Hakuna cha Kamera, wala ushirikina - Polisi

Hakuna cha Kamera, wala ushirikina - Polisi

Nilipotembelea bongo mwaka 2006 niliona utofauti MKUBWA SANA na nikawa ninajiuliza maswali mengi mengi sana na nikawa sina jibu.

Nikawa nikidhani labda ni kwasababu ya majambazi kuwa wengi!

Lakini ukweli wabongo walikuwa wanatia huruma na kila mahali ukipita kama kweli una empathy basi machozi yatakutoka!

Mpaka kieleweke kama wewe ni Mbowe utakumbuka tulikutana ukiwa na Zitto nilikwenda kumcheki jamaa yangu Tumanini.

Nilikwenda Dar kubadili passport yangu lakini nikajuta kwani wenzangu walilipa dola 50 tu hapa na mimi kimbelembele changu kwenda kubadili huko Dar kilini cost laki mbili...Karibia mara nne ya original cost!

Njiani wakati narudi niliona mengi!

Hata kituo cha mafuta nilisimama kuweka mafuta na service kidogo kabla ya kurudi moshi lakini walinzi wa kituo hicho ni harassment tupu utadhani mimi si mteja na nimeenda kuomba msaada!

Na sasa hata huko Moshi askari wanaolinda hata duka ama bureau de change anageuka kuwa askari wa bara barani na kila kitu!

Yani wakipewa bunduki sasa wao ndio wenye mamlaka yasiyo na mipaka!

Mimi kwasababu nilikuwa nikiona habari za ujambazi kila siku basi nikasema labda ni haki!

Lakini sasa nimegundua kuwa tuli tafsiri vibaya ubepari!

Kwani eti sasa hata maaskari wanalinda watu binafsi kwasababu ulinzi wa mali za umma haupo tena!

Ulinzi wa mali za umma haupo tena kwasababu mali hizo za umma ziko mikononi mwa mafisadi na polisi hao njaa wanalinda mali hizo na mafisadi wake!

Ni wazi kuwa mwenye pesa ndiye mwenye kulindwa na kuamuwa nini kifanyike!

Na ubepari wa kibongo ni wa KIMAFIA!

Kwani sasa jeshi la POLISI SI LA KUWATUMIKIA WANANCHI TENA BALI MAFISADI!

NA MWENYE ULINZI NDIOYO ALIYEKO SALAMA!

MWENYE ULINZI NI MAFISADI KWANI WAMEUPORA USALAMA WA WANANCHI AMBAO NI MALI ZAO!

Machozi yanakutoka. Ubaya zaidi ni kwamba ni shida ambazo zinaweza kuepukika! Kuna baadhi ya watu wanasema watu wajiendeleze wenyewe, ila wanasahau Nchi ni tajiri sana na kama viongozi walikuwa wanajua cha kufanya na kukifanya mambo yangekuwa tofauti kabisa.

Ila ni hao viongozi ambao hawana hata aibu ya kuweka mabillioni huko Jersey na halafu wanapishana na hawa binadamu wenzao wanaotaabika barabarani kila siku. Hata wizi ungekuwa kwenye damu, ndio waibe kiasi hicho?
 
Haya kweli ni mambo!!!!!! Hii ni vunja mbavu, pamoja na kuwa implication yake ni kubwa kwa taifa letu. Mimi nadhani Spika amepigwa chenga ya mwili. Anahitaji support yetu. Hapa wote tumefungwa la kisigino, lakini nasisi tumemfunga la kisigino Rostam na KKKT. Mapambano yanaendelea
 
Spika asingekuwa taahira kupeleka police ''NOTHING''. Wana maana ni mwehu!
 
1. Chiligati awe na la kujibu kwa kutudanganya kuwa kuna matu alikuwa anatafuta kwa kukaa, na pia atueleze alionaje? maana camera hazikuona hicho kitendo,

2. watuambie huo unga waliutoa wapi, na kwa nini waliupima wakati hakuna aliengia ndani ya bunge kutafuta kiti wala kumwaga unga?

3. Wote watueleze kwanini lakini wanatufanya sisi wajinga kiasi hicho? yaani haya ni matusi tena ya nguoni kwa wananchi wote!!!!

samahanini kwa lugha mbaya, nimeudhika mno
 
I smell something fishy here..my poor country TZ where are you heading to??
Inauma sana tunaposoma uozo na aibu za chama tawala siku hadi siku.
 
Tunataka MOTIVE!
KWANINI UNGA ULIKUWA BUNGENI NA KWANINI ULIPELEKWA KWA MKEMIA NA TUNATAKA KAULI ZA WALIOHOJIWA!
POLISI WASEME WALITUMIA VIGEZO GANI KUFIKIA CONCLUSION!
ACHENI HIZO BANA!

Mhhh!!!!!!!!!!
 
Ina maana Mzee wa kujiridhisha na ushahidi alipeleka mkanda polisi kwa ajili ya uchunguzi bila ya yeye kuuona na kujiridhisha kwamba kulikuwa na watu wawili? Yeye alijuaje kwamba kuna watu 2 walionekana wakiwa wanazunguka? Je, alijuaje kwamba mmoja ni Mbunge na mwingine ni Afisa wa Bunge? Alikubalije kutangaza habari ambayo hakuwa na uhakika nayo ama bila yeye mwenyewe kujiridhisha?

Chiligati alipata wapi maelezo kwamba walioonekana kwenye ukumbi wa Bunge walikuwa wanatafuta kiti cha kukaa ama na yeye aliropoka bila kuwa na uhakika?

Serikali ya Tanzania pamoja na Chama Twawala imeshikiliwa na wachache na ndiyo maana wanaweza kucheza na chochote kile kama wanavyopenda wao wenyewe!

Good/hard questions!
More questions than answers...
 
Jeshi la Polisi limetoa ripoti yake kuhusu uchunguzi wa kile kilichodaiwa vitendo vya kishirikina Bungeni karibu mwezi mmoja uliopita ambapo ilidaiwa mmojawapo wa wabunge alionekana akimwaga unga kwenye viti mbalimbali. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma amesema kuwa (kati ya niliyoyanasa kwa haraka)

a. Hakuna Kamera iliyozimwa kuanzia mwaka 2006 (don't ask me walisema zilikuwa zimezimwa)
b. Kwenye mkanda uliodaiwa hakuna mtu aliyeonekana akifanya jambo lolote lile (mkanda mtupu?)
c. Vumbi lililoenda kuchunguzwa halikuwa na sumu yoyote inayotambulika.
d. Hakuna kitendo cha kishirikina.

Hayo yamesemwa na Kamanda huyo wa Mkoa Bw. Omar Mganga alipotoa taarifa kwa Kamati ya Uongozi ya Bunge kuhusu uchunguzi huo uliofuatia matukio ya wiki chache zilizopita. Vyanzo vingine vinasema kuwa kati ya mambo yaligundulika katika uchunguzi huo ni pamoja:

a. Kamera mbili kuwa mbovu kwa muda mrefu bila ya kufanyiwa matengenezo na nyuingine mbili zilikuwa zimegeuzwa (tilted) ingawa sijui zilikuwa zinaangalia upande gani!
b. Na mojawapo ya madai ya kushtua kabisa ambayo wenu mtiifu ameyasikia ni kuwa baadhi ya watu wanaolipwa kuzikodolea macho hizo kamera walikuwa wameuchapa!

Hii ni aibu sana, ila naamini MWISHO WA UBAYA AIBU
 
Nimewaambia tukubali hamtaki nyie mmeng'ang'ania tu.. mnafikiri watatoa majibu tofauti na haya?
 
Jeshi la Polisi limetoa ripoti yake kuhusu uchunguzi wa kile kilichodaiwa vitendo vya kishirikina Bungeni karibu mwezi mmoja uliopita ambapo ilidaiwa mmojawapo wa wabunge alionekana akimwaga unga kwenye viti mbalimbali. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma amesema kuwa (kati ya niliyoyanasa kwa haraka)

a. Hakuna Kamera iliyozimwa kuanzia mwaka 2006 (don't ask me walisema zilikuwa zimezimwa)
b. Kwenye mkanda uliodaiwa hakuna mtu aliyeonekana akifanya jambo lolote lile (mkanda mtupu?)
c. Vumbi lililoenda kuchunguzwa halikuwa na sumu yoyote inayotambulika.
d. Hakuna kitendo cha kishirikina.

Hayo yamesemwa na Kamanda huyo wa Mkoa Bw. Omar Mganga..........

Je hiyo vumbi waliitoa wapi?...walifagia bunge na kukusanya vumbi?...au je waliikusanya katika sehemu(viti vya kina Mwakyembe and Co) tu?...kama hivyo ni kwa nini?

Hivi jamani si ingekuwa bora waongee uwongo uliopo karibu na ukweli?....huu ni uwongo wa ngapi tumepata kutoka vyombo vya dola?...Muungwana kama una masikio na macho ,huoni kuwa vyombo vya dola hivi vina ku undermine?....serikali yako inaonekana ni uozo?
 
Tunataka MOTIVE!
KWANINI UNGA ULIKUWA BUNGENI NA KWANINI ULIPELEKWA KWA MKEMIA NA TUNATAKA KAULI ZA WALIOHOJIWA!
POLISI WASEME WALITUMIA VIGEZO GANI KUFIKIA CONCLUSION!
ACHENI HIZO BANA!

Lakini Hata Hosea alisema mkataba wa richmond hauna hata chembe ya ufisadi
kiko wapi sasa
Wote tunajua ngoma ya kitoto siku zote huwa haikeshi
 
Meremeta ni mali ya jeshi kwa hiyo hairuhusiwi by sheria kuiongelea kwenye public!,

Sasa ni vumbi tu lililokutwa bungeni, huu ni uchunguzi wa polisi uliochukua zaidi ya mwezi mmoja!

Only in Tanzania!
 
Kwangu haya sio matokeo ya kushangaza. NI kweli ameshika dume sisi tumeshika magalasa. This guy will get away with everything, nguvu ya fedha, inasema yeye si fisadi na hakufanya lolote baya. Kama serikali inashindwa kupropve kuwa yuko guilty inawezekana siku watanzania wakafanya hivyo na wakatoa hukumu.
 
Yooote hayo yalitabiriwa hapa JF kwamba at the end of the day hakutapatikana chochote bungeni kuhusu ule unga na hata hizo video.
 
Kweli tunachekwa sana na wenetu wa nje tunaonekana ni taifa la wapumbavu. Kuna mambo ambaye ni exclusivley Tanzanian. Leo nimeeulizwa "is there anything good comes out of here?" Kusema kweli nimeshindwa kujibu, and that is when i say i am not proud of ........
 
Meremeta ni mali ya jeshi kwa hiyo hairuhusiwi by sheria kuiongelea kwenye public!,

Sasa ni vumbi tu lililokutwa bungeni, huu ni uchunguzi wa polisi uliochukua zaidi ya mwezi mmoja!

Only in Tanzania!

Kwangu haya sio matokeo ya kushangaza. NI kweli ameshika dume sisi tumeshika magalasa. This guy will get away with everything, nguvu ya fedha, inasema yeye si fisadi na hakufanya lolote baya. Kama serikali inashindwa kupropve kuwa yuko guilty inawezekana siku watanzania wakafanya hivyo na wakatoa hukumu.

Mkora said:
Lakini Hata Hosea alisema mkataba wa richmond hauna hata chembe ya ufisadi
kiko wapi sasa
Wote tunajua ngoma ya kitoto siku zote huwa haikeshi .

Hebu tuangalie upande wa pili wa thumni.....inawezekana kuna njama za kuifanya serikali ya Muungwana kuwa ni mbovu?.....au ndio anatafutiwa njia ya vote of no confidence?.......huko tuendako inawezekana hizi ni harakati za impeachment?....(ni mawazo tu)
 
Hebu tuangalie upande wa pili wa thumni.....inawezekana kuna njama za kuifanya serikali ya Muungwana kuwa ni mbovu?.....au ndio anatafutiwa njia ya vote of no confidence?.......huko tuendako inawezekana hizi ni harakati za impeachment?....(ni mawazo tu)

Kama ni Mwungana mbona amekaa kimya? Hawa ni watendaji chini yake. Amewachukulia hatua gani. Usilaumu njama. Laumu inaction ya Mwungana. He is his own worst enemy.
 
Hebu tuangalie upande wa pili wa thumni.....inawezekana kuna njama za kuifanya serikali ya Muungwana kuwa ni mbovu?.....au ndio anatafutiwa njia ya vote of no confidence?.......huko tuendako inawezekana hizi ni harakati za impeachment?....(ni mawazo tu)

Hata hivyo nakubaliana na MT kwa msharti kuwa kabla ya wabunge wote hawajajadili MUSTAKABALI WA NCHI ESP KUHUSU RIPOTI...Taarifa zote za wabunge wote na hisa ama nafasi wanazomiliki kwenye makampuni ziwekwe wazi ili kusiwe na bias bali THE TRUTH!
 
Hebu tuangalie upande wa pili wa thumni.....inawezekana kuna njama za kuifanya serikali ya Muungwana kuwa ni mbovu?.....au ndio anatafutiwa njia ya vote of no confidence?.......huko tuendako inawezekana hizi ni harakati za impeachment?....(ni mawazo tu)

Ukweli ni kwamba hawa jamaa wa hili kundi wana nguvu sana, ni almost serikali ndani ya serikali yetu, muungwana naye pia inaonekana kuwa either wamemizdi nguvu au yuko nao, kwa sababu haiwezekani hata Waziri Mkuu akaogopa watu ndani ya serikali ambayo yeye ndiye kinara, sasa anamuogopa nani?

Maana sio siri tena among wakuu wa taifa kuwa uamuzi wake on Meremeta, haukuwa wa kwake, kwa sababu according to the data in the private anaongea maneno mazito sana dhidi ya mafisadi, sasa iweje akija public anakuwa bubu? Anamuogopa nani? Hatuwezi kusema kuwa anamuogopa Shein,

Sasa Pinda anamuogopa nani? Hata huu uamuzi wa polisi na unga wa vumbi, hauwezi kuwa umeamuliwa bila ya kumfahamisha mapema, ndio maana umechukua karibu mwezi mzima kuutoa maana yake ni kwamba walikuwa kwanza wana-touch base zote kwanza!
 
Back
Top Bottom