Hakuna mtu mwenye kujitambua na mwenye Akili Timamu anayeweza kuishabikia au kuiunga mkono CHADEMA kwa Sasa

Hakuna mtu mwenye kujitambua na mwenye Akili Timamu anayeweza kuishabikia au kuiunga mkono CHADEMA kwa Sasa

Kwa kuwa Nahitaji kuona Amani ikitamalaki na siyo kuvurugwa na watu Kama chadema

Wewe unatatizo sehemu. Chadema haipo bungeni Wala kwenye Halmashauri au kwenye mitaa na vijiji, lakini inakuhangaisha. Bila Mbowe kuongelea tozo unadhani ingefutwa?. Aliongea siku moja leo Waziri kafanya mabadiliko. CHADEMA is there to stay.
 
Nyie si mlikimbia ndani ya ukumbi wa bunge la katiba, Sasa kwanini mnaanza kulia Lia hapa Tena?
Tutakaaje Rasimu mkaiongezea upupu, shombo na Kila aina ya uvundo!!!!

Chama chenye laana mkampiga Mzee WARIOBA aibu adabu hamna!!!

Tunairudisha mezani RASIMU alosimamia Judge WARIOBA, ifanyiwe marekebisho kdg, tupate Katiba mpya.
 
Hela alizotoa sabodo mlipeleka wapi Kama hata ofisi zinewashinda kujenga?

Unahangaika Sana. Unazionea donge pesa ya Sabodo lakini unafurahia ufisadi wa CCM miaka nenda Rudi. Kemea kwanza ufisadi CCM ndio uanze kuulizia pesa za chadema zimetumikaje.
 
Labda hamtambuu Samiah Kama Rais wake. Usimlazimishe kumkubali mtu asiyemtaka. Uchaguzi haramu huzaa Viongozi haramu.
 
Kwa Sasa hakuna mtu mwenye Akili Timamu na anayejiheshimu anayeweza akaanza kuiunga mkono Chadema, kwanza mwenyekiti wake ni gaidi aliyepanga njama za kuuwa viongozi wa serikali na ushahidi upo mpaka mahakama ikamkuta na kesi ya kujibu, Pili makamu mwenyekiti wake Tundu Lisu ameng'ang'ania getoni kwa Amsterdam ,tatu Lema analishwa yeye na mke wake na lizungu huko Canada.

Kwa Sasa Ni chama kilichokosa dira na muelekeo, Ni chama kilichokosa uongozi wenye kufanya maamuzi ya mwisho na yakaheshimika na kufuatwa na wanachama wake, Ni chama ambacho kimejaa vijana wenye mihemuko, kukurupuka,wasio na adabu Wala heshima, hawana staha Wala Subira, hawana utulivu Wala vifua, Ni Kama makambale tu kila mtu ana ndevu na Hakuna wakumheshimu Wala kumsikiliza kiongozi wake, ndio maana unaweza ukaona kakijana kadogo kiumri kanamtukana mtu mwenye umri sawa na babu au Bibi yake

Ni chama ambacho kila mtu Ni kiongozi kwenye ukurasa wake wa kimtandao na atakachokiandika anataka iwe ndio msimamo wa chama chote, kila mtu Anayo Amri ndani ya chama, Haieleweki Nani msemaji wa chama au Nani katibu wachama, Haieleweki nani mtoa msimamo wa chama na Nani mfafanuzi wa masuala ya chama maana kila mtu ni mjuaji na Nikiongozi hata Kama unaona kabisa huyu kichwani hamna kitu na Hana taarifa za kutosha

Ni chama kilichojaa vijana ambao Ni Kama wamekosa malezi ya wazazi wao, Ndio maana unaona wao wanaweza mtukana yeyote Yule kwa matusi ya nguoni na wakawa wanapongezana na kusema huyu ndio kamandaa na kupigiwa debe la kupewa uongozi kwa kuwa mtukanaji mzuri, kwao adabu Ni Kama almasi kwao maana hawana msamiati huo katika vinywa vyao,

Ni chama kilicho jaa vijana walio na upeo mdogo Sana, wao hubeba taarifa na kuishadadia hata Kama hawajuwi ukweli wake, Ni chama kilichokosa Sera na ajenda za kugusa maisha ya watanzania wanyonge, hakina dira Wala muelekeo, hakina hoja zenye mashiko Wala mvuto kwa watu kuweza kuwaunga mkono

Ndio maana watu wenye akili kwa Sasa wanawakwepa na Wala hawapo tayari kuwasaidia kwa lolote, hata wapige kelele vipi hakuna anayewasikiliza Wala kuwajari maana wamepuuzwa na watanzania, wamekuwa Kama vibaraka wa wanyonyaji, maana chadema wapo tayari kuungana hata na shetani kuleta machafuko hapa nchini

Jiulize Nani mwenye akili anayewatetea hao chadema kwa Sasa,?jiulize wale wafadhiri waliokuwa wanawasaidia huko awali wamekwenda wapi kwa Sasa,? Utasaidiaje mtu asiyejitambua? Hivyo Basi kwa kuwa hawajitambui Ni lazima waongozwe nakunyooshwa njia ya kufuata na kupita, hawawezi wakaachwa hivihivi maana hawawezi kujiongoza hivyo Ni lazima waongozwe na CCM Tuuu watake wasitake lazima wasonge mbelee
Mtoa mada anamakasiriko Sana, watu weupe sio wazuri aisee
 
CCM inafanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa ilani yake namna inavyotekelezwa, CCM ndio yenye dhamani ya kuwahudumia wananchi kwa kuwa ndio chama kilichopewaa Ridhaa hiyo, Sasa hao chadema wafanye mikutano ya Nini? Kwani Marekani ulishaona wanazulula mitaani uchaguzi ukiiisha? Huu Ni muda wa kazi, tuiache ccm iwahudumie watanzania

CCM ilipewa ridhaa lini?. Uchaguzi ulitakiwa kurudiwa sio kwa ujinga ule. Unatumia billioni 60 kwa kitu ambacho ukiamini.
 
CCM yenye dira na uelekeo ndio imetufikisha hapa tulipo.Mkitumia kigezo Cha maendeleo Ni kitu endelevu kuficha aibu za kushindwa kufikia malengo na propaganda zenu.
Mmekongoroa nchi wezi nyie.
 
Sasa kibaya Ni kuwa chadema umekosa Safi ya uongozi yenye kutoa msimamo na muelekeo wa chama ikaheshimika na kupokelewa na wanachama,

Huo mwelekeo wanautolea wapi? Wakati Mwenyekiti wa CCM amewakataza kutofanya siasa miaka Saba Sasa?. Unapoongea kitu jaribu kuwa mkweli
 
Tindo ndugu yangu hivi nyie si mlikimbia Wenyewe kwenye bunge la katiba? Sasa mnataka katiba ipi Tena Tindo ndugu yangu, Nenda Katoe maoni kwenye kikosi kazi kilichoundwa, Mimi Naheshimu Sana michango yako humu

Tulisusia bunge la katiba baada ya CCM kuanza kuchezea maoni halali ya wananchi. Nikatoe maoni kwenye kikosi ya nini wakati kila kitu kiko kwenye rasimu ya Warioba? Kikosi kazi ni matumizi mabaya ya kodi za wananchi, wakati mchakato halali wa kukusanya maoni ya wananchi ulishafanywa na tume ya Jaji Warioba.
 
Endelea na dharau zako. Walikuwepo wengi zaidi yako walioitumia chadema Kama ngazi ya uteuzi, ila leo hawapo.
 
Atawa
Anakwenda kuwakubali covid wao na ruvuku wanapokea kama kawaida, chadema ni rubbish

Punguza ujuaji atawakubalije Covid 19 wakati kesi ipo mahakamani na wameifungua wao Covid 19. Halafu kwa ufupi ili Covid 19 warudi uanachama, inatakiwa halmashauri kuu ikae Tena.
 
Ninyi hat ofisi ya chama tu imewashinda kujenga, Sasa Nani awape nchi nyie? Si mtabomoa hata vilivyojengwa? Hamna nafasi ya uongozi kwa watu Kama nyie hapa, mtaishia kukusanyana hapo hapo ufipa kupiga stori

CHADEMA ndio agenda yako?. Mbona serikali yako yenye Kodi, tozo, mikopo na misaada imeshindwa kujenga vyoo vya shule za msingi?. Ndio nikakuambia anzia kukosoa ndani mwako.
 
Ninyi hat ofisi ya chama tu imewashinda kujenga, Sasa Nani awape nchi nyie? Si mtabomoa hata vilivyojengwa? Hamna nafasi ya uongozi kwa watu Kama nyie hapa, mtaishia kukusanyana hapo hapo ufipa kupiga stori
Ni ofisi ngapi ccm imejenga kwa fedha zake zaidi ya hizi walizorithi kutoka chama kimoja?!
 
Hata Uhuru ulionao wa kuandika na kutukana hapa Ni matokeo ya kazi njema ya CCM ya kusitawisha demokrasia na Uhuru hapa nchini

Punguza uongo. Demokrasia gani unazuia vyama vingine visifanye siasa inafanya CCM pekee yake. Halafu kuhusu Uhuru wa maoni kamuulize mwanachama wa CCM anaitwa Ndugai alichofanyiwa.
 
Punguza uongo. Demokrasia gani unazuia vyama vingine visifanye siasa inafanya CCM pekee yake. Halafu kuhusu Uhuru wa maoni kamuulize mwanachama wa CCM anaitwa Ndugai alichofanyiwa.
Mnataka mpewe Uhuru gani ndio mlizike? Mbona mnatukana viongozi wetu na Hakuna anayewakamata? CCM inachofanya Ni ukaguzi wa utekelezaji wa ilani yake
 
😂😂😂😂 hivi vijamaa vinalala na uoga 2025 hawatoamini macho yao
 
Back
Top Bottom