Hakuna derby kati ya Azam na Simba au Azam na Yanga!

Hakuna derby kati ya Azam na Simba au Azam na Yanga!

Akili yangu ina shida,niambie derby inaangalia nini?

Sent using Jamii Forums mobile app


Derby ni match ya team za mji/kitongoji kimoja,

Simba Vs KMC ni derby,
Sema utofaut ni kuwa kuna derby zina mvuto nyingine hazina mvuto, zenye mvuto ndio hizo zina vitu unasema wew, kama fanbase kubwa, history inayofanana, history ya kuibiana wachezaji etc,

Ila hata bila ya hivyo hapo juu match ya team za mji mmoja ni derby
 
Fc Porto mji wa Porto vs Benfica mji wa Lisbon, Dortmund B vs B Munich hizi ni nini? Hizo zote ziko miji tofauti tofauti na zimeorodheshwa ni moja kati ya derby kubwa ulaya

Bayern Vs Dortmund sio Derby
 
mkuu, kuna derby za miji, kuna derby za mikoa, kuna derby za mitaa. Kwahiyo unatakiwa upeleleze makini usikurupuke.
Mnaokurupuka ni nyie mnaosema derby ni mpaka wote mtoke jiji moja. Sasa hivi ndio mnashtuka baada ya kuwaletea ushahidi kuna derby za wapinzani kutoka majiji tofauti.
 
Derby ni mechi kati ya timu za mji mmoja.
Kuna London derby halafu kuna north London derby

London derby= arsenal VS chelsea
North London derby= arsenal VS Tottenham

Azam na simba ni Dar es Salaam derby
Simba vs Yanga ni Kariakoo derby

Kama ile timu ya African Lyon ingekuwa bado ipo ndio ingekuwa Mbagala derby kati ya Azam na African Lyon
Nataka niseme uko sahihi lakini najiuliza je KMC na Simba Kwa muktadha wako zinaweza nazo zikawa Derby??
 
Mnaokurupuka ni nyie mnaosema derby ni mpaka wote mtoke jiji moja. Sasa hivi ndio mnashtuka baada ya kuwaletea ushahidi kuna derby za wapinzani kutoka majiji tofauti.

narejea tena kuna mji, kuna mtaa, kuna mkoa, na vyenginevyo, hatujasema kuwa lazima iwe ni mji tu.
 
London Derby Chelsea Vs Arsenal
North London Derby Totenham vs Arsenal
Mersey Side Derby Everton Vs Liverpool
Manchester Derby Man City vs Nyumbu Utd


West Ham, Fulham, Nottingham Forest, Crystal Palace, Brentford hizi zote ziko London lakini husikii zinaitwa Derby baina ya Chelsea, Arsenal au Totenham.
Ujuaji mwingi utachapwa Mashine


Kafuatilie Derby zingine za London Sasa uwe unaacha kiherehere
Screenshot_20240210-094744.jpg
 
Sijui kwanini Azam media wanalazimisha timu yao ya Azam kwamba ni derby dhidhi ya wakongwe wa Kariakoo?

Kwanza ni timu ya juzi hakuna derby kati ya baba na mtoto,

Mafanikio ya mataji haiwezi kufika hata robo ya Simba na Yanga

Kwa mashabiki hata robo ya hizo timu Azam haifiki.

Sasa wanavyosema azam ni derby kwa Simba na Yanga ni derby kwenye nini hasa hawana umri sawa kuanzishwa,hawana mashabiki, wana kikombe kimoja tu cha ligi.

Kama wanaangalia timu ambazo zote zipo Dar basi Azam anafaa kuwa derby na KMC maana hata umri wanaendana kwa mbali.

Azam kuwa derby kwa Simba na Yanga ni kuzishusha hadhi Simba na Yanga.

Sent using Jamii Forums mobile app
Yanga na Simba ni timu za Kariakoo, Azam ni timu ya Mbagala-Chamazi.
Mechi zilikuwa zikichezwa taifa, watu wa Mbagala walikuwa hawajawahi kukaa kusubiri hadi filimbi ya mwisho, walikuwa wanaondoka mapema kwa ajili ya kuwahi muda na magari, wale wa Kariakoo zinapotoka Simba na Yanga hao walikuwa wakibaki hadi mwisho.

Siku hizi Mechi zinachezwa Chamazi, kwenye Uwanja wa Azam. Sasa hivi watu wa Kariakoo na kwingineko zinapotoka Simba na Yanga ndiyo hutakiwa kuondoka mapema ili kuwahi usafiri (Shukrani kwa nyakati kubadilika ambapo magari hufuata watu pia yapo ya kutosha, zamani watu walikuwa wakitafuta magari), lakini wale wa Chamazi hubaki.
Derby inaenda beyond ulinganifu wa Makombe pekee, Derby inaangaliwa hadi katika viwango vya mafanikio na uchumi wa timu, je mpaka hapo bado utasema Mtibwa Sugar ni zaidi ya Azam?
 
Ujuaji mwingi utachapwa Mashine


Kafuatilie Derby zingine za London Sasa uwe unaacha kiherehere View attachment 2899302
DOgo tuliza kalio. Wenzako wanakuja kistaarabu wanapewa maelezo wanapita kushoto. Naona wewe unakuja na miwasho ya tako nitaishia kukupaka upupu tu.

Hiki ulichoniandikia kuna wenzako wawili wameshakieleza na nimeshasema siwezi kurudia, soma comments zote usianze kujiona mjanja kuja kichwa kichwa. Nimemaliza
 
Derby ni mechi kati ya timu za mji mmoja.
Kuna London derby halafu kuna north London derby

London derby= arsenal VS chelsea
North London derby= arsenal VS Tottenham

Azam na simba ni Dar es Salaam derby
Simba vs Yanga ni Kariakoo derby

Kama ile timu ya African Lyon ingekuwa bado ipo ndio ingekuwa Mbagala derby kati ya Azam na African Lyon
Umeweka vzr sana ..kwangu mimi nimeelewa
 
Watani Wa Jadi Ni Simba vs Yanga Tu




Hakuna KMC, AZAM, Dhidi Ya Simba vs Yanga
 
Back
Top Bottom