Hakuna mtu mkubwa kuzidi Simba SC, kwanini Wanasimba bado wanamzungumzia Manara?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Simba ni club kubwa mno

Hakuna mtu mkubwa kuzidi Simba

Mtu akiachana na simba inapaswa asahaulike maana sio tena mwanasimba

Nashangaa huko mitandao ya simba ni kumzungumzia Manara tu, mtu mdogo huyu iwaje awape taabu.

Hakuna mtu mkubwa kuzidi simba, kuna tetesi Al Ahly wamemnunua Luis na wanamtoa kwa mkopo kwenda Yanga, Luis ni mtu tu, Hakuna mtu mkubwa kuzidi simba, kama ameamua kuondoka basi kwaheri.

Hio ndio mtazamo wa simba, kwa wengine ni kwamba ili kitu kiwe kikubwa basi panshitaji kuwe na ushirikiano wa watu huku mchango wa kila mtu ukithaminiwa ndio team iwe kubwa.

Au mnaonaje?
 
Kati ya vitu ambavyo Yanga wanakosea wanaamini wamevunja uimara wa Simba kwa sababu Manara kajiunga nao.

Hii si kweli na wale wanaoumia kuondoka kwa Manara ni mashabiki waliokuwa wanahitaji booster ya Manara ili aingie uwanja, ili afuatilie timu yake na ili aipende.

Manara ni mdogo sana kuliko Simba, hata akiendelea huko Yanga hawezi kuwa mkubwa kuliko hiyo Yanga bali ataendelea kupiga kelele ila suala litakaloipa Yanga ukubwa ni matokeo mazuri uwanjani sawa na ambavyo Simba wamepata ukubwa kwa ajili ya matokeo yake.

Masau Bwire anapiga sana kelele huko Mlandizi ila timu yake haina matokeo hivyo matokeo bora huinua timu yoyote ile hata kama haina watu/mashabiki.

Leicester wakati wanatwaa ndoo ya EPL hawakutumia maneno walitumia dakika 90 ndani ya uwanja.

Hongereni Yanga kwa kupata mtu ambaye mnaamini ni mkubwa kuliko klabu yenu.
 
Kama ni mashabiki ni haki yao kwasababu akuna jambo latatokea kwa Simba au Yanga alafu mashabiki wa hizi timu wakabaki kimya.
Kikubwa kinachonipa imani ni viongozi wa Simba kuwa watulivu huku wakiendelea na mikakati ya kuhakikisha Simba anamaliza vizuri maandalizi ya pre season msimu huu.
 
Labda ungeelezea pia namna anavyozungumzwa ili ubalance post yako.

Niweke sawa:
  • Manara hasemwi na Simba kama Timu bali Anasemwa na Washabiki wa Simba, hivyo usihusishe Timu kwenye hili kwani kama ulivyosema Timu ni kubwa kuliko Manara.
  • Manara anazungumzwa kuhusu usaliti alioukana kuwa anasingiziwa na Babra kwasababu yeye anaipenda Simba na kamwe hawezi kuisaliti, wengi tuliamini maneno yake lakini kutokana na kitendo chake cha kuhamia Yanga tunaamini kwamba Barba alikua sahihi.
Hatuoingi Manaraka kuajiriwa Simba kwani naye pia anahitaji kuishi, lakini namna ya uendaji wake na yale anayoyapost Instagram yanatia shaka juu ya Utumishi wake alipokuwa Simba.
  • Anasemwa sana na Washabiki wa Simba kwa kitendo cha kumeza matapishi yake! Manara aliwahi nukuliwa akisema Yeye hatohamia Yanga labda ihamie maiti yake. Hivyo Anasemwa akionekana ni Mtu muongo na asiyejiamini kwa hiyo hata aliyomshambulia Babra yanatufanya tuone kuwa yeye ni Muongo.
  • Baadhi ya Washabiki wa Yanga waliahidi kuwa endapo Manara atahamia Yanga wao watahama Yanga! Hili limetufanya tumzungumzie Manara kuhusu kusababisha watu hao kuhama Yanga. Tunasubiri watekeleze ahadi zao.

Nawasilisha.
 
Watu hawamhitaji manara Bali wanamzodoa kutokana na mauongo yake ya kuwatukana viongozi wa Simba hapo kabla. Watu ndo wameamini kuwa viongozi Simba walimfukuza kihalali tofauti na maneno yake.
 
Kama mlivyotangulia kusema hakuna mtu mkubwa kuliko Simba sc basi hakuna umuhimu wa kuweka uzi hapa
Hebu ifike hatua hata mashabiki, wanachama na wapenzi wa Simba tuwe hatua bora zaidi. 👈Naishia hapo
 
Na ndivyo uthibitisho wa kuwa washabiki wa Yanga ni vilaza, yaani wanashangilia ujio wa Haji ilhali GSM imevurunda kuanzia usajili hadi kambi ya preseason,timu imesajili shikamoo jazz wa kikongo wao wanaona poa tu.
 

Pole kwa maumivu makali
 
Na ndivyo uthibitisho wa kuwa washabiki wa Yanga ni vilaza, yaani wanashangilia ujio wa Haji ilhali GSM imevurunda kuanzia usajili hadi kambi ya preseason,timu imesajili shikamoo jazz wa kikongo wao wanaona poa tu.
Pole kwa maumivu makali
 
Huyu anayeanzisha uzi ama ni Manara mwenyewe au ana vinasaba naye ukifatilia post zake toka manara anahama Simba utaona jinsi alivyokuwa akiangaika kupost
 
Huyu anayeanzisha uzi ama ni Manara mwenyewe au ana vinasaba naye ukifatilia post zake toka manara anahama Simba utaona jinsi alivyokuwa akiangaika kupost
Yupo sana huku, we sema tu neno zeruzeru au mzee tozi wa bandari uone moderators wanavyoliliwa post ifutwe anajifanya ni BULLY sana ila hana lolote as long as ataendelea kuongea pumba tutahangaika naye siku 365 ila viongozi wanyamaze kimya hivihivi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…