Wameacha kulawiti watoto makanisani?Kwa kweli wamefanya kazi ya kitume katika tamko lao kuhusu mkataba wa serikali na DP World
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wameacha kulawiti watoto makanisani?Kwa kweli wamefanya kazi ya kitume katika tamko lao kuhusu mkataba wa serikali na DP World
Wewe tuambie walifanikiwa nini?Angalia utachekwa sana kwenye huu mjadala unapiga Dana Dana na kuruka ruka! Hata yeye akisoma atakushangaa.
Ilikuwa zamani hiyo enzi za Nyenyere.Kwa kifupi kabisa, Viongozi wa Serikali yetu hawawezi hata kidogo kushindana na TEC.
TEC hawana tabia ya kuropoka ropoka, lakini wana power kweli kweli.
Utamani iwe hivyo?kutoka ndani ya korido za vatican
1 . dubai wakipewa bandari mfumo wa udini utakua kwa kasi na kuleta mpasuko mkubwa
2. kuna agenda ya siri nyuma ya bandari kwamba wakishaingia rasmi.. taratibu watahakikisha mfumo wa utawala na uongizi nchini unatoka dini ya kiislam...
3. vikundi vya kigaidi vitaibuka na upitishwaji wa silaha kiholela utaongezeka kwa kasi kubwa na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe(watanzania) yataibuka
4.mfumo wa ajira utakuwa wa dini moja ya kislam na kuwacha wakristo kwa idadi kubwa bila ajira
5. umasikini utaongezeka kwa kasi kubwa maana bandari zote na maeneo mengi ya nchi kavu yatakuwa mikononi mwa waarabu na wazawa watapewa mashart magumu sana hata kufika maeneo hayo.
6. watahakikisha bara inaingia kwenye machafuko na hapo zanzibata itavunja muungano..ikumbukwe bandari za zanzibar hazimo kwenye mkataba.
'' the vatican intelligence and its fields of resources are second to none''
Ulisimuliwa au ulikuepo? Slaa lini aligombea urais na lini alionesha Nia ya kugombea urais,Wewe tuambie walifanikiwa nini?
TEC walipiga jalamba makanisani nchi nzima kumwangusha JK, mpk wagalatia wa CCM wakaungana na kanisa.
Mtoto wa mjini akaiingiza familia yake kwenye kampeni mwisho wa siku hiyo TEC haikuweza kumweka Padri Slaa
TEC, watakula aibu yaona huu ndo msumari wa mwisho kwenye jeneza.
Kulewa kwako ni haramu ila RUSHWA,KUUWA NA KUPORA MALI ZA WATU ni halali kwako.Jifunze hta kuandika 🤣🤣...Mimi sili rushwa wala kulewa ni haramu kwangu kabisa..
Nataenda haki na sio kuwa mjinga wa kupelekwa na tamaa za kidunia ,naheshimu mawazo ya kila mtu bila kuleta vitisho kama kikund chenu cha ngoma hicho .
Jibu ni kwamba ALIPINGA hakuna cha kuhama mada,Msema kweli ni mpenzi wa Mungu.Mbona unahama mada,kwenye post yako unasema Magufuli alipingana na TEC kwenye kuvaa barakoa na akashindwa.
nikakujibu Magufuli hakupinga barakoa ila alitoa tahadhari ya barakoa zinazotoka nje.
nikasema ni kumchafua Magufuli kwamba alipingana na TEC wakati si kweli,Magufuli hakuwai kupingana na taasisi yeyote ya dini hata waraka wa TEC wa kupingana na Magufuli kuhusu Covid haupo ni uzushi wako tu wa kusema alishindana na TEC na akashindwa.
Unachonganisha kanisa na watu wasiolipenda ujue?! Sio sifa. Hii inapelekea vita vya chini kwa chini na watu kutengeneza agenda za kuwaangamiza. Stop this foolishness.Kwa wajuzi wa historia ya Tanzania wameishajua kuwa Tamko la Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) la kuhusu mkataba baina ya serikali ya Tanganyika AKA Tanzania na DP World ni kaa la moto mkali ambao unazidi kumchoma vikali muhusika mkuu na chama chake mpaka watakapokufa kisiasa mapema kama wataendelea kushupaza shingo.
Katika historia ya Tanzania hakuna mwanasiasa au Rais aliwahi kupambana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) halafu akashinda. Haijawahi kutokea na haitawahi kutokea katika miaka hii ya karibuni. Kufanya hivyo ni kujiangamiza kisiasa(political suicide).
Unaweza kuukataa huu ukweli lakini kuukataa kwako hakuwezi kuubadilisha kuwa uongo.
Mwl. Nyerere pamoja na nguvu zote za kikatiba alizokuwa nazo katika utawala wake lakini hakuwahi kutumia nguvu katika kupitisha ajenda zake za kisiasa pale ambapo maaskofu walikuwa na shaka au kumpinga. Alitumia nguvu ya ushawishi wa hoja kwa kujadiliana nao mpaka wakamwelewa na kukubali.
Nguvu za Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) zimeendelea hivyo katika tawala zote nchini. Hakuna mwanasiasa mwenye uelewa wa Tanzania na akili timamu aliweza kupuuza sauti ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).
Muhusika mkuu wa mkataba wa DP World hakutegemea kama TEC wanaweza kutoa waraka mkali kama waliotoa kwa sababu sehemu ya 17 ya waraka imepigilia msumari wa mwisho wa jeneza la mkataba.
TEC IMEITAKA SERIKALI IACHANE NA MKATABA HUU.
Sehemu ya 17 ya waraka wa TEC inasema, “Hivyo tukiwajibika kimaadili, tunaona ni jukumu la serikali kusikiliza wananchi wanaotaka mkataba huu ufutwe. Kwa kuwa tumeonesha kuwa Tanzania tumeshawekeza na kuendeleza bandari, reli na bandari za nchi kavu; niwajibu miradi hii tuiendeshe Watanzania wenyewe huku tukikaribisha ubia tunaoudhibiti wenyewe. Hiki ndicho wananchi wanachokililia kusudi tujenge uwezo wetu wenyewe. Kwa vile tumegundua mapungufu yetu ya uendeshaji wa bandari, tunaweza kujizatiti kurekebisha mapungufu hayo wakati njia za kiuchumi zikibaki mikononi mwetu. Kwa sababu hizo na maelezo yote ya hapo juu, sisi Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania hatuungi mkono Mkataba huu”.
Baada ta waraka kutolewa, muhusika mkuu na genge lake akaanza kuhaha akitafuta jinsi ya kukabiliana nao. Amemtuma kiongozi mkuu wa nchi mstaafu ili ajibu hoja lakini hakufanikiwa kuzima moto, amejaribu kutumia mbinu za kidini kwa kuwatuma baadhi ya mashekhe ili wawajibu TEC katika misingi ya kidini lakini pamoja na juhudi zote, moto wa waraka wa TEC ndio unashika kasi ya kumchoma kisiasa. Ametuma “wajinga” fulani washambulie haiba ya maaskofu badala ya kujibu hoja hawajafanikiwa.
Alichofanya kwa sasa ni kuwatuma baadhi ya viongozi ndani ya serikali kwenda Dubai ili kuwaeleza wenye DP World kuhusu moto unavyowaka nchini ili waangalie namna ya kufanya ili kuondokana na moto mkali kisiasa ili kuepuka maafa ya kisiasa. Kwa hivi karibuni ndege ya Rais imekuwa na safari nyingi za kwenda Uarabuni na kurudi.
Katika hali hiyo ya kutapatapa ametangaza eti tenda ya kukaribisha wawekezaji kwenye bandari Terminal 2 ili ionekane hakutaka kugawa bandari zote kwa DP World wakati mkataba(IGA) unabainisha ni bandari zote na maziwa yote ya Tanganyika AKA Tanzania bara. Mjinga gani atakuja kuwekeza kwenye terminal 2 wakati kuna IGA inasema uwekezaji wowote katika bandari na maziwa nchini lazima kwanza uridhiwe na DP World.
Tumeona pia amemuondoa waziri wa katiba na sheria ili eti ionekane kama ndiye aliyesababisha hili sakata la DP World wakati kwenye IGA kuna saini ya Rais! Huku ni kutapatapa.
Kama isingekuwa waraka wa TEC, mchakato wa kuzifuta Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Rasilimali na Maliasili na Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba inayohousu Rasilimali na Maliasili za Nchi za mwaka 2017 ungefanyika bungeni na hili tangazo lingine la tenda ya kukaribisha wawekezaji lisingetolewa! Hii yote ni imefanyika katika hali ya kutapatapa baada ya tamko la TEC.
Hakika.Yule alikuwa mwehu tu na ndo mana alikufa kizembe
Hivyo vyote sifanyi kwa vile dini yangu hairuhusu.!Kulewa kwako ni haramu ila RUSHWA,KUUWA NA KUPORA MALI ZA WATU ni halali kwako.
Sudan,Somalia,Pakstan,Mali,Ethiopia hiyo dini haipo?Hivyo vyote sifanyi kwa vile dini yangu hairuhusu.!
🚶🚶🚶🚶Uharo unanuka!
Mkuu, ninachokiona katika hoja zako ni personal incredulity fallacy!
Yaani kwa fikra zako unadhani TEC kwa historia yake nchini wanaweza kupambania suala ambalo halina maslahi kwa taifa?
Nadhani wewe ndiye unayedhani hoja za TEC niza kidini.
Wanaoamin wanashindana na Tec ni hawa vidampa wa DP World humu jamvini tu but viongoz wanajua kua hawawez shindana na TEC.
Mkuu, Nakubaliana na mtazamo wako kwa kiwango kikubwa!Bila waraka, maliasili nayo ingepigwa mnada.
Bibi must go 2520.
Mkuu, kwani Rais hajui kama "wanaomzunguka" wanangombanisha na Watanganyika?Raisi Samia lazima awe makini na watu wanaomzunguka.
Wanamgombanisha na Watanganyika.
Hao wapigaji.
Wapigaji (Wanaume) kwa niaba ya Dr. Mongela.
Ila Raisi lazima atuombe radhi Watanganyika.
Tulisha uzwa kwa Waarabu