Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Je huwa unaogopa kuishi maisha yako kwa kuhofia watu watakuonaje?
Huwa unaogopa kuchangia mijadala mbali mbali ili usionekana hauna uelewa wa kutosha?
Huwa unaogopa kupost kwakuwa unadhani sio mwandishi mzuri?
Huwa unaogopa kujichanganya na watu kwakuwa unahisi wewe sio mzungumzaji mzuri?
Ngoja nikwambie kitu expert,jua kwamba hakuna anayejali kuhusu wewe,kila mtu ana mambo yake binafsi yanayo mshughulisha,machoni pako na mawazoni mwako unaweza hisi watu wanakufuatilia au wanazungumza kuhusu wewe ila ukweli ni kwamba,kila mtu ana dili na mambo yake
Kwahiyo acha kufikiri kwamba watu wanakufuatilia laa,acha kuwaza kwamba watu wanakuwekea kipaumbele,jibu ni hapana,kila mtu anashughulishwa na mambo yake
Kwahiyo you are in your own,fanya mambo yako na ishi vile unavyoishi maadamu humkwazi mtu,haumvunjii mtu heshima yake,ishi maisha yako
Ni hayo tu!