Yaani mkuu umeelezea my feelings kabisa ambayo huwa naipata nikipita eneo nililokulia (Tabata Bima), huwa nasikitika sana. Maeneo yenye kumbukumbu zinazoibua hisia kali, now yamekua baa, lodge, na ma fremu ya biashara. Maeneo ya viwanja tulivyocheza mpira enzi hizo utotoni, now yote ni majengo ya biashara. Mara zote nikipita yale maeneo napata hisia za huzuni sana.
Kuna uwanja mmoja wa mpira ulikua karibu na shule ya St Mary's pale, tulikua tunaenda kupiga boli pale timu yetu ya mtaa, tunakiwasha vibaya kabisa. Sasa hivi pote pamepigwa frame.
Kuna shortcut moja tulikua tunapita kutoka Bima kwenda Tabata Kimanga, tunakatiza bondeni hadi Kimanga....! Ile njia now haipo, kote ni majengo.
Wakati umekwenda wapi?