Kwa mujibu wa maelezo ya watu waliokuwapo ndani ya ndege na kufanikiwa kujiokoa, ndege ilijaa maji ndani ya dakika moja tangu ilipoanguka ziwani. Walilazimika kupanda juu ya viti upande wa nyuma.
Ushahidi wa picha za ndege ilipokuwa ziwani unaonesha upande wa mbele wote ukiwa ndani ya maji. Hakuna uwezekano wa mtu aliyekuwa nje kuweza kuona ndani kupitia kioo cha mbele kwasababu kulikuwa na giza kutokana na maji yaliyojaa.
Mfumo wa kielektroniki wa ndege ulikuwa umezimika baada ya kuzimika kwa injini hivyo kusingeweza kuwa na mawasiliano. Hata ukiangalia ndege baada ya kutolewa unaona dhahiri kwamba maji yaliingia kupitia upande wa chini ulioharibika.
Sasa natoa wito kwa shujaa Majaliwa na mkuu wa mkoa wa Kagera ndugu Chalamila kujitokeza na kuomba radhi kutokana na udanganyifu waliofanya.
Sisi watanzania ni Mungu tu anatusaidia ila kwa kweli tuna matatizo makubwa kiufahamu Kwenye hili hakuna cha Msomi wa asiyesoma
Hata Mtu akisoma ndio anakuwa hovyo kabisa.
Mnaandika viposti vya kijinga kabisa kisa ni wivu wa kijana wa Watu.
Uliyeandika hii post sidhani kama unajua kuogelea Kwa kina kile Ile ndege ilipokuwa hakuna giza chini. Kwa taarifa yako Giza linakuwa kwenye kina kirefu mno. Huyu mtoto Majaliwa Hadi sasa sijaona uongo wowote amesema
Lingine. Kama wahudumu walitoa lock ya kitasa ili wapate msaada kwa watu walioko nje Sasa hapo tatizo liko wapi? Walipaswa kutoa ushirikiano ili waokolewe. Labda wewe ulitakaje?
Hivi unafikiri ni Jambo rahisi au ni ujasiri wa namna gani kusogelea chombo kama Ndege kwenye ajali ambayo hujui principles zake za uokozi wala madhara unayoweza kukutana nayo?
Wengi tunakumbuka ajali ya lory la mafuta Morogoro kilichokuwa kimetokea
Sasa twende na picha Ile pale na madhara yake.
Then Angalia Majaliwa alivyojitoa mhanga akawapa na wengine ujasiri wa kuliendea tukio
Hilo Kwangu naona linatosha Sana kusema Majaliwa anastahili si zawadi tu, Bali pia tuonyeshe tumeheshimu mchango wake na wenzie pia
Imagine wote tungeamua kuwa watazamaji na kuchukua video kusambaza mtandaoni nini kingetokea?
Naomba Sana tulinde Upendo na Mshikamano wetu, Mwenzetu akifanya Jambo nzuri tulikubali
na kumpongeza badala ya wivu na majungu
Ili wawepo akina Majaliwa wengine wa kesho watakaokubali kuingia gharama kwa ajili ya wengine
Asante. Ni hayo tu.