Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Hakuna mkoa mzuri wa kuishi kama Mbeya hapa Tanzania

Mbeya hakuna mji pale hasa mjini imekaa kama kijiji.

Maeneo yafuatayo ni mbeya mjini chini ya kilometer 2 kutoka city center lakini yote ni hovyo kwa mtogole tandale irudi shule.

Sinde
Ilolo
Mabatini
Isanga
Iwambi
Ilemi
Itende
Ilomba
Hovyo kabisa

Kidogo forest ndio kidogo sana waweza sema mji
 
Mbeya hakuna mji pale hasa mjini imekaa kama kijiji.

Maeneo yafuatayo ni mbeya mjini chini ya kilometer 2 kutoka city center lakini yote ni hovyo kwa mtogole tandale irudi shule.

Sinde
Ilolo
Mabatini
Isanga
Iwambi
Ilemi
Itende
Ilomba
Hovyo kabisa

Kidogo forest ndio kidogo sana waweza sema mji
Hayo ndio ya Maskini Sasa Mwanza unaijua? Maskini na matajiri wamechanganyikana humo humo,hakuna mitaa Kila sehemu ni uswazi na Kuna nuka 😁😁

Mara mia Mbeya Ina maeneo ya maskini na matajiri
 
Nimeishi mkoa wa Mbeya miaka 3 ni best place ever in TZ ,Bila kusahau kwa watani zangu Songea ni pazuri sana nyanda za juu kusini kuna uzuri usio na shaka
mbeya moja
soko matola moja hiyo
 
Nimeishi mkoa wa Mbeya miaka 3 ni best place ever in TZ ,Bila kusahau kwa watani zangu Songea ni pazuri sana nyanda za juu kusini kuna uzuri usio na shaka
mbeya moja
soko matola moja hiyo
Shida ya Songea ni rangi nyekundu ya vumbi 😁😁
 
Mbeya city home sweet home
20230519_093816.jpg
20230519_094149.jpg
20230519_093831.jpg
20230519_093448.jpg
20230519_094357.jpg
20230519_094229.jpg
20230418_122826.jpg
20230418_122159.jpg
20230325_164727.jpg
20230325_163314.jpg
 
Mkoa wa Mbeya ni Kati ya Mikoa mitano iliyopo Nyanda za Juu Kusini sanjali na Mikoa ya Ruvuma, Iringa, Songwe, Njombe na Rukwa. Mbeya ilianzishwa mwaka 1961.

Mkoa wa Mbeya umejaaliwa kila kitu unachokijua wewe.

Kwa hapa Tanzania sijaona Mkoa Mzuri wa Kuishi kushinda Mbeya.

1. Kiuchumi
Mbeya ni ya 3 Kwa kuchangia pato la Taifa yaani GDP Tanzania.

Mbeya ni ya 3 Kwa kuwa na Watu wenye kipato kikubwa.

 2. Hali ya Hewa na Mandhari
Mbeya Ina Hali ya hewa ya majira yote yaani Bariadi na joto na mvua ni uhakika sio tia maji tia maji kama Mikoa mingine.

3. Usafiri
Uwanja wa ndege wa Songwe
Usafiri wa Barabara kutoka Mikoa yote na Nchi jirani Kupitia Barabara kuu ya Tanzam. Usafiri wa kwenye Maji via Ziwa Nyasa. Pia Kuna usafiri wa reli nzuri kabisa unakufikisha Zambia kutokea Dar.

4. Kilimo
Mbeya Ina Ardhi nzuri ya kulima Kila aina ya zao kuanzia mbogamboga, matunda, nafaka Hadi pareto na chai.

5. Madini na Nishati
Mkoa una Kila aina ya Madini kuanzia Dhahabu za Chunya Hadi Makaa ya Mawe ya Kiwira bila kusahau Madini ya gas asilia ya CO2. Umeme ni wa uhakika unaozalishwa kutoka migodi ya Kiwira na Geothermal.

6. Elimu
Mbeya ni Kati ya Mikoa ya Wasomi hapa Tanzania. Mkoa wa Mbeya una vyuo Vikuu zaidi ya 5 mfano MUST, Mzumbe, CuCoM, UDSM, Tumaini, nk.

Mkoa una mamia ya vyuo vya kati na shule za kutosha eg St.Francis hivyo ni ideal pia Kwa issues za Elimu.

7. Utalii
Hapa kwenye Utalii ndio Kuna fursa nyingi maana sehemu kubwa ni underdeveloped.

Kuna Milima ya Kawetere, bwawa la Mungu, Hifadhi ya Kitulo na pia unafika Kwa urahisi Ruaha au Katavi NP kutokea Mbeya.

8. Viwanda na Biashara
Kuna viwanda vya aina mbalimbali kama Saruji, vinywaji vikali na laini kama soda, bia, wine nk.
Kuna viwanda vya magodoro, vifaa vya ujenzi, home appliances nk.

Aisha kama unataka kujenga viwanda Kuna maeneo ya kutosha yametengwa Kwa Ajili hiyo.

Mbeya ndio Kitovu Cha Uchumi wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

9. Makazi na Accomodations
Kuna fursa kubwa Bado ya ujenzi wa hoteli za kitalii na hoteli za kawaida maana ni Mkoa wa Biashara hivyo itakulipa.

Pia Hapa ni wewe tuu maana ujenzi wa Mbeya sio costful kama Mikoa mingine,unachagua ijengee tofauti au blocks au hata tofari mbichi udongo una nata vizuri kabisa.

10. Watu
Mbeya Ina idadi ya watu zaidi ya milioni 2.3 Kwa Mkoa mzima wanaokuhakikishia soko.

Aidha watu wake ni Wapambanaji ndio maana huwezi kusikia Mbeya ikitajwa kwenye mambo ya umaskini na shida ndogo ndogo,hawalalamiki kusubiria serikali.

11. Michezo na Burudani.

Mbeya Ina Wasanii wakubwa Toka kitambo ila icon ya Mkoa ni kina Sugu,VanBoy na Stamina.

Kwenye Michezo hapo ndio nyumbani hususani football.Mbega Ina Timu 3 Ligi kuu za Prisons,Ihefu,Mbeya City na Timu 3 Ligi daraja la kwanza za KenGold,Mbeya Kwanza na Tukuyu Stars.Na Ina Wachezaji Wakubwa wengi tuu na makocha.

Kiufupi hiyo ni summary ndogo sana Kati ya Mengi mazuri yaliyopo Mbeya,Karibuni sana Mbeya.






Ngoja wachangiaji wengine waje tuskie wanase.a nini kuhusu mbeya
 
Back
Top Bottom