Hakuna Fao la Kujitoa NSSF duniani kote - Ramadhan Dau

Hakuna Fao la Kujitoa NSSF duniani kote - Ramadhan Dau

Unasema nini wewe wakati kwa mara ya kwanza tunaona wakulima wakisaidiwa na mifuko ya pensheni? huyo huyo ambae ameboresha NSSF huyo huyo aliyeleta huo mpango mzuri wa mafao uzeeni huyo huyo ndiye kwa mara ya kwanza tunaona hizo fedha zetu zikijenga madaraja, vyuo vikuu, na zikisaidia wakulima na wafanya biashara, hata Mbowe alikopoa huko mamilioni kibao kuendeleza disko lake la bilicanasa, au hujui?

Kuhusu wakulima soma chini hapa fata na hiyo link, na kwa mara ya kwanza tunaona mifuko ya pensheni ikianza kufikishwa kwa wakulima, ambao ni zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania. walikuwa wapi wa kabla ya Dau na Kikwete? kwanini hatukuyaona yote hayo?

Wakulima wahakikishiwa huduma bora

Tatizo mmeshazipangia pesa zetu mzitumie kwenye uchaguzi 2015 kununulia kanga na fulana siyo!!
Imekula kwenu pesa yetu ni chungu hailiwi.Tunajua Dau ni rafiki wa Dhaifu wamekaa na kushauriana
huu ujinga aliokuja kuusema.Hii itawagharimu kuliko inavyomgharimu Zuma S.A
 
Sheria ya workmana compnsation mpaka leo haijasainiwa hii ya mifuko ya jamii imesainiwa haraka sana kuna ajenda gani nyie???
 
Dau asituzingue na historia ya wenzetu. Inamaana kama kenya wanakunya barabarani kwa hiyo na sisi tuige kunya barabarani?
Kenya baadhi ya wastaafu au walioachishwa kazi wakiwa na umri mdogo wengi wao wamepoteza haki zao. Tusiige upumbavu tuige uwerevu
 
mlitegemea nini kutoka kwa RAMADHANI? haya huyu hapa nimemzungushia duara yupo kijiweni

attachment.php
 
Bwana Barubaru, Ki Jiolojia, Heavy metals and other minerals tabia haziko sawa kabisa na madini (sijui kama nayo yanasifa ya madini) yaitwayo mafuta, Dhahabu, Almasi n.k huwa migodi yake inafungwa, mfano ni Buhemba na Tulawaka plus Nzega, itafungwa very soon! Chukua muda wa kufanya kautafiti kidogo, hilo moja, pili, security ya kazi huko Uarabuni na huku kwetu ni vitu viwili tofauti, wapo wenzetu wengi tu huko wanafanya kwenye migodi ya jinsi hii, hata mshahara tu, mgeni hawezi kumzidi mwenyeji kama wapo rank sawa, huku kwetu sisi sio issue ya rank tu, mgeni hata kama unamzidi Rank, bado atakuzidi tu mshahara, so point yangu hapa ni hii, kulinganisha vitu mjaribu kua fair, angalieni in all angles, sio kuangalia just a single angle only!

Mazindu M.

Unachozungumza ni kweli kabisa lakin huku kwetu sisi thamani kubwa ipo kwa mzawa na mgeni baadae. Sera zetu zote zinamwangalia mwananchi zaidi kuliko mgeni na hata panapotokea ilmu ipo sawa baina ya mgeni na mwenyeji basi mwenyeji anapata ujira zaidi kulinganisha na mgeni.

Kifupi sera zetu zinalinda sana wenyeji tofauti na huko Sera zenu zinamwangalia na kulinda wageni zaidi kuliko wazawa.

Kumbuka huku kwetu mfanyakazi anaweza kujengewa au kununua nyumba kutokana na mafao yake ya Uzeeni. Anapata hata mikopo ya kuanzishia Biashara mbalimbali na security yake ni pesa zake za uzeeni.

Ni wakti muafaka kuangalia wazawa kwanza na kunufaisha wazawa zaidi ya wageni. Wenye mamlaka ya kufanya hayo yote ni Serikali na Bunge.

 
Ni kweli anayosema lakini atutajie nchi yoyote ambayo pesa zao za mafao zinawekezwa kwa stahili ya uwekezaji wa tanzania ambapo pesa zinatolewa kienyeji ili kuifuraisha serikali au wakubwa wa serikali na ukopeshaji kwa watu wasio wanachama kama Manji kuwataja wachache
Atueleze namna gani atarudisha pesa zilizowekezwa kwenye miradi ambayo mpaka sasa hivi haijarudisha pesa kama machinga complex,general tyre,kiwira mine kuitaja kwa uchache
Pia atueleze kwanini riba wanayotoa kwa mafao ya wafanyakazi ni ndogo 1.8% kwa mwaka ambayo hailingani na riba za kibenki wala mfumuko wa bei wa Tanzania
hatueleze kwanini wafanyakazi hawapewi hisa kwenye miradi ya uwekezaji wa nssf wakati ni pesa zao ndio zinatumika
 
Tatizo mmeshazipangia pesa zetu mzitumie kwenye uchaguzi 2015 kununulia kanga na fulana siyo!!
Imekula kwenu pesa yetu ni chungu hailiwi.Tunajua Dau ni rafiki wa Dhaifu wamekaa na kushauriana
huu ujinga aliokuja kuusema.Hii itawagharimu kuliko inavyomgharimu Zuma S.A

WEB%20PAGE%20NSSF_Page1.png


Na hawa ni mashahidi wa miaka ijayo:

Wanafunzi+wa+darasa+la+pili+katika+shuile+ya+msingi+Mnazi+Mmoja+jijini+Dar+es+Salaam+wakiangalia+mchoro+wa+daraja+la+Kigamboni-.jpg
 
Dr, dau . Wewe unalala gorofani unakula mpaka unasaza , sitarehe zote duaniani ukipenda unapata ebu fikiria wachimaji na wafanyakazi wengine wanaacha kazi hali zao mbaya ,kiukweli wanatisha , wana umri wa mika 23 mpaka 40 eti wasubiri mpaka 55 to 60 haiwezekani. Fikiria hata hawa masikini hawa . Usione kwa kuwa wewe unmejaliwa kipato ukadhani wote ni hivyo hapana. Kwa wale wanaoendelea na kazi hao sawa .lakini wanaoacha tafadhalia sana dau wapeni fedha zao. Wewe kinakuuma nini. Au umejengea madaraja na mabweni dodma? Kuwa mwenye upendo kwa masikini na wewe utabarikiwa kwa kauli yako ya jana ni kama wewe si mtanznia . Kuwa nahuruma walau kidogo dr. Dau. Utajiri wako unaweza kugeuka kuwa laana kama utaendele kudharau masikini hawa.
 
Sijui DUNIANI kote anakuelewaje?

Types of UK Pensions.

Brief explanations of the different types of UK pensions are given below, please follow the links for more information.

Basic state pension.
Although an entitlement for most people, the amount received from the basic state pension will depend on the amount of national insurance contributions paid. more >>

State Second Pension.
On 6 April 2002, the State Second Pension (S2P), introduced by the Child Support, Pensions and Social Security Act 2000 replaced the State Earnings Related Pension Scheme (SERPS). more >>

Personal and Stakeholder pensions.
Personal pensions, introduced on 1 July 1988, originally aimed to give people who were not part of a company pension scheme their own portable pension, designed on a money purchase basis although since April 2001 certain individuals who are members of company pension schemes can also take out personal pensions. more >>

Occupational pension schemes.
Employers can set up occupational pension schemes for their employees.Public sector schemes typically offer pension accrual of 1/80th of final remuneration for each year of service up to a maximum of 40 years plus a tax free lump sum of up to 1.5 x final remuneration.
Private sector schemes can be either final salary schemes known as defined benefit schemes or money purchase schemes known as defined contribution schemes. more >>

Additional Voluntary Contributions (AVCs).
It is now compulsory for companies to offer employees the opportunity to invest additional contributions into their occupational scheme where there is one, in order to boost retirement benefits. more >>

Free Standing Additional Voluntary Contributions (FSAVCs).
Free standing additional voluntary contribution schemes (FSAVCs) were introduced in 1987. more >>

Self Invested Personal Pension Schemes (SIPPS).
From April 6th 2006 Government proposals for pension simplification came into effect. This has lead to many new opportunities for people to invest their savings for the long term with greater flexibility when it comes to retirement and ways of generating an income. more >>


State Earnings Related Pension Scheme (SERPS).
The State Second Pension (S2P) replaced SERPS with effect from 6 April 2002. more >>
 
Ustaadhi Ramadhani Dau anapotulinganisha na nchi nyingine in terms of hii sheria ya fao la kujitoa, pia aende mbali atueleze ni kwa namna gani mifuko ya NSSF katika nchi hizo inawanufaisha wananchama kwa kuwakopesha kujenga nyumba, kusomesha watoto wao ama wao wenyewe ikiwa ni pamoja na kujifanyia shughuli nyengine za kimaendeleo kwa kutumia hizo michango zao za pensheni. Lakini pia atuambie kiwango cha security ya ajira katika nchi nyengine kama kinawiana na hapa kwetu.

Kama hayo niliyoyataja yanafanyika huko kwa wenzetu na hapa kwetu hayafanyiki basi anatakiwa aache kutuletea ujuaji wa kijinga ambao hauna maana yoyote kwa wananchama ambao ndiyo wenye fedha zao. Wakijifanya kuziba masikio sasa kwa mara ya kwanza wataiona hasira ya wafanyakazi mwaka huu.

Na wabunge wetu nao wakiamua kulikalia kimya suala hili bila kuilazimisha serikali kurudisha fao la kujitoa katika mifuko yote ya pensheni kama ilivyokuwa awali basi watambue kwamba hatutawaelewa kamwe katika hili, na vita yetu itaelekezwa kwao moja kwa moja.
 
Waarabu tunausemi unaosema '' NI RAHISI SANA KUWADANGANYA WATU, LAKIN NI VIGUMU SANA KUWAFAHAMISHA WATU KUWA MUMEDANGANYWA"

Je WaTz mnaweza kuishi dunia ya peke yenu? Dr amesema hakuna kitu kama hicho sasa kama mnabisha pitia mifumo yote ya pension Duniani muhakikishe maneno yake.

Lakin mimi namini kabisa alichobainisha ni kile kinachotumika Duniani kote. Ushauri wangu kwenu ni kuwa Murekebishe SERA zenu za Ajira na kazi
1.ziwe zinamlinda zaidi mwananchi badala ya mgeni.
2. Pesa za pension ziwe zinaweza kusimama kama dhamana kwa mwanachama kuweza kukopa bank.
3. Pension ziwe na saccos zake kukopesha wanachama wake.
4. Kuboresha mafao kwa wananchama.

Yote yatawezakana kama Serikali yenu na Bunge lenu litakapo jaribu kuangalia nchi nyingine zinafanyaje.
 
Hivi mi nauliza "where are these hounourable members?" Tuliwachagua kufanya nini? Jamani tumeshachoka na maamuzi ya kiimla. Wasiporekebishia wafanyakazi fao la kujitoa, ni vizuri tupate orodha ya waheshimiwa wetu ambao hawakutusupport, maana 2015 siyo mbali. Halafu ndo na wao waelewe msemo adui muombee njaa. (maana wakishindwa kurekebisha na wao pia wabanwe na huo huo msumeno).
 
Watu wa Maifa Makubwa ya ulaya na Marekani wanapenda kuweka historia ya jambo fulani,
hasa kwa kuanzisha kitu au Mfumo mpya then Dunia inaiga/ kufuata..., hapa kwetu is unlike kwani
wataalamu na Viongozi wetu wengi ni vihiyo, hawana uwezo wa kuleta new ideas na ubunifu kwani
wamezoea "Copy and Pest", bila hata aya na kukosa kujiamini , jitu linasema bila ya kuangalia uhalisia
wa mifumo ya kazi ya wananchi...,kwakweli hana Mashiko kimtazoma wa Mawazo.



 
Ahahaha!!!! Dau anataka kuhalalisha wizi wa duniani kwingine Tanzania. Kwi kwi kwi kwi kwi kwi!!!
Hii fukuza fukuza hata ya serikali iliyokuja kwa jina la kustaafisha kila siku watu wanastaafishwa kwenye mashirika mbali mbali hiyo nayo iko duniani kote?? Sawa hakuna shida lakini sio kila kitu cha duniani kote ni halali kwetu. Huu ndio ujuha tulionao wa kukopi na kupesti ili wahalalishe matumizi mabaya ya wafanyakazi maskini wanaoishi kwa kupunjwa mishahara!
Kazi kwenu wafanyakazi msipochangamka shauri yenu. Mmeshaliwa na wakina Dau ambao mwisho wa siku wanatafuta wapewe nafasi ya kugombea uongozi kupitia bunge au lichama linaitwa sisi M.
 
Dah inauma sn,mtu uache kazi usubiri miaka 60 km unataka kujiajiri kwa capital hiyo je,..kweli tusikubali.na uyo mkuu atujibu ikifka hyo miaka 60 kuna kinachoongezeka km faida au unapewa pesa hyohyo?km vp hakuna haja ya hayo mamifuko bora tuchimbie chini au benki,kwanza nilickia nao nssf wataanza kukopesha??upu...z hela yako afu unaikopa tena

Na kuvumilia kwenye kazi ya kusuasua, bosi mwenye majungu na written warnings kibao, halafu tena ubaniwe hela yako...Aisee hata ladha ya mate inakuwa shubiri.
 
Mazindu M.

Unachozungumza ni kweli kabisa lakin huku kwetu sisi thamani kubwa ipo kwa mzawa na mgeni baadae. Sera zetu zote zinamwangalia mwananchi zaidi kuliko mgeni na hata panapotokea ilmu ipo sawa baina ya mgeni na mwenyeji basi mwenyeji anapata ujira zaidi kulinganisha na mgeni.

Kifupi sera zetu zinalinda sana wenyeji tofauti na huko Sera zenu zinamwangalia na kulinda wageni zaidi kuliko wazawa.

Kumbuka huku kwetu mfanyakazi anaweza kujengewa au kununua nyumba kutokana na mafao yake ya Uzeeni. Anapata hata mikopo ya kuanzishia Biashara mbalimbali na security yake ni pesa zake za uzeeni.

Ni wakti muafaka kuangalia wazawa kwanza na kunufaisha wazawa zaidi ya wageni. Wenye mamlaka ya kufanya hayo yote ni Serikali na Bunge.


Nakuunga mkono Barubaru, ndio maana mwanzoni nilipingana na wewe kulinganisha issue ya fao hilo la kujitoa hapa Tanzania na huko kwenu, hapa kwetu nidhamu ya pesa hakuna kabisa, mashirika mengi ya umma yalikufa sababu zikiwa ni nyingi, moja wapo ni hii, serikali kujichulia pesa na kwenda kufanya mambo ambayo hayana uhusiano wowote na hiyo shirika, utakuta pesa inachukulia kwenda kwenye kampeni za ccm, mbio za mwenge, safari za waheshimiwa au posho za vikao, kwa mwendo huu wa akina Dau, sitashangaa nikisikia mifuko hii imefirisika siku moja, biashara lazima ifuate miiko yake, ni kweli suala la kujengwa daraja la kigamboni ni la muhimu, na ni kweli kwamba ujenzi wa chuo kikuu cha dodoma aua hosteli za Mabibo ni muhimu, lakini hebu tujaribu ku imagine, Mkurugenzi mkuu wa mashirika haya angekua Mzungu, hivi unadhani wangechukua hizo pesa na kwenda kufanyia mambo hayo? siasa za ccm ndio zinazofirisi nchi hii, uliisha wahi kujiuliza, how comes waastafu wa uliokua jumuia ya Africa mashariki kwa nchi zingine waliisha lipwa, mbona hapa Nyumbani badala ya kulipwa wamenunuliwa gari la maji ya kuwasha? ukweli ni huu, mimi kama mfanyakazi, sina imani kabisa na serikali ya ccm kwamba inaweza kunitunzia pesa zangu hadi nitakapo fika uzeeni, kama waliweza kuiba pesa za EPA ili tu ccm iingie madarakani, na kumbuka wakati ule wa uchaguzi wa 2005 ccm haikua na upinzani mkubwa kama leo, hivi 2015 watatumia pesa kiasi gani ili waendelee kua madarakani, na hizo pesa watatoa wapi?

Nashukuru kwa kunipa masikio yako.
 
Me nashangaa, sijui hata hawafikiriii hawa watu???? hivi fikiria umefanya kazi na kampuni kama sita na pengine ni mikoa tofauti, hivi utakapofikisha umri wa kustaafu hizo fomu za mafao yako anakujazia nani???? au ndo unaanza kuzunguka tena kutoka ofisi moja hadi nyingine??? na hiyo gharama unapata wapi??? si matokeo yake utakuta mafao yako utakuta umeshayamalizia kwenye gharama za kufatilia hizo fomu zako zijazwe?????? na huwezi jua wakati mwingine hizo ofisi zilishafungwa na kufa. Mimi nina wasi wasi hiyo hela wameshakula wanatafuta njia rahisi ya kututapeli pesa zetu. sidhani kama wanaona mbali hawa watu, la sivyo ni wabinafsi, wanajali matumbo yao na familia zao wanatusahau sisi ambao kimsingi ndio mabosi wao maana hayo hayo mafao yetu ndo yanawaweka hapo maofisini.
 
Unasema nini wewe wakati kwa mara ya kwanza tunaona wakulima wakisaidiwa na mifuko ya pensheni? ....
Kuhusu wakulima soma chini hapa fata na hiyo link, na kwa mara ya kwanza tunaona mifuko ya pensheni ikianza kufikishwa kwa wakulima, ambao ni zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania. walikuwa wapi wa kabla ya Dau na Kikwete? kwanini hatukuyaona yote hayo?


Wakulima wahakikishiwa huduma bora

Kumbe " Asasi ya Kusaidia Uwekezaji Kwenye Kilimo (Pass)" ni ya NSSF?
 
Mkurugenzi wa NSSF Dr Ramadhan Dau amesema Fao la kujitoa limeondolewa ili kuendana na mfumo wa kimataifa kwani duniani kote hakuna Fao la kujitoa.

Amesema hata Zanzibar na Kenya hakuna kitu kama hicho.

Mkurugenzi huyo alitoa tamko hilo alipokuwa akihojiwa na Kamati ya bunge ya mashirika ya umma inayoongozwa na Zitto Kabwe.

Source: ITV Habari

UPDATES.
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Muswada wa mafao wawaliza wafanyakazi




Muswada wa marekebisho ya sheria ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ambao unatarajiwa kuwasilishwa katika mkutano wa Kumi wa Bunge, umewaacha solemba wanachama wa mifuko mingine baada ya marekebisho hayo kurejesha fao hilo kwa mfuko mmoja pekee.

Sheria ya mafao ilipitishwa katika mkutano wa Bunge wa Aprili mwaka huu na kuwazuia wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii kuruhusiwa kuchukua mafao yao hadi wafikishe umri kati ya miaka 55 na 60.

Baada ya wanachama wa mifuko hiyo na wadau wengine wakiwamo wabunge kuipinga sheria hiyo, serikali iliahidi kuwa itaifanyia marekebisho na kuwasilisha muswada kwa hati ya dharura.

Tayari Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, amekwishawasilisha muswada huo katika Ofisi Ndogo za Bunge, jijini Dar es Salaam, ikiwa na maana kuwa utajadiliwa kwenye Mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza wiki ijayo.

Muswada huo unakusudia kufanya marekebisho ya sheria mbalimbali.

Kwa mujibu wa muswada huo, ambao NIPASHE imeuona, sehemu ya sita inapendekeza marekebisho kwenye Sheria ya Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF), sura ya 372 kwa kuongeza kifungu kipya cha 44 ili kutoa fursa kwa mfuko huo kutoa fao la kujitoa kwa mwanachama wake.

Kwa maana nyingine ni kwamba wanachama wa mifuko mingine kama NSSF itaendelea kutumia sheria ambayo imelalamikiwa na wafanyakazi.

HOJA YA JAFO YAZIKWA

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kisarawe (CCM), Seleman Jafo, ambaye wakati wa mkutano wa Bunge wa Bajeti, alitaka kuwasilisha muswada binafsi, alisema amepata barua kutoka kwa Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashillilah, ikimtaarifu kwamba, serikali itawasilisha muswada wa marekebisho hayo, hivyo hana sababu ya kuandika muswada mpya.

Jafo alisema kwa kuwa alikwishawasilisha hoja ya kutaka marekebisho kwenye sheria ya hifadhi ya jamii, Bunge lilimweleza kwamba ni fursa kwa serikali au Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii; hivyo serikali imeazimia kuiwasilisha kwenye mkutano ujao.

“Lakini kwa hali hii ni kwamba serikali haitatatua matatizo ya msingi ya hoja yangu, muswada unatakiwa uguse mifuko yote kwa sababu malalamiko ni ya wafanyakazi wote,” alisema.

SUGU AIONYA SERIKALI

Kwa upande wake, Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu, aliionya serikali kutochezea wafanyakazi kwa kuwa kufanya hivyo ni kuhamasisha fujo.

Alisema ni vyema marekebisho yatakayowasilishwa bungeni yakarejesha fao la kujitoa kwa mifuko yote kwa kuwa wafanyakazi wengi hawana usalama kazini.

“Tunajua faida ya pensheni uzeeni kwa sababu ni msaada mtu anapostaafu, lakini kwa mfumo wa nchi yetu ambayo wafanyakazi hawana usalama wa kazi haiwezi kufanyakazi ipasavyo,” alisema.

Sugu alisema wafanyakazi kama wa migodini au hostelini wanafanyakazi katika mazingira magumu na wanaweza kuachishwa kazi wakati wowote hivyo fao la kujitoa litawasaidia.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhan Dau, alisema fao la kujitoa katika mifuko ya hifadhi ya jamii halimo katika sheria za kimataifa.

Dk. Dau, alisema hayo alipokuwa akijibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) katika kikao kati ya kamati hiyo na bodi na menejimenti ya shirika hilo, katika Ofisi Ndogo za Bunge, jijini Dar es Salaam jana.

Alisema pia ni Tanzania Bara pekee ndiko ambako kuna fao la kujitoa katika mifuko hiyo, lakini katika nchi za Kenya, Uganda, duniani kote, hata Zanzibar, suala hilo halipo.

Hata hivyo, alisema mwanachama wa NSSF anapoamua kujitoa, anaupunguzia Mfuko mzigo wa kumtunzia pensheni yake ya uzeeni, badala yake na kujiumiza mwenyewe.

Shinikizo la kutaka serikali kuirekebisha sheria hiyo ili wanachama wa mifuko walipwa mafao wakati wanapoacha kazi, liliilazimisha serikali kukubali yaishe na kuahidi kuwasilisha muswada wa marekebisho ya sheria ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii wa mwaka 2012.

Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, aliliambia Bunge la bajati kwamba kabla ya kuwasilishwa, muswada huo utapelekwa kwa wadau ili watoe maoni na pia Mamlaka ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) itatoa elimu kuhusu fao la kujitoa.

Hata hivyo, alisema wapo baadhi ya watu waliotafsiri kuwa kusitishwa kwa fao la kujitoa kwamba mifuko ya hifadhi ya jamii imefilisika kwa kuwa imewekeza kwenye miradi mibaya, jambo alilosema sio la kweli.

Kabaka alisema kuwa mifuko hiyo haina hali mbaya kifedha wala haijafilisika na kwamba kuzuia fao la kujitoa ni utekelezaji wa sheria.

Waziri Kabaka alisema mchakato wa kuwasilisha muswada huo utaanza mara moja kwa kuwashirikisha wadau wote wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii.

Kabla ya kauli ya Kabaka, Bunge lilipitisha Azimio lililowasilishwa na Jafo, la kuletwa bungeni muswada wa dharura wa marekebisho ya Sheria Na. 5 ya mwaka 2012 inayozungumzia marekebisho ya Sheria ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ambayo ndani yake inaelezea kuzuiwa kwa fao la kujitoa kwa wafanyakazi.

Kutokana na mapendekezo ya muswada huo kutowatuhusu wanachama wa mifumo kingine kuchukua mafao kabla ya miaka 55 au 60, wanachama hao huenda wakashinikiza kwa njia za maadamano na migomo.

Aidha, upo uwezekano wa kuzuka mjadala mkali bungeni kwa kuwa na wabunge nao ni wanachama wa m
ifuko hiyo.


Naomba kuuliza Udaktali wa Ramadhani Dau ni wa MIFUGO au Phd? Kila nikimtafakari sipati jibu hata kidogo. Uwezo wake wa kuelewa mambo ni mdogo sana na huenda ameathiliwa na madrasa. Amefanikiwa kupanda mbegu ya UDINI katika Shirika la NSSF sasa ameamua kuleta maisha magumu kwa wafanyakazi. Tunajua utajiri mkubwa alioupata ni kutokana na miradi mibivu aliyoianzisha tangu awe Mkurugenzi wa NSSF. Sasa amekuwa tajiri kiasi cha kuanza kuiga kila jambo linalofanywa na MABWANA wa inje.

Tanzania sio lazima kufuata mambo yanayofanywa na jirani zetu au Ulaya. Tanzania ni Nchi huru inatakiwa kufuata mambo yake. Kama kwa wenzetu hawana fao la kujitoa; sio lazima na sisi tuwafuate. Kenya kula mirungi ni kitu cha kawaida, lakini Tanzania ni sawa na dawa za kulevya. Tanzania tunaruhusu kushafirisha sandalwood, wakati Kenya imezuiliwa. Bila shaka Mr. Dau elimu yake ni kukopi na kupesti ndo maana kila kitu anawaza kuiga nje na jirani wanafanya nini.

Wanachama wote wa mifuko ya hifadhi ya jamii wanahitaji kuyachukua mafao yao mara baada ya kuacha au kuachishwa kazi. Ajira za Tanzania hazina uhakika ukilinganisha na hizo Nchi anazotaka kukopi mambo yao.

Anadai eti kujitoa kwa Mwanachama kwenye mifuko ya hifadhi ni faida kwa mfuko husika. Sasa kwanini anakataa kujitoa kwa Mwanachama? Au tuamini maneno ya mtaani kuwa NSSF imewekeza kwenye miradi feki mingi kiasi kwamba wamefilisika?

Time value of money vipi? Wao wanawekeza pesa zetu kwenye mabenki kwa RIBA hadi ya 20% kwa mwaka, wakati Mwanachama hapati gawio la faida ya RIBA. Huu ni wizi wa mifuko ya hifadhi ya jamii dhidi ya pesa za Wanachama. Mr. Dau asifikili Watanzania ni wajinga hata kama wameufumbia macho uozo alioufanya pale NSSF kwa kuligeuza Shirika la Uma kuwa taasisi ya KIDINI.

Mimi na familia yangu tumeamua kufunga na kuomba ili laana ya Mungu aliye hai ishuke juu yake na uzao wake wote. Maana mbegu anayoipanda ni sumu katika Taifa letu na sasa anaingilia Uchumi wa Watanzania wasio kitu.
 
Back
Top Bottom