Hakuna Fao la Kujitoa NSSF duniani kote - Ramadhan Dau

Hakuna Fao la Kujitoa NSSF duniani kote - Ramadhan Dau

Kitakusaidia nini? wakati bado una nguvu zako na unaweza kufanya kazi. Kumbuka hizo fedha zinawekwa pale utapokuwa umeishiwa na nguvu na madhara ya kupewa mapema yameonekana ndio maana kwa upande wangu naona ni bora inavyofanywa sasa kwani ukiwa hauna nguvu huna haja ya kuwa Matonya.

Nakushangaa!!!!!!. Hivi ni watanzania wangapi walioajiriwa kama sio idadi ndogo sana? je hao ambao hawajawahi wala hawajaajiriwa hawahitaji kuangaliwa maisha yao uzeeni? kuna utaratibu mwingine walioandaliwa watu hao?

Kuna mahitaji ya msingi kabisa ambayo hivi sasa serikali imeshindwa kutoa kwa wananchi wake ikiwa ni pamoja na maji safi, huduma bora za afya, usalama wa raia, elimu bora pamoja na usafiri nk nk, itakuwaje serikali hiyo hiyo iniandalie maisha bora ya uzeeni? huu ni wizi wa mchana kweupee!!

"Mtu mwenye akili akikueleza kitu cha kijinga huku akijua una akili anakudharau" mwl. J.K. Nyerere.
 
Naomba kueleweshwa...ni nssf pekee au na ppf pia....nataka kuongoza kiwango cha hasira kwa ccm na kikwete
 
Nimemsikiliza huyu mkurugenzi akiwa anaongea. Yaani ilibaki kidogo nipate hasara ya ka TV nilikokuwa nakaangalia kwa jirani. Kaonyesha wazi kuwa yeye sio mbunifu. Anasema eti hata wapi sijui huko hakuna fao la kujitoa. Mwambieni siku zote mambo mazuri ndio ya kuigwa. Wanatakiwa hao Ambao hawana hili fao awaalike waje waone tumewezaje sisi kuwa nalo kwa miaka yote na mifuko ikawa bado imara. Kwa akili yake kama ulaya au Amerika hawafanyi jambo fulani sisi hatutakiwi kulifanya?

Hawa watu wana matatizo, siku zote walipokuwa wanaruhusu fao la kujitoa walikuwa wanawaza nini, kinachotakiwa watoe sababu za msingi kwanini zamani walikuwa wanatoa tena walikuwa wanakuacha mpaka miezi 6 ipite kama hujapata ajira wanakupatia iweje leo waondoe fao hilo. Kwa uzoefu tu si kwamba watu wengi wanapenda kujitoa na wengi tu wamekuwa wakiendeleza michango yao pindi wanapopata ajira mpya ila zogo limekuja baada ya wao kufuta kabisa hilo fao kiasi kwamba wame-disturb akili za watu ambao wakati wanafanya kazi za mikataba huwa wanawaza pia incase mkataba umeisha na wasipo pata ajira kuna fao la kujitoa (wategemee mapato yao kushuka kwani kuna uwezekano watu wakachakachua hata viwango vya mishahara, chezea sekta binafsi kila kitu kinawezekana mtu analipwa million 2 dcoument zinaonyesha analipwa laki 5 alafu ela zingine anazichukua direct na mshahara)

Penshion zao waache kwa watumishi wa serikali ambao wana ajira za kudumu na tumeshuhudia baba zetu wakifa mapema kwa kupata pendion pasua kichwa ya 80,000/= kwa mwezi, kipi bora hapa kuacha let say milioni 20 mpaka afikishe miaka 55 wakati ana miaka 40 ambapo katika kipindi chote hiki ataishi kwa shida. mie kwangu maisha ni haya tuliyonayo na kwa taarifa watu walioko sekta binafsi wamejipanga kimaisha kuhakikisha mambo yapo sawa kabla ya kustaafu kutokana na nature na changamoto ya kazi yao.

Wakiruhusu tu hata hiyo PPF wategemee wengi kujitoa hasa watu wa machimboni maana kuna watu wamechangia zaidi ya milioni 30 hivyo mtu atachukua chake mapema na kutafuta kazi nyingine ili azifanyie mchakato maana serikali yetu ni kigeugeu
 
Naamini atakuwa katumwa na sheikh kikwete kuongea ujinga huo
 
Kwa sasa ni afadhali kufanya kazi kwa mhindi tu,no NSSF wala Loan Board!
 
Hii ndiyo Bongo. Kuna waziri mmoja alipendekeza rais ampe DAU tuzo ya nishani kwa utendaji uliotukuka. Kama kila kitu lazima kianzie kwa wazungu basi ni wakati muafaka CCM na sirikali yake watafute wazungu kuwa mawaziri na watendaji wakuu wa mashirika kama nssf ....
 
Baba yangu mapaka leo hajalipwa stahili zake za EAC. Je duniani kote linafanyika hili? Kenya na Zanzibar zikiwemo?
 
Dah inauma sn,mtu uache kazi usubiri miaka 60 km unataka kujiajiri kwa capital hiyo je,..kweli tusikubali.na uyo mkuu atujibu ikifka hyo miaka 60 kuna kinachoongezeka km faida au unapewa pesa hyohyo?km vp hakuna haja ya hayo mamifuko bora tuchimbie chini au benki,kwanza nilickia nao nssf wataanza kukopesha??upu...z hela yako afu unaikopa tena
 
Kwa tamko lake inaonyesha mswada wa kupelekwa bungeni umekufa kifo cha kawaida.

Inawezekana kauli yake ikawa ni muhtasari wa yatakayojiri kikao kijacho cha bunge...wabunge wapiganaji inabidi sasa wabadili mbinu.....nashauri wapeleke muswada wa marekebisho ya sheria ili kuchangia mifuko ya pensheni iwe ni hiari ya mwajiriwa. Nipe changu nile sasa...nani ana uhakika wa kufika uzeeni? Besides, kwa mfumuko huu wa bei hata ulipwe bilioni wakati wa kustaafu hazitakuwa na maana kwa vile kumwona daktari tu inaweza kuwa vimilioni kadhaa...nauli ya daladala vilaki kadhaa...Mungu tunusuru waja wako. Amen
 
Wewe ndo mdini na unacho mchukia ni kwa sababu ya dini yake sio kingine.Mtajibeba chadomo 2015 na u ukristo wenu kama mtagusa ikulu.
Huyu kilaza Dau ni janga sana kwa taifa letu na pia ana udini sana. Natamani 2015 ifike haraka ili tumuondoe hapo haraka sana.
 
Katika hali ya kuthibitisha unafiki kwa vitendo Zitto Zuberi Kabwe ameuthibitishia umma wa walala hoi kuwa hayuko nao kwakuwa atavuta zake baada ya miaka mitano ijayo pale alipokubaliana na (-DR) Ramadhani Dau kuwa duniani kote hakuna fao la kujitoa na akajichekesha kwa unafiki uliotukuka, eti huyu anataka kuwa rais. Inakera sana hii lazima tukemee unafiki kwenye maslahi ya umma na umaskini huu .....NSSF ndio mkombozi ......baada ya miaka 55 NSSF watapiga hesabu ya inflation au ni wizi mtupu?????
 
Kwa sasa ni afadhali kufanya kazi kwa mhindi tu,no NSSF wala Loan Board!

Kweli though unanyonywa but mwisho wa siku ukiachishwa kazi unakuwa stress free kwani huna akiba yoyote unajipanga upya kulikoni sasa hivi unapigwa chini aloafu NSSF una milion kadhaa na kazi hupati, shida zinaongezeka kiasi kwamba kila ukifikiria hela zako za NSSF ambazo umeshindwa kuzipata mpaka ufikishe miaka 55 unazidi kuchoka psychologically, hakuna kitu kibaya kuwa na shida alafu unamdai mtu hela hakupi, shida huwa inakuwa kubwa kuliko mtu mwenye shida ambae hana mtu wa kumdai
 
Angekuwa mbele ya uso macho yako, ungempa adhabu gani?
Je ni kitu gani ulukisema moyoni mwako kimyakimya baada ya kumsikia.
Tiririka wanja ni wako. Hiwe abari ndi hiyo kwake

attachment.php
 

Attachments

  • dau_300_222.jpeg
    dau_300_222.jpeg
    7.3 KB · Views: 220
Yaani kuna wakati inabidi kufanya tathmini yakinifu kuwa hivi hii nchi ina wawakilishi wa wananchi au ma box matupu?? Hapa watub wakiambiwa wanafikiria kwa kutumia masaburi wanakuwa wakali. Pesa ya kwako,wewe ndio umeamka asubuhi kila siku hadi jumapili na kila siku ni vikumbo kwenye daladala kwa kwenda mwezi na daily umesimama kuwahi kazini,hili ni jasho letu ila sasa inakuwaje linatokea jitu ambalo linaendesha gari la kifahari na asubuhi anakupita bila hata huruma pekeake na dereva wake tu ndani ya aidha STK au SU ambayo yote ni kodi zetu hadi mafuta na kusema bila hata punje ya aibu kuwa mafao hadi umri wa kustaafu. This is way too much and quite unbearable
 
Lazima tufanye mgomo wa kutisha. Wao wanamwaga mboga na sisi tumwage ugali. Bora kukosa wote. Wanasiasa wamekosa heshima kabisa. Laana inatembea nao siku zote.
 
Mlikuwa hamuamini unafiki wa zitto sasa oneni wenyewe...............huyu alishavuta epa yake toka ccm utamwambia nini mzee wa hummer? Anababaisha tu watz
 
Mkuu waziri ameshasema hiyo hoja haipo bunge hili labda mpaka bunge la mwakani.

Waziri mkuu alishasema kwamba hoja itasoma bunge hili la october/november sasa kama waziri wa kazi kasema halitakuwepo ngoja tuone itavyokuwa maana kauli ya PMinister ndio ya mwisho....
 
Back
Top Bottom