Haki ya mtoto huyu wa nje ya ndoa ikoje?

Haki ya mtoto huyu wa nje ya ndoa ikoje?

Mitihani

Senior Member
Joined
Sep 17, 2013
Posts
158
Reaction score
46
Baada ya kuoana na kuzaa watoto 4 na kuishi kwenye ndoa pamoja kwa miaka 15 na kuchuma mali zetu pamoja maana wote ni watumishi na kuandika majina yetu mawili kama wamiliki.

Mume anakuja kusema kabla hajanioa alikuwa na mtoto alizaa anaomba nimtambue. Hapa sheria au haki ya huyu mtoto ikoje?
 
Hakuna mtoto anaitwa wa nje tafadhali sana heshimu haki za watoto na kwamba huyo mtoto kama mumeo alimzaa kabla ya kuwa nawe na kwamba kosa lake ni kutokukuambia mapema bado hailalalishi wewe kumwita ni mtoto wa nje na kwa minajili hiyo ni kama unataka kusema humtambui

Jitahidi uondokane na roho ya namna hiyo na jifunze kukubali uhalisia kwani hata kama ukimkataa atabaki kuwa ni mtoto wenu au wako kama utamkumbatia kwa dhati na kumpenda kama uliyemzaa mwenyewe, kama ungekuwa ni wewe mezalishwa na mwanaume ambaye baadae akakukacha na baadae akataka kumhudumia mwanao ungekataaa?

kila mtoto anahaki na kwamba neno mtoto wa nje halipaswi litamkwe kwenye vinywa vya watu wenye kujua maana ya utu
 
sio kweli kuwa hakuna mtoto wa nje, mtoto wa nje yupo na sheria inatambua kuwa huyo ni mtoto wa nje. maana ya mtoto wa nje ni kwamba, huyo ni mtoto wa nje ya ndoa.watoto wanatakiwa kutokana na ndoa, kama hawajatokana na ndoa wanaitwa watoto wa nje. kama ni kupata haki wanaweza kupata haki lakini ile status yao kama watoto wa nje ya ndoa haibadiliki kwasababu sio watoto wa ndani ya ndoa.

kitu cha muhimu kuelewa ni kwamba, kama unao watoto wa nje ya ndoa, hawawezi kupata haki zao hadi pale utakapowathibitisha/wakomboa. maana ya kuwathibitisha/kuwakomboa kuna namna nyingi kutokana na makabila mbalimbali ya Tanzania, wengine wanapeleka ng'ombe kwa wazazi wa mama mtoto, wengine wanaenda na washenga na kutoa fungu la pesa kutambulisha kuwa mtoto huyo ni wa kwao hivyo awe included kwenye ukoo wao etc.hatari yake ni kwamba, mfano kwa sheria za mirathi, kama hautamthibitisha kwa namna hiyo na akawekwa wazi kuwa ni mtoto wako, ukifa hawezi kurithi mali zako kabisa labda kama umeandika kwenye wosia lakini si kwasababu yeye ni mrithi halali.

pili, huwezi kuondoa dhana ya mtoto wa nje ya ndoa kwamba ipo, kwasababu kwamfano kwa dini ya kiislam, mtoto wa nje ya ndoa ni haram hata akithibitishwa hatambuliki katika dini hiyo, na sheria mfano; za mirathi za kiislam haziwezi kumtambua kabisa. ni mtoto wa uzinifu/haram na huwezi kukukifanya kitu haram kuwa si haram.

utanisamehe sana, kwasababu najua wengi humu ni watoto wa nje ya ndoa, Mungu anawapenda kuliko wanadamu, hata kama dunia itawakataa Mungu anawatambua. kuna umuhimu sheria zetu kuwekwa vizuri zaidi ya hapa ili watoto wote wapate haki zote, pamoja na kwamba, utakatifu wa ndoa nao ni muhimu sana, in order to keep the sanctity of marriage, children born out of wedlock wasiwe kama ni altenative.

View attachment 115643

View attachment 115644View attachment 115644
 
umefafanua vizuri sana, maana hata ishmael hakurithi pamoja na Issack kwa baba yake ila Mungu alimtafutia mahali pengine.
 
Hakukuambia kwa sababu ya woga wa kukupoteza. Elewa hilo kwanza.

Pili, mtoto mwenye umri say wa miaka 20 huwezi kumkumbatia na kumpenda kama wa kwako. Amelelewa malexi tofauti kabisa na ulivyolea wanao, utabahatika kama ana tabia nyingi za kupendeza lakini usiwe na mategemeo makubwa sana kuhusu yeye kwa sababu humjui. Mkubali, msamehe mumeo na endelea na maisha yenu.

Sheria hailazimishi umtunze wala kuishi nae. Mfanye kama binamu za wanao. Aje kuwatembelea. Lakini hana haki ya kurithi chochote ulichochuma na baba yake, hiyo ni wazi. Katika maongezi usilitaje sana hili ili upate habari za ziada.

Pole Mitihani, muambie mumeo akuambie mengine anayokuficha.
Baada ya kuoana na kuzaa watoto 4 na kuishi kwenye ndoa pamoja kwa miaka 15 na kuchuma mali zetu pamoja maana wote ni watumishi na kuandika majina yetu mawili kama wamiliki.
Mume anakuja kusema kabla hajanioa alikuwa na mtoto alizaa anaomba nimtambue. Hapa sheria au haki ya huyu mtoto ikoje?
 
Last edited by a moderator:
Unapokuwa unaandika jitahidi kuoanisha mawazo yako na jukwaa husika...

Toa vifungu vya kisheria na sio maneno mengi ya counselling...

Hakuna mtoto anaitwa wa nje tafadhali sana heshimu haki za watoto na kwamba huyo mtoto kama mumeo alimzaa kabla ya kuwa nawe na kwamba kosa lake ni kutokukuambia mapema bado hailalalishi wewe kumwita ni mtoto wa nje na kwa minajili hiyo ni kama unataka kusema humtambui...
 
from the decision of the Court of Appeal in VIOLET ISHENGOMA KAHANGWA & JOVIN MUTABUZI V. THE ADMINISTRATOR GENERAL & MRS EUDOKIA KAHANGWA (1990) T.L.R. 72

where it was inter alia stated that; ''.......... A child as defined under the Law of Marriage Act, 1971, does not include an illegitimate child, thus the word ''children'' in section 129 (1) of the L.M.A does not include illegitimate children. A putative father's obligation to his illegitimate children is personal and ends with his death it does not survive him won and cannot attach to his estate upon his dying inter state'' (stare decis- stand for what was decided before)
 
from the decision of the Court of Appeal in VIOLET ISHENGOMA KAHANGWA & JOVIN MUTABUZI V. THE ADMINISTRATOR GENERAL & MRS EUDOKIA KAHANGWA (1990) T.L.R. 72

where it was inter alia stated that; ''.......... A child as defined under the Law of Marriage Act, 1971, does not include an illegitimate child, thus the word ''children'' in section 129 (1) of the L.M.A does not include illegitimate children. A putative father's obligation to his illegitimate children is personal and ends with his death it does not survive him won and cannot attach to his estate upon his dying inter state'' (stare decis- stand for what was decided before)

Umesite kesi ya mwaka 90 kama precedent? Najua hiyo kesi mnasoma vyuoni sababu ndo ni ya CAT na ndo TLR mlizonazo kwa wingi..lakini Hujui position imebadilika hasa baada ya kuja into force The Law of the Child Act,2009 iloanza rasmi kutumika mwaka 2010?
 
Hakukuambia kwa sababu ya woga wa kukupoteza. Elewa hilo kwanza.

Pili, mtoto mwenye umri say wa miaka 20 huwezi kumkumbatia na kumpenda kama wa kwako. Amelelewa malexi tofauti kabisa na ulivyolea wanao...

:A S-confused1:Umegusa ikulu mkuu...ina maana wengine tumezaliwa bahati mbaya siyo?
 
.......kwa dini ya kiislam, mtoto wa nje ya ndoa ni haram

.....ni mtoto wa uzinifu/haram na huwezi kukukifanya kitu haram kuwa si haram.

.....Mungu anawapenda kuliko wanadamu, hata kama dunia itawakataa Mungu anawatambua
Dunia inawakataa kivipi wakati umesema ni dini - yani Mungu - ndio anawakataa?

Halafu hapo hapo unarudi kinyume nyume unajaribu kumpa Mungu credit kwa kuwapenda hawa watoto wakati wewe mwenyewe umesema ni watoto wa uzinifu na ni haramu na hawatakasiki hata ufanyeje! Sasa kama ni watoto haramu hiyo haramu ni kwa mujibu wa nani, shetani? Haramu kwa Mungu no less! Mbona mnapenda kumfagilia huyu Mungu kwa vitu senseless vinavyodhihirisha kwamba dini hai make sense at all?


from the decision of the Court of Appeal in VIOLET ISHENGOMA KAHANGWA & JOVIN MUTABUZI V. THE ADMINISTRATOR GENERAL & MRS EUDOKIA KAHANGWA (1990) T.L.R. 72

where it was inter alia stated that; ''.......... A child as defined under the Law of Marriage Act, 1971, does not include an illegitimate child, thus the word ''children'' in section 129 (1) of the L.M.A does not include illegitimate children. A putative father's obligation to his illegitimate children is personal and ends with his death it does not survive him won and cannot attach to his estate upon his dying inter state'' (stare decis- stand for what was decided before)
technical comment, a very rare brand at JF.
 
Sheria mpya ya watoto ya mwaka 2009 imeleta mabadiliko makubwa sana. Mtoto wa nje katika sheria ya zamani hawakuwa na haki ya kurithi,katika sheria mpya mtoto huyu anahaki zote kama watoto waliozaliwa ndani ya ndoa.
Na baba wa mtoto huyu anawajibu wa kumtuza kama watoto wengine na anahaki ya kuwafahamu ndugu zake wote.
Kama mmeo akifariki (god forbid), mtoto anahaki ya kurithi na pia kuhudumiwa kama watoto wengine. Haijalishi kama aliletwa nyumbani au laa. If he can prove kuwa yule ni baba yake na alikuwa anamuhudumia, then he is very much entitled.
Sasa ilikuondokana shari baadae, andikeni will, muende kwa mwanasheria awasaidie. Na pili amjenge huyu mtoto nyumba au ata amnunulie kiwanja amuachie.
 
sio hivyo bwana. mbona kama nimeongea very reasonably.
hakuna aliezaliwa bahati mbaya, wala hakuna asie na faida. mimi nina kaka wa kambo, na tunapendana kuliko kakangu wa kuzaliwa mama mmoja.
:A S-confused1:Umegusa ikulu mkuu...ina maana wengine tumezaliwa bahati mbaya siyo?
 
una uhakika aisee? ina maana mama yake yeye ale maisha huko na kulala gesti hausi na mie nnaekula shurba hapa tunapandisha tofali pamoja na baba yao then tugawane?
kama kweli sheria inasema hivyo juu ya urithi nadhani ni makosa kabisa. na je mama akizaa na mtu mwingine ilhali ndani ya ndoa, hiyo sheria nzuri inasemaje juu ya urithi? manake yanatokea hayo na tunayaona
Sheria mpya ya watoto ya mwaka 2009 imeleta mabadiliko makubwa sana. Mtoto wa nje katika sheria ya zamani hawakuwa na haki ya kurithi,katika sheria mpya mtoto huyu anahaki zote kama watoto waliozaliwa ndani ya ndoa.
Na baba wa mtoto huyu anawajibu wa kumtuza kama watoto wengine na anahaki ya kuwafahamu ndugu zake wote.
Kama mmeo akifariki (god forbid), mtoto anahaki ya kurithi na pia kuhudumiwa kama watoto wengine. Haijalishi kama aliletwa nyumbani au laa. If he can prove kuwa yule ni baba yake na alikuwa anamuhudumia, then he is very much entitled.
Sasa ilikuondokana shari baadae, andikeni will, muende kwa mwanasheria awasaidie. Na pili amjenge huyu mtoto nyumba au ata amnunulie kiwanja amuachie.
 
Sad to be a bastard in this weaked world dahhhhhhhh
 
1.Watoto waliokwishazaliwa wote ni wa nje, wa ndani bado wamo matumboni mwa mama zao.

2. Wanafamilia kuweni wazi kuhusu mahusiano yenu kuepusha matatizo. Wosia muhimu.

3. Naweza kuelewa suala la kutafuta haki kwa mtoto aliye chini ya miaka 18.Mtoto mwisho miaka 18, zaidi ya hapo kukodolea sana "haki" za urithi etc ni umasikini, mwisho wake ndo watu wanaomba wazazi wafe, au hata kuwaua ili kupata urithi. Mtu aliyezidi miaka 18 anatakiwa kufikiria zaidi jinsi gani yeye anaweza kuisaidia familia yake.Hili linajitokeza sana nchini mwetu, badala ya kuchanganya akili tunakaa kutafuta rent, kwenye madini na na unprocessed natural resources, bila kufikiri how do we add value.

4. Wanaobaguliwa kwa sababu ni "watoto wa nje" wafanye kazi kwa bidii kujikwamua wenyewe. Heshima na mafanikio haviji kwa sababu ni mtoto wa "ndani" au wa "nje" bali kwa kazi. Hata hivyo vitabu vinavyoitwa vitakatifu vimeandika jiwe lililokataliwa na waashi linaweza kuwa jiwe la msingi. Nilikuwa naangalia documentary ya "Marley" ya mwaka 2012. Kuna ndugu yake mmoja Bob Marley anasema kwamba ndugu zake Bob Marley kwa upande wa baba walikuwa wanamkana na hawakutaka hata kumsikia kwa sababu alikuwa "illegitimate", lakini ajabu Bob ndiye katokea kuwa marufu na aliyefanikiwa kuliko ndugu zake wote. Ukifanikiwa hata kilema kinaonekana kama kitu kizuri. Ma pirate walioweka eye patches kwa sababu walipofuliwa macho katika duels, walipofanikiwa kibiashara na kuwa legends kina Morgan, waliowezesha ufalme wa Uingereza, watu mpaka leo wanaweka eye patches kama fashion.

Huyo Nyerere "baba wa taifa" mwenyewe, wanaojua historia yake watakwambia kwamba mama yake Mgaya "alitoka" na Mzee Burito "akasaidiwa", kurudi akawa tayari kashaitika, kwa hiyo Nyerere si mtoto wa Chifu Burito. Ila Kizanaki baba si kitu cha muhimu sana (kwa sababu labda hakukuwa na njia ya kuhakikisha) bali mama na mjomba, hata kurithi mtoto anarithi mali ya mjomba (Nyerere said this last part in one of his speeches).

Utajuaje kwamba baba yako ndiye baba yako na si baba yako mkubwa/ mdogo, au mtu baki kibaiolojia? Hata DNA yenyewe haiwezi kukupa jibu kamili!

5. Usipooa na ku create a false sense of entitlement huna haja ya ku deal na upuuzi huu wote wa nani mtoto wa ndani na nani mtoto wa nje.
 
sio hivyo bwana. mbona kama nimeongea very reasonably.
hakuna aliezaliwa bahati mbaya, wala hakuna asie na faida. mimi nina kaka wa kambo, na tunapendana kuliko kakangu wa kuzaliwa mama mmoja.

Binafsi ni zao la so called nje ya ndoa...zaidi mimi ni mtoto wa saba out of sita wa 'kwenye ndoa'! Mbaya zaidi mama yangu na 'mama wa ndoa' wa baba ni mtu na dada yake! Leo mama yangu kaolewa kwenye ndoa nyiginge(kwa kuwa alinizaa kabla hajakuwa na ndoa) na wapo ndugu zangu wengine watatu 'wa kwenye ndoa ya mama' Kwa mujibu wako King'asti niandike tu mmaumivu siyo? Ila namshukuru huyu baba 'aliyemwoa mama' kwa kunisomesha! Na mimi naomba Mungu aniepushie mtoto 'haramu' kama mimi navyoonekana!
 
Last edited by a moderator:
Hakuna mtoto anaitwa wa nje tafadhali sana heshimu haki za watoto na kwamba huyo mtoto kama mumeo alimzaa kabla ya kuwa nawe na kwamba kosa lake ni kutokukuambia mapema bado hailalalishi wewe kumwita ni mtoto wa nje na kwa minajili hiyo ni kama unataka kusema humtambui

Jitahidi uondokane na roho ya namna hiyo na jifunze kukubali uhalisia kwani hata kama ukimkataa atabaki kuwa ni mtoto wenu au wako kama utamkumbatia kwa dhati na kumpenda kama uliyemzaa mwenyewe, kama ungekuwa ni wewe mezalishwa na mwanaume ambaye baadae akakukacha na baadae akataka kumhudumia mwanao ungekataaa?

kila mtoto anahaki na kwamba neno mtoto wa nje halipaswi litamkwe kwenye vinywa vya watu wenye kujua maana ya utu
asante sana mkuu its so offensive
 
Binafsi ni zao la so called nje ya ndoa...zaidi mimi ni mtoto wa saba out of sita wa 'kwenye ndoa'! Mbaya zaidi mama yangu na 'mama wa ndoa' wa baba ni mtu na dada yake! Leo mama yangu kaolewa kwenye ndoa nyiginge(kwa kuwa alinizaa kabla hajakuwa na ndoa) na wapo ndugu zangu wengine watatu 'wa kwenye ndoa ya mama' Kwa mujibu wako King'asti niandike tu mmaumivu siyo? Ila namshukuru huyu baba 'aliyemwoa mama' kwa kunisomesha! Na mimi naomba Mungu aniepushie mtoto 'haramu' kama mimi navyoonekana!
astakhafurlah mhhhhhh??
 
Back
Top Bottom