Hakika uanasiasa unamdhalilisha na kumuanika Spika Tulia A. Mwansasu

Hakika uanasiasa unamdhalilisha na kumuanika Spika Tulia A. Mwansasu

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Spika Dr. Tulia Ackson Mwansasu, msomi wa kiwango cha Shahada ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cape Town, Afrika ya Kusini sasa anadhalilishwa na kutwezwa na siasa. Msomi huyu na Mhadhiri wa zamani wa UDSM (mwanangu ambaye kwasasa naye ni Mhadhiri hapo alifundishwa naye) sasa ni dhahiri anazidiwa nguvu na siasa.

Siasa za kisasa zinataka matumizi sahihi ya fani, ujuzi na uzoefu juu ya mambo ambayo mwanasiasa anajihusisha nayo. Hata kwenye michakato ya kuwapata viongozi kwenye mihimili na kwingineko, mambo hayo huzingatiwa. Bunge ni chombo cha kutunga sheria na kuisimamia Serikali. Kinapaswa kuongozwa na mwerevu wa, pamoja na mambo mengine, sheria.

Pamoja na kwamba kwasasa amehama kwenye tasnia ya sheria (alikofika ngazi ya Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali) na kuhamia siasani, Dr. Tulia anapaswa kuwa mfano mwema. Anapaswa kuwaonesha watanzania kuwa taaluma yake ya sheria inatusaidia sote kupitia nafasi ya Uspika aliyonayo. Bado anapaswa kuzungumza kama mwanasheria-kuzungumza facts zaidi ya porojo na hoja kuliko vihoja.

Jambo hili la Mkataba wa DP World ni la kisheria. Sote tulimtegemea tangu Bungeni kulizungumza na kuliongoza kisheria kwa maslahi mapana ya Tanzania yetu. Lakini, siasa ikamzidi nguvu. Akafanya alivyoagizwa kichama na kiserikali badala ya kadiri ya taaluma yake. Bado, huko Mbeya, anaendelea kuliletea porojo, dhihaka na kebehi jambo hili na wale wanaolizungumzia. Siasa inamdhalilisha na kumtweza.

Katika mifumo ya kiintelijensia na kiutawala, sisi wabobevu wa mambo ya kiuongozi huwa tunaamini kuwa yeyote anayepewa chochote asichostahili au bila kutegemea, huyo huwa mnyenyekevu hadi kuwa mbovu. Anayestahili akipata husimama imara. Kukosa sifa huleta woga. Huleta kutojiamini. Hukufanya kuangalia pande zote kila mara. Huleta 'utumwa' wa kifikra.

Rais Samia, maoni yako ni yapi kuhusiana na Mkataba wa DP World?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Elimu haijawahi kuwabadilisha watu wa pande izo. Mtu hata awe na digrii mia, bado vile vitabia vya kinyakyusa vinakuwepo.
Unakumbuka jinsi Daktari Mwakyembe msomi mwenye digrii nne alivyomchamba na kumsagia kunguni waziri mkuu wa kipindi kile Eddo Ngoyai Lowasa. Bila hata ya kumsitiri kwa kumuacha na kipensi, mzee wa watu alivuliwa nguo zote mbele ya kadamnasi, katikati ya vikao vya bunge.
Msomi mwakyembe alikuwa anachamba kuliko wale wanawake wa kiswahili wa Buza na Mbagala! Unakumbuka!
 
Spika Dr. Tulia Ackson Mwansasu, msomi wa kiwango cha Shahada ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cape Town, Afrika ya Kusini sasa anadhalilishwa na kutwezwa na siasa. Msomi huyu na Mhadhiri wa zamani wa UDSM (mwanangu ambaye kwasasa naye ni Mhadhiri hapo alifundishwa naye) sasa ni dhahiri anazidiwa nguvu na siasa.

Siasa za kisasa zinataka matumizi sahihi ya fani, ujuzi na uzoefu juu ya mambo ambayo mwanasiasa anajihusisha nayo. Hata kwenye michakato ya kuwapata viongozi kwenye mihimili na kwingineko, mambo hayo huzingatiwa. Bunge ni chombo cha kutunga sheria na kuisimamia Serikali. Kinapaswa kuongozwa na mwerevu wa, pamoja na mambo mengine, sheria.

Pamoja na kwamba kwasasa amehama kwenye tasnia ya sheria (alikofika ngazi ya Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali) na kuhamia siasani, Dr. Tulia anapaswa kuwa mfano mwema. Anapaswa kuwaonesha watanzania kuwa taaluma yake ya sheria inatusaidia sote kupitia nafasi ya Uspika aliyonayo. Bado anapaswa kuzungumza kama mwanasheria-kuzungumza facts zaidi ya porojo na hoja kuliko vihoja.

Jambo hili la Mkataba wa DP World ni la kisheria. Sote tulimtegemea tangu Bungeni kulizungumza na kuliongoza kisheria kwa maslahi mapana ya Tanzania yetu. Lakini, siasa ikamzidi nguvu. Akafanya alivyoagizwa kichama na kiserikali badala ya kadiri ya taaluma yake. Bado, huko Mbeya, anaendelea kuliletea porojo, dhihaka na kebehi jambo hili na wale wanaolizungumzia. Siasa inamdhalilisha na kumtweza.

Katika mifumo ya kiintelijensia na kiutawala, sisi wabobevu wa mambo ya kiuongozi huwa tunaamini kuwa yeyote anayepewa chochote asichostahili au bila kutegemea, huyo huwa mnyenyekevu hadi kuwa mbovu. Anayestahili akipata husimama imara. Kukosa sifa huleta woga. Huleta kutojiamini. Hukufanya kuangalia pande zote kila mara. Huleta 'utumwa' wa kifikra.

Rais Samia, maoni yako ni yapi kuhusiana na Mkataba wa DP World?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Madaraka yanalevya kuliko madawa ya kulevya.J k nyerere
 
Spika Dr. Tulia Ackson Mwansasu, msomi wa kiwango cha Shahada ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cape Town, Afrika ya Kusini sasa anadhalilishwa na kutwezwa na siasa. Msomi huyu na Mhadhiri wa zamani wa UDSM (mwanangu ambaye kwasasa naye ni Mhadhiri hapo alifundishwa naye) sasa ni dhahiri anazidiwa nguvu na siasa.

Siasa za kisasa zinataka matumizi sahihi ya fani, ujuzi na uzoefu juu ya mambo ambayo mwanasiasa anajihusisha nayo. Hata kwenye michakato ya kuwapata viongozi kwenye mihimili na kwingineko, mambo hayo huzingatiwa. Bunge ni chombo cha kutunga sheria na kuisimamia Serikali. Kinapaswa kuongozwa na mwerevu wa, pamoja na mambo mengine, sheria.

Pamoja na kwamba kwasasa amehama kwenye tasnia ya sheria (alikofika ngazi ya Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali) na kuhamia siasani, Dr. Tulia anapaswa kuwa mfano mwema. Anapaswa kuwaonesha watanzania kuwa taaluma yake ya sheria inatusaidia sote kupitia nafasi ya Uspika aliyonayo. Bado anapaswa kuzungumza kama mwanasheria-kuzungumza facts zaidi ya porojo na hoja kuliko vihoja.

Jambo hili la Mkataba wa DP World ni la kisheria. Sote tulimtegemea tangu Bungeni kulizungumza na kuliongoza kisheria kwa maslahi mapana ya Tanzania yetu. Lakini, siasa ikamzidi nguvu. Akafanya alivyoagizwa kichama na kiserikali badala ya kadiri ya taaluma yake. Bado, huko Mbeya, anaendelea kuliletea porojo, dhihaka na kebehi jambo hili na wale wanaolizungumzia. Siasa inamdhalilisha na kumtweza.

Katika mifumo ya kiintelijensia na kiutawala, sisi wabobevu wa mambo ya kiuongozi huwa tunaamini kuwa yeyote anayepewa chochote asichostahili au bila kutegemea, huyo huwa mnyenyekevu hadi kuwa mbovu. Anayestahili akipata husimama imara. Kukosa sifa huleta woga. Huleta kutojiamini. Hukufanya kuangalia pande zote kila mara. Huleta 'utumwa' wa kifikra.

Rais Samia, maoni yako ni yapi kuhusiana na Mkataba wa DP World?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Naanza kujiuliza hivi PhD ina maana gani? Maana hizi zilizopo bungeni sijaona zinatunufaishaje. Sina haja ya kuzutaja kwani nahisi mnazijua silizotolewa jalalani, baadhi zimo serikalini lakini ndizo zinazotuingiza mkenge kila uchao, zingine zipo bungeni lakini michango yao haina tofauti na kibajaj wa darasa la saba ama Dr. Musukuma. Sijajua tatizo ni nini.


Sent from my Infinix X689F using JamiiForums mobile app
 
Kusema ukweli huyu anatakiwa kusaidiwa na wanaompenda, mimi najionea aibu as if ni mimi
 
Elimu haijawahi kuwabadilisha watu wa pande izo. Mtu hata awe na digrii mia, bado vile vitabia vya kinyakyusa vinakuwepo.
Unakumbuka jinsi Daktari Mwakyembe msomi mwenye digrii nne alivyomchamba na kumsagia kunguni waziri mkuu wa kipindi kile Eddo Ngoyai Lowasa. Bila hata ya kumsitiri kwa kumuacha na kipensi, mzee wa watu alivuliwa nguo zote mbele ya kadamnasi, katikati ya vikao vya bunge.
Msomi mwakyembe alikuwa anachamba kuliko wale wanawake wa kiswahili wa Buza na Mbagala! Unakumbuka!
Ulitaka asitili majizi?,wewe ni hopeless kabisa,Mwakyembe alitimiza wajibu wake kama Mbunge,tofautisha na Tulia anaeilinda Serikali
 
Samia ni bubu kwenye hili la DPW, anajua akisema atakuwa upande wa waarabu.
 
Spika Dr. Tulia Ackson Mwansasu, msomi wa kiwango cha Shahada ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Cape Town, Afrika ya Kusini sasa anadhalilishwa na kutwezwa na siasa. Msomi huyu na Mhadhiri wa zamani wa UDSM (mwanangu ambaye kwasasa naye ni Mhadhiri hapo alifundishwa naye) sasa ni dhahiri anazidiwa nguvu na siasa.

Siasa za kisasa zinataka matumizi sahihi ya fani, ujuzi na uzoefu juu ya mambo ambayo mwanasiasa anajihusisha nayo. Hata kwenye michakato ya kuwapata viongozi kwenye mihimili na kwingineko, mambo hayo huzingatiwa. Bunge ni chombo cha kutunga sheria na kuisimamia Serikali. Kinapaswa kuongozwa na mwerevu wa, pamoja na mambo mengine, sheria.

Pamoja na kwamba kwasasa amehama kwenye tasnia ya sheria (alikofika ngazi ya Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali) na kuhamia siasani, Dr. Tulia anapaswa kuwa mfano mwema. Anapaswa kuwaonesha watanzania kuwa taaluma yake ya sheria inatusaidia sote kupitia nafasi ya Uspika aliyonayo. Bado anapaswa kuzungumza kama mwanasheria-kuzungumza facts zaidi ya porojo na hoja kuliko vihoja.

Jambo hili la Mkataba wa DP World ni la kisheria. Sote tulimtegemea tangu Bungeni kulizungumza na kuliongoza kisheria kwa maslahi mapana ya Tanzania yetu. Lakini, siasa ikamzidi nguvu. Akafanya alivyoagizwa kichama na kiserikali badala ya kadiri ya taaluma yake. Bado, huko Mbeya, anaendelea kuliletea porojo, dhihaka na kebehi jambo hili na wale wanaolizungumzia. Siasa inamdhalilisha na kumtweza.

Katika mifumo ya kiintelijensia na kiutawala, sisi wabobevu wa mambo ya kiuongozi huwa tunaamini kuwa yeyote anayepewa chochote asichostahili au bila kutegemea, huyo huwa mnyenyekevu hadi kuwa mbovu. Anayestahili akipata husimama imara. Kukosa sifa huleta woga. Huleta kutojiamini. Hukufanya kuangalia pande zote kila mara. Huleta 'utumwa' wa kifikra.

Rais Samia, maoni yako ni yapi kuhusiana na Mkataba wa DP World?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Fursa nyingine kwa DP world "HILI NALO MKALITAZAME"...
 

Attachments

  • IMG140723 (1).jpg
    IMG140723 (1).jpg
    56.1 KB · Views: 4
Elimu haijawahi kuwabadilisha watu wa pande izo. Mtu hata awe na digrii mia, bado vile vitabia vya kinyakyusa vinakuwepo.
Unakumbuka jinsi Daktari Mwakyembe msomi mwenye digrii nne alivyomchamba na kumsagia kunguni waziri mkuu wa kipindi kile Eddo Ngoyai Lowasa. Bila hata ya kumsitiri kwa kumuacha na kipensi, mzee wa watu alivuliwa nguo zote mbele ya kadamnasi, katikati ya vikao vya bunge.
Msomi mwakyembe alikuwa anachamba kuliko wale wanawake wa kiswahili wa Buza na Mbagala! Unakumbuka!
Kwamba Mwakyembe kuanika ukweli ilikuwa kosa na 'vitabia vya kinyakyusa'? Na huyu spika kukumbatia ujinga pia ni kosa? Pick a lane!

Lowasa alikuwa mwana mtandao wa mafisadi. Alishiriki kikamilifu kwenye uhuni wote wa 2005.
 
Kipindi wanaujadili huo mkataba ulikuwa vilevilee kwa lugha ya kingereza ama??
 
Back
Top Bottom