Hakuna mtu aliwasiliana na rubani wa ndege iliyoanguka ziwani, shujaa Majaliwa na Chalamila watuombe radhi

Hakuna mtu aliwasiliana na rubani wa ndege iliyoanguka ziwani, shujaa Majaliwa na Chalamila watuombe radhi

mkuu unaamini kuna time inafika hali ya hewa hairuhusu tena ndege kupanda juu tena, fanya ufanyavyo ngoma haendi??
ndiyo hali ya hewa ikiwa mbaya unatakiwa urudi ulikotoka au utafute uwanja ulio jirani utue.
 
Sina utaalam huo kwa kweli.ila najaribu kuwaza tu.wanasema alikuwa na machaguo mawili kurudi mwanza au kutua ziwa viktoria.
Najiuliza kwanini alichagua kutua ziwa viktoria na sio kurudi mwanza
Ni rahisi kurahisisha kwamba angeweza kwenda lakini mambo ni mengi sana hasa kukiwa na radi. Hakuna anayependa kufa wakati kuna uwezekano wa kubaki hai.
 
Point ya msingi majaliwa hakuwa pekee yake na alikua mstar wa mbelee kuokoa watu watu walifungua mpira yeye akaenda nao chini ya maji ukafyatuka akazimia zoez lilikua la watu wengi sema yeye ndio man of the match
 
yaani acha tu mkuu. ni kama daladala....mafuta ya kwenye vidumu
Hayo ndiyo matatizo ya kuruhusu wawekezaji wajanja wajanja,wao kila kitu wanahonga ili utaratibu usifuatwe! Maana naamini kabla ndege yoyote ile haijaruka lazima ikaguliwe kila kitu, hadi kiasi Cha Mafuta kinachotakiwa kuwepo!
 
Tatizo watu maskini mnawaza kuhusu hela tu ndio maana hamshirikishi akili zenu. Ingekuwa rubani ni ndugu yako au mzazi wako pengine akili ingekukaa sawa.
Sasa ww unawaza badala ya Ku opt kupata taarifa kamili. Una MB za mawazo!!??
 
Kwa mujibu wa maelezo ya watu waliokuwapo ndani ya ndege na kufanikiwa kujiokoa, ndege ilijaa maji ndani ya dakika moja tangu ilipoanguka ziwani. Walilazimika kupanda juu ya viti upande wa nyuma.

Ushahidi wa picha za ndege ilipokuwa ziwani unaonesha upande wa mbele wote ukiwa ndani ya maji. Hakuna uwezekano wa mtu aliyekuwa nje kuweza kuona ndani kupitia kioo cha mbele kwasababu kulikuwa na giza kutokana na maji yaliyojaa.

Mfumo wa kielektroniki wa ndege ulikuwa umezimika baada ya kuzimika kwa injini hivyo kusingeweza kuwa na mawasiliano. Hata ukiangalia ndege baada ya kutolewa unaona dhahiri kwamba maji yaliingia kupitia upande wa chini ulioharibika.

Sasa natoa wito kwa shujaa Majaliwa na mkuu wa mkoa wa Kagera ndugu Chalamila kujitokeza na kuomba radhi kutokana na udanganyifu waliofanya.
Maswali yangu mimi hayako kwa ajili ya Majaliwa wala Chalamila. Kwa majaliwa hiyo ndo ilikuwa njia ya yeye kutoka kwa sababu hajatengeneza ajali yeye. Swali ambalo tunapaswa kujiuliza kwa nini Bukoba Airport Tower controllers hawajajitokeza kuelezea mawasiliano ya mwisho kati yao na rubani? Ikiwa rubani alishatangaza kutua na kuandaa abiria manake hali ya hewa ilikuwa inaruhusu kutua, tofauti na hapo Tower controllers wasingemruhusu kushusha ndege, bali angeelekezwa kuelekea kiwanja cha jirani mara moja. Na eneo la karibu kwake lilikuwa ni Mwanza na Musoma. Na vipi rubani alishindwa kuona uwanja ili hali abiria walikuwa wanaweza kuona maeneo yote alikokuwa wanaweza kupita.
Kwa hiyo nadharia kuwa tairi za ndege ziligoma kushuka linaweza kuwa na ukweli, ukumsikiliza ABIRIA mmoja anaseka kuna muda cabin Crew mmoja alikuwa anakuja nyuma anachungulia anarudi kwa rubani kulikuwa na vitu anaangalia. Kuna abiria anasema kuna wakati rubani alitaka kushusha ndege shambani au uwanja wenye nyasi.

Lakini ndege hii PW 494 kama mwezi hivi kuna mtu aliipoti kuwa wako angani na injini moja imezima. Na walilazimika kutua uwanja wa karibu.
 
Sasa natoa wito kwa shujaa Majaliwa na mkuu wa mkoa wa Kagera ndugu Chalamila kujitokeza na kuomba radhi kutokana na udanganyifu waliofanya
🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔 🤔
 
Point ya msingi majaliwa hakuwa pekee yake na alikua mstar wa mbelee kuokoa watu watu walifungua mpira yeye akaenda nao chini ya maji ukafyatuka akazimia zoez lilikua la watu wengi sema yeye ndio man of the match
Mpira gani unaouongelea hapa?
 
Shida vile vimilioni alivyopewa majaliwa.
Mmejiuliza chanzo cha ajali ni Nini?
Mmejiuliza rubani alishindwa vipi kurudi mwanza mpaka akaamua kwenda kutua ziwa viktoria?
Kurudi Mwanza au kwenda Mwanza!!?
 
Maswali yangu mimi hayako kwa ajili ya Majaliwa wala Chalamila. Kwa majaliwa hiyo ndo ilikuwa njia ya yeye kutoka kwa sababu hajatengeneza ajali yeye. Swali ambalo tunapaswa kujiuliza kwa nini Bukoba Airport Tower controllers hawajajitokeza kuelezea mawasiliano ya mwisho kati yao na rubani? Ikiwa rubani alishatangaza kutua na kuandaa abiria manake hali ya hewa ilikuwa inaruhusu kutua, tofauti na hapo Tower controllers wasingemruhusu kushusha ndege, bali angeelekezwa kuelekea kiwanja cha jirani mara moja. Na eneo la karibu kwake lilikuwa ni Mwanza na Musoma. Na vipi rubani alishindwa kuona uwanja ili hali abiria walikuwa wanaweza kuona maeneo yote alikokuwa wanaweza kupita.
Kwa hiyo nadharia kuwa tairi za ndege ziligoma kushuka linaweza kuwa na ukweli, ukumsikiliza ABIRIA mmoja anaseka kuna muda cabin Crew mmoja alikuwa anakuja nyuma anachungulia anarudi kwa rubani kulikuwa na vitu anaangalia. Kuna abiria anasema kuna wakati rubani alitaka kushusha ndege shambani au uwanja wenye nyasi.

Lakini ndege hii PW 494 kama mwezi hivi kuna mtu aliipoti kuwa wako angani na injini moja imezima. Na walilazimika kutua uwanja wa karibu.
Kama tairi ziligoma kutoka na rubani akaamua kutua ziwani basi itakuwa ni jambo la ajabu kabisa kutowapa taarifa abiria kabla ya kwenda kutua ziwani. Hii itakuwa highest form of unprofessionalism.

Pia bukoba hakuna control tower.
 
Shida vile vimilioni alivyopewa majaliwa.
Mmejiuliza chanzo cha ajali ni Nini?
Mmejiuliza rubani alishindwa vipi kurudi mwanza mpaka akaamua kwenda kutua ziwa viktoria?
Mi pia hili ndo limenishinda kuelewa katika hii issue nzima
 
Kama tairi ziligoma kutoka na rubani akaamua kutua ziwani basi itakuwa ni jambo la ajabu kabisa kutowapa taarifa abiria kabla ya kwenda kutua ziwani. Hii itakuwa highest form of unprofessionalism.

Pia bukoba hakuna control tower.
Ndege inashuka na kuruka vipi mkuu. Hata kama siyo tower kama tower I hope kuna control room haiwezekanani iwe ni blindness kiasi hicho.
 
Kama tairi ziligoma kutoka na rubani akaamua kutua ziwani basi itakuwa ni jambo la ajabu kabisa kutowapa taarifa abiria kabla ya kwenda kutua ziwani. Hii itakuwa highest form of unprofessionalism.

Pia bukoba hakuna control tower.
Huu muda aliotumia kuzunguka hapo bukoba mjini si angefika mwanza mkuu? tusubiri ripoti ya boeing hiyo ndo haitoficha kitu
 
Ndege inashuka na kuruka vipi mkuu. Hata kama siyo tower kama tower I hope kuna control room haiwezekanani iwe ni blindness kiasi hicho.
Wanaongozwa na control tower ya mwanza.
 
Huu muda aliotumia kuzunguka hapo bukoba mjini si angefika mwanza mkuu? tusubiri ripoti ya boeing hiyo ndo haitoficha kitu
Kuzunguka ni standard procedure kama hali ya hewa au jambo lingine limesababisha uwanja usiweze kutumika. Viwanja vya karibu vipo vingi hivyo hapo itabidi tusubirie ripoti ni kwanini alitua ziwani.
 
Sina utaalam huo kwa kweli.ila najaribu kuwaza tu.wanasema alikuwa na machaguo mawili kurudi mwanza au kutua ziwa viktoria.
Najiuliza kwanini alichagua kutua ziwa viktoria na sio kurudi mwanza
Hivi ni mimi ndo sielewi nini maana ya kurudi au ni nini? ni arudi au aende!??
 
Back
Top Bottom