martial jb
JF-Expert Member
- Oct 21, 2021
- 863
- 1,462
Habari waungwana
NDIO AMEONDOLEWA TENA!!! Huyu si mwingine ni dar young africans, hakika hata kipenzi chetu Mwl. JK NYERERE anaweza kushtushwa na taarifa hizi huko alipo, huku akijiuliza "wanashida gani hasa!!??"
Hali kadhalika swali la wengi ni kwa nini kila siku aondoshwe yeye!!? Je, ana laana fulani inayomtafuna? Je hana kiwango!? Je, karogwa kwa kuwekewa zindiko na kunuiziwa kutotoboa kimataifa!!?? Mwisho wa siku klabu hiyo inakosa majibu.
Wakati huo majirani zao wanazidi kujenga heshima kimataifa na umaarufu na kujengeka kibiashara, leo hii michuano ya kimataifa imepelekea Simba kufahamika duniani, kuwa na wafuasi wengi mitandaoni, kufanya mauzo ya jezi nyingi nje ya nchi, kutengeneza mashabiki wengi nje ya NCHI. Na kuipa heshima NCHI.
Masikini muda huo wenzao Yanga wanafurahia mafanikio yao ya ndani na ya muda mfupi kwa viongozi wao wasio na tija na malengo.Kwani leo hii hata Twitter haifahamu kuwa YANGA ni klabu ya soka!! What a shame!!
Kuna jamaa yangu alienda misri akaulizia kuhusu SIMBA SC, hakuamini kwani watu wengi walionyesha kuipenda na kuifahamu vizuri ikiwemo na wachezaji wake, cha kusikitisha wengi wao walimshangaa alipoulizia kuhusu YANGA.
Kiukweli nawapa pole sana Yanga kwa hili janga linalowasibu masikini, nahisi sasa ni muda sahihi wa wao kufanya mabadiliko ya klabu yao kwani hawajachelewa
Na hakika nimeamini mkubwa ni mkubwa siku zote na rekodi zina nafasi yake kwenye mpira, kwani kuvunja rekodi si kitu rahisi. Yanga hana rekodi ligi ya mabingwa Africa na hilo ameendelea kudhihirisha
Kama kurogwa, basi aliyemroga Yanga ana kesi ya kujibu kwa Mungu, na kama wana laana na michuano ya kimataifa basi nawaamuru haraka watubu laana yao kwani itaendelea kuwatafuna.
Namaliza uzi kwa kusema siku zote mzoea vya udalali vya duka haviwezi, na ngoma ikilia sana ujue yaelekea kupasuka
NDIO AMEONDOLEWA TENA!!! Huyu si mwingine ni dar young africans, hakika hata kipenzi chetu Mwl. JK NYERERE anaweza kushtushwa na taarifa hizi huko alipo, huku akijiuliza "wanashida gani hasa!!??"
Hali kadhalika swali la wengi ni kwa nini kila siku aondoshwe yeye!!? Je, ana laana fulani inayomtafuna? Je hana kiwango!? Je, karogwa kwa kuwekewa zindiko na kunuiziwa kutotoboa kimataifa!!?? Mwisho wa siku klabu hiyo inakosa majibu.
Wakati huo majirani zao wanazidi kujenga heshima kimataifa na umaarufu na kujengeka kibiashara, leo hii michuano ya kimataifa imepelekea Simba kufahamika duniani, kuwa na wafuasi wengi mitandaoni, kufanya mauzo ya jezi nyingi nje ya nchi, kutengeneza mashabiki wengi nje ya NCHI. Na kuipa heshima NCHI.
Masikini muda huo wenzao Yanga wanafurahia mafanikio yao ya ndani na ya muda mfupi kwa viongozi wao wasio na tija na malengo.Kwani leo hii hata Twitter haifahamu kuwa YANGA ni klabu ya soka!! What a shame!!
Kuna jamaa yangu alienda misri akaulizia kuhusu SIMBA SC, hakuamini kwani watu wengi walionyesha kuipenda na kuifahamu vizuri ikiwemo na wachezaji wake, cha kusikitisha wengi wao walimshangaa alipoulizia kuhusu YANGA.
Kiukweli nawapa pole sana Yanga kwa hili janga linalowasibu masikini, nahisi sasa ni muda sahihi wa wao kufanya mabadiliko ya klabu yao kwani hawajachelewa
Na hakika nimeamini mkubwa ni mkubwa siku zote na rekodi zina nafasi yake kwenye mpira, kwani kuvunja rekodi si kitu rahisi. Yanga hana rekodi ligi ya mabingwa Africa na hilo ameendelea kudhihirisha
Kama kurogwa, basi aliyemroga Yanga ana kesi ya kujibu kwa Mungu, na kama wana laana na michuano ya kimataifa basi nawaamuru haraka watubu laana yao kwani itaendelea kuwatafuna.
Namaliza uzi kwa kusema siku zote mzoea vya udalali vya duka haviwezi, na ngoma ikilia sana ujue yaelekea kupasuka