMBARCELONA, mpira kapetini!
 
Simba ndio timu pekee isiokuwa na uwanja tangu Mwaka 1938 hadi Leo. Ongezea nyingine.
 
Huu ni ujinga na majungu kama ulivyo ujinga mwingine,ndo maana hizi timu zetu haziendelei kazi kuendekeza ujinga kama,nawachukia kishenzi Simba na Yanga katika ustawi wa mpira wa Tanzania,eti mtu anajisifu kupanda ndege wakati hata uwanja hana!!!
 
atoto ebu njoo huku kwanza ule fact. Soma uzi wenye facts!
Vyura fc tupa kule, hapa ni MNYAMA aka SIMBARCELONA, mpira kapetini!
Hana ishu hiyo Manara, anatafuta kumletea kesi Murro tu, hivi akimkimbiza mchana ili amuadhibu unadhani wananchi watamsaidia nani?
 
haji manara sijui tatizo lako haswa nini!hebu tulia kwanza tusubir wanaume walioenda kutafuta warudi tuwapokee halafu ndo uje na huu upuuzi wako.
 
Simba ndio timu pekee isiokuwa na uwanja tangu Mwaka 1938 hadi Leo. Ongezea nyingine.
Angalau tuna eneo la kujenga uwanja, hivi Vyura Fc lile bwawa la samaki na vyura mnaita uwanja?? Basi kituko!
 
Kwa kuwa anazungumzia Simba FC ukilinganisha na timu ya Yanga,nilidhani angelilinganisha na kulinganua (Compare and Contrast) kumbe ameorodhesha tu zile za Simba tofauti na dhamira yake..Katika historia Uingereza ndiyo ilikuwa ndio nchi ya kwanza kuwa na Viwanda,uliza leo kama bado wanaongoza.
 
Kwamba ndio walivaa viatu wa kwanza, walivaa suit wa kwanza, walipanda ndege wa kwanza..... Vp leo je hata hiyo ndege ya kuvuka mpaka wanapanda kwel? Tuzungumze leo upo ktk hali gan sio kusema tulikuaga ambao hata kwenye miaka aliosema wengne tulikuwa hatujazaliwa
 
Back
Top Bottom